Mgomo mkubwa wanukia nchini

Mgomo mkubwa wanukia nchini

mkwereeeeeee mambo yake valuvalu. Magufuli kazi anayo[/QUOTE

Mkwereeeee anaweweseka haamini kuwa andio anahama magogoni baada ya wiki; angekuwa na akili angeisha hamia kijijini!! Haamini na ndio maana bado hajafunga vilago vyake!!
 
Utashangaa bado kuna wafanyakazi wa serikali wanaoiunga mkono CCM licha ya kupuuzwa kwa kiwango hiki!

Mkuu Ndiyo Wale Mkapa Aliowaita MALOFA NA WAPUMBAVU. Hakututukana Sisi Tunaojitambua Na Kutaