Mh. Rais Kikwete Akiwa Ziarani Jamaica: Picha ya kukumbukwa!

MwanaFalsafa1,

..kama Raisi alikuwa na hamu ya kufanya michezo-michezo basi ingefaa ziara iwe ya KIBINAFSI.

..hizi ziara zina GHARAMA kubwa sana kwa walipa kodi wa Tanzania. ni vizuri tukawa makini na selective ktk ziara za Raisi wetu.
 
In fact Chadema changamkeni jamani picha kama hii mnaitengenezea tangazo safi ... kuwa wakati wananchi hawana umeme... Raisi aenda kubembea halfu mnasambaza... sisa ndio hivyo FITINA na hapa naona ni nafasi nzuri kabisa..
 
11_09_hmaerh.jpg



Kumekuwa na maoni mbalimbali kuhusu picha ya Rais akiwa kwenye bembea Jamaica. Mimi binafsi nimejiuliza maswali kadhaa juu ya jambo hilo.

Kubwa kuliko yote ni potential threats to the president's personal safety kwenye lile tukio. Kwenye ile picha, tumemuona Rais wetu mpenzi na Mama Salma Kikwete wakiwa na maafisa wawili wa Jamaica kwenye bembea.

Swali la kujiuliza ni maafisa wa Usalama wa Taifa wa Tanzania (yaani Tanzania Intelligence and Security Service) walikuwa wapi? Moja ya kazi muhimu sana ya Usalama wa Taifa ni kuhakikisha kuwa Rais anakuwa salama wakati wote. Hii ni pamoja na kuchukua tahadhari ya hatari zote zinazoweza kutokea na kuhakikisha kuwa kuna askari wa Usalama wa Taifa hatua chache ya kila mahali ambapo Rais anakuwepo in public.

Je, Rais angeteleza, kupata shambulio au kuishiwa nguvu ghafla akiwa juu ya bembea iliyokuwa hatua nyingi kutoka ardhini, Usalama wa Taifa wangepaa juu kumuokoa au wangemdaka kabla hajadondoka chini?

Je, Usalama wa Taifa walishindwa nini ku-insist kuwa mmoja wa maafisa wa Jamaica watoe nafasi ili askari wetu apande juu na kuweza kutoa ulinzi kwa Rais na Mama Salma wakiwa kwenye bembea?

Tena wakiwa juu ya bembea, sijaona hata kama kulikuwa na mikanda ya kuhakikisha usalama wa kiongozi wetu mpendwa.

Kazi ya Usalama wa Taifa ni kutoa "physical protection" kwa Rais popote anapokuwa. Je, Rais alipokuwa kule juu kwenye bembea, Usalama wa Taifa walikuwa wanatoa physical protection gani kwake?

Nimejaribu kudodosa kwenye Mtandao kuhusu Secret Service ya Marekani ambayo ina jukumu la kumlinda Rais Obama na viongozi wengine wakuu.

"In general, permanent protectees, such as the president and first lady, have details of special agents permanently assigned to them. The protection of an individual is comprehensive and goes well beyond surrounding the individual with well-armed agents. As part of the Secret Service's mission of preventing an incident before it occurs, the agency relies on meticulous advance work and threat assessments developed by its Intelligence Division to identify potential risks to protectees."

Je, Usalama wa Taifa walifanya threat assessments gani kabla ya kumruhusu Rais apande kwenye bembea bila ya ulinzi wa karibu?? Ni Kudra tu za Allah kuwa alituepusha na janga. Kama Rais angeishiwa nguvu akiwa juu ya bembea kama ilivyotokea Mwanza, ingekuaje?

Kwa maoni yangu kama layman wa maswala ya Usalama wa Taifa, THIS WAS A VERY SERIOUS SECURITY BREACH!
 
Watu juzi wame gate crash state dinner ya Obama...kwa hiyo hata hao secret service wa Marekani huchemsha vilevile
 
Tina... umewahi kusikia kitu kinaitwa "Photo oppotunity"? Unachoona kwenye picha sio lazima ndio kinachoendelea. Kwa taarifa yako jamaa wa TISS na usalama wa Jamaica walikua wametanda sehemu yote.

