Mh.Spika Mimi naunga hoja Mkono 100%, Lakini kule..

Mh.Spika Mimi naunga hoja Mkono 100%, Lakini kule..

JACADUOGO2.

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2010
Posts
930
Reaction score
220
Nashangaa sana wabunge karibia wote wa CCM wanaposimama kuongelea suala la kuunga au kutokuunga mkono hoja utasikia wakisema "kabla sijaongea naunga mkono hoja asilimia mia" na ukiwasikia wakiongea wanalalamika kweli kweli kuhusu suala husika.

Je, wanajali maslahi ya wananchi au maslahi ya CCM?
Hawa jamaa hawaeleweki kabisa Mbunge anasimama na kusifu Serikali kuwa ni sikivu,inajali watu wake,inamipango madhubuti kuiniua uchumi wa watu wake na kadharika ikiwa sambamba na kuunga mkono hoja zitolewazo na mawaziri katika kuwasilisha bajeti.

Wanapokuja kunichosha ni kuwa baada ya kutoa sifa zote hizo,Mbunge husika anaanza kulalamika mara ooh serikali imetutelekeza wakazi wa jimbo la ..... mara ooh serikali haikamilishi miradi kwa wakati muafaka na kero nyingi nyingi.

Ni bora mnapopata nafasi kuchangia muwe straight to point sio kuzunguka zunguka.

Spika: Sasa ni zamu ya mheshimiwa Udhaifu Sitaki

Udhaifu Sitaki: Asante Spika kwa kuniona

Kwanza nianze kwa kusema naunga mkono hoja hii ya bajeti kwa asilimia 500

1.Sikubaliani na kuongeza kodi katika vinywaji(soda na pombe) na sigara. kodi hizi zipunguzwe serikali
haiwezi kutegemea vyanzo hivi ya mapato,badala yake tutazame vyanzo vingine vya mapato

2.Pili,sikubaliani na suala la sehemu kubwa ya bajeti yetu kwenda kwenye matumizi badala ya miradi ya maendeleo
Mheshimiwa spika,asilimia 30 iliyotengwa kwa miradi ya maendeleo ni ndogo sana ukilinganisha na mahitaji ya wananchi katika nyanja mbalimbali.Tupunguze matumizi,katika gharama za uendeshaji wa serikali

Mengi yameongelewa hapa ila mimi nimeona nichangie katika haya mawili ambayo nadhani tunahitaji kuyafanyia marekebisho, nimalizie tena kwa kusema Naunga mkono hoja asilimia 500! Asante


Mimi: Hivi staili kama hizi za kuunga mkono hoja hazimaanishi huenda kuna nguvu za kurogwa hapa ?

Sijajua sasa wanawakilisha Serikali au Wananchi,

Utasikia naipongeza sana serikali yangu ya CCM kwa kuturetea maendeleo katika uongozi wake, mbele anaanza kuleta vilio kibao kutoka kwa wananchi wake, kwamba kuna ukosefu wa Umeme, Maji, Dawa, Barabara na huduma nyingi mbovu kwanini Serikali haiwasaidii Wananchi?,

Sasa unajiuliza Serikali aliyo isifia ni ipi? na anyoililia ni ipi.

CCM oyee
 
Tusiwashangae,
hawajui maana ya 100%
hawajui kua wanaweza kuunga mkono hoja kwa 51% hizo 49 ndio zikawa kero zao. Maana anatoa hoja zaidi 3 kupinga hoja iliyotolewa sasa asilimia 100 itakamilikaje na mapungufu yake.
 
Inaonesha hutazami Bunge, ni wabunge wengi tu wa CCM huwa wanasema siungi hoja mkono. Usitudanganye, jana tuu kwa uchache, Kilango, Mkono, na wengine siwajui majina yao wamesema hawaungi mkono hoja mpaka wapate ufafanuzi wa kina. Hapo umenoa.
 
nadhani wangali na ile dhana ya kidumu ccm kwani utaanzaje kuunga mkono kitu halafu ukikosoe ???
 
