Mgomo wa wahadhiri UDOM wanukia

Mwanzo tulianza na NSSF, watu wakapandwa jazba sana ila ndio ukweli wenyewe,
Now ni Udom,kiukweli chuo hicho kina udini sana angalia mawarden vilaza kutoka zanzibar wamejazana pale
bila hata qualification za maana!!Njoo kwenye depart ya finance My God utaimba haleluyah,kajaza ofisi nzima
masheikh!!Huyu prof uchwala mlacha ajiandae kwenda mahakama ya hague few years to come lol!!
yani haya mambo ya ajabu sana!waislam wamekuwa wakilaumu kwa kipindi kirefu kwamba si vyuoni tu bali serikalini kwa ujumla kuna upendeleo mkubwa kwa wakristo kuajiriwa huku wakitoa.data.hoja iliyotolewa na serikali na wakristo ni kwamba serikali huangalia uwezo na sifa na si dini katika kumpa mtu majukumu flani (hoja ambayo kimsingi mimi niliipenda kwa sababu ni ya kitaalam japo mimi ni muislam na si kuwa na kazi).saasa leo nashangaa sana ndugu zangu wakristo wakiibuka na kusema kwamba udom kuna udini mkubwa sababu wafanyakazi wake wengi ni waislam!.sasa pengine niulize maswali kadhaa anayeweza ajibu.je! ni sahihi taasisi flani ikiwa na watu wengi wa dini flani kusema ina udini?ni kweli kwamba watu wamekuwa wakiajiriwa nchini kwa sababu ya dini zao?je!ajira zinazozingatia udini zimeanzia udom?je!udini upo kwa waislam tu au hata wakristo?ikiwa udom kinazingatiwa kigezo cha udini kuajiri watu wasio na sifa kwa kuwa waislam wamekuwa wengi,je!maprofesa kama kikula pia walipata uprofessa kwa kuwa ni waislam? je!waalimu waliowafundisha maprofessa wa udom nao walikuwa waislam?kwa kuwa udsm nako watumishi wengi ni wakristo,je!wameajiriwa kwa kuwa ni wakristo! kama alie leta udini udom ni kikwete (kwa kuchagua viongozi wa chuo ambao ni waislam je nani aliyechagua na anaechagua viongozi wa udsm?ajab sana!

 
  • Thanks
Reactions: Ame
hivi tukisema tulist hapa wafanyakazi wa serikali kuanzia ikulu mpaka wilaya unajua ratio ya waislam kwa wakristo ni ngapi? angalia hata UDOM ratio ya watu kutoka dini hizo mbili. yaani kuwepo shabani mlacha kwenu ni tatizo, na si kingine bali kwa sababu ya uislamu wake. Nyie endeleeni, mpaka kitanuka ndo mjue madhara ya myafanyayo.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
iii) Hiki ni chuo ambacho non-christian anakuambia mwakani nataraji kuajiriwa UDOM na kweli akaajiriwa. Hiyo nayo ni nini? Taasisi gani ya UMMA ambayo mtu anaweza kupredict kuwa ataajiriwa nayo kama hajui chochote na kama taasisi hiyo itatangaza ajira?
iv) Unadai umefanya kazi na Prof na Dr amme ambae ni Director Graduate studies, kama hawa watu ni wachapakazi inakuwaje alieajiriwa kama mhadhiri msaidizi mwaka 2009 analingana mshahara na mhadhiri msaidizi alieajiriwa hata jana ama kesho alhamisi tarehe 1/11/2012? Nakuuliza tena hayo UDSM, SUA, MZUMBE , DUCE ama MUCE yanafanyika?
hebu jaribu kuoanisha mambo kwa kutumia vigezo vya kitaalam kuliko hisia.vivi mfano mtu akikuambia ataajiriwa wizara ya fedha mwaka kesho halafu huyu mtu ni muislam,mwanaume,mpare,ana mke muhaya,ana masters ya utawala,ana ndugu yake anafanya kazi kilimo na sifa njingine mchanganyiko.je!ikitokea akiajiriwa kweli na wewe ukiju na moja kwa moja ukasema "jamaa kaajiriwa kwa sababu ni non-christian"unadhani hoja yako itakuwa ni ya kitaalam au ni emotional?
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Amri kumi za MUNGU kwenye Biblia inasema ..."MPENDE MUNGU WAKO ......" na amri ya pili inasema "..... mpende jirani yako .....sasa nyie wa UDOM mmekaa wote na mnagoma sababu ya chuki kwa waislamu kuajiriwa, ukweli siwaelewi kabisa.

