Mh. Rais mbona umetuachia njiani ???

Mh. Rais mbona umetuachia njiani ???

Rais alikuwa sawa.

Na pia waziri mkuu yuko sawa.

Tatizo lilipo biashara ya mazao imeingiliwa na walanguzi,

yaani wanalangua mazao yote na kuyahodhi na kisha kuyapeleka kenya,
huku wanaacha unga bei juu,mchele bei juu,
ilikuwa haijawahi kutokea tangu uhuru hii nchi wakati wa mavuno eti unga unakuwa na bei juu kuliko mchele,
kumbe walanguzi mahindi yote wanapeleka kenya,

mchele msimu wa mavuno unashuka hadi 1000 kwa kilo leo kabla ya zuio mchele unagota 2000.

Kumbe mchele wote unavuka kwenda Rwanda,congo etc.

Wanaofaidi ni walanguzi na sio wakulima ,
zuio liendelee
 
Tabia hii ya serikali ya kumfanya mkulima kama chombo cha serikali cha kudhibiti mfumuko wa bei ndicho kinachofanya kilimo Tanzania kimekuwa chukizo. Tunalima ili kupata chakula chetu na si kilimo biashara. Tangazo hilo limenikumbusha sera ya Lowasa ya kuruhusu wakulima kuuza mazao yao popote penye tija. Hebu fikiri ulime mwenyewe kwa gharama zako na shamba serikali ichukue kodi halafu ukiivisha inakuwa mali ya serikali ni kweli?!! .Ngoja niishie hapo nina uchungu mkali sana....

Pole mkuu yan kwa ili hawa viongozi wa serikali wametukwamisha sana hawa watu hawa ngoja tuendelee kutunza hasira zetu
 
Wakulima naomba munielweee...
Nilichosema Ni muuze popote kwa kufuata taratibu zilizowekwa Na serikali yangu.

Narudia tena ambae hataki kuuza hapa Tanzania aache yabunguliwe tutawapa kuku...kwani utajiri lazima uuze Kenyaa!!?Rwandaa!!?Burundii!?somaliaa!?

Wewe uzaaa akija mwenye ng'ombe debe mojaa muuzie kwa ng'ombe watatu..uone kama hutatajirika.
Eti wakulima nasema uongo jamani!!?

Eeeeeh musemakweli Ni mupenzi wa MUNGU!!!

Dahhhhumenifanya nicheke wkt haya mambo yametupa stress
 
Rais alikuwa sawa.

Na pia waziri mkuu yuko sawa.

Tatizo lilipo biashara ya mazao imeingiliwa na walanguzi,

yaani wanalangua mazao yote na kuyahodhi na kisha kuyapeleka kenya,
huku wanaacha unga bei juu,mchele bei juu,
ilikuwa haijawahi kutokea tangu uhuru hii nchi wakati wa mavuno eti unga unakuwa na bei juu kuliko mchele,
kumbe walanguzi mahindi yote wanapeleka kenya,

mchele msimu wa mavuno unashuka hadi 1000 kwa kilo leo kabla ya zuio mchele unagota 2000.

Kumbe mchele wote unavuka kwenda Rwanda,congo etc.

Wanaofaidi ni walanguzi na sio wakulima ,
zuio liendelee

Watu tunafanya kilimo biashara iweje nipangiwe pakupeleka
Km serikali inawapenda wananchi wake nao si walime wawauzie wananchi bei wazipendazo
Kila kitu shida ukigusa huku tamko ukigeuka huku tamko
 
Back
Top Bottom