Mhashamu Methodius Kilaini ahamishiwa Jimbo la Bukoba

Uko sawa kabisa mkuu. Nafikiri wangeruhusiwa kuoa rate ya udhalilishaji wa vijana (watoto wadogo wa kiume) huenda ingekuwa ndogo. Mapadri wengi tu leo wana watoto wengi tuuu mitaani kitu kinachoonyesha unafiki wa hali ya juu kuhusu suala hili. Jamaa hawawezi kukaa hivyo hivyo bila tendo la ndoa kwa sababu wana maisha maisha mazuri ya duniani yakiambata na kula vizuri na hivyo kuufanya mwili uwe kwenye uhitaji mzuri wa kufanya tendo la ndoa. Si mpango wa MUNGU tangu mwanzo mwanaume aishi maisha yake yote bila kuoa. Mbaya zaidi huingilia sana hata ndoa za washirika wao kama vile marehemu askofu Butibubage wa Mwanza alivyovunja ndoa ya Pius Msekwa baada ya kuzaa naye mtoto (watoto). Mhhh! Mbaya kabisa hii. Mapokeo mabaya kabisa haya jamani.

Binafsi siwezi kusema ndoa ndiyo inayoondoa udhalilishaji au kukosa uaminifu katika maisha ya mtu. Ni uamuzi wa mtu mwenyewe kuwa mwaminifu au kutokuwa mwaminifu.

Mbona baadhi ya waliooa wana nyumba ndogo, wanafanya mapenzi hata wanawalawiti watoto wao wa kuzaa au kuwapa mimba wanafunzi? Kitu tusichokielewa kwenye Kanisa ni maisha ya kujitoa sadaka na mara nyingi tunayatafsiri kulingana na tunavyoona sisi wenyewe. Maisha ya useja yalikuwepo hata kabla ya Yesu. Kwani wakati huo Mungu hakuwepo? Kuna njia nyingi za kumtafuta/kumtumikia Mungu.

Ni kweli ndoa imewekwa na Mungu hasa kwa nia ya 'companionship' na 'reproduction'lakini siyo amri kuwa mtu lazima aoe. Maana hata katika kuoa kuna suala la 'choice'. Unaweza ukapenda kuoa na usimpate mwenza anayependezwa na wewe au tabia yako au unaweza kumpenda mwanamke na yeye asikupende.
Kwa hiyo, kama mtu fulani kwa imani yake anaamua kutooa ni uamuzi wake na mwingine akiamua kuoa ni uamuzi wake pia.

Kwani hujui wanandoa ambao wana watoto nje licha ya kwamba wameoa? Na wengine mambo yanajulikana baada ya mume kuaga dunia ndipo mke wa nyumba ndogo anapojitokeza kudai sehemu ya urithi. Kukosa uaminifu ni tatizo letu wote na siyo mapadre tu. Juzijuzi hapa magazeti yaliripoti kuwa mchungaji (ambaye ana mke) alifumaniwa na mke wa mtu. Hata wakati mwingine tunasikia shehe au imamu (ambao wana wake zaidi ya mmoja) kalawiti au kafumaniwa. Je, ni kwa sababu gani?
 
Wakuu naomba kuelimishwa,

Mhashamu Kilaini anaweza kuwekwa katika kundi gani kimitizimo kati ya manne hapo chini...

A)Radical, B)Liberal, C)Conservative, D)Extremist?

Je, vipi kuhusu Mwadhama Pengo?

Je kuondoshwa/kuhamishwa kwa Kilaini kunaweza kuwa na athari gani katika suala zima la mahusiano ya kijamii katika nchi yetu ukichukulia kuwa Dar es Salaam ni chungu cha mengi kama siyo yote Tanzania na hali ilivyo sasa?


omarilyas


Kwa Kilaini, naweza kusema hivi: Ni askofu ambaye ni very 'knowlegeable'. Amesoma kwa level ya PhD (hata Pengo) na kweli anauelewa mpana sana.
Huwa ana kipindi Radio Tumaini (kinaitwa Chimbachimba) kuhusu historia ya Kanisa. Kwa kweli Kilaini ni kisima cha historia. Watu wanaweza kudhani kusomea historia ya Kanisa basi mtu unakuwa akijua tu hiyo historia lakini ukweli ni kwamba ni historia yote - yaani unajifunza World History halafu unapiga Church History. Yaani, huyo askofu ni kichwa!