Hivi kweli ninyi ni wakristo wa ukweli? Umoja wenu wa wahadhiri hivi pia kuna Waislamu mnaowachukia na mpo nao kwenye mgomo wa kuwataka wasiajiliwe?
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Niambieni

Mengine yote nakuunga mkono..Ila hapo CHADEMA umeihusishaje na haya? Ww mwenyewe unakataa ubaguzi na hapo hpo unabagua wengine?
 
Last edited by a moderator:
yani haya mambo ya ajabu sana!waislam wamekuwa wakilaumu kwa kipindi kirefu kwamba si vyuoni tu bali serikalini kwa ujumla kuna upendeleo mkubwa kwa wakristo kuajiriwa huku wakitoa.data.hoja iliyotolewa na serikali na wakristo ni kwamba serikali huangalia uwezo na sifa na si dini katika kumpa mtu majukumu flani (hoja ambayo kimsingi mimi niliipenda kwa sababu ni ya kitaalam japo mimi ni muislam na si kuwa na kazi).saasa leo nashangaa sana ndugu zangu wakristo wakiibuka na kusema kwamba udom kuna udini mkubwa sababu wafanyakazi wake wengi ni waislam!.sasa pengine niulize maswali kadhaa anayeweza ajibu.je! ni sahihi taasisi flani ikiwa na watu wengi wa dini flani kusema ina udini?ni kweli kwamba watu wamekuwa wakiajiriwa nchini kwa sababu ya dini zao?je!ajira zinazozingatia udini zimeanzia udom?je!udini upo kwa waislam tu au hata wakristo?ikiwa udom kinazingatiwa kigezo cha udini kuajiri watu wasio na sifa kwa kuwa waislam wamekuwa wengi,je!maprofesa kama kikula pia walipata uprofessa kwa kuwa ni waislam? je!waalimu waliowafundisha maprofessa wa udom nao walikuwa waislam?kwa kuwa udsm nako watumishi wengi ni wakristo,je!wameajiriwa kwa kuwa ni wakristo! kama alie leta udini udom ni kikwete (kwa kuchagua viongozi wa chuo ambao ni waislam je nani aliyechagua na anaechagua viongozi wa udsm?ajab sana!


Hao wanaofanya haya sidhani kama ni wakristo..Hao wanadini yao nyingine ila wamejipa majina ya ukristo kutimiza taa yao ya kimwili....Mkristo anaye lalamika eti fulani kani onea wa wapi huyo? Katika kristo yupi huyo..Huyu huyu mimi ninayemwabudu aliyemfuata shetani kuzimu na kumnyang'anya funguo za kuzimu na kuwatoa mateka wote aliowafunga katika magereza yake? Duuh hata huyo Kristo atakuwa anasikitika kusikia matapeli wanatumia jina lake kufanya ujambazi...Hao wanaoitwa waislamu wanaweza kuwa na-ukristo (wapakwa mafuta) zaidi kuliko hawa ambao wanafanya utapeli wa majina ya watu....

Labda kuwe na la ziada lakini so far hao wanaogoma kama kweli kwa sababu hizo za mleta mada basi lazima tuwe na wasiwasi na watoto wetu wanasoma Udom kwamba hawapati elimu sahihi...
 
.... Mbona mnasema daladala kwanini msizitumie nasikia zipo dala dala za UDOM nyingi tu. Kwani sera zinasemaje kuhusu kupewa Nyumba? Nchi inafuata utaratibu wa kutibiwa kwa bima, au ndio ninyi wa UDOM tu mnataka kutibiwa bure jamani?. Kama kweli Dept. ya fedha ni waisilimu watupu basi nawapongeza. Maana ndio hao hao ambao waliowafanyia mipango mizuri ya kuishi vizuri, kwani nasikia ni Chuo Kikubwa na kizuri sana. Kwa hiyo Bursar wenu na timu yake inafanya kazi vizuri hadi kufikia kuongeza idadi ya wanafunzi na walimu. Mafanikio bwana ni mipango mizuri ya hawa mabwana.