Inasikitisha kwamba pamoja na ukweli ulio wazi kuwa haifai kuruhusu ununuzi wa mali/mitambo/vitu vilivyotumika, inaonekana hoja ya kutunga sheria mpya ya manunuzi ya umma itaungwa mkono kwa satili ya kujibu swali la spika "wanaounga mkono hoja waseme ndiyo". Halafu wabunge wetu watajibu "Ndiyoooooooo". Mimi ni kati ya wale walio kinyume hadi kifungu cha ununuzi wa mali chakavu kitakapoondolewa, yaani nitasema "Siyooooo".

Wewe unajibu gani?
 
Siyoo siyoo siyoo siiiiiiiiyooooooooooooo*100
 
Inasikitisha kwamba pamoja na ukweli ulio wazi kuwa haifai kuruhusu ununuzi wa mali/mitambo/vitu vilivyotumika, inaonekana hoja ya kutunga sheria mpya ya manunuzi ya umma itaungwa mkono kwa satili ya kujibu swali la spika "wanaounga mkono hoja waseme ndiyo". Halafu wabunge wetu watajibu "Ndiyoooooooo". Mimi ni kati ya wale walio kinyume hadi kifungu cha ununuzi wa mali chakavu kitakapoondolewa, yaani nitasema "Siyooooo".

Wewe unajibu gani?
Siyoo lakini ujue hayo masaburi ya magamba wamejipanga kuiba tuu!!! tulipochagua fisi mwitu tukaacha binadamu tuliliwa toka wakati ule.
 
Tatizo kuna mkakati wa kupitisha hili ili litoe nafasi ya kufanya ufisadi mkubwa kuliko tunavyofikiri, tukishakubali kununua vitu vilivyotumika ni ngumu mno kwenye manunuzi ya Umma kupambanua kitu kilichotumika kimetumika muda gani na kitadumu tena kwak muda gani. Fikiria kwa akili nyepesi tu kwamba sheria iliyopo inakataza kununua vitu vilivyotumika, lakini wanachakachua na kununua vitu vilivyotumika na havikai muda vinakufa. Je, kama wataruhusu vitu "used"... si watanunua maiti kabisa?
 
siyo tena kwa herufi kubwa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mheshimiwa Spika
Mimi nitaunga mkono muswada huo kama, kutakuwa na vipengele ambavyo vinatoa sharti la kununuliwa kwa magari chakavu ya rais, mawaziri na Ma RC. hilo litakuwa ni njia nzuri kabisa ya kuonyesha kuwa serikali yatu ni "sikivu"

kadhalika nitaunga mkono muswada huu endapo kutakuwa na kipengele ambacho kinaeleza kwamba; kwakuwa rais wetu anastahili kusafiri kwa hadhi na heshima tumnunulie ndege iliyotumika kule DRC tena ina ya Antonov kwa sababu tunaona kuwa tukitumia pesa nyingi kununua mpya kama ile ya Gulfstream ni mzingo mkubwa wa taifa kama letu

vilevile mshehimiwa spika, tutaunga mkono muswada huu kama, kutakuwa na kipengele ambacho kitaeleza kuwa serikali yatu inaongozwa na watu wenye uwezo mdogo sana kumbukumbu kiasi wamesahau suala la rada

juzi juzi tume ambiwa kuwa wakoloni wetu wameturudishia chenji za rada baada ya kubainika kuwa kuna mchezo mchafu ulifanyika katika ununuzi wake, hiyo sio hoja yangu lakini nakumbuka kipindi tunanunua hiyo rada WB na wengine kadhaa walituambia kuwa tunaweza kununua rada ya bei nafuu , viongozi wentu ndani ya serikali walisema haiwezekani, tunahitaji ya gharama kubwa. sasa leo kwa nini kutunga sheria ya kununua vitu chakavu kwa maelezo kwamba vina gharama kubwa!

vinginevyo, Mheshimiwa spika mimimi, Ashakumu si matusi. kuendeleza na mjadala wa kutunga sheria ya kununua vitu vya mitumba ni upuuzi na ujuha mkubwa, watu wenye akili wanatushangaa kama kweli tunafikiri sasawa hivi kweli tunatunga sheria ya kununua mitumba, tuna akili kweli sisi.

