Muda wa mavuno (UCHAGUZI) umewadia , hizi semina elekezi mtazisikia sanaa. Mtaitwa nyie ndio mabalozi, nyie ndio wenye nchi hii, nyie ndio mmeniweka madarakani, nyie ndio mmenichagua, hivyo mimi nawatumikia nyie, na maneno kama hayo, watu wanahamishwa idara, kwa muda na wanarejea baadaye kwa style mpya, hiyo ndiyo siasa.
TRA, na Polisi wanatumika kuwasafisha wakubwa, jana mmeona kakana kuwatuma isipokuwa alimtuma LUKUVI peke yake, lakini hawa TRA alio kuwa akiwahimiza wahakikishe wanakusanya kodi, na tunakumbuka kuna wafanyabiashara waliambiwa wafunge maduka na waondoke lakini jana tumesikia tofauti, Serikali ilikuwa hamtumi mtu, wao vwatawala ni wasafi isipokuwa TRA ndiyo wabaya sana hawa hahaha, Ngojeni mkiisha jaa upepo mkawachagua mtaona muziki wake tena, maana binadamu wepesi sana kusahau, akiumwa njaa siku tano, siku ya sita akila akashiba anasahau mateso ya zile siku tano zilizopita, tunasema yaliyopita si ndwele tugange yajayo. Watanzania muwe nakumbukumbu, msidanganywe kirahisi hivyo.
Leo wamekataa katakata kwamba siyo wao kabisa hahaha, yangu macho mtakuja kukumbuka, mtaanza kuandika humu kwa uchungu, kazi yetu kusoma tu.