Mheshimiwa John Mnyika: What is Plan C

Mr rocky nna uhakika unajidai umelala na cku zote anayejidai amelala ni vigumu kumuamsha. ata kama hutaki kuamka cc 2takupa ukweli ivoivo mwisho utaamka tu. najua akifa baba ako au mama ako kwa tatizo la umeme hospitalini utaamka 2 kwan nnaona unaona wanakufa mahospitalini kwa kukosa operation juu ya tatizo la umeme unawaona kama wanyama tena wale wasio na faida duniani. mwogope mungu ongea ukweli acha kujidai umelala.

Mkuu sidhani kama umenitendea haki kwa hapa
Sishabikii kukosekana kwa umeme wala sishabikii kinachoendelea hapa tanzania kwa sasa na naliona ni taztizo zaidi ya tatizo lenyewe maana hili kwa wengi ni janga tena kubwa sana
NApenda nioone suluhisho la haya napenda nione ufumbuzi na ufumbuzi huo uwe kwa njia yoyo-te ile ila upatikane pale ambapo tatizo la umeme litakuwa historia
pale tutakapoona uongozi wa nchi umerespond kweney matatizo ya wananchi wake
pale tutakapoona uongozi unawajibika kwa hilo na kutake action
Ndo hapo nasema naungana na wote wale ambao wanaitakia mema nchi hii katika kuhakikisha kuwa tunaondokana na uongozi huu wa kuiga wa kuachia kila kitu kiende kinavyotaka
 
Heshima Mbele Mkuu na Hongera kwa Kazi Nzuri....<br />
<br />
Ni kweli kwamba nyie sio wakusanya Kodi lakini tulipofika tunahitaji msaada sababu kinachofanyika sasa hakifanyi kazi….<br />
<br />
<b>Plan A</b>: Serikali, Waziri Ngereja na watu wake wameshindwa kazi kinachoendelea sasa ni usanii na watu hatupewi majibu yanayoeleweka<br />
<br />
<b>Plan B</b>: Kuandamana mpaka kieleweke lakini sidhani kama hii itasaidia na je isiposaidia ni nini kitafuata…. what is <b>Plan C</b>:<br />
<br />
Sababu watu waliotakiwa kufanya kazi yao wameshindwa tunaomba wewe Waziri kivuli tushauliane ni nini cha kufanya, na tuone kama sisi wananchi tunaweza kujinasua wenyewe katika hii laana ya kujitakia ambayo imepelekea uchumi kusimama...<br />
<br />
Ni ukweli usiopingika kwamba sasa hali ni mbaya sana sehemu kama Mbeya, Arusha na Mwanza watu hawana umeme kwa takriban wiki sasa. Yaani umeme haurudi hata dakika moja watu wamebadilisha fridge kuwa kabati na kuvaa nguo ambayo haijanyoshwa imekuwa fashion.<br />
<br />
Mwanza huwa wanapata mgao wa<b> 42MW</b> kutoka grid wakati sasa wanapewa <b>4MW</b>… Sasa Je tatizo ni nini je ni mitambo au mafuta ndio hayapo na kama ni mafuta kwanini tunakodi mitambo ambayo itakuja kutumia mafuta hayo hayo na kama ni mvua iweje baada ya bajeti kupita ndio maji kuisha kabisa (yaani ule umeme tuliopata wakati bajeti haijapita ulitoka wapi..)<br />
<br />
<b>Pendekezo</b><br />
Sababu Serikali imeshindwa Je sisi wananchi tunaweza kuchangia nini..?, Kama tatizo ni mafuta ni vema tukajua hayo mafuta gharama ni kiasi gani ili wananchi na wadau tuweze kujitolea (sababu ni more expensive kutumia generator ndogo ndogo kuliko generator kubwa za Tanesco ambazo ni more efficient). Mfano Nyakato Mwanza huwa kuna Generator sasa kama hizi hazijawashwa nina uhakika wafanya biashara wote watakuwa tayari kuona kwamba hizi zinawashwa hata kwa kuchangia gharama...<br />
<br />
Kwa niaba ya wananchi wengine tunakuomba tuchangie mawazo ni kipi tunaweza kufanya ili kuondokana na huu usumbufu.., hata kwa kuonyesha mfano kwa kuondoa huu usumbufu hata kwa kusaidia mtaa mmoja au kuhakikisha inapita harambee ya kuchangia mafuta… (kama tatizo ni mafuta..) (nina uhakika hii italipa dividends come 2015)<br />
<br />
Ninaomba mawazo yako mkuu wewe kama Waziri Kivuli na Mwana-Jamvi mwenzetu sababu hii <b>emergency solution</b> kama itafanikiwa <b>December ambapo mvua zitaanza sioni </b>kwanini ziitwe emergency kwangu mimi zinaonekana<b> kama long term solution</b>
<br />
<br />
 
Tanzania wake up!!!!!!!!!!!yaani unasikitisha unamuuliza Mnyika what next?yeye amekwambia wewe una mpango ngani kuikomboa nchi hii,good luck you!!you are well informed!!wewe kama wewe unnafanyaje?Tanzania wake up!!!!!!!!!!!!!
 
Wakuu kwa mnaosema kuingia barabarani kama Egypt, Tunisia na Libya inabidi tujiulize yafuatayo:-
  • Ni kweli mpo tayari na wenzenu wapo tayari..., hata kuendelea na demonstration za nguvu kwa miezi na miezi, kumbuka kwamba Tunisia ilichukua muda vilivile Egypt walikuwa tayari (na Jeshi lililkuwa upande wa wananchi) na bila Nato sidhani kama Gadafi angetoka
  • Na tukiondoa mafisadi waliopo sasa je ni kweli kuna system in place ya kuwazuia watakaoingia wasigeuke mafisadi wenyewe..., kumbuka system inabidi ibadilishwe ama sivyo tutakuwa tunabadilisha watu waendelee na kazi ile ile.
  • Je hakuna njia ya kuweza kuwatoa hawa.., (best case scenario ni kifo cha CCM) na kuongezeka kwa nguvu za upinzani ili chama kitakachokuwa madarakani kiogope kwamba kikichemsha mwenzake atachukua madaraka.
Kwahiyo wakuu ni kweli scenario ya Misri, Egpyt, na Tunisia ni sawasawa na hapa..., na watu kweli wapo tayari...? (na hapa simaanishi mmoja au wawili kati ya watu kumi) kumbuka watanzania wengi bado hawajui haki zao..
 
Tanzania wake up!!!!!!!!!!!yaani unasikitisha unamuuliza Mnyika what next?yeye amekwambia wewe una mpango ngani kuikomboa nchi hii,good luck you!!you are well informed!!wewe kama wewe unnafanyaje?Tanzania wake up!!!!!!!!!!!!!

Mkuu katika suala la umeme ni nani wa kuwauliza zaidi ya hawa wafuatao:-
Serikali...... (bahati mbaya wamelala)
Waziri wa Nishati...... (huyu hata cha kusema sina)
Waziri Kivuli..............(huyu ndio ninamuuliza Mnyika..., mfano maandamano yasipofanikiwa ni nini kinafuata...?)

Kumbuka umoja ni nguvu na mtanzania mmoja mmoja hawezi kuleta tofauti na umoja lazima huwe galvanised kwahiyo hata watu waungane kunahitajika mwanaharakati wa kuwaonganisha ili nguvu zao zielekezwe sehemu moja (we need plan and vision).

Au wewe mkuu zaidi ya kuwaambia watanzania waamke (wake-up) unashauri nini...?, wakiamka wafanye nini...?
 
Unajua kinachoendelea hapa Tanzania ufisadi, kulindana katika maovu, ili hali watanzania wanaendelea kupata shida kila kukicha na hakuna mtu aliye diriki kumwambia mfalme Juha kwamba yuko uchi.

Tunaendelea kushangilia, hata tukae barabarani NATO hawezi ku support kwani marekani mafisadi wakubwa wanawatumia mafisadi wa ndani kubadilisha vyandarua na migodi yetu nguvu tulibaki nayo ni sisi wananchi tu ambao ni yatima hatuna baba hata mama.

Samahani afadhali ya chokara anapata na msaada lakini siyo maskini wa tanzania tunaumia, ndiyo maana it will reach a point where we have nothing to loose than our lives
 
Kwahiyo sisi kama jamii hatuna mawazo ya kuweza kujinusuru na hili janga?!!!!

Na mnao sema dawa ni kuwangoa madarakani waliopo..., Swali ni kwa vipi tutawangoa na kwa njia ipi ? (kama sikosei tulipoteza chance mwaka jana kwenye kura...)

Na kama ni kuwaiga Eqypt ni nani mwenye plan na je ni kweli watanzania wana stamina za kuweza kufanya kama yaliyofanyika Egypt..?

