Mhadhiri Bashir Ally (UDSM) Atafutiwe Jimbo!

Mhadhiri Bashir Ally (UDSM) Atafutiwe Jimbo!

....

Ili Taifa liweze kunufaika na weledi wa Bwana Bashiru, naomba ashawishiwe kujiunga rasmi na siasa za majukwaani na atafutiwe jimbo ili kuanzia 2016 inshallah Taifa linufaike na vipawa vyake. ....
Kote huko tulikuwa pamoja ila kwa hili sikubaliani na wewe....yaani akiwa anafundisha taifa halinufaiki na vipawa vyake...au unataka kuniambia atakuwa mbunge na wakati huo akiwa mwalimu. Muache naye atengeneze watanzania wenye weledi kama yeye au hata kumzidi. Tumeona walimu/wahadhiri wengi waliojiunga na siasa wameshidwa kutumia vipawa vyao vizuri...hatutaki kumtumbukiza Bwana Bashiru huko.
 
bashiru.jpg

Bwana Bashiru Ally, Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Bwana Bashiru Ally ni miongoni mwa vijana waliofuzu makuzi ya kitaaluma na kijamii kutoka kwa watu wanaoheshimika na historia ya nchi hii; ile ambayo haikuhifadhiwa rasmi vitabuni. Enzi zetu tukiwa masomoni Bwana Bashir na Omar Ilyas ni miongoni mwa vijana waliopendwa na kujiweka karibu na Marehemu Prof. Haroub Othman (former VC-UDSM). Hali halisi inajidhirisha kuwa Bwana Bashir ndiye aliyefuzu kuyashika vema mafunzo na weledi wa Prof. Haroub Othman. Baada ya kuachana kitambo, miaka ya hivi karibuni nimekuwa nikimsikiliza, kumuona au kumsoma kupitia vyombo vya habari. Mara nyingine kwa bahati tumewahi kukutana kwenye mikutano.

Hivi majuzi Bwana Bashiru alishiriki mjadala wa DW juu ya miaka 15 ya mapambano dhidi ya ugaidi. Msimamo na utetezi wa mtazamo wake juu ya jinsi vita hii inavyopiganwa nakubaliana nao kwa asilimia 100—“Mbinu zinazotumika kupambana na ugaidi ni za kigaidi na hivyo zinazidisha ugaidi”

Bwana Bashiru ni mtu aliyejipambanua kuwa na msimamo usiyoyumba katika masuala ya Kitaifa na yale yote anayoyaamini baada ya kuyatafiti kwa kina. Si mtu wa papara na kuropoka. Hisia zake juu ya jambo lolote hazijathibitika kufungamana na imani au itikadi. Kiufupi ni mtu-huru, mwenye fikra chanya kwa mustakhabari wa jambo lolote analoshiriki kulitenda au kulipendekeza. Tuna uhaba wa watu wenye sifa hizi katika utungaji wa sera na kuisimamia serikali. Kumuacha aendelee kuongea na makaratasi au kuwasilisha hoja zake kwa Power Point mikutanoni na kisha akitoka ukumbini hakuna wa kuzitekeleza ni matumizi mabovu ya rasilimali watu wa nchi hii.

Ili Taifa liweze kunufaika na weledi wa Bwana Bashiru, naomba ashawishiwe kujiunga rasmi na siasa za majukwaani na atafutiwe jimbo ili kuanzia 2016 inshallah Taifa linufaike na vipawa vyake. Binafsi sijali atajiunga na CHADEMA, CUF, NCCR, TLP, n.k ilimradi tu asijiunge na ccm, mahali ambako mawazo mapya na utendaji ni dhambi. Akitaka Jimbo nitamchagulia Bukoba Vijijini na nitakuwa tayari kuanza kumpigia kampeni. Naamini maeneo yenye wapiga kura wengi kama Ibwera na Katoro hatutakuwa nahaja kabisa ya kupita kupiga kampeni.

Eid Mubraak!

