Mh Mkapa; Kauli yako inahitaji maelezo ya ziada, otherwise.....!

kanyagio

JF-Expert Member
Dec 10, 2009
1,021
365
nimeona kwenye taarifa ya habari jana na leo na pia nimesoma kwenye magazeti kuwa Mh Rais Mstaafu Benjamin Mkapa amekemea wale wote waliojilimbikizia mali wakati wa Kongamano kumbumkuka Mwl nyerere.

naomba ninukuu alichosema ...... Sisi sote ni mashahidi wa baba wa taifa wakati wa uahi wake aliishi maisha ya kawaida, hakuwa na uchu wa madaraka, hakujilimbilikizia mali, na alipenda usawa kwa kila mtu....... ni wakati muafaka kwa watanzania kuendelea kuishi maisha ya kawaida kama alivyoishi Nyerere ambapo alihakikisha anaweka misingi imara ya kuwatetea wanyonge na kuwaunganisha watu wote kwa kuona rushwa ni adui ya haki".

baada ya kunukuu alichosema Mh. Mkapa, naomba niseme kuwa nasikitika kuona kuwa anatambua misingi mizuri aliyokuwa anasimamia baba wa taifa lakini yeye kwa makusudi kabisa akaivunja,. narudia tena kwa makusudi kabisa akaivunja. nasema haya nikiongozwa na matukio yafuatayo:

  1. Mh Mkapa ulianzisha kampuni ya ANABEN ukiwa ikulu na ukanunua kiwanda cha Kiwira kwa bei ya kutupa (nasikia ulikipata kwa bei chee).. sasa hapo kweli ulikuwa umesahau misingi ya mwalimu.. Je kama mwalimu aliishi maisha ya kawaida pasipo kuiba rasilimali za nchi wewe ulishindwa nini.
  2. wakati wa utawala wa mzee Mkapa tulishuhudia nyumba za serikali zikiuzwa kwa bei ya kutupwa. na waliouziwa hizo nyumba wameziuza kwa bei ya kutupa na wengine inawezekana hawakukamilisha malipo. Kama Mwl alijenga hizo nyumba, kwa nini wewe usimamie uporaji wa namna hii. Je mbona watumishi sasa wanahaha kupata mahali pa kuishi. Mfano mzuri na Mh. Nahodha alivyotekekeza mamilioni ya watanzania kuishi hotelini kisa hajapewa nyumba na serikali
  3. Wakati wa utawala wa mkapa tulishuhudia uuzwaji wa makampuni yaliyoanzishwa na Mwl tena kwa bei ya kutupa.. hebu jamani tukumbuke NBC.
  4. wakati wa utawala wako mh. Mkapa tumeshudia, makampuni makubwa yakichukua ardhi kwa ajili ya uchimbaji dhahabu, huku wachimbaji wadogo wadodo wakiachwa hawana kitu. tena wengine nasikia (narudia kusema nasikia kwa sababu sina uhakika 100%) walifukiwa mashimoni. Je hii ndo msingi aliokuachia Mwl Nyereree
  5. Mh Mkapa wakati wa utalawala wako vitendo vya rushwa vilishamiri kwelikweli, nakuimbuka ndo kipindi hiki hata rushwa ndani ya polisi ilishamiri kisawasawa- huku mheshimiwa ukimfumbia macho IGP wa kipindi hicho.
  6. Mh. Mkapa, wakati wa utawala wako ndo kashifa nzito zilitokea zikiwemo EPA, Deep Green, Buhemba etc.
  7. Mh. Mkapa wakati wa kipindi chako ndo tumeshuhudia kampuni ya TIPER ikivunjiliwa mbali kwa hila. sasa matokeo yake tunayaona kwa upande wa mafuta ya petroli, dizeli etc (hapa nakumbuka mchango wa Mbunge wa Muleba alivyolalamika wakati anachangia hotuba ya bajeti ya Mh. Ngeleja).
  8. wakati wa utawala wako, ndo tulishuhudia ukwasi wa kutupa kwa viongozi wetu wakiwemo mawaziiri, makatibu wakuu, wakurugenzi wakipata ukwasi wa ajabu ambao wakati mwingine hauelezekii (ref. kina Balali, Lowasa, etc) . Mbona hukusimama kidete kuwaambia waishi maisha ya kawaida kama ya mwl Nyerere
  9. wakati wa utaawala wako kipato kati ya matajiri na masikiini kilizidi .. mkuuu ina maana haukuyaona haya?
  10. Wakati wa kipindi chako, tulishuhudia wanafunzi vyuoni wakigoma.
ninayomengi ya kueleza lakini, ni vema anaposimama jukwaani na kukemea wanaojilimbikizia mali, ni vema atueleze kwa nini alifanya yaliyobainishwa katika point kumi hapo juu. Asipofanya hivyo mimi nitaona ni kokoto na anasema tu mdomoni na hayatoki moyoni mwake!
 
Binafsi nimeshangazwa na kauli yake,halafu akaenda mbali kwa kusema sisi(WATANZANIA) eti wavivu wa kufikiri,so yeye m2 wa msumbiji ni mwepec wa kuwaza,hop ana2ng'ong'a tu
 
Another controversial statement from Mkapa

~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*
Saturday, 15 October 2011 21:39


By Florence Mugarula
The Citizen Reporter
Dar es Salaam.

Retired leaders yesterday advised Tanzanians to start taking action instead of merely complaining if they wanted to have a better future.

The leaders were contributing to the theme ‘The Tanzania we want' during a discussion held in Dar es Salaam to commemorate the 12th anniversary of Mwalimu Julius Nyerere's death and 50 years of independence.