Jichunguzeni, Bunge lilianza Jana. Au wakuu wa Chadema waliwafikia na kuwapandikiza kitu na ndipo mmeanza?. Eti walimu wanaacha kazi n... kwani waliopo hapo walipotoka si waliacha kazi kwingine na kuja UDOM. Huyo Nowe si aliacha Chuo sijui SUA na kuja UDOM?.
Mkuu heshima mbele, kwa maelezo uliyoanza nayo hapo juu inaonekana nawe ni muhadhiri au upo karibu na fani hiyo (samahani kama nimekosea). Katika maelezo yako mareeeefu, nasikitika kusema hujaweza kujenga hoja ya kushawishi (kama ni muhadiri, jamii inategemea zaidi ya hapo). Angalau kwenye mistari niliyoweka rangi ya blue kuna mantiki umeongea lakini ulipofika nilipoweka rangi nyekundu ukaamua kutumia masaburi kujenga fikra zako.
 
I think watu walio nje ya udom wanaweza kujudge vyovyote wapendavyo bt ambao wamevivaa viatu wanajua vinapoumiza! Waislam kuwepo udom sio shida...tatizo qualification zao hasa hao malecturer wa kizenji! Wako shalow ktk ufundishaji, hawana confidence yaani wanaboronga mbaya! Nasapoti kikao endelevu kiwepo kuanzia kesho pale chimwaga....mpaka kieleweke jameni!
 
Well said my dear but I think it will be better to support them when it comes a time of missing to attend lecture due to this matter......the mass of udom student may help these lecturers to air out their complains against Vasco da Gama Gvts!


Waislam nchi hii ya Udom washakuwa kero kero! Kumbe hadi ninyi waalim mwapata shida? Nkajua sie wanafunzi tu bwana. Hlo la maprof kuondoka limetuathiri weng cuz wametuondolea prof Nwoye wetu! Sasa jamani kitumbo buku 2 per day afu migari yenyewe ile ka mapango ya panya inawezekana kweli? They are so unfair to u jamani! Wanakusanya hela za kampeni za ccm 2015 kwa migongo yenu? Mkiyakubali hayo bs mjue mmekwisha! Yeye mlacha, kikula na wengneo hayo magari SU wanalipia how much? Wao kwanza ndo wangetakiwa walipe house alowance cuz wana hela ndefu! Yaani ktk hayo mtakayosimamia kugoma, basi gomeni mpaka kieleweke, ikibidi wafunge mchuo wao bhana. Nimegundua nyie mnanyanyaswa hvo afu hasira mnatumalizia sisi kwa kutukong'oli SUP na makarai sio? NAWAOMBEA USHINDI, HAO PIMBI WAZEE WAONDOKE CUZ WASHAKUWA KERO!!
 
Wasomi wenzangu, je hamjui namna ya kufuatilia matatizo yenu kwa njia sahihi? Kwani migomo ndio inayotatua?. Mbona ni suala dogo tu?. Kama mnashida fulani mfano ya kifedha inavyoonekana sehemu kubwa ya mada yenu ya mgomo, ni vema mkatuma wawakilishi kuanzia ngazi ya idara kama mnayo and then faculty na baadae ngazi ya chuo na ikishindikana sehemu husika mfano hazina kama mnavyosema na sio kwa Mh. Pinda au sijui kuilaumu CCM sijui na kulaumu mtu binafsi kama Misilamu au Mkristo fulani au Mzanzibar ???????.

Mimi nawalaumu watu wanaoleta hoja za udini na ukabila na ukanda katika hili jambo...ukweli ni kuwa matatizo ya UDOM ni ya muda mrefu sana. Na wanatia aibu, ni chuo pekee cha umma ambacho kina migogoro ya wafanyakazi na menejimenti, tofauti na vyuo vingine vya umma ambavyo vina migogoro ya menejimeti na wanafunzi kwa kiasi kikubwa. Kuna tatizo la msingi UDOM.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Tukio hili kwanza limechochewa na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Balozi Mwapachu, wiki iliyopita kwenye baraza la chuo alimtukana Mwenyekiti wa jumuiya ya wahadhiri kwa kumuita Mugabe kwa sababu hataki kuitisha uchaguzi. Na akaamuru kikao kijacho asiingie kama uchaguzi hamna. [Tunaamini wana mpango wa kupandikiza mtu wao]

.....