Whether ni A) Radical, B) Liberal, C) Conservative, D) Extremist? Sijui. Ila ni 'very informed as far as history is concerned'. Pengo simjui sana maana huwa anasikika mara chache chache.
 
Umenikumbusha huyu rafiki yangu Padre Privatus karugendo. Huu nilikaa nae vizuri sana kule kayanga, karagwe enzi zile . Yeye anatokea Ibwera, ndugu zake ni Primu, na Prudence wote ni waandishi.

nazipenda sana makala zake pamoja na zile za mdogo wake Prudence.

nasikia anaishi tabata siku hizi.

Ustaadh.......karibu Omurushaka aisee
 
Binafsi siwezi kusema ndoa ndiyo inayoondoa udhalilishaji au kukosa uaminifu katika maisha ya mtu. Ni uamuzi wa mtu mwenyewe kuwa mwaminifu au kutokuwa mwaminifu.

Mbona baadhi ya waliooa wana nyumba ndogo, wanafanya mapenzi hata wanawalawiti watoto wao wa kuzaa au kuwapa mimba wanafunzi? Kitu tusichokielewa kwenye Kanisa ni maisha ya kujitoa sadaka na mara nyingi tunayatafsiri kulingana na tunavyoona sisi wenyewe. Maisha ya useja yalikuwepo hata kabla ya Yesu. Kwani wakati huo Mungu hakuwepo? Kuna njia nyingi za kumtafuta/kumtumikia Mungu.

Ni kweli ndoa imewekwa na Mungu hasa kwa nia ya 'companionship' na 'reproduction'lakini siyo amri kuwa mtu lazima aoe. Maana hata katika kuoa kuna swala la 'choice'. Unaweza ukapenda kuoa na usimpate mwenza anayependezwa na wewe au tabia yako au unaweza kumpenda mwanamke na yeye asikupende.
Kwa hiyo, kama mtu fulani kwa imani yake anaamua kutooa ni uamuzi wake na mwingine akiamua kuoa ni uamuzi wake pia.

Kwani hujui wanandoa ambao wana watoto nje licha ya kwamba wameoa? Na wengine mambo yanajulikana baada ya mume kuaga dunia ndipo mke wa nyumba ndogo anapojitokeza kudai sehemu ya urithi. Kukosa uaminifu ni tatizo letu wote na siyo mapadre tu. Juzijuzi hapa magazeti yaliripoti kuwa mchungaji (ambaye ana mke) alifumaniwa na mke wa mtu. Hata wakati mwingine tunasikia shehe au imamu (ambao wana wake zaidi ya mmoja) kalawiti au kafumaniwa. Je, ni kwa sababu gani?


Mkuu kweli wewe ni kichwa (samahani kama hupendi nitumie hilo neno). Ila kweli nimependa unavyoyachambua mambo hapa kwenye hii thread. Umenifanya nikumbuke mbali sana...

Mkuu MAGOBE T, Keep it up..ni wengi tunafaidika na knowldge yako hapa.

Is it possible kwamba Timanywa akistaafu huyu mkulu Kilaini akakabidhiwa mikoba ya jimbo? au hata akapewa jimbo la Mayala mwanza? Anyway najua Niwemugizi ni contender wa kuwa Archibishop wa Mwanza.

In all, ni mtumishi wa Mungu..he can serve God and HIS people wherever he is sent. May peace of Lord be upon Him.

Masanja,
 
Mkuu kweli wewe ni kichwa (samahani kama hupendi nitumie hilo neno). Ila kweli nimependa unavyoyachambua mambo hapa kwenye hii thread. Umenifanya nikumbuke mbali sana...

Mkuu MAGOBE T, Keep it up..ni wengi tunafaidika na knowldge yako hapa.

Is it possible kwamba Timanywa akistaafu huyu mkulu Kilaini akakabidhiwa mikoba ya jimbo? au hata akapewa jimbo la Mayala mwanza? Anyway najua Niwemugizi ni contender wa kuwa Archibishop wa Mwanza.

In all, ni mtumishi wa Mungu..he can serve God and HIS people wherever he is sent. May peace of Lord be upon Him.

Masanja,

Of course, kila kitu kinawezekana! Ila inategemea na yeye pia (afya yake). Yeye binafsi anaweza kupendekeza achaguliwe mtu mwingine. Kitu muhimu kwa Kanisa ni kumtumikia Mungu na siyo kuwa askofu.
 
