Mhadhiri Bashir Ally (UDSM) Atafutiwe Jimbo!

Mhadhiri Bashir Ally (UDSM) Atafutiwe Jimbo!

I knw the Guy in and out,we unambeza kwa kuangalia paradigm ya mijadala ya TV na redio una bahati mbaya sana.
Bashiru ukiachilia kukulia mikononi kwa pro.Haroub Othman (R.I.P) baada ya kufariki akaendelea kuwa chino ya Prof.Issa Shivji.
Bashiru Ana maandiko yake mengi tu,nakushauri ukayasome na ujitahidi kuelewa msimamo wake juu ya mustakabali wa taifa hili.
Binafsi ninamjua kama ni mjamaa,mzalendo,mtaifa na asiyeona haya kuusema ukweli bila kujali ni mchungu kwa kiasi gani.
Mwisho,aendelee kuwa mhadhiri ( taaluma) bungeni wataenda wengine maana kwa ninavoona awamu ijayo wataenda wazuri wengi sana watakaotuwakilisha kwa upana sana. yeye tukihutaji mawazo yake tutayapata vitabuni na kwa wachambuzi wengine anaozalisha pale mlimani.
 
bashiru.jpg

Bwana Bashiru Ally, Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Bwana Bashiru Ally ni miongoni mwa vijana waliofuzu makuzi ya kitaaluma na kijamii kutoka kwa watu wanaoheshimika na historia ya nchi hii; ile ambayo haikuhifadhiwa rasmi vitabuni. Enzi zetu tukiwa masomoni Bwana Bashir na Omar Ilyas ni miongoni mwa vijana waliopendwa na kujiweka karibu na Marehemu Prof. Haroub Othman (former VC-UDSM). Hali halisi inajidhirisha kuwa Bwana Bashir ndiye aliyefuzu kuyashika vema mafunzo na weledi wa Prof. Haroub Othman. Baada ya kuachana kitambo, miaka ya hivi karibuni nimekuwa nikimsikiliza, kumuona au kumsoma kupitia vyombo vya habari. Mara nyingine kwa bahati tumewahi kukutana kwenye mikutano.

Hivi majuzi Bwana Bashiru alishiriki mjadala wa DW juu ya miaka 15 ya mapambano dhidi ya ugaidi. Msimamo na utetezi wa mtazamo wake juu ya jinsi vita hii inavyopiganwa nakubaliana nao kwa asilimia 100—“Mbinu zinazotumika kupambana na ugaidi ni za kigaidi na hivyo zinazidisha ugaidi”

Bwana Bashiru ni mtu aliyejipambanua kuwa na msimamo usiyoyumba katika masuala ya Kitaifa na yale yote anayoyaamini baada ya kuyatafiti kwa kina. Si mtu wa papara na kuropoka. Hisia zake juu ya jambo lolote hazijathibitika kufungamana na imani au itikadi. Kiufupi ni mtu-huru, mwenye fikra chanya kwa mustakhabari wa jambo lolote analoshiriki kulitenda au kulipendekeza. Tuna uhaba wa watu wenye sifa hizi katika utungaji wa sera na kuisimamia serikali. Kumuacha aendelee kuongea na makaratasi au kuwasilisha hoja zake kwa Power Point mikutanoni na kisha akitoka ukumbini hakuna wa kuzitekeleza ni matumizi mabovu ya rasilimali watu wa nchi hii.

Ili Taifa liweze kunufaika na weledi wa Bwana Bashiru, naomba ashawishiwe kujiunga rasmi na siasa za majukwaani na atafutiwe jimbo ili kuanzia 2016 inshallah Taifa linufaike na vipawa vyake. Binafsi sijali atajiunga na CHADEMA, CUF, NCCR, TLP, n.k ilimradi tu asijiunge na ccm, mahali ambako mawazo mapya na utendaji ni dhambi. Akitaka Jimbo nitamchagulia Bukoba Vijijini na nitakuwa tayari kuanza kumpigia kampeni. Naamini maeneo yenye wapiga kura wengi kama Ibwera na Katoro hatutakuwa nahaja kabisa ya kupita kupiga kampeni.

Eid Mubraak!

