Mgomo wa Simu Utafeli...

Mgomo wa Simu Utafeli...

Mimi mpaka saa hizi lain zangu zote nimeshatia mfukoni! kuna line moja ambayo siipendi ndo ninayotumia saa hii.
 
hii hoja iliwasilishwa na mnyika kuanzia katika ngazi ya kamati hadi bungeni lakini si unajua ccm wasipotaka jambo lipite kwa kuwa wao ni wengi wanapitisha kwa kupiga kura. option unayobaki nayo inakuwa ni kuwaambia wananchi juhudi ulizofanya na wapi ulikwama. ndicho mnyika alichofanya sasa ulitarajia afanye nn zaidi

Siku sheria ya kodi inajadiliwa wabunge wetu walikuwa msibani Arusha, Hata waziri kivuri wa Fedha hotuba yake haikusommwa na benge likaendelea
 
Mwanzisha uzi ni moja kati ya magamba yanayovuliwa na kuishia kiunoni

Habari zilizoingia hivi punde kutoka Lindi na Mtwara zinaeleza kuwa watu wako hewani wakiendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa kama kawaida.

Mgomo UMEFELI...
 
Habari zilizoingia hivi punde kutoka Lindi na Mtwara zinaeleza kuwa watu wako hewani wakiendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa kama kawaida.

Mgomo UMEFELI...

taarifa kutoka kanda ya ziwa watu wakohewani24hrs
 
taarifa kutoka kanda ya ziwa watu wakohewani24hrs

Habari zilizoingia muda huu kutoka visiwani Unguja na Pemba zinasema mfungo wa Ramadhan unaendelea vizuri na watu wako hewani kama kawaida.

Mgomo UMEFELI...
 
Tusikubali uchochezi watanzania wenzangu kwamaana taifa letu lina potezwa na watu wachache wanaotaka madaraka kwa manufaa yao binafsi.
 
abbas mwaki, hivi unajua maana halisi ya neno uchochezi au wewe ni mmojawapo wa wale tunaowaita Bendera Fuata Upepo?

Kama hujui kitu fulani bora uulize kuliko kukurupuka kama nyau aliyetimuliwa akiiba mboga jikoni.

Enzi za Apartheid nchini Afrika Kusini makaburu walikiita chama cha ukombozi ANC kuwa cha kigaidi na kumkamata kiongozi wake Nelson Mandela kwa makosa lukuki, mojawapo likiwemo uchochezi.

Wadai haki wakaitwa magaidi na wachochezi. Mandela akaishi gerezani miaka 27 ambako aliandika kitabu Long Walk to Freedom.

Hatimaye Mandela, mchochezi na gaidi aliachiwa huru, huku watawala makaburu wakiwa wamejawa hofu kubwa ya Mungu.

Wananchi walitoa tamko kwamba iwapo Mandela angefia gerezani kutokana na hali yake kuwa mbaya kiafya, basi wangemwaga damu yao wazalendo na makaburu hadi bahari igeuke nyekundu.

Walisema: Tumefikia ukomo wa uvumilivu. Tumechoka. Imetosha. Mwachieni Madiba wetu la sivyo tutawanchinja ninyi wote na vizazi vyenu vyote, popote mtakapokimbilia.

Kuliko kuchinjwa kama kuku, makaburu wakaogopa na kumwachia Madiba, gaidi, mchochezi, mpigania haki na KIONGOZI SHUPAVU.

Mandela hakuwa mpenda madaraka kwa hiyo kilipokwisha kipindi chake cha kuwa rais wa kwanza mzalendo aliachia ngazi ili wengine waiongoze nchi hiyo. Alibembelezwa sana kubaki madarakani lakini alisema atabaki kuwa mshauri wa chama. Aliacha shughuli zote za siasa.

Unapotuambia tusiwasikilize wachochezi, unamaanisha nini? Hivi unafikiria kabla ya kutoa matamshi yako?

Hebu jifunze kufikiria. Jifunze historia. Nakushauri ukitafute kitabu cha Mandela ukisome. Utajifunza mengi.

Walevi wa madaraka daima huwaona wanaodai haki yao kuwa wachochezi.