Ndio maana ukiangalia picha nyingi za viongozi wa nchi kama Marekani, UK, Germany..n.k. utaona hakuna hao jamaa wa usalama katika picha kwani kazi za hao usalama zinafanyika "covertly".
 
Kama mzee mwinyi alipigwa kofi na wao wapo ije jk kuanguka kutoka kwenye bembea? Angetua chini kama nazi
 
Tina mama/dada,
Mbona unajaribu kumbebesha Sungura mzigo anaobebaNdovu/Tembo. Hicho ulichokiona ndio kiwango cha vijana wetu.Kuwafananisha na wamarekani.........sijui lakini Julius amemaliza nao pia huchemsha!.
 
http://www.dailynews.co.tz/pics/11_09_hmaerh.jpg


Kumekuwa na maoni mbalimbali kuhusu picha ya Rais akiwa kwenye bembea Jamaica. Mimi binafsi nimejiuliza maswali kadhaa juu ya jambo hilo.

Kubwa kuliko yote ni potential threats to the president's personal safety kwenye lile tukio. Kwenye ile picha, tumemuona Rais wetu mpenzi na Mama Salma Kikwete wakiwa na maafisa wawili wa Jamaica kwenye bembea.

Swali la kujiuliza ni maafisa wa Usalama wa Taifa wa Tanzania (yaani Tanzania Intelligence and Security Service) walikuwa wapi? Moja ya kazi muhimu sana ya Usalama wa Taifa ni kuhakikisha kuwa Rais anakuwa salama wakati wote. Hii ni pamoja na kuchukua tahadhari ya hatari zote zinazoweza kutokea na kuhakikisha kuwa kuna askari wa Usalama wa Taifa hatua chache ya kila mahali ambapo Rais anakuwepo in public.

Je, Rais angeteleza, kupata shambulio au kuishiwa nguvu ghafla akiwa juu ya bembea iliyokuwa hatua nyingi kutoka ardhini, Usalama wa Taifa wangepaa juu kumuokoa au wangemdaka kabla hajadondoka chini?

Je, Usalama wa Taifa walishindwa nini ku-insist kuwa mmoja wa maafisa wa Jamaica watoe nafasi ili askari wetu apande juu na kuweza kutoa ulinzi kwa Rais na Mama Salma wakiwa kwenye bembea?

Tena wakiwa juu ya bembea, sijaona hata kama kulikuwa na mikanda ya kuhakikisha usalama wa kiongozi wetu mpendwa.

Kazi ya Usalama wa Taifa ni kutoa "physical protection" kwa Rais popote anapokuwa. Je, Rais alipokuwa kule juu kwenye bembea, Usalama wa Taifa walikuwa wanatoa physical protection gani kwake?

Nimejaribu kudodosa kwenye Mtandao kuhusu Secret Service ya Marekani ambayo ina jukumu la kumlinda Rais Obama na viongozi wengine wakuu.

"In general, permanent protectees, such as the president and first lady, have details of special agents permanently assigned to them. The protection of an individual is comprehensive and goes well beyond surrounding the individual with well-armed agents. As part of the Secret Service's mission of preventing an incident before it occurs, the agency relies on meticulous advance work and threat assessments developed by its Intelligence Division to identify potential risks to protectees."

Je, Usalama wa Taifa walifanya threat assessments gani kabla ya kumruhusu Rais apande kwenye bembea bila ya ulinzi wa karibu?? Ni Kudra tu za Allah kuwa alituepusha na janga. Kama Rais angeishiwa nguvu akiwa juu ya bembea kama ilivyotokea Mwanza, ingekuaje?

Kwa maoni yangu kama layman wa maswala ya Usalama wa Taifa, THIS WAS A VERY SERIOUS SECURITY BREACH!

Point!
 
Sasa usalama wa Taifa unahusika vipi na rais kupanda bembea?