2. Kwenye baraza la chuo, walitangaziwa Prof. Shaban Mlacha ameongezewa miaka minne na Raisi Jakaya Kikwete. Wahadhiri wanahoji mgomo wa mwaka jana,wa walimu na wanafunzi,waziri Mkuu Mizengo Pinda aliahidi atarudi kuja kutoa ufafanuzi hatua zilizofikiwa na serikali, hajarudi, wala ripoti ya tume alizounda haijatolewa, manunguniko ya wafanyakazi, na wanafunzi hayajafanyiwa kazi kabisa. Hili limesababisha wastani wa wafanyakazi watatu wakiwemo Prof. na madaktari huacha kazi kila mwezi. Kuanzia July 2011, hadi July 2012, jumla ya wafanyakazi 42 wameondoka chuo kwa sababu mbalimbali ikiwemo kuacha kazi (resignation). Mbaya zaidi kumekuwa na ulipizwaji kisasi wa hali ya juu. Wahadhiri wamefukuzwa sana kazi, na baadhi ya kesi zipo mahakamani. Kibaya zaidi imethibitika kikwete kawaongezea muda viongozi wote wa chuo. Prof. Kikula alistaafu 15 December 2012, ameongezewa nae mkataba, pamoja na lawama zote. Hili wamelichukulia kama Serikali haiwajibiki na imeonyesha dharau kubwa sana, lakini kibaya zaidi hili limechukuliwa kwenye taswira ya Udini, ambao umekuwa ukikitafuna chuo, kufikia hatua ya kuunda kamati ya kushughulikia suala hilo, ambayo pia inasemekana *ilivunjika bila mafanikio kabla hata ya kuanza kazi.

Ndugu mleta mada! Pole kwa kutumia muda mwingi kuandika hii habari kwenye ukurasa huu kwa faida ambayo mimi bado sijaijua bado, na kama wewe ulitumwa na hicho kikao uje hapa JF uelezee azimio hilo au la sijajua bado, kama ndivyo basi nina mashaka na uelewa wa wajumbe wa hicho kikao. Turudi kwenye point zako ulizotoa.

Kwanza kabisa umesema mwenyekiti wa baraza la chuo ALIMTUKANA KIONGOZI WA UDOMASA KWA KUMUITA MUGABE ,Hivi unataka kuaminisha wanajukwaa kuwa Mugabe ni tusi??, Je ni tusi la kabila gani, kwa maana ktk misamiati ya matusi ya Kiswahili halipo. Kama huyo kiongozi alichaguliwa na wajumbe, na muda wake umekwisha taratibu si zinasema uchaguzi unabidi ufanyike? Ni imani yangu kuwa katiba yenu inaelekeza hivyo, sasa kama hakuna maelezo yenye mantiki ya kwa nini hajaitisha uchaguzi huoni kuwa mwenyekiti wa baraza la chuo ana kila sababu ya kuhimiza hilo lifanyike?? Kwa nini aamini kuwa yeye ndiyo kiongozi pekee mwenye uwezo wa kuongoza hiyo jumuiya? Huoni kuwa hilo ni tatizo??? Unataka kuniambia kuwa hao wahadhiri watagoma kwa kuwa kiongozi wao kaitwa Mugabe????

Suala la chuo kuletewa pesa kidogo kutoka serikalini hivyo kulazimisha kufanya cost sharing. Hembu tuwe wazalendo jamani, hivi vitu tujaribu kuviown!. Sasa kama Chuo kinapokea hela kidogo kutoka serikalini, mnatarajia pesa ya kugharamia hizo huduma zitatoka wapi??. Wewe kama mwalimu umetumia elimu yako kwa kiasi gani kukiingizia chuo kipato. Mimi nafahamu kuwa mwalimu unatakiwa uandike miradi na ufanye consultancy cervices, ambazo malipo yake partly yanaingia chuoni na kiasi kidogo unapata wewe, sasa kweli university lecturer unakaa unataka kugoma kwa sababu ya kuondolewa sh 500?? Kwa sababu zinazojulikana. Hata kama hamjapenda hilo suala haliwezi kuwa linacall for mgomo, ni suala linalovumilika wakati majadiliano na njia nyingine za kulitatua zinaendelea.

Kama Mlacha na hao wenzake wameongezewa mkataba tatizo ni nini? Kwani tatizo ni dini yake au ni utendaji wake wewe hujaupenda? Je unafikiri akiletwa mkristo tatizo unaloliona kwa mlacha hutoliona tena, au akisha kuwa mkristo tayar wewe uko happy??. Na unatuambia kuwa kuendelea kwa uwepo wa mlacha na wenzake kumefanya maprof na ma Dr kuacha kazi, mimi ninawasiwasi na elimu za hao walioacha kazi kwa hizo sababu!! Au walitarajia wangeteuliwa wao? Huo utakuwa ni ubinafsi uliokithiri!