Vijana amkeni. Mbona mnalala wakati kumekucha?
 
Last edited by a moderator:
lakini my beloved gloria si bunge ndo limepitisha jamani?

Tatizo hapa wanataka litenguliwe bila kufuata process za kibunge na mambo hayaendeshi kwa amri za kutoka kwenye viblog au harakati za mmarekani mtanzania...kama ilishapitishwa na bunge si inabidi bunge ndo litengue,hivi hata rais anawezaje kutengua hapo?.
Wakati watu hapa wanazima simu na kurudi kuwasiliana kwa sanduku la posta,mwanakijiji akiwa amerika ataendelea kujinafasi kwa mawasiliano kwa raha zake.mimi sizimi ng'o.

Sasa hiyo kodi imepitishwa na bunge lakini hamna proper mechanism ya kukusanya hiyo kodi maana haijulikani wanakata hela yote kwa mkupuo au kidogo kidogo..pili napata picha hujui hata principles za taxation huwezi kata kodi tajiri ma masiki kiwango kimoja daah sijui wewe jamaa ni mtu wa namna gani..soma canons of taxations halafu utajua..pili ili kuenforce hicho kitu unahitajika mtambo wa kumonitor simu zilizo online ambao ni wa cost kubwa sasa nashangaa mtu hujui principles hata kwenye google zipo kazi tu kushadadia vitu..
 
Mgomo mbona umeishaanza ndugu kuna watu tulikuwa na line kwenye moderm na zingine tunazo kwenye simu lakini kwa sasa iwe kwenye moderm au simu natumia laini moja tu ya kwenye simu na katika mitandao nimebakiza laini hiyo hiyo ndiyo ninayoiongezea salio, kwa hiyo kwa ujinga huu wa Serikali wajue kabisa baadhi ya mitandao hususani Zantel na Tigo itafilisika na sijui watapata wapi hizo kodi.
 
Naona wazee wa Sembe mnangangania kututoa kwenye mawazo ya sembe!
 
Zaidi ya robo tatu ya watanzania hawajui JF ni nini, hawamjui mnyika ni mtu gani na huyo mwanakijiji hawajui ni kitu gani? Hata huo mgomo uliotangazwa humu JF haelewi kitu na walioona FB walilaani. Mbaya zaidi walituambia ni leo, jion wananitumia sms eti kesho. Hapa hakuna kitu wala mgomo. Ni unafiki tu wa baadhi ya watu wanaojiita wanaharakati kumbe pumba tupuu
 
Zaidi ya robo tatu ya watanzania hawajui JF ni nini, hawamjui mnyika ni mtu gani na huyo mwanakijiji hawajui ni kitu gani? Hata huo mgomo uliotangazwa humu JF haelewi kitu na walioona FB walilaani. Mbaya zaidi walituambia ni leo, jion wananitumia sms eti kesho. Hapa hakuna kitu wala mgomo. Ni unafiki tu wa baadhi ya watu wanaojiita wanaharakati kumbe pumba tupuu

Tumepata ujumbe toka Katavi kuwa mgomom huu hawana taarifa yake na wala hawaoni mantiki yake...
 
Sasa mwanakijiji anaficha wapi uso?
Lakini na sikia huo mgomo utakuwa ni kwa zamu kwa smkard,sasa sijui anajuaje kuwa watu wana smkadi zaidi ya moja,wakati hiyo fasheni ilishaisha baada ya malipo kuwa sawa kwa mitandao yote,sikuhizi watu wengi wamebaki na laini moja,labda kwa wale wenye simu za double laini,ambao nao sio kuwa wanatumia laini zote kila siku.kwa ufupi hakuna mgomo wa kupiga simu.
 
Tumepata ujumbe toka Katavi kuwa mgomom huu hawana taarifa yake na wala hawaoni mantiki yake...

Wengine hawajui hata kama kuna tozo ya buku. Wakikusikia unasema watoe line hawakuelewi. Kwanza ni ujinga kumfuata mwanakijij aliyeko marekani akishirikiana na wamarekani kutunyonya.
 
Back
Top Bottom