Magobe T,
Naomba unifafanulie hili la ukabila Maaskofu kuajili watu kutoka makabila yao na kuwaacha mapadre wachapakazi na tena vijana wasomi na kuajiri wazee kwa sababu wanatoka Kabila moja. Mfano ni marehemu Askofu Samba tulipokuwa Makoko Seminary tulizoea kumuita Pum**,alikuwa ni mchaga basi mapadre wote viongozi walikuwa ni wachaga hata ugawaji wa magari aliwapatia mapadre wachaga wakati mapadre wazalendo wa Musoma walikuwa wakitumia pikipiki halafu tena alikuwa na tabia ya kuendeshwa na masista wachaga hakutaka kuajiri dreva kutoka pale Musoma. Alikuwa AKIENDA PALE KWENYE SHIRIKA LA EMACULATE ANACHAGUA VI SISITER VIDOGO VIDOGO VICHAGA NA KUVIFANYA NDIVYO VILEZI NA WAFANYA USAFI WA HEKALU LAKE HUKU AKIWAOA NA KUWABADILISHA KAMA NGUO.



heee kumbe kuishi kwingi ni kuona na kusikia mengi ,

Hawa ndio wale Wanaokusamehe dhambi zako ??????
 
Padri Privatus Karugendo hakuwahi kuwa padri wa jimbo la Bukoba ambalo liko chini ya Askofu Nestory Timanywa tangu mwaka 1974. Yeye amekuwa padri wa jimbo la Rulenge lilikouwa chini ya Askofu Mwoleka na baadae akarithiwa na askofu Severin NiweMugizi ambaye hawakuiva na Karugendo.

Hata hivyo jimbo lake la Rulenge limegawanywa mwaka jana na kuzaa jimbo jipya la Kayanga lililoko wilaya ya Karagwe na Rulenge ya NiweMugizi ikaitwa Rulenge-Ngara.

Umenielimisha kupita kiasi ndugu yangu, nahisi wewe ni Mseminari ama? Anyway naomba unisaidie japo in a synopsis ilikuwaje Karugendo akaondoka kwenye kazi ya kichungaji?
 
Kwanini inakuwa issue sana kwa muhashamu Askofu Kilaini kuhamishiwa Bukoba, kwanini mkuu uulize kama ni demotion au promotion nani kakwambia ile ni kazi ya kuomba , au ina mshahara? Wana kondoom wa Dar na Bukoba wote ni sawa katika kanisa katoliki. Amepewa nafasi ya kupeleka utumishi wake jimbo la Bukoba basi hakuna jingine. Hongera Kilaini kwa Baba Mtakatifu kutambua kazi yako ya kichungaji.
 
Bora kuwa mwanachama wa CUF au Chadema!!! this is free msn organisation, leaded by mafia, old white people with no relgon subst. to hell
 
Bora kuwa mwanachama wa CUF au Chadema!!! this is free msn organisation, leaded by mafia, old white people with no relgon subst. to hell
Sidhani kama unachosema ni sawasawa. Heshimu dini za watu kama ya kwako inavyoheshimiwa.
 
Jamani ,mie nadhani ni uhamisho wa kawaida tu,nadhani Askofu wa huko karibu anastaafu kwahiyo anatayalishwa yeye Kilaini.
 
Na Mwandishi wetu
6th December 2009



Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Askofu Kilaini, ambaye amekuwa akimsaidia Askofu Mkuu Jimbo Kuu la Dar es Salaam kwa miaka mingi, ameruhusiwa kuendelea kushika Kiti cha Jimbo la Strumnizza.

Naomba tuelimishane hapa, Strumnizza ni kintu gani? Nani anashika mbadala wake kwa Pengo? Au ndio anaandaliwa kuwa "Pengo" akapate mazoezi Bukoba? Au alikuwa anamuwekea kauzibe Pengo kwa umaarufu Dar? Au...?

Leka
 
Kwa tunaojua kinachoendelea tunanyamaza kimya subirini mtajua karibuni ni nini kinaendelea huko!

HABARI YOYOTE IKIJULIKANA NA MTU MMOJA SI HABARI.

kama umeamua kukaa kimya hata hayo usimgeyaandika. kaa kimya huku ukijua kukaa kimya sio sifa ya MEMBERS
 
Sasa anajiandaa kuwa Askofu mkuu jimbo la Bukoba. Kwani askofu wa kule ana muda mfupi sana kustaafu.

Hongera sana KILAINI, Uaskofu ni wako tu kule Bukoba kuwa na Subra.
 