Hivi unataka kutuaminisha kuwa, waajiriwa wengi hapo udom ni waislam, na hao hao waislam kwa wingi wao ndo wameadhimia kwenye hicho kikao chenu kumuondoa mlacha kwa sababu kuna uislamu sana hapo mahali????. Unajua mimi nawashauri kama mnataka mfanikiwe kwenye mambo yenu ya msingi hili suala la Udini msilizungumze kabisa, kwa maana linawagawa ninyi kwa ninyi kuwa ktk makundi mawili yenye interest tofauti, tumieni elimu zenu vizur kupambanua mambo.

Suala la kupunjwa mishahara na kuchelewa kupanda vyeo ni jambo ambalo halihitaji mgomo, mnaweza kutumia majadiliano na uongozi wa chuo mkishirikiana na watu wa hazina ili muone kuwa tatizo ni Mlacha ndiye hataki mpandishwe vyeo au ni nini? Hi indo namna ya kutatua mambo. Unapokuwa na Mtazamo hasi dhidi ya mtu matokeo yake ndo haya.
 
Kwanza namshangaa mleta post kwa jambo moja, ameuunganisha mkutano wa UDOMASA uliofanyika jana na ajenda ambazo hazipo na wala hazikujadiliwa. Hakuna ajenda yoyote kuhusu ajira kuwa na upendeleo iliyojadiliwa, hakuna dini yoyote iliyotajwa kwenye kikao hicho, ni kibaya zaidi jana hoja nyingi zilizokuwa zikijadiliwa ni kuhusu UBOVU wa elimu ya UDOM ambayo inasababishia kiitwe CHUO CHA KATA au A WARD UNIVERSITY. Na malalamiko makubwa yalikuwa ni juu ya upungufu wa nyenzo za kufundishia, kiasi kwamba wanafunzi wanachangishana kununua betri kwa ajili ya Microphone. Hakuna mtu mwenye akili timamu asiyekubali kuwa UDOM kuna tatizo, mfano mgomo wa mwaka jana wa wahadhiri na wanafunzi ulionyesha hilo. Ni taasisi gani ya UMMA ambayo mtu anaajiriwa bila kupewa pesa ya kujikimu? Baada ya mgomo ule watumishi wote wa UDOM kuanzia messenger mpaka VC mwenyewe walipewa zile pesa, tena bila kujali DINI zao.

Ukweli ni kuwa, hakuna hata siku moja ambapo wahadhiri au wafanyakazi wa UDOM wamewai kulalamika kama jumuiya kuwa kuna DINI FULANI imejaza watumishi wa UDOM. Hii imekuwa ni maono ya wahadhiri au wafanyakazi mmoja mmoja na sio jumuiya. Na kwahiyo mleta post kaleta hoja hii kwa namna ambavyo imeongezewa mambo yasiyo ya jumuiya yaani UDOMASA isipokuwa ni mawazo yake binafsi. Ni wakati watanzania tukafahamu kuwa, hii nchi inaelekea pabaya, kinapoinuka kundi au jamii fulani kudai haki zao, ni lazima kitafutwe kitu cha kuua nguvu yao na umoja wao. Mfano; Waislamu walipoanza kudai haki zao wanazodhani kuwa ni muhimu, Serikali ilisema PONDA sio raia na anakikundi kinachoendesha vurugu. Madaktari na walimu waliambiwa ni wanasiasa ndio wanachochea. Huu ni uzandiki na ushetani mkubwa!!!!

Naomba mleta post uwe makini na hoja hii maana imeleta michango isiyokuwa sahihi na umewachafua wahadhiri wa UDOM kuwa ni wadini wakati si kweli. Katika AJENDA za kikao kile cha mwaka kulikuwa hakuna hoja yoyote inayohusiana na UDINI. Wala malalamiko ya UDINI, cha kushangaza aliyelalamikiwa sana jana ni DVC-ARC Prof. Kinabo ambaye ni MKRISTO tena MKATOLIKI kweli kweli. Maana yeye ndie mlezi wa WAHADHIRI lakini aonyeshi msaada wa kuboresha elimu ya UDOM.