Na kama ni ruksa kuweza kuzalisha umeme je sisi kama jamii hatuwezi kuungana na kuzalisha japo MW chache au hatuwezi kama Jamii kufanya hii kazi hata kwa kutumia Biomass kuwasaidia na ndugu zetu huko kijijini
 
Why asking John Mnyika, and not the Government. Serikali haina cha plan A wala Z. Ila kuna siku haya mambo yataeleweka tu wala wewe usihangaike na Mnyika.
 
As long as we are using oil as a souce of energy, we will always have a CRISIS, it happened a long time before and it will happen again.The movement should be "KIWIRA BILA HILA,AU BILA BILA!"-Wake up mofos!!
 
Why asking John Mnyika, and not the Government. Serikali haina cha plan A wala Z. Ila kuna siku haya mambo yataeleweka tu wala wewe usihangaike na Mnyika.

Kwahiyo plan yetu sisi wanajamii ni kusubiri siku mambo yatakapoeleweka..?
Na waziri kivuli hawezi kusema au kufanya lolote kama waziri na serikali imeshindwa kazi...?
Na sisi wananchi je hatuwezi kufanya lolote pia?
 
imagine nasoma huu mjadala nikiwa gizani, yaaani serikali yetu imejaaa uozo na sio compitent staff kama ambavyo hujisifia. upinzani ndo nafasi yake hiii kutia chachu kwa serikali
 
Mimi nadhani kama ikifikia hatua ya sisi kuchangishana kwa ajili ya umeme hakuna sababu ya kuwa na serikali. Naona ni heri kuitoa serikali kwanza then tuangalie ustaarabu mwingine.
 
Mimi nadhani kama ikifikia hatua ya sisi kuchangishana kwa ajili ya umeme hakuna sababu ya kuwa na serikali. Naona ni heri kuitoa serikali kwanza then tuangalie ustaarabu mwingine.
<br />
<br />
duh!mkuu next time jitahidi kuzingatia taratibu za uandishi....USHAURI TU!
 
Plan C ni ku campaign kwa kila hali kubadilisha uongozi wa nchi hii. Hawa magamba wameshazoea kutuburuza watakavyo na kutudanganya kama watoto wadogo. Kabla ya kupitisha bajeti ya nishati na madini umeme uliwashwa muda wote karibu wiki 2 mfululizo! Hayo maji yalitoka wapi? Sasa hivi ndio hawana mpango kabisaa, wamebaki kuzungumzia ya Jairo tu! Eti uchumi unakua! Uongo mtupu! Nchi imebaki mifupa mitupu! Agha!
 
<font color="#4b0082"><font size="3"><span style="font-family: century gothic">Mnaruka ruka weee, kuweni wawazi bana kuwa mnataka kuandamana kama Misri, Tunisia na kwingine ili kuingoa serikali kwanguvu</span></font></font>
<br />
<br />
Hilo unalisema wewe na naamini kuwa unaamini ktk ulilolisema.
 
Ndugu yangu "senior expert member" sitaki kuamini kwamba tunachokijadili hapa hukijui na ndo maana unatoa mapendekezo ambayo kwa mtazamo wangu "hayawezi kusaidia". Nataka nikukumbushe tu kwamba hitaji la umeme sio hitaji dogo la kufanyia harambee kama mnavyofanya kwa ajili ya kicheni party, send-off, harusi au kuchangia mtoto aliyekosa ada ili aende shule. Tunaongelea hitaji la mamilioni, kama sio mabilioni ya pesa ili kuendesha miradi mikubwa ya kuzalisha umeme.

Kumbuka pia kwamba mafuta yanayohitajika si kwa kiasi cha kufanyia harambee kama unavyopendekeza. Hayo yote tisa, la mwisho, ambalo kimsingi ndiyo hoja yangu, nataka kukumbusha kwamba kama ni harambee wananchi tumefanya nyingi na za kutosha, na bado tunaendelea kufanya kwa ajili ya kutatua matatizo tuliyonayo kwa maendeleo ya nchi yetu-ikiwa ni pamoja na umeme.

Pengine utajiuliza tunafanya harambee hizo kwa njia gani! Jibu liko wazi: Ni kupitia kodi yako na yangu, na ya watanzania wote. Mimi binafsi nalipa zaidi ya Tsh 150, 000 kama kodi ya mapato kila mwezi-achilia mbali kodi kubwa ninayolipa kupitia kununua bidhaa na huduma itokanayo na VAT. Wewe pia unajua ni kiasi gani unalipa na wengine wote. Hata kama hulipi kodi ya mapato kwa maana ya kwamba wewe si mfanyabiashara wala mfanyakazi katika sekta rasmi (serikali na taasisi zake au mashirika ya umma na binafsi), bado unalipa kodi nyingi tu kupitia kila kitu unachonunua maana kuna kodi ya ongezeko la thamani (VAT) ambayo inajumuishwa katika garama ya kila bidhaa unayonunua au huduma unayolipia.


