Mh Rais amemgundua mnyama mkali TRA

Mh Rais amemgundua mnyama mkali TRA

Rushwa itazidi mara TATU. Na nitawaambia kwa nini. Fikiria scenario hii:

Mtu kateuliwa kwenye nafasi ambayo mtangulizi wake "katumbuliwa" karibuni. Mteuliwa mpya haoni kosa alilofanya mtangulizi wake (kwa mantiki hiyo nae anajua kutumbuliwa kwake sio la kuuliza "kama nitatumbuliwa" bali "lini nitatumbuliwa". Mteuliwa huyu ni LAZIMA ajiandae kisaikolojia kutumbuliwa anytime of the day. So, atumbuliwe bila kuambulia kitu wakati kuna possibility ya kuchukua kitu kidogo?
Ungekuwa wewe ungefanyaje?
Mtazamo wako.. hauwezi kupingwa..
Ila watz tunatabia ya kutaka sifa tukiwekwa nafasi za aliyetenguliwa... Making sure naonekana nafaa
Siku ya 1 ofisini.. "mimi sio kama yule aliyewalea msinichezee..."
It might help pia... ni mtazamo wangu tu not conclusive
 
Karibu Njombe mzee Kichere mwenye sura mbaya kama yeye
 
Hongera Rais JPM Sina Shaka na IQ yako.
1.Nimefurahia Chenga uliopiga kwa wasio litakia taifa letu mema kwa propaganda kua Unawachukia wafanya biashara na hivo nchi yetu ni hatari kwa uwekezaji.
2.Mtaji wa kisiasa kwa jinsi ulivoonyesha kuguswa na kero na kwa weredi wa hali ya juu kuwabaini wajanja wajanja miongoni mwa walalamikaji. I wish all you would wish for yourself my dear President in 2020.
3.Nguvu ya taasisi ya uraisi na maamuzi kwa Wakati na yenye busara ilidhihirika.
Ninafahamu kua mwishowasiku serikali lazima ikusanye kodi,hatahivo nashauri kua ili kupata impact kwa maana ya manufaa ya kikao Cha Jana ninadhani ifanyike assessment ya hicho kinachoitwa uhuni wa vijana wa TRA kimeathiri kwa asilimia ngapi biashara nchini,tozo za kujirudia ni ngapi na ni asilimia ngapi ya athari, tozo za taasisi za udhibiti zimeathiri kwa asilimia ngapi nk. Ukilinganisha na miaka ya serikali awamu zilizopita..
Wasi wasi wangu japo Mimi sio mtaalam wa fedha Wala kodi, isijekua Sheria ya TRA yenyewe na mfumo wa ukusanyaji ndo mchawi wa haya malalamiko, kadhalika kwenye taasisi za udhibiti.
Naamini likifanyika hili tutakua na uhakika kua hatua zinazochukuliwa zitazaa matunda ya kukuza biashara nchini.
 
Kichere hakumsaidia Rais wala nchi yetu. Alitengeneza TRA ya watu wenye lengo la kuhakikisha biashara zote zinakufa. TRA inahutaji kufumuliwa upya. Wafanyakazi wake wengi hawana sifa za kukaa kwenye mamlaka ile ya kodi. Wanafikiria rushwa tu.
 
Shida sio t.r.a shida ni mkuu wenu wa nchi kila kitu anaongea yeye kashaona uchaguzi uko matakoni ivyo lazma ajipendekeze kwenu na kwa jinsi watanzania tulivyo mbuzi wala hatutakumbuka urefu wa kamba tulizofungwa hapo awali
Hili suala liko wazi, ni watanzania wengi humu mtandaoni wataleta kila aina ya story kwa sababu ndio hao hao wanao husika na ndio hao hao walio banwa. Ebufikiria wewe ukiwa umeajiria hapo TRA na hapo zamani ukawa kila unapoingia ofisini unarudi nyumbani na bunda la pesa sasa ule mrija ukabanwa, utafanya nini baada ya hapo? Ni wazi kwamba utatafuta kila aina ya njia kuivuruga huo mpangilio mpya na hao walio leta huo utaratibu mpya waonekne ni wabaya. Sasa hawa TRA ndio wamefanya biashara nyingi zi dorore. Kama Mh. Rais nataka kuliondoa hili tatizo kubwa aunde kamati ya kuwadhibiti hawa vijana wahuni. Kuna vijana wengi mitani wana.wlimi nzuri na wanatafuta kazi.
 