WATANZANIA WOTE NI NDUGU, ILA KUNA WACHACHE WANATUCHANGANYA.
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WABARIKI WAKRISTO KWA WAISLAMU.
 
wanagoma nn wakati walishkubali kuwa sehemu ya kitengo cha propaganda cha ccm?
 
Ndugu mleta mada! Pole kwa kutumia muda mwingi kuandika hii habari kwenye ukurasa huu kwa faida ambayo mimi bado sijaijua bado, na kama wewe ulitumwa na hicho kikao uje hapa JF uelezee azimio hilo au la sijajua bado, kama ndivyo basi nina mashaka na uelewa wa wajumbe wa hicho kikao. Turudi kwenye point zako ulizotoa.

Kwanza kabisa umesema mwenyekiti wa baraza la chuo ALIMTUKANA KIONGOZI WA UDOMASA KWA KUMUITA MUGABE ,Hivi unataka kuaminisha wanajukwaa kuwa Mugabe ni tusi??, Je ni tusi la kabila gani, kwa maana ktk misamiati ya matusi ya Kiswahili halipo. Kama huyo kiongozi alichaguliwa na wajumbe, na muda wake umekwisha taratibu si zinasema uchaguzi unabidi ufanyike? Ni imani yangu kuwa katiba yenu inaelekeza hivyo, sasa kama hakuna maelezo yenye mantiki ya kwa nini hajaitisha uchaguzi huoni kuwa mwenyekiti wa baraza la chuo ana kila sababu ya kuhimiza hilo lifanyike?? Kwa nini aamini kuwa yeye ndiyo kiongozi pekee mwenye uwezo wa kuongoza hiyo jumuiya? Huoni kuwa hilo ni tatizo??? Unataka kuniambia kuwa hao wahadhiri watagoma kwa kuwa kiongozi wao kaitwa Mugabe????

Suala la chuo kuletewa pesa kidogo kutoka serikalini hivyo kulazimisha kufanya cost sharing. Hembu tuwe wazalendo jamani, hivi vitu tujaribu kuviown!. Sasa kama Chuo kinapokea hela kidogo kutoka serikalini, mnatarajia pesa ya kugharamia hizo huduma zitatoka wapi??. Wewe kama mwalimu umetumia elimu yako kwa kiasi gani kukiingizia chuo kipato. Mimi nafahamu kuwa mwalimu unatakiwa uandike miradi na ufanye consultancy cervices, ambazo malipo yake partly yanaingia chuoni na kiasi kidogo unapata wewe, sasa kweli university lecturer unakaa unataka kugoma kwa sababu ya kuondolewa sh 500?? Kwa sababu zinazojulikana. Hata kama hamjapenda hilo suala haliwezi kuwa linacall for mgomo, ni suala linalovumilika wakati majadiliano na njia nyingine za kulitatua zinaendelea.
Kama Mlacha na hao wenzake wameongezewa mkataba tatizo ni nini? Kwani tatizo ni dini yake au ni utendaji wake wewe hujaupenda? Je unafikiri akiletwa mkristo tatizo unaloliona kwa mlacha hutoliona tena, au akisha kuwa mkristo tayar wewe uko happy??. Na unatuambia kuwa kuendelea kwa uwepo wa mlacha na wenzake kumefanya maprof na ma Dr kuacha kazi, mimi ninawasiwasi na elimu za hao walioacha kazi kwa hizo sababu!! Au walitarajia wangeteuliwa wao? Huo utakuwa ni ubinafsi uliokithiri!

Hivi unataka kutuaminisha kuwa, waajiriwa wengi hapo udom ni waislam, na hao hao waislam kwa wingi wao ndo wameadhimia kwenye hicho kikao chenu kumuondoa mlacha kwa sababu kuna uislamu sana hapo mahali????. Unajua mimi nawashauri kama mnataka mfanikiwe kwenye mambo yenu ya msingi hili suala la Udini msilizungumze kabisa, kwa maana linawagawa ninyi kwa ninyi kuwa ktk makundi mawili yenye interest tofauti, tumieni elimu zenu vizur kupambanua mambo.

Suala la kupunjwa mishahara na kuchelewa kupanda vyeo ni jambo ambalo halihitaji mgomo, mnaweza kutumia majadiliano na uongozi wa chuo mkishirikiana na watu wa hazina ili muone kuwa tatizo ni Mlacha ndiye hataki mpandishwe vyeo au ni nini? Hi indo namna ya kutatua mambo. Unapokuwa na Mtazamo hasi dhidi ya mtu matokeo yake ndo haya.

umejaribu kujengo hoja mbazo zina sound kwa kiasi fulani lakini sidhani kama umemwelewa mwenye uzi! Kama madai yao siyo ya leo au jana na mpaka PM aliwapromis kusolve matatizo yao na nothing has done then what is solution?
 