Hivyo ni vema watanzania tukajua kwamba heal inazozitumia serikali ni hela zetu. Kwa lugha nyingine: Watanzania tunaji-mobilize kila siku kufanya harambee kupata hela ambazo ndizo akina Jairo na wengine wanazitumbua. Kwa msingi huo sioni mantiki ya hoja ya watanzania "kuji-mobilize kwa hali na mali" ili kondokana na matatizo tuliyo nayo ilihali tayari tumejimobilze vya kutosha. Itoshe watanzania tukaelewa kwamba wale tuliowapa dhamana ya kuzitumia hela hizo kutuletea maendeleo wameamua kuzitumia kwa namna wanayojua wao ili wajiletee maedeleo yao binafsi kwa jasho letu watanzania.

KWA MSINGI HUO, NAKUBALIANA NA HOJA YA WATANZANIA "KUJI-MOBILIZE" LAKINI KWA LENGO MOJA TU, NALO NI "KUIONDOA SERIKALI YA SISIEMU AMBAYO IMELEWA NA KUJISAHAU KIASI KWAMBA HATA SERIKALI YENYEWE INAPINGANA KIMAAMUZI. MFANO WA HIVI KARIBUNI NI LILE SUALA LA NDG DAVID JAIRO. WATANZANIA TUMEONA NAMAN SERIKALI YETU ILIVYOSINZIA KIASI KWAMBA KILA KIONGOZI ANAKUJA NA MAAMUZI YAKE AMBAYO NAWEZA KUSEMA NI MAWAZO BIANFSI YA MTU HUSIKA KWA MASLAHI YAKE..
 
Ndugu yangu "senior expert member" sitaki kuamini kwamba tunachokijadili hapa hukijui na ndo maana unatoa mapendekezo ambayo kwa mtazamo wangu "hayawezi kusaidia". Nataka nikukumbushe tu kwamba hitaji la umeme sio hitaji dogo la kufanyia harambee kama mnavyofanya kwa ajili ya kicheni party, send-off, harusi au kuchangia mtoto aliyekosa ada ili aende shule. Tunaongelea hitaji la mamilioni, kama sio mabilioni ya pesa ili kuendesha miradi mikubwa ya kuzalisha umeme.
Mkuu gharama unazotoa sasa na unazoingia sasa kwa kukosa umeme ni maradufu kuongeza na kodi zako pia unazotoa.., ni ukweli usiopingika kwamba gharama ya kutumia generator moja moja ni zaidi ya gharama za kutumia generator za Tanesco za mafuta mazito.., ofcourse long term solution ni kuondokana na tegemezi la umeme wa mafuta na Tanzania tuna vyanzo vingi sana, hapa ndio serikalin inabidi ije na miradi ya kufaa (ambacho mpaka sasa hawajafanya..) hivyo basi tufanye nini ili tuweze kuwaforce wafanye kazi zao..., iwapo sisi wananchi tunaweza kuonyesha njia tutawaondolea kile ambacho kila siku wanasema hakiwezekani (kama wewe ulivyosema hapo juu) na hivyo basi watashindwa kuwadanganya wananchi kwa issue ya umeme ni ngumu...

Pia tunaweza kuwahamasisha vijijini watu wakatumia Bio-fuel ambako umeme hautafika leo wala kesho.

Kumbuka pia kwamba mafuta yanayohitajika si kwa kiasi cha kufanyia harambee kama unavyopendekeza. Hayo yote tisa, la mwisho, ambalo kimsingi ndiyo hoja yangu, nataka kukumbusha kwamba kama ni harambee wananchi tumefanya nyingi na za kutosha, na bado tunaendelea kufanya kwa ajili ya kutatua matatizo tuliyonayo kwa maendeleo ya nchi yetu-ikiwa ni pamoja na umeme.