Cc: FaizaFoxy, Ritz, omar Ilyas, njiwa, Nivea
Mimi nadhani aandike vitabu vya kitaaluma zaidi vitakavyosomwa na vijana hata akitoweka duniani kama Prof H Othaman. Lakini huku kwenye siasa kwa wanaomsikiliza BBC Swahili au DW akichangia mada mbali mbali hasa zinazohusu dunia mbili za Magharibi na Watu Mashariki ya kati huchelewi kuona biasses kwenye michango yake ikilalia upande mmoja. Unaweza ukashawishi watu zaidi kwa kuandika maandishi ambayo yanakuwa researched na kuwa-backed na facts zaidi kuliko hisia (emotions) za kiimani. Vinginevyo atabakia kuwa kama maprofesa wetu wengi bongo wanaosifika kwa title za u-profesa lakini hakuna vitabu maktaba walivyo andika, zaidi ni kuchangia articles kwenye majarida!

Wachangia hoja ambao utawasikiliza bila wewe kuhisi imani zao kuathiri uchambuzi (balanced analysis) wao ni kama Jenerali Ulimwengu, Zitto Kabwe na baadhi wengine...
 
Wewe mleta hoja yawezekana una matatizo, au kuna hisia fulani zimekusukuma kuandika uzi huu.
Mwanzoni sikuweza kung'amua unachokimaanisha ila nimekuja kukuelewa kwa hapa "agombee Bukoba Vijijini, hasa Ibwera au Katoro" why Ibwera na Katoro, na si kwingine? Je, ndiko anakozaliwa? Kwa mtu anayesoma tu bandiko lako hawezi kung'amua kitu gani au ni msukumo gani uliyo ndani ya moyo wako, isipokuwa kwa mtu anayeweza kuyasoma mazingira. Huyu jamaa unayempigia promo inasemekana ni mdini sana.
 
Hapo kwenye red: Unamaanisha Dr. Bashiru yupo kwenye kundi la Dr. Benson Bana; yule mpiga tarumbeta maarufu wa Lumumba? Kama yupo kwenye kundi hili naye hana maana zaidi ya wachumia tumbo.
Si kila Mhadhiri wa UDSM ni PHD holder....

Bashiru Ally sio Daktari wa Falsafa....Sio Dk. Kama unavyodhani...
 
Anafaa sana kuwa imamu wa msikiti!
Tukumbuke na ma-Imam pia wanafaa kuwa viongozi kama walivyo Mch. Msigwa (MB), Mch. G. Rwakatare (MB), Mch. Natse (MB), Mch. Mwanjelwa (MB) au alivyokuwa Dr.W.Slaa (retired-MB)
Wewe mleta hoja yawezekana una matatizo, au kuna hisia fulani zimekusukuma kuandika uzi huu.
...... Huyu jamaa unayempigia promo inasemekana ni mdini sana.
weka wazi matatizo yangu nipate kutafuta tiba. By the way "mdini" maana yake ni nini?
Definition ya mdini Hapa Tanzania ni Muislamu yoyote ambaye yupo katika wazifa wowote ule...
So sad, Poor us!
....Mdini mkubwa huyu hope anatumia kiarabu kufundisha huko na si Kiingereza .
Onyesheni udini wake badala ya kuandika kwa kutumia hisia zisizo na hata chembe ya ushahidi. Kwa nini kila mmoja anaandika tu bila ushahidi walau wa tukio moja linaloonyesha kuwa Mhadhiri Bashiru ni "mdini"? Kwa kuwa Kyenju, TUKUTUKU, Lunyungu na wenzenu mnaotoa tuhuma tu bila ushahidi, mie nikisema nyie ndio wadini wakubwa nitakuwa nakosea? Kwa nini mnakuwa na hisia kali juu ya majina kuliko uhalisia?
 
tukumbuke na ma-imam pia wanafaa kuwa viongozi kama walivyo mch. Msigwa (mb), mch. G. Rwakatare (mb), mch. Natse (mb), mch. Mwanjelwa (mb) au alivyokuwa dr.w.slaa (retired-mb)

weka wazi matatizo yangu nipate kutafuta tiba. By the way "mdini" maana yake ni nini?

So sad, poor us!

Onyesheni udini wake badala ya kuandika kwa kutumia hisia zisizo na hata chembe ya ushahidi. Kwa nini kila mmoja anaandika tu bila ushahidi walau wa tukio moja linaloonyesha kuwa mhadhiri bashiru ni "mdini"? Kwa kuwa kyenju, tukutuku, lunyungu na wenzenu mnatoa tuhuma tu bila ushahidi, mie nikisema nyie ndio wadini nitakuwa nakosea? Kwa nini mnakuwa na hisia kali na majina kuliko uhalisia?

mbona waliomsifia ujawaomba watoe ushahidi?acha ujinga mkuu,huyu mtu wako anafaa sana kuwa imamu wa msikiti,kwani kuwa imamu wa msikiti ni kitu kibaya?
 