Wahadhiri,

Na hii ya kuomba ruhusa ikulu ukitaka kwenda ku-present paper Kenya hamjaona inaleta ugumu kimaendeleo ya taaluma?
 
Nawajua vizuri wasomi hawa,huwa wanasimamia vyema haki zao,nakumbuka support mliyotupa wakati tunadai haki zetu
 
Malalamiko hapo juu hayana uhusiano wowote na dini ya watu. Huyo Prof. Kikula ametumikia kama Director IRA pale UDSM, akaenda ARU/UCLAS kama Principal mbona hajawahi kulalamikiwa kuwa ni mwislamu? hata Juma Mwabachu ana CV kubwa sana lakini kwa sababu tu amekuja UDOM basi ni mwislam. JAMANI ACHENI HIZO BIASNESS ZA UDINI, unless una evidency ya jambo lililofanyika la udini - mwandishi unapotosha umma.

hizo nafasi za juu kuna akina Mkapa, mbona hawatajwi? DVC academic ambaye anaajiri waalimu ni mkristo mbona hatajwi? acheni KUPOTOSHA jamani. unataka kusema kuna mwalimu alishindwa kuajiriwa akiwa na sifa kwa sababu ni mkristo?

Ndugu huo udini uanaweza usitoke moyoni mwao moja kwa moja, kinachowafanya wawe hivyo ni yule wanayemtumikia, maagizo yote yanatoka kwake, tofautisha na walipokuwa katika institutions nyingine. Ikiendelea hivi wanafunzi wa UDOM wataanza kupiga tution
 
Mi nilidhani ukiwa Muadhiri tayri ni great thinker, but sidhani kama kuna great thinker yeyote hapa duniani anayeweza kuamini ahadi za Mizengo Pinda, huyu jamaa huwa anaongea tu na huwa hakumbuki tena alichoongea na hanaga mipango ya utekelezaji. Kama Wahadhiri mmeshindwa kujua kuwa Pinda ni msanii nina mashaka na elimu mnayowapa watoto zetu, Liwalo na Liwe...

I know Dr Ahmed Ame, is one of the best statistics lecturers in eastern and central africa, kumbe ni MUISLAM eehh, i did'nt know his religious views.
 
I think watu walio nje ya udom wanaweza kujudge vyovyote wapendavyo bt ambao wamevivaa viatu wanajua vinapoumiza! Waislam kuwepo udom sio shida...tatizo qualification zao hasa hao malecturer wa kizenji! Wako shalow ktk ufundishaji, hawana confidence yaani wanaboronga mbaya! Nasapoti kikao endelevu kiwepo kuanzia kesho pale chimwaga....mpaka kieleweke jameni!

Hapo mzee sina uhakika na maneno yako. Mimi nawajua walimu kadhaa walioajiriwa UDOM, sio wazanzibari wala waislamu, ambao uelewa wao ni finyu sana. Wengine wamesona SUA miaka mitatu, hawajawahi kusimama mbele ya darasa hata kujibu swali! Leo ni walimu. Wameshindwa interview sehemu nyingi za kawaida, wamepata UDOM na ni "LECTURERS". Wenyewe wanaona hata aibu ukikutana nao wanaposema wao wapo UDOM hawataji kazi gani.

Tukubaliane kuwa UDOM kuna standard nyingine ya kuajiri walimu. Sio zile za vyuo vingine TZ.

Lakini, Tanzania tumezoea kutengeneza viwango vyetu na kuviita "vya kimataifa". Soko la Kibaigwa, Uwanja wa ndege wa Mwanza, Songwe, vyote ni vya kimataifa! Hata kufaulu kwenda FOrm I bila kujua kusoma na kuandika ni elimu ya kimataifa.

Tulishaharibu Vyuo vyetu vizuri kwa minajili ya siasa. Vyuo vyote mazingira ya kusoma yamekufa! Hakuna maabara, maktaba bado zinatumia card kutafuta jounal ya mwaka 1985!

Kweli tutafika? Msiwalaumu UDOM, hata huko kwingine nako kumekufa.
 
Back
Top Bottom