Umenielimisha kupita kiasi ndugu yangu, nahisi wewe ni Mseminari ama? Anyway naomba unisaidie japo in a synopsis ilikuwaje Karugendo akaondoka kwenye kazi ya kichungaji?

Nasikia tetesi kuwa huyo askofu Severini na padri Karugendo walikuwa na tabia ya kugombea wasichana tangu walipokuwa seminari Segerea, na mara zote Karugendo alikuwa anampiku mwenzie. Walipoenda kufanya kazi huko Ngara, mambo yakawa hayohayo. Severini alipoteuliwa kuwa askofu ndio ikawa 'kichaa kapewa rungu', akaamua kulipiza yote kwa kumtimua Karugendo kwenye upadri.
 
Maandiko ktk Biblia yanasema, "iweni tayari wakati unaofaa na wakati usiofaa; mahali panapofaa na mahali pasipofaa".

Tofauti na uongozi wa siasa, kazi ya uaskofu, ni kwa ajili ya uangalizi - Askofu maana yake ni mwangalizi wa kanisa. Kwa hiyo, kama Kilaini amehamishiwa mahali ambapo anaweza akatumika vyema kama mwangalizi, na kupitia uangalizi huo, mahali hapo pakainuliwa, atakuwa amefanya kazi kubwa sana kuliko kuendelea kuwepo Dar, mahali ambapo pamekomaa.

Kuinua sehemu ambayo bado ni changa, kunahitaji uzoefu wa kutosha na hekima na vipawa fulani vya kuweza kuhimili huduma ya eneo changa. Eneo changa wakati wote hukumbana na upinzani wa ukuaji wa injili. Hivyo basi, vipawa na hekima ya Kilaini, inahitajika zaidi mahali pa changa kuliko mahali palipoendelea zaidi.

Kanisa limefanya uamzi sahihi.
 
Sidhani kama unachosema ni sawasawa. Heshimu dini za watu kama ya kwako inavyoheshimiwa.



Sikuzote nitaheshimu dini za watu wote, ninachoongelea hapa ni, political organisation, leaded by few old white people. hii ni chama inayoongozwa kutumia jina la dini.
 
Sikuzote nitaheshimu dini za watu wote, ninachoongelea hapa ni, political organisation, leaded by few old white people. hii ni chama inayoongozwa kutumia jina la dini.


Hapo mkuu umechemka, kwamba RC ni chama ni zaidi ya kuchemka!!!. Uelewe kwamba kazi ya kanisa siyo tu kuwaelekeza waumini wao Kiroho, bali pia katika maisha yao ya kila siku, ikiwemo siasa. Unamaanisha nini unaposema leaded by few old white people???. Unaweza kuthibitisha kwamba RC ni chama!!. Biblia inasema katika Waraka wa tatu wa Yohana 1: 2 kwamba Wapenzi mfanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema kadri roho zenu zinavyofanikiwa. Kwa hiyo, ni lazima Roho ianze kufanikiwa, kisha ifuatiwe na mafanikio ya masuala mengine. Kwa hiyo, ukifahamu kwamba kazi ya kanisa siyo tu kuhusika na maisha ya Rohoni, hauwezi kuchangia mawazo kwamba kanisa linapochangia mawazo yake katika siasa basi limekuwa ni chama cha kisiasa.

Ningeshauri uingie kwenye ulingo wa dini ukutane na wazee kama MaxShimba na wengineo tukuelimishe, kisha urejee huku uanze kuchangia mada zinazoeleweka!!.

Usitoe Vague arguments; toa hoja zinazojieleza na kueleweka. Usipofahamu jambo fuatilia mjadala vizuri, siyo tu kuingia ktkt ili ionekane umeongeza idadi ya mada ulizochangia. Huko, ni kuchafua matumizi halisi ya chombo hiki, JF.
 
Nina jiuliza kitu kimoja kwa nini hakupewa u Archbishop wa Mwanza? kapelekwa Bukoba kama Askofu msaidizi je anamsaidia nani? Kwa heshima kubwa aliyokuwa nayo pale Dar halafu anahamishiwa Bukoba kama Askofu msaidizi naona ni kama Demotion vile.

Unataka kusema kuwa BUKOBA hakuna watu? Kwa taarifa yako huko ukristu ndipo ulipo kuliko Dar na huyu ni mtumishi wa kanisa sio siasa, hebo!!!
 
Back
Top Bottom