Cc: FaizaFoxy, Ritz, omar Ilyas, njiwa, Nivea

nilikuwa naangalia kipima joto leo cha itv nna imani kuwa huyu ni yule nlimuona kule akitoa hoja zake(i stand to be corrected)..turudi kwenye mada...binafsi niko pamoja na mleta mada kuwa watu wenye ufahamu mkubwa kama hawa ndio wanatakiwa waingie katika nyadhifa za uongozi kwa sababu wataweza kutoa maamuzi sahihi kutokana na ujuzi wao...nifupishe tu na niseme kuwa tunahitaji wahandisi(engineers),madaktari(medical doctors) na wataalamu wengine katika nyadhifa muhimu kama bunge. Ni miongoni mwa makosa wataalamu wengi wanafanya kwa kuacha siasa then wanakaa kulaumu viongozi mara vilaza mara vihiyo wanasahau kuwa wao ndo walikosea kwa kutotafuta uongozi WITO WANGU:let us STOP making STUPID people famous
 
Nchi hii watu wanasoma ili wawe wanasiasa? ...why why why my country? Prof Anna Tiba, Mwandosya, Hemed Msolla et al. Yani uprof wenu mnaiexercise bungeni ambako hata non-elite anaweza perform?
.....nifupishe tu na niseme kuwa tunahitaji wahandisi(engineers),madaktari(medical doctors) na wataalamu wengine katika nyadhifa muhimu kama bunge. Ni miongoni mwa makosa wataalamu wengi wanafanya kwa kuacha siasa then wanakaa kulaumu viongozi mara vilaza mara vihiyo wanasahau kuwa wao ndo walikosea kwa kutotafuta uongozi WITO WANGU:let us STOP making STUPID people famous
644232_622936594403854_1038289225_n.jpg



 
Ni kati ya wasomi makini sana. Hata mimi nimekuwa nikimfuatilia kwa muda mrefu. Ingawa simshauri kujiunga na vyama vya upinzani maana huko nilishapoteza imani nao, ni kama kuna wachumia tumbo na wala sio wanamageuzi wa kweli kama tunavyofikiria. Simshauri kupoteza Heshima yake amabayo ametumia muda mrefu kuijenga. Anaweza kujiunga na CCM bado akawa chachu ya mabadiliko ndani ya hicho chama au akaendelea na kazi yake akiwa mtaalamu anayetoa ushauri bila kuegemea upande wowote.
 
I knew it'd turn out this way! There is nothing nowadays that could be discussed in here regarding Tanzanian society without this :'udini' thing, especially when a muslim or muslims are part of the subject. The stone age still exists.

Wewe hujaona hao aliwa-cc....it tells all
 
Anatoka Bukoba. Unashangaa nn?

wewe ni mkabila sana ndugu yangu na ntakupa mifano mingine ili ukatafiti tujue na hao watu kama wanatokea huko Bkb

jamaa anaitwa Afande Mkisi pale Jiteute twambie anakotoka

jamaa anaitwa Prof.Maghembe waziri wako twambie anatoka Bkb upande upi?

jamaa anitwa Mwigulu Nchemba naye utwambie anatokea Bkb sehemu gani?

ukimaliza hao list ni kubwa tutaomba utusaidie na wengine
 
Nakupa changamoto moja. Nchi ya Tanzania mpaka sasa imeongozwa na maraisi wanne (4): wawili wakristo na wawili waislamu. Hebu kuwa mkweli na utuambie ni viongozi gani walioonesha uhodari wa kuongoza na kusimamia maslahi ya Taifa, badala ya kuporomosha matusi hovyo humu jamvini! Hata kwa huyo mteja wako unayemnadi hamna kitu hapo. Huo ni umaarufu wa kuonekana kwenye runinga tu ambao hata "LULU" wa marehemu Kanumba anao!

Katika hii dunia ukiona mtu anajali usafi wa nguo alizovaa badala ya mwili wake-huyo mtu ni hatari sana manake akili zake haziko sawa!

kwann mkiona majina ya kiislam roho zenu zinawajaa chuki, husda, fitna na upumbavu? Mnadhani mnayofundishwa huko makanisani na akina slaa hatuyajui? Hii nchi siyo ya kanisa wala ya wakristo peke yao wala sio ya waislam peke yao. Ndio chuki mliyonayo kwa kikwete kisa dini yake. Mtakufa km mimbwa koko na chadema yenu ya kiliberali
 
Dah!! Hatuishi vituko watanzania. Ngozi ya fisi haijifichi hata akijichanganya na kondoo.
 
haha..mmeshafikia hapo?Si wa kile kitengo cha wapiga matarumbeta wa kukodi toka chuo kilichoipa nchi hasara UDSM.?Haha...napita tuu.

