kanyagio
JF-Expert Member
- Dec 10, 2009
- 1,021
- 365
nimeona kwenye taarifa ya habari jana na leo na pia nimesoma kwenye magazeti kuwa Mh Rais Mstaafu Benjamin Mkapa amekemea wale wote waliojilimbikizia mali wakati wa Kongamano kumbumkuka Mwl nyerere.
naomba ninukuu alichosema ...... Sisi sote ni mashahidi wa baba wa taifa wakati wa uahi wake aliishi maisha ya kawaida, hakuwa na uchu wa madaraka, hakujilimbilikizia mali, na alipenda usawa kwa kila mtu....... ni wakati muafaka kwa watanzania kuendelea kuishi maisha ya kawaida kama alivyoishi Nyerere ambapo alihakikisha anaweka misingi imara ya kuwatetea wanyonge na kuwaunganisha watu wote kwa kuona rushwa ni adui ya haki".
baada ya kunukuu alichosema Mh. Mkapa, naomba niseme kuwa nasikitika kuona kuwa anatambua misingi mizuri aliyokuwa anasimamia baba wa taifa lakini yeye kwa makusudi kabisa akaivunja,. narudia tena kwa makusudi kabisa akaivunja. nasema haya nikiongozwa na matukio yafuatayo:
naomba ninukuu alichosema ...... Sisi sote ni mashahidi wa baba wa taifa wakati wa uahi wake aliishi maisha ya kawaida, hakuwa na uchu wa madaraka, hakujilimbilikizia mali, na alipenda usawa kwa kila mtu....... ni wakati muafaka kwa watanzania kuendelea kuishi maisha ya kawaida kama alivyoishi Nyerere ambapo alihakikisha anaweka misingi imara ya kuwatetea wanyonge na kuwaunganisha watu wote kwa kuona rushwa ni adui ya haki".
baada ya kunukuu alichosema Mh. Mkapa, naomba niseme kuwa nasikitika kuona kuwa anatambua misingi mizuri aliyokuwa anasimamia baba wa taifa lakini yeye kwa makusudi kabisa akaivunja,. narudia tena kwa makusudi kabisa akaivunja. nasema haya nikiongozwa na matukio yafuatayo:
- Mh Mkapa ulianzisha kampuni ya ANABEN ukiwa ikulu na ukanunua kiwanda cha Kiwira kwa bei ya kutupa (nasikia ulikipata kwa bei chee).. sasa hapo kweli ulikuwa umesahau misingi ya mwalimu.. Je kama mwalimu aliishi maisha ya kawaida pasipo kuiba rasilimali za nchi wewe ulishindwa nini.
- wakati wa utawala wa mzee Mkapa tulishuhudia nyumba za serikali zikiuzwa kwa bei ya kutupwa. na waliouziwa hizo nyumba wameziuza kwa bei ya kutupa na wengine inawezekana hawakukamilisha malipo. Kama Mwl alijenga hizo nyumba, kwa nini wewe usimamie uporaji wa namna hii. Je mbona watumishi sasa wanahaha kupata mahali pa kuishi. Mfano mzuri na Mh. Nahodha alivyotekekeza mamilioni ya watanzania kuishi hotelini kisa hajapewa nyumba na serikali
- Wakati wa utawala wa mkapa tulishuhudia uuzwaji wa makampuni yaliyoanzishwa na Mwl tena kwa bei ya kutupa.. hebu jamani tukumbuke NBC.
- wakati wa utawala wako mh. Mkapa tumeshudia, makampuni makubwa yakichukua ardhi kwa ajili ya uchimbaji dhahabu, huku wachimbaji wadogo wadodo wakiachwa hawana kitu. tena wengine nasikia (narudia kusema nasikia kwa sababu sina uhakika 100%) walifukiwa mashimoni. Je hii ndo msingi aliokuachia Mwl Nyereree
- Mh Mkapa wakati wa utalawala wako vitendo vya rushwa vilishamiri kwelikweli, nakuimbuka ndo kipindi hiki hata rushwa ndani ya polisi ilishamiri kisawasawa- huku mheshimiwa ukimfumbia macho IGP wa kipindi hicho.
- Mh. Mkapa, wakati wa utawala wako ndo kashifa nzito zilitokea zikiwemo EPA, Deep Green, Buhemba etc.
- Mh. Mkapa wakati wa kipindi chako ndo tumeshuhudia kampuni ya TIPER ikivunjiliwa mbali kwa hila. sasa matokeo yake tunayaona kwa upande wa mafuta ya petroli, dizeli etc (hapa nakumbuka mchango wa Mbunge wa Muleba alivyolalamika wakati anachangia hotuba ya bajeti ya Mh. Ngeleja).
- wakati wa utawala wako, ndo tulishuhudia ukwasi wa kutupa kwa viongozi wetu wakiwemo mawaziiri, makatibu wakuu, wakurugenzi wakipata ukwasi wa ajabu ambao wakati mwingine hauelezekii (ref. kina Balali, Lowasa, etc) . Mbona hukusimama kidete kuwaambia waishi maisha ya kawaida kama ya mwl Nyerere
- wakati wa utaawala wako kipato kati ya matajiri na masikiini kilizidi .. mkuuu ina maana haukuyaona haya?
- Wakati wa kipindi chako, tulishuhudia wanafunzi vyuoni wakigoma.