Pengine utajiuliza tunafanya harambee hizo kwa njia gani! Jibu liko wazi: Ni kupitia kodi yako na yangu, na ya watanzania wote. Mimi binafsi nalipa zaidi ya Tsh 150, 000 kama kodi ya mapato kila mwezi-achilia mbali kodi kubwa ninayolipa kupitia kununua bidhaa na huduma itokanayo na VAT. Wewe pia unajua ni kiasi gani unalipa na wengine wote. Hata kama hulipi kodi ya mapato kwa maana ya kwamba wewe si mfanyabiashara wala mfanyakazi katika sekta rasmi (serikali na taasisi zake au mashirika ya umma na binafsi), bado unalipa kodi nyingi tu kupitia kila kitu unachonunua maana kuna kodi ya ongezeko la thamani (VAT) ambayo inajumuishwa katika garama ya kila bidhaa unayonunua au huduma unayolipia.
Mkuu hakuna mtu anayeibisha kwamba serikali inabidi ituangalie kwa pesa inazochukua, na maliasili zetu inazochezea, tena inabidi sio kutupa umeme tu, bali hata afya ya bure, elimu ya bure na uhakika wa kutuangalia tunapozeeka.., lakini swali ni kwamba je wanafanya hivyo...?, au tuendelee kukaa tu mpaka watakapoanza kufanya hivyo...??

Hivyo ni vema watanzania tukajua kwamba heal inazozitumia serikali ni hela zetu. Kwa lugha nyingine: Watanzania tunaji-mobilize kila siku kufanya harambee kupata hela ambazo ndizo akina Jairo na wengine wanazitumbua. Kwa msingi huo sioni mantiki ya hoja ya watanzania "kuji-mobilize kwa hali na mali" ili kondokana na matatizo tuliyo nayo ilihali tayari tumejimobilze vya kutosha. Itoshe watanzania tukaelewa kwamba wale tuliowapa dhamana ya kuzitumia hela hizo kutuletea maendeleo wameamua kuzitumia kwa namna wanayojua wao ili wajiletee maedeleo yao binafsi kwa jasho letu watanzania.

Ndio maana nikauliza upinzani (ambao kila siku unatuambia kwamba wenyewe wakiingia madarakani mambo yatakuwa mazuri) tena nikamuuliza na waziri kivuli wa hii wizara.., kwamba tunafanya nini?, kama ataweza kumobilize watu na kufanya kitu hata kama ni kidogo tu na kwa kitongoji au mtaa mmoja anaweza akasema unaona nilichofanya..?, tena bila kuwa na kodi za wananchi..., kwahiyo tukipewa serikali tutafanya makubwa zaidi..., na huu utakuwa mtaji mkubwa wa kuweza kuwangoa serikali kwa upinzani kuonyesha they can do better.

KWA MSINGI HUO, NAKUBALIANA NA HOJA YA WATANZANIA "KUJI-MOBILIZE" LAKINI KWA LENGO MOJA TU, NALO NI "KUIONDOA SERIKALI YA SISIEMU AMBAYO IMELEWA NA KUJISAHAU KIASI KWAMBA HATA SERIKALI YENYEWE INAPINGANA KIMAAMUZI. MFANO WA HIVI KARIBUNI NI LILE SUALA LA NDG DAVID JAIRO. WATANZANIA TUMEONA NAMAN SERIKALI YETU ILIVYOSINZIA KIASI KWAMBA KILA KIONGOZI ANAKUJA NA MAAMUZI YAKE AMBAYO NAWEZA KUSEMA NI MAWAZO BIANFSI YA MTU HUSIKA KWA MASLAHI YAKE..
Kwa hiyo mkuu waTanzania watajimobilize lini (ambayo ni kazi kubwa sababu wengi wetu wapo usingizini); na hata kama tutafanya maandamano mpaka miguu ikaingia tumboni kwa kutembea ni kweli tutaleta mabadiliko...????

Kumbuka serikali ina-spin hayo maandamano kwamba ni fujo na hata hao wapinzani wakiingia madarakani hali itakuwa mbaya zaidi ( na watu wanaamini..).., sasa je mkuu huoni kwamba ni vema kuwa na plan nyingine (njia nyingine ya kuonyesha watu kwamba wapinzani ndio wanaweza kuleta mabadiliko..?)

Ndio maana mkuu nikauliza mmoja wa wapinzani Ndg Mnyika kwamba... Tunajua Plan A ya Serikali imeshindikana..., na Plan B ya kuandama ikishindikana ni nini kifuate..?? ni nini Plan C...???....., na mkuu kumbuka (there is more than one way to skin a cat)... na wapinzani wanaweza kufanya mambo ambayo hayawezi yakawa misqouted na mtu yeyote..... Hivi upinzani ukianzisha mradi wa biogas huko kijijini na kuweza kuwaletea wanakijiji energy ya kutosha ya kupikia hicho kijiji kweli kitawasahau come 2015..... na gharama ya kutengeneza hii sio zaidi ya mifuko kadhaa ya cement.., pesa ambayo hata wakiamua wabunge wanne tu hawashindwi...
 
Back
Top Bottom