Ni haki yake kugombea nafasi yoyote, lakini sio lazima wasomi wote waingia kwenye siasa. Mwl Bashiru anafanya kazi nzuri UDSM, anaweza kuleta mabadiliko hapo alipo bila kuingia kwenye siasa kwa kufundisha vijana wengine waje kuleta mabadiliko.
 
mbona waliomsifia ujawaomba watoe ushahidi?
Tunawasha taa ili kuondoa mwanga au tunaondoa giza kwa kuwasha taa?
acha ujinga mkuu...
....dalili ya kukosa hoja!
mkuu,huyu mtu wako anafaa sana kuwa imamu wa msikiti,kwani kuwa imamu wa msikiti ni kitu kibaya?
uliposoma hii post ulielewa?
..tukumbuke na ma-imam pia wanafaa kuwa viongozi kama walivyo mch. Msigwa (mb), mch. G. Rwakatare (mb), mch. Natse (mb), mch. Mwanjelwa (mb) au alivyokuwa dr.w.slaa (retired-mb)
 
Hivi kila mjenga hoja akikimbilia bungeni wasomi watazalishwa na nani?
 
Ingawa naheshimu maoni yako ila jua kuwa siyo kila msomi mzuri lazima awe mwanasiasa. Anaweza kujenga nchi akiwa kule kule chuoni.
 
Mh! Mbona hiyo PhD yake hadi kesho hajaimaliza?!?
Bashiru Ally amepata promotion mwezi July 2013 kutoka Assistant Lecturer na kuwa Lecturer...Ameitafuta muda mrefu Phd kwa sababu ya ukiritimba uliopo kwenye system ya Elimu Tanzania huku wenzie wakienda Ulaya hususani Ujerumani na Uingereza na kurudi na Phd ndani ya miaka mitatu. Ni Mwalimu mzuri sana
 
Si kila Mhadhiri wa UDSM ni PHD holder....

Bashiru Ally sio Daktari wa Falsafa....Sio Dk. Kama unavyodhani...
Hujapata updates Mkuu....Jamaa amepata PhD Mwezi uliopita sasa ni Dr. Pita noticeboard pale UDSM utakuta tangazo la Promotion. Hata hivyo jamaa kasotea sana hiyo PhD
 
yawezekana ni hazina kama ulivyoeleza, lakini kwa sura yake na maeneo anayotoka yawezekana ni kati ya wanaotakiwa kurudi kwao. tumwachie kanali Masawe aendelee na kuhakiki uhalali wa wanaosadikiwa kuingia nchini bila kufuata taratibu
bashiru.jpg

Bwana Bashiru Ally, Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Bwana Bashiru Ally ni miongoni mwa vijana waliofuzu makuzi ya kitaaluma na kijamii kutoka kwa watu wanaoheshimika na historia ya nchi hii; ile ambayo haikuhifadhiwa rasmi vitabuni. Enzi zetu tukiwa masomoni Bwana Bashir na Omar Ilyas ni miongoni mwa vijana waliopendwa na kujiweka karibu na Marehemu Prof. Haroub Othman (former VC-UDSM). Hali halisi inajidhirisha kuwa Bwana Bashir ndiye aliyefuzu kuyashika vema mafunzo na weledi wa Prof. Haroub Othman. Baada ya kuachana kitambo, miaka ya hivi karibuni nimekuwa nikimsikiliza, kumuona au kumsoma kupitia vyombo vya habari. Mara nyingine kwa bahati tumewahi kukutana kwenye mikutano.

Hivi majuzi Bwana Bashiru alishiriki mjadala wa DW juu ya miaka 15 ya mapambano dhidi ya ugaidi. Msimamo na utetezi wa mtazamo wake juu ya jinsi vita hii inavyopiganwa nakubaliana nao kwa asilimia 100—“Mbinu zinazotumika kupambana na ugaidi ni za kigaidi na hivyo zinazidisha ugaidi”

Bwana Bashiru ni mtu aliyejipambanua kuwa na msimamo usiyoyumba katika masuala ya Kitaifa na yale yote anayoyaamini baada ya kuyatafiti kwa kina. Si mtu wa papara na kuropoka. Hisia zake juu ya jambo lolote hazijathibitika kufungamana na imani au itikadi. Kiufupi ni mtu-huru, mwenye fikra chanya kwa mustakhabari wa jambo lolote analoshiriki kulitenda au kulipendekeza. Tuna uhaba wa watu wenye sifa hizi katika utungaji wa sera na kuisimamia serikali. Kumuacha aendelee kuongea na makaratasi au kuwasilisha hoja zake kwa Power Point mikutanoni na kisha akitoka ukumbini hakuna wa kuzitekeleza ni matumizi mabovu ya rasilimali watu wa nchi hii.