One of the participants, retired President Benjamin Mkapa, emphasized the need for all Tanzanians, especially the youth, to start thinking critically and take action instead of complaining on everything.

He noted that most seminars and workshops held currently to deliberate on the country's future were characterised by apportioning of blame, anger and complaints, a trend that does not help to get rid of the problems they purport to address.

He warned that if Tanzanians fail to think strategically and remain a complaining lot, there was a danger of foreigners taking advantage of the situation by pushing through unfavourable policies, like the Economic Partnership Agreements (EPA) between East African countries and the European Union.

According Mkapa, the EPA arrangement is meant to benefit the Europeans, and not East African countries.

"The terms of agreement include establishment of industrial partnerships and tax free exportation of goods, among others… However, East Africa cannot compete with European countries in those areas, so we need to think critically to oppose this," said Mr Mkapa.




 
Naona ni makosa ya kupokezana vijiti ndo yanaleta changamoto za sasa. Succession plan kwenye nchi hii hakuna mwisho wa siku hela zimewafanya opportunists wasio na uwezo wowote kuingia kwenye uongozi na kushika madaraka
 
kanyagio, mi na kuunga mkono asilimia miamoja na thread yako...ila inabidi pia tufike wakati yusema TOSHA..na tuchukue hatua. Suku hiyohiyo Mzee warioba alisema kila mtu leo hii ndani ya Tanzania ni mlalamishi si Viongozi na si raia wa kawaida nakumbuka na akamwambia Hussein Bashe kuwa vijana inabidi tuungane na tuache kulalamika..Kingunge nae akasema watu tunamakosa yaani wazee kwa Vijana....Nilipokuwa nasikiliza mdahalo wa katiba uliofanyika SAUT..Professor Chris Peter Maina alisema kama Rais kuna makosa alifanya akiwa madarakani akiondoka anaeza kushtakiwa, ikiwa makosa hayo hayahusiani na utekekelezaji wa shughuli zake za Uraisi, sasa ni kwanini tusimshitaki Mh????
 
Makosa ambayo mengine JK anayabeba yametokana na Mkapa kwa asilimia kubwa sana. Kama CCM ikifa au kupoteza mamlaka basi Mkapa indirect anahusika. Yeye ndiye muasisi wa maovu mengi na akatumia ukali na kutokukubali kushaurika kwa manufaa yake binafsi. I hate Mkaa aka Mzee wa Kokoto.
 
Mkuu pole, Usiimize kichwa kwani hiyo hotuba:
  1. Kaandikiwa
  2. Yeye ni msomaji tu
  3. Na hakupata muda wa kuipitia
  4. Na angeipitia basi kuna vipengele angebadilisha maana vingemsuta
 
Mkuu pole, Usiimize kichwa kwani hiyo hotuba:
  1. Kaandikiwa
  2. Yeye ni msomaji tu
  3. Na hakupata muda wa kuipitia
  4. Na angeipitia basi kuna vipengele angebadilisha maana vingemsuta
Upo sahihi kabisa na kama aliipitia basi hakuwa na jinsi ya ku edit maana litakuwa labda ni shinikizo.
 
hana aibu mie ninawasisi alikuwa anwaangalia watu au kainamisha uso? aliwaleta wazungu tannesco wakaingia ofisini wakilindwa na ffu.....agh umeme umeenda sioni vizuri nimeinamisha lap top ili nione key board
 
Mkapa is a lot of worse things.. Ufisadi... ikiwa moja wapo (thou not yet proven).... But katika Maraisi walopita (Mwalimu pembeni) the most intelligent na the most calculated akijua fika nini anafanya. Jamaa anajua hali ni mbaya ya CCM na siwezi shangaa kama anatafuta upenyo wa kuhemea so that hata Chama kipya kikishinda waone ni mwenzao. Juu ya Mkapa na habari zake yananishangaza mambo mawili:-
  1. Ni kiongozi ambae alikua anakwepa saana vyombo vya habari wakati wa Uraisi na hata baada tu ya kustaafu na hasa pale zilipo rise kashfa juu yake... Kitu gani kimemfanya saizi ghafla bin vuu yupo kwenye Siasa related activities katika sura ya Media... na kwa nini saizi yupo more confident kuongelea Utawala na madhaifu yake.... Very very iff.... (IMO)
  2. Wanahabari wetu wa hapa Tanzania... Kitendo cha kusema wanakutana na the guy face to face na badala ya kumuuliza yale maswali ambayo yana linger katika back of our brains and for long... Wana entertain upuuzi wa kuendelea kuchapisha habari ambazo ni kama anajikosha... Hivi kwamba hawa wanahabari wamenunuliwa na hawana guts ya kuuliza the right questions... AU kwamba anawasiliana tu na wale wana habari ambao wapo katika his back pocket??
 
hana aibu mie ninawasisi alikuwa anwaangalia watu au kainamisha uso? aliwaleta wazungu tannesco wakaingia ofisini wakilindwa na ffu.....agh umeme umeenda sioni vizuri nimeinamisha lap top ili nione key board

Ashukuru Mungu hakuzaliwa China, wangeshamfanya kitu kibaya miaka mingi sana, halafu haoni hata aibu kutoa kauli zake zilizojaa utata na wakati huo huo hataki kuzungumza lolote lile kuhusu ufisadi mbali mbali alioufanya alipokuwa madarakani.

Sijui yeye kafanya lini hiyo "critical thinking" na alichukua actions zipi katika kulinasua Taifa katika matatizo chungu nzima yanayosababishwa na mafisadi ndani ya CCM/Serikali.
 
Back
Top Bottom