baada ya kusema hayo nasema sitaunga mkono muswada huu hadi hapo mapendekezo niliyotoa yataingizwa kwenye muswada huu
 
Mheshimiwa Spika
Mimi nitaunga mkono muswada huo kama, kutakuwa na vipengele ambavyup vinatoa sharti la kununuliwa kwa magari chakavu ya rais, mawaziri na Ma RC. hilo litakuwa ni njia nzuri kabis aya kuonyesha kuwa serikali yatu ina "usikivu"

kadhalika nitaunga mkono muswada huu endapo kutakuw ana kipengele ambacho kinaeleza kuw akw akuw arais wetu anastahili kusafiri kwa hadhi na heshima tumnunulie ndege iliyotumika kule DRC tena ina ya Antonov kwa sababu tunaona kuwa tukitumia pesa nyingi kununua mpya kama ile ya Gulfstream ni mzingo mkubwa wa taifa kama letu

vilevile mshehimiwa spika, tutaunga mkono muswada huu kama, kutakuwa na kipengele ambacho kitaeleza kuwa serikali yatu inaongozwa na watu wenye uwezo mdogosa na kumbukumbu kiasi wamesahau suala la rada

juzi juzi tume ambiwa kuwa wakoloni wetu wameturudishia chenji za rada baada ya kubainika kuwa kuna mchezo mchafu ulifanyika katika ununuzi wake, hiyo sio hoja yangu lakini nakumbuka kipindi tunanunua hiyo rada WB na wengine kadhaa walituambia kuwa tunaweza kununua rada ya bei nafuu , viongozi wentu ndani ya serikali walisema haiwezekani, tunahitaji ya gharama kubwa. sasa leo kwa nini kutunga sheria ya kununua vitu chakavu kw amaelezo kwmaba vina gharama kubwa!

vinginevyp, mhehsimiwa spika mimimi, Shkakumu si matusi. kuendeleza na mjadala w akutunga sheria ya kununua vitu vya mitumba ni upuunzi na ujuha mkubwa, watu wenye akili wanatushangaa kama kweli tunafikiri sasawa hivi kweli tunatunga sheriaya kununua mitumba, tuna akili kweli sisi.

baada ya kusema hayo nasema sitaunga mkono muswada huu hadi hapo mapebndekezo niliyotoa yataingizwa kwenye muswada huu


Ndugu, inaonekana hoja zako ni za msingi. Fikisha ujumbe kwa wengine!
 
Inasikitisha kwamba pamoja na ukweli ulio wazi kuwa haifai kuruhusu ununuzi wa mali/mitambo/vitu vilivyotumika, inaonekana hoja ya kutunga sheria mpya ya manunuzi ya umma itaungwa mkono kwa satili ya kujibu swali la spika "wanaounga mkono hoja waseme ndiyo". Halafu wabunge wetu watajibu "Ndiyoooooooo". Mimi ni kati ya wale walio kinyume hadi kifungu cha ununuzi wa mali chakavu kitakapoondolewa, yaani nitasema "Siyooooo".

Wewe unajibu gani?
mimi sitaunga mkono hoja. kuna Mwanajamii mmoja aliwahi kuandika kuwa wabunge wengi kutoka chama cha wamagamba ni Dk wa kuunga mkono hoja,na sasa wameongeza mmoja.Wataunga mkono hoja.

Nami nina swali.Wabunge wa CCM wanawawakilisha wananchi waliowachagua bungeni,wanaiwakilisha serikali au maslahi yao binafsi?
 
(NDIO)..... kama hatuna uwezo wa kununua brand new.... mkono wa pili mbona safi tu
 
Na mbaya zaidi mwenye mamlaka ya kuamua hii imetumika au la ni mtu mmoja tu, so itategemea na akili ya huyo mhusika kuamua kama hii ni used, recondition au .............. aisee haka kanchi katamu sana ukikapatia, mweeeeeee! Eneo lingine la watu kula dili kiulainiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!
 
Naiunga mkono sheria hii. Utekelezaji ndo issue!
 
Back
Top Bottom