Ili Taifa liweze kunufaika na weledi wa Bwana Bashiru, naomba ashawishiwe kujiunga rasmi na siasa za majukwaani na atafutiwe jimbo ili kuanzia 2016 inshallah Taifa linufaike na vipawa vyake. Binafsi sijali atajiunga na CHADEMA, CUF, NCCR, TLP, n.k ilimradi tu asijiunge na ccm, mahali ambako mawazo mapya na utendaji ni dhambi. Akitaka Jimbo nitamchagulia Bukoba Vijijini na nitakuwa tayari kuanza kumpigia kampeni. Naamini maeneo yenye wapiga kura wengi kama Ibwera na Katoro hatutakuwa nahaja kabisa ya kupita kupiga kampeni.

Eid Mubraak!

Cc: FaizaFoxy, Ritz, omar Ilyas, njiwa, Nivea
 
And the only reason Bashir anaonekana kuwa bora ni kwa sababu anapewa airtime ya kutosha na vyombo vya habari mbali mbali huku akiwa anazungumzia mambo ambayo jamii ya watanzani iko addicted kwayo: siasa, chadema vs ccm, 2015 nani atakuwa nani, well, na ugaidi wa kitaifa na kimataifa.

Lakini kuna other unsung academic heros. Hawa hawapewi airtime zozote zile na kwa hiyo watanzania hawawajui kabisa na pengine ni wataalamu wa fani ambazo watanzania hawajui kuwa ni muhimu kuliko hata siasa.

Hivi kwa nini vyombo vya habari haviwezi siku moja kwenda kwenye vyuo vyetu vikawapa airtime baadhi ya maprofesa tofauti na Ayoub Rioba, Bensoni Bana, Mukandara na huyu wa leo, Bashiru Ali? Siasa bongo?

Si kweli kwamba wanavuma kwa sababu wanapewa AIR TIME, bali wanavuma kwa sababu kuna waliowaona kwamba ni mahiri na walipopata air time wakaitumia vizuri na kwa hiyo vyombo vya habari hupenda kuwatumia. lakini una hoja, kwa maana kwamba waandishi wa habari wenye kiburi cha utafiti, wanaweza kuwafuatilia wasomi na wachambuzi wengine wengi tu na kuwaibua. tatizo ni kwamba mwandishi au mwanahabari mwingine akitaka kupata maoni ya wachambuzi anawafuata hao hao. nadhani hawatutendei haki. binafsi nilishangaa wakati wa Kongamano la kujadili Amani Tanzania miaka 50 ijayo, lililoandaliwa na UDASA wiki mbili zilizopita, kwamba hawakutangaza mapema majina ya watoa mada. na kwa kweli ukiacha Ayoub Rioba, wale wawili; Prof. Bernadeta Killian na Bw. Onesmo (mwanasheria) sikuwahi kuwasikia katika anga za uchambuzi. lakini walidhihirisha kwamba ni wachambuzi mahiri sana na kwa hiyo tuwashukuru UDASA kwamba hawakutuletea watu wale wale, bali walitafuta "damu mpya".

Lakini kwa upande mwingine, hawa wanaovuma ni kwamba wanavuma kutokana na umahiri wao, na kwa kuwa vyombo vya habari pia vinapenda kuuza, wengi watapenda kusikia Bashiru kasema kitu gani kwenye ishu fulani. binafsi napenda sana kusikia uchambuzi wa Bashiru. jamaa namkubali sana tena sana tu.
 
nakubaliana na wewe tena inakuwa aibu unapokuta msomi mwenye hadhi ya Phd ama Prf. anakuwa weak - narrow sana anapokosolewa na kupewa changamoto na mtu kama Anna kilango, Pfo.Maji marefu, Serukamba etc wa aina hiyo. Hebu fikiria watu kama Dr.Msabaha walivyoaibika, au angalia Prof.Maghembe au Dr. Matayo Daudi Matayo, Prof.Tibaijuka, Prof.Msolla (Kilolo) ambao hata sijui wamekuwa majuha waliyosahau professionals zao - ila ni maoni yangu tu
Nchi hii watu wanasoma ili wawe wanasiasa? Mtu anakuwa doctor au prof anaacha kuhudumia wananchi kwa kufanya research ili kuweka mazingira mazuri ya utafit anakimbulia kazi ambazo hata Lusinde darasa la 7 anafanya na ofcpz hawana tofauti ktk output zao.