Hapo kwenye red: Unamaanisha Dr. Bashiru yupo kwenye kundi la Dr. Benson Bana; yule mpiga tarumbeta maarufu wa Lumumba? Kama yupo kwenye kundi hili naye hana maana zaidi ya wachumia tumbo.
 
Wanazuoni wabaki kwenye taaluma zao ili wakosoe mamlaka zilizoko madarakani. Wakiingia kwenye siasa wengi wao hugeuka kuwa vipofu baada ya kulambishwa peremende zipatikanazo huko kwenye siasa.
 
And the only reason Bashir anaonekana kuwa bora ni kwa sababu anapewa airtime ya kutosha na vyombo vya habari mbali mbali huku akiwa anazungumzia mambo ambayo jamii ya watanzani iko addicted kwayo: siasa, chadema vs ccm, 2015 nani atakuwa nani, well, na ugaidi wa kitaifa na kimataifa.

Lakini kuna other unsung academic heros. Hawa hawapewi airtime zozote zile na kwa hiyo watanzania hawawajui kabisa na pengine ni wataalamu wa fani ambazo watanzania hawajui kuwa ni muhimu kuliko hata siasa.

Hivi kwa nini vyombo vya habari haviwezi siku moja kwenda kwenye vyuo vyetu vikawapa airtime baadhi ya maprofesa tofauti na Ayoub Rioba, Bensoni Bana, Mukandara na huyu wa leo, Bashiru Ali? Siasa bongo?
 
bashiru.jpg

Bwana Bashiru Ally, Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Bwana Bashiru Ally ni miongoni mwa vijana waliofuzu makuzi ya kitaaluma na kijamii kutoka kwa watu wanaoheshimika na historia ya nchi hii; ile ambayo haikuhifadhiwa rasmi vitabuni. Enzi zetu tukiwa masomoni Bwana Bashir na Omar Ilyas ni miongoni mwa vijana waliopendwa na kujiweka karibu na Marehemu Prof. Haroub Othman (former VC-UDSM). Hali halisi inajidhirisha kuwa Bwana Bashir ndiye aliyefuzu kuyashika vema mafunzo na weledi wa Prof. Haroub Othman. Baada ya kuachana kitambo, miaka ya hivi karibuni nimekuwa nikimsikiliza, kumuona au kumsoma kupitia vyombo vya habari. Mara nyingine kwa bahati tumewahi kukutana kwenye mikutano.

Hivi majuzi Bwana Bashiru alishiriki mjadala wa DW juu ya miaka 15 ya mapambano dhidi ya ugaidi. Msimamo na utetezi wa mtazamo wake juu ya jinsi vita hii inavyopiganwa nakubaliana nao kwa asilimia 100—“Mbinu zinazotumika kupambana na ugaidi ni za kigaidi na hivyo zinazidisha ugaidi”

Bwana Bashiru ni mtu aliyejipambanua kuwa na msimamo usiyoyumba katika masuala ya Kitaifa na yale yote anayoyaamini baada ya kuyatafiti kwa kina. Si mtu wa papara na kuropoka. Hisia zake juu ya jambo lolote hazijathibitika kufungamana na imani au itikadi. Kiufupi ni mtu-huru, mwenye fikra chanya kwa mustakhabari wa jambo lolote analoshiriki kulitenda au kulipendekeza. Tuna uhaba wa watu wenye sifa hizi katika utungaji wa sera na kuisimamia serikali. Kumuacha aendelee kuongea na makaratasi au kuwasilisha hoja zake kwa Power Point mikutanoni na kisha akitoka ukumbini hakuna wa kuzitekeleza ni matumizi mabovu ya rasilimali watu wa nchi hii.