In actual fact wana mambo ya muhimu zaidi ya kumfuatilia Rais na kupanda bembea zake

Hiyo ni kazi ya RESIDENTAL GUARD UNIT na hawa ndio waliofanya security assessment kabla bosi hajapanda hilo bembea

Mimi sioni kama kulikuwa na hatari kwa taifa if anything wahusika wako huko foreign na advance team iliyokwenda huko JA

hebu wapumzisheni watu wa TISS kwenye hili..wapo wenye kulaumiwa na nashangaa hamtaki kuwataja
 
Naona wamepelekwa kwenye bembea za chekechea huku jamaika anadanganywa kuwa ni kivutio cha watalii

Na wewe nyamaza banaa, ni mtoto wa chekechea wa binadamu wa wapi atakayeweza kukaa kwenye bembea kama hiyo!!!
 
Pia unatakiwa kukumbuka kwamba Bushi alikuwa likizo wakati jamaa yetu yuko kule kikazi ingawa hatujui hasa ni kazi ipi!!!!

Sasa hebu nikuuliza mkuu.Tuseme wewe umeenda sehemu kikazi kwani utakua unafanya hiyo kazi 24/7? Baada ya kazi ukiamua tuseme uende shopping kununulia familia zawadi ya kurudi nalo itakua ni kosa? Msiwe wagumu kiasi hicho kuelewa. Mtu kwenda sehemu kikazi haimaanishi 24/7 ni kazi tu.
 
Kuna swala moja naona kuna watu humu dani wanali shikia bango sana. Nadhani hilo lina tokana na ufahamu mdogo. Kuna watu wana sisitiza kwa nini counterpart wake kutoka Jamaica hakupanda. Kwanza mutambue kuwa kiongozi wa nchi hawezi kuacha kufanya shughuli zake kisa kuna mgeni. Kwa hiyo kiongozi fulani akienda nchi nyingine haimaanishi atakua na mwenyeji wake 24/7. Raisi mwenyeji anakua na ratiba zake na mgeni nae anakua na ya kwake siyo kwamba wana ongozana kila sehemu.
 
Kuna swala moja naona kuna watu humu dani wanali shikia bango sana. Nadhani hilo lina tokana na ufahamu mdogo. Kuna watu wana sisitiza kwa nini counterpart wake kutoka Jamaica hakupanda. Kwanza mutambue kuwa kiongozi wa nchi hawezi kuacha kufanya shughuli zake kisa kuna mgeni. Kwa hiyo kiongozi fulani akienda nchi nyingine haimaanishi atakua na mwenyeji wake 24/7. Raisi mwenyeji anakua na ratiba zake na mgeni nae anakua na ya kwake siyo kwamba wana ongozana kila sehemu.

labda inategemea ni rais wa wapi na ameenda kule kufanya nini na kwa muda gani. angekuwa rais wa Marekani 'n the like labda shughuli zingine za rais zingesimama mpaka aondoke....
 
JK anatakiwa ku leta hii "bembea" na hapa kwetu basi ili na sisi watalii wakija wabembee au yeye mwenyewe akitaka kurelax kidogo, mbona hapa kwetu milima ipo mingi tu tena ya kila aina?
 
labda inategemea ni rais wa wapi na ameenda kule kufanya nini na kwa muda gani. angekuwa rais wa Marekani 'n the like labda shughuli zingine za rais zingesimama mpaka aondoke....

Sasa basi una uhakika Shughuli aliyo endea Kikwete ili require counterpart wake wa Jamaica asimamishe shughuli zote na kumfuata kila sehemu?
 
Sio mchezo Raisi tunaye!

Wakuu,
Nilipoona picha hii na kusoma mjadala unaoendelea juu yake, nimejiuliza upya juu ya maana ya kilichotokea siku ile Mhe.Kikwete alipoteuliwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM, mtakumbuka machozi yalimtoka! Yalikuwa machozi ya nini? Alilia kwa furaha ya kupata fursa.., kwa kufikia lengo binafsi.., au kwa sababu ya majukumu yaliyokuwa mbele yake...?
Nimewaza sana, hata nikafukua yaliyoandikwa magazetini wakati ule...mf.