Magu ni mtu ambaye anataka akikuchapa usilie hata kama maumivu hayavumiliki . kulia huwa kunamsumbua sana ingawa viboko anachapa yeye. Wafanyabiashara kawatight sana, wanapopiga kelele anawageukia TRA kwamba hataki kusikia vilio vya wafanyabiashara ingawa haachi kutembeza mboko. Huku mitaani maRC, maDC na wakurugenzi wa serikali za mitaa nao wamemjua boss wao kwamba hapendi vilio ingawa anachapa vibiko, wanahimiza vitambulisho vya wajasilia mali lazima viuzwe vyote, watumishi wanapowabana wasionavitambulisho utasikia wanasema msiwafanye wananchi wakaichukia serikali yao. Ukimchapa mtoto akalia mwache alie ilimradi kumchapa kwako kuna dhumini la kumfundisha asifanye makosa zaidi baadaye.
Boss wa TRA aliyetumbuliwa hii ndo style ya awamu hii ambayo alipaswa kucheza NATO
 
Vip, babaako ndio anafaa kuwa Rais ili tuwakabidhi ikulu au sio..?

Soma tena comment yangu, hakuna niliposema baba yangu anafaa kuwa Raisi, nilichosema ni kuwa jiwe hafai kuwa Raisi, atoke madarakani na vyeti vyake vikaguliwe, hata wewe kama una vigezo waweza kuwa Raisi hivyo hepuka kujidharau kama wafanyavyo Lumumba fc
 
Mtazamo wako.. hauwezi kupingwa..
Ila watz tunatabia ya kutaka sifa tukiwekwa nafasi za aliyetenguliwa... Making sure naonekana nafaa
Siku ya 1 ofisini.. "mimi sio kama yule aliyewalea msinichezee..."
It might help pia... ni mtazamo wangu tu not conclusive

Let's examine the facts on the ground. Kama unaamini mtazamo wako, kumekuwa na mabadiliko ya mawaziri na makamishna wa TRA mara ngapi tangu 2015? Kwa mtazamo wako, Hali inakuwa nzuri au mbaya zaidi?
I rest my case.
 
yale ni maigizo tu, TRA wanachokifanya ni maelekezo / shinikizo toka juu! kila mwezi wanawekewa malengo ya makusanyo na serikali ni wakali kweli kwa TRA wanapolegalega kukusanya ushuru. huko nyuma ya pazia shinikizo la kuwataka wawe 'aggressive' linatoka juu na wao wanatii, njia pekee ya kufikisha malengo ni kuwa wakali na kutoa makadirio makubwa ya kodi kwakua walipaji na walewale.
(japo ni kweli kuna tatizo la rushwa, ambalo sio la TRA peke yao bali ni serikali yote)
👍 👍
 
TRA rushwa ndiyo tatizo, hasa ukitaka kuina vizuri nenda pale kariakoo. Pia TRA hawatumii common sense, yaani rushwa kwanza, uzalendo baadaye. Naamini serikali ilishalifanyia kazi hilo suala la waharifu ndani ya TRA, maaana unakuta lile kabila la wezi walikuwa wamejazana, na ndiyo maana TRA imeshutumiwa
Nchi hii ina kabila la majizi?!
 
Mh ni msanii acha unaweza chinja mwanao kwa unafiki wake anajua A to Z hapo anatafuta sympathy za watanzania tuone TRA ndio wana tatizo siyo yeye, kitu ambacho si kweli

Kumbuka zoezi la vitambulisho vya wajasilia mali wakurugenzi wa halmashauri waliofanya vibaya kuuza kawafanya nini kawatumbua wote hapo ndio utajua big dady ni bonge la snitch na ni muiigizaji nzuri sana zaidi ya ray kigosi anajua kupritend balaa kuwa yanayofanyika hayajui kumbe wapi anajua A to Z sema anataka tuhadaa watanzania
I disagree,nilichokiona kikubwa ni kwamba Watumishi wengi wa Serikali hawajamuelewa Rais!Wanafanya kazi kwa kuangalia picha ndogo,kibakuli cha mlo wa siku,siyo ghala ya chakula...President sees a bigger picture but interpretors sees backwards!Tra of course lazima walazimishwe kufikia malengo BUT tools za ku approach hiyo biashara ziko-The simplest one ni CUSTOMER Care na Instituted laws...they dont apply,instead wanafanya kazi za hovyo kabisa(Threatening,bullying,frustrating and corruptying)!Mbona wafanyabiashara wanabembeleza wsteja na wanavuka malengo...?Acha awanyooshe!Sisi tumemuelewa na tutafanya kazi na nchi itaenda!!
Kudos!
 