Ili Taifa liweze kunufaika na weledi wa Bwana Bashiru, naomba ashawishiwe kujiunga rasmi na siasa za majukwaani na atafutiwe jimbo ili kuanzia 2016 inshallah Taifa linufaike na vipawa vyake. Binafsi sijali atajiunga na CHADEMA, CUF, NCCR, TLP, n.k ilimradi tu asijiunge na ccm, mahali ambako mawazo mapya na utendaji ni dhambi. Akitaka Jimbo nitamchagulia Bukoba Vijijini na nitakuwa tayari kuanza kumpigia kampeni. Naamini maeneo yenye wapiga kura wengi kama Ibwera na Katoro hatutakuwa nahaja kabisa ya kupita kupiga kampeni.

Eid Mubraak!

Cc: FaizaFoxy, Ritz, omar Ilyas, njiwa, Nivea

I do not call this guy msomi nadhani he is a looser anaye amini kwamba CIA walilipua Kanisa Arusha wakitaka kutuchanganya ili wachukue gas nk na huku anawalinda wa China .Huvu huyu ana chuki hivi huko UDSM anafundisha kutumia lugha gani ? Mdini mkubwa huyu hope anatumia kiarabu kufundisha huko na si Kiingereza .
 
bashiru.jpg

Bwana Bashiru Ally, Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Bwana Bashiru Ally ni miongoni mwa vijana waliofuzu makuzi ya kitaaluma na kijamii kutoka kwa watu wanaoheshimika na historia ya nchi hii; ile ambayo haikuhifadhiwa rasmi vitabuni. Enzi zetu tukiwa masomoni Bwana Bashir na Omar Ilyas ni miongoni mwa vijana waliopendwa na kujiweka karibu na Marehemu Prof. Haroub Othman (former VC-UDSM). Hali halisi inajidhirisha kuwa Bwana Bashir ndiye aliyefuzu kuyashika vema mafunzo na weledi wa Prof. Haroub Othman. Baada ya kuachana kitambo, miaka ya hivi karibuni nimekuwa nikimsikiliza, kumuona au kumsoma kupitia vyombo vya habari. Mara nyingine kwa bahati tumewahi kukutana kwenye mikutano.

Hivi majuzi Bwana Bashiru alishiriki mjadala wa DW juu ya miaka 15 ya mapambano dhidi ya ugaidi. Msimamo na utetezi wa mtazamo wake juu ya jinsi vita hii inavyopiganwa nakubaliana nao kwa asilimia 100—“Mbinu zinazotumika kupambana na ugaidi ni za kigaidi na hivyo zinazidisha ugaidi”

Bwana Bashiru ni mtu aliyejipambanua kuwa na msimamo usiyoyumba katika masuala ya Kitaifa na yale yote anayoyaamini baada ya kuyatafiti kwa kina. Si mtu wa papara na kuropoka. Hisia zake juu ya jambo lolote hazijathibitika kufungamana na imani au itikadi. Kiufupi ni mtu-huru, mwenye fikra chanya kwa mustakhabari wa jambo lolote analoshiriki kulitenda au kulipendekeza. Tuna uhaba wa watu wenye sifa hizi katika utungaji wa sera na kuisimamia serikali. Kumuacha aendelee kuongea na makaratasi au kuwasilisha hoja zake kwa Power Point mikutanoni na kisha akitoka ukumbini hakuna wa kuzitekeleza ni matumizi mabovu ya rasilimali watu wa nchi hii.

Ili Taifa liweze kunufaika na weledi wa Bwana Bashiru, naomba ashawishiwe kujiunga rasmi na siasa za majukwaani na atafutiwe jimbo ili kuanzia 2016 inshallah Taifa linufaike na vipawa vyake. Binafsi sijali atajiunga na CHADEMA, CUF, NCCR, TLP, n.k ilimradi tu asijiunge na ccm, mahali ambako mawazo mapya na utendaji ni dhambi. Akitaka Jimbo nitamchagulia Bukoba Vijijini na nitakuwa tayari kuanza kumpigia kampeni. Naamini maeneo yenye wapiga kura wengi kama Ibwera na Katoro hatutakuwa nahaja kabisa ya kupita kupiga kampeni.

Eid Mubraak!

Cc: FaizaFoxy, Ritz, omar Ilyas, njiwa, Nivea
huyu nshomile mwenzangu anaweza kabisa, akija bukoba vijijini kura za itahwa, maruku,katoma zote zake
 
Back
Top Bottom