Uteuzi wa Kikwete: CCM kutawala karne nzima

2005-05-16 14:52:55
Na Simon Mhina, Jijini


Imeelezwa kwamba mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Bwana Jakaya Kikwete, atakifanya chama hicho kiendelee kutawala kwa zaidi ya karne moja, kwa vile atatumia muda wake wa miaka kumi, kutengeneza �vikwete� wengine wa kumrithi.

Akizungumza na Alasiri Jijini jana, mkereketwa na mpiga debe, wa CCM wilayani Ilala, Bw. Hamoud Jumaa, amesema kuchaguliwa kwa Kikwete kushika nafasi hiyo, kumetoa mwanya kwa chama chao kutawala miaka nenda rudi.

Akasema ni kweli kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, akichaguliwa atakaa madarakani kwa miaka kumi, lakini kwa usongo alionao mgombea huyo, muda huo unamtosha kutengeneza makada wenye tabia kama yake.

\'Maadamu tumempata Kikwete wapinzani hawana lao tena, tumemmpata mtu ambaye atakifanya chama chetu kiwe na maendeleo endelevu, na kukifanya kitawale karne moja ijayo,\'akasema.

Bw. Hamoud, akasisitiza kwamba falsafa aliyoonyesha mgombea huyo, tangu akiwa kada mdogo wa CCM hadi sasa, inaonyesha kwamba ni mtu mwenye uwezo wa kuleta mabadiliko bila woga.

Akasema yeye binafsi anampongeza sana Kikwete, lakini jambo kubwa zaidi, Watanzania wanatakiwa wajipongeze wenyewe kwa kumpata kiongozi huyo shupavu.

Akasisitiza kuwa mchakato mzima wa kumpata mgombea huyo, umedhihirisha na kwamba CCM ni baba wa demokrasia nchini.

\'Falsafa mpya ya ari mpya aliyotujulisha Kikwete tangu anachukua fomu, inatufundisha kwamba uongozi wake hautakuwa kinyume chake, na kwa mapenzi yake ya kuona aliyoanzisha yanaendelea, lazima atakuwa ameandaa mtu kama yeye.

\'Kwa hiyo kuchaguliwa kwake ni mwanzo mzuri kwa Watanzania kupata viongozi kama yeye kwa karne nzima ijayo,\'akasema.

Bw. Hamoud akatabiri kwamba kutokana na mapenzi makubwa ambayo Watanzania wameyaonyesha kwa mgombea huyo, ni dhahiri kwamba Bw. Kikwete atakuwa Bill Clinton wa Bongo.

Vilevile akasema ujio wa Kikwete utakifanya chama cha Mapinduzi kuwa na nguvu na kuaminiwa na Watanzania kuliko wakati mwingine wowote.

\'Kitaaminiwa na kuwa jabali mbele ya wapinzani, kwavile kinaendeshwa na kiongozi anayeaminiwa na watu,\'akasema.

Mkereketwa huyo, akamuomba mgombea huyo kutumia muda wake mwingi �kutengeneza� Vikwete wengine kibao, ili ndani ya CCM pawepo na viongozi kama yeye wasiopungua 11.

\'Namuomba kwa kuanzia, baraza lake la mawaziri na viongozi anaowateua yeye, asilimia 75 wawe ni vikwete na asilimia iliyobaki ndio aweke watu wengine.

Afanye hivyo bila woga kwa vile Watanzania wameshaonyesha kwamba wanapenda watu wenye msimamo kama wake,\'akasema.

Akawakumbusha Watanzania kwamba atakayefanikiwa kwa juhudi za Kikwete sio mgombea huyo, bali Watanzania wote.

Akasema hata Rais Benjamin Mkapa anastahili sifa na pongezi kwa uteuzi wa Kikwete, na kwamba ameonyesha uwezo wake wa kukijenga chama.

Bw.Hamoud amewashauri wapinzani, kuwa japo hali kwao ni ngumu kisiasa, lakini hawana budi kujikita zaidi katika kugombea ubunge, kwani rais ameshapatikana.

SOURCE: Alasiri
 
Back
Top Bottom