Why why why my country? Prof Anna Tiba, Mwandosya, Hemed Msolla et al. Yani uprof wenu mnaiexercise bungeni ambako hata non-elite anaweza perform?

Sasa kijana kama huyu anataka kuzamia huko nae, mweeee kazi iko. Nimekuwa mfuatiliaji wa siasa za nje kidogo, ukichunguza mabunge mengi wazee ndio wako huko wkt ss vijana ndio option yenye ulaji tunaiona. Ka
MzLendo si uanzishe kitu ili kusaidia watu wengi kwa kutumia ujuzi wako wa darasani?

Inakatisha tamaa wasomi kukimbilia dodoma kwa kweli na vyuoi wanabaki ma-TA na Ass Lecturers
 
Kwani nasi hatujui wakuu wa idara za kitaaluma na wahadhiri wanavyofanya kwa wanafunzi wakiislamu na mabaya kwa wakristo kusudi muonekane mnafaulu kumbe wapi majina yenu

Kilalo tuambie yafanywayo na wakuu wa idara kwa wanafunz wa kiislam na chuo waweza kitaja pia
 
Last edited by a moderator:
Si kweli kwamba wanavuma kwa sababu wanapewa AIR TIME, bali wanavuma kwa sababu kuna waliowaona kwamba ni mahiri na walipopata air time wakaitumia vizuri na kwa hiyo vyombo vya habari hupenda kuwatumia. lakini una hoja, kwa maana kwamba waandishi wa habari wenye kiburi cha utafiti, wanaweza kuwafuatilia wasomi na wachambuzi wengine wengi tu na kuwaibua. tatizo ni kwamba mwandishi au mwanahabari mwingine akitaka kupata maoni ya wachambuzi anawafuata hao hao. nadhani hawatutendei haki. binafsi nilishangaa wakati wa Kongamano la kujadili Amani Tanzania miaka 50 ijayo, lililoandaliwa na UDASA wiki mbili zilizopita, kwamba hawakutangaza mapema majina ya watoa mada. na kwa kweli ukiacha Ayoub Rioba, wale wawili; Prof. Bernadeta Killian na Bw. Onesmo (mwanasheria) sikuwahi kuwasikia katika anga za uchambuzi. lakini walidhihirisha kwamba ni wachambuzi mahiri sana na kwa hiyo tuwashukuru UDASA kwamba hawakutuletea watu wale wale, bali walitafuta "damu mpya".

Lakini kwa upande mwingine, hawa wanaovuma ni kwamba wanavuma kutokana na umahiri wao, na kwa kuwa vyombo vya habari pia vinapenda kuuza, wengi watapenda kusikia Bashiru kasema kitu gani kwenye ishu fulani. binafsi napenda sana kusikia uchambuzi wa Bashiru. jamaa namkubali sana tena sana tu.

binafsi si mhadhiri lakini huwa napigiwa simu na Idhaa ya Kiswahili ya DW,Pamoja na Redio Iran na huwa natoa uchambuzi,kwa mara ya Mwisho Ujio wa Obama,Nilipigiwa Sim na DW redio na nikatoa maoni yangu juu ya UJIO WA MJALUO OBAMA,nadhan pia hivi vyombo vya habar huwa vinaangalia jinsi unavyoweza kujieleza
 
Bashiru Ally amepata promotion mwezi July 2013 kutoka Assistant Lecturer na kuwa Lecturer...Ameitafuta muda mrefu Phd kwa sababu ya ukiritimba uliopo kwenye system ya Elimu Tanzania huku wenzie wakienda Ulaya hususani Ujerumani na Uingereza na kurudi na Phd ndani ya miaka mitatu. Ni Mwalimu mzuri sana

niliskia anaifanyia Ujeruman,since 2010,,,,hajamaliza
 
Back
Top Bottom