Kama ulikuwa una mfuwatilia mh Rais jana alifika mahali wakati anaongea Mwambe alipo maliza akasema. Amegunduwa kuna mnyama mkali ambaye ni TRA.
Ukweli nikwamba TRA imeumiza watu kiasi chuki iliopo kati ya TRA na wateja nikubwa kiasi cha watu hata kutaka kuuwana.

Na ukichunguza mzizi wote wa fitina upo kwenye kitengo cha Estiment watu wengi wamefunga biashara na hata kufunga akaunti kutokana na watu kupewa bils mbaya zisizo za haki na hii ni kwa sababu TRA ni mnyama mkali anauwa biashara badala yakuzikuza na kuzilinda.

Niukweli usio pingika ikiwa Rais angeunda kamati kufuwatilia nyendo za Tra na unyama tra umewafanyia watu wake nadahni 75% ya watumishi Tra wangepukutishwa nimambo yakutisha nahakuna anathubutu kusema why?
Stay tune
Mkuu TumainiEl naomba nitofautiane na wewe kidogo. Pamoja na matatizo yake TRA kuna tatizo dogo ambalo hamtaki kulisema. Misingi ya kukusanya kodi iko wazi na iko kisheria yaani Assessment, Collection Accounting and TRADE FACILITATION na iko wazi hata kwa mfanyabiashara. Toka mwanzo serikali iliiagiza TRA kutekeleza majukumu hayo kwa njia ya kulipa kodi kwa hiari (Voluntary compliance) na ikaundwa Idara maalumu kuhamasisha ulipaji kodi kwa hiari.
Ulipaji kodi kwa hiari uliangalia mazingira ya biashara ya mfanyabiashara na uwezo wake wa kulipa kodi na uliruhusu kulipa kwa awamu kama ikishindikana kulipa kwa mkupuo. Utaratibu ulipotea ghafla ikawa ni kulipa kwa mkupuo tu bila "room of manoeuvre" kwa mfanyabiashara. Pili Assessment ikawa ya upande mmoja bila kumshirikisha mfanyabiashara kama anakubaliana nayo au la na kama hakubaliani nayo atoe uthibitisho wa mazingira yake na ufanisi wa biashara yake.
Niipongeze Serikali imeliona hilo na pamoja ya kwamba halijawekwa bayana lakini ni imani yangu kwamba ukaribu wa TRA na Wafanyabiashara ni muhimu ili Serikali ipate maduhuli yake na Wafanyabiashara nao wawe na mazingira mazuri ya biashara zao.
Ni mawazo yangu!
 
Bila shaka estiment ni mtoto wa huyo mnyama mkali.
Btw
Estiment,hao vijana wa estiment hawajui kitu aidha kwa makusudi au kutokuelewa. Mimi kama mfanyabiashara napeleka makadirio ya kodi kama sheria invyosema cha ajabu wao wanakataa wanasema ni ndogo!
Nikawauliza unasema ndogo kwa vigezo vipi anaweweseka tu.
 
Yale ni maigizo tu, TRA wanachokifanya ni maelekezo / shinikizo toka juu! kila mwezi wanawekewa malengo ya makusanyo na Serikali ni wakali kweli kwa TRA wanapolegalega kukusanya ushuru.

Huko nyuma ya pazia shinikizo la kuwataka wawe 'aggressive' linatoka juu na wao wanatii, njia pekee ya kufikisha malengo ni kuwa wakali na kutoa makadirio makubwa ya kodi kwakuwa walipaji na walewale.

(japo ni kweli kuna tatizo la rushwa, ambalo sio la TRA peke yao bali ni Serikali yote)
halafu hayo malengo kila mwaka yanapanda wakati walipa kodi ni walewale
 
TRA itaendelea kutumbua makamishna kama hawatokuwa tayari kubadilika.

Sehemu hii ndio inayoitafuna TRA na kuwafanya waonekane wanyanyasaji kwa wafanyabiashara.

Kikokotoo cha kodi.
Hapa wasimamizi na wakokotozi wa kodi hulazimika kumtoza mfanyabiashara asilimia 30 ya mauzo yake. Na hiyo ni sheria za makusanyo ya kodi. Hebu angalia kwenye biashara nyingi unapoweka mtaji wa 10,000|= basi itazalisha 1000/= au zaid ni 2000|= . Sasa TRA wao hawataki tukatane kwenye faida wao wanaangalia mauzo yako kama ni mauzo ya 500,000|= wanataka asilimia 30 ya laki tano. Huo ni wizi

Sheria za TRA hazina urafiki na mfanyabiashara zina uadui mkubwa na zinamlazimisha mfanyabiashara kuwa mbali na TRA.

Anatakiwa kiongozi wakubadilisha hii kama atataka kudumu kwenye kiti chake.
 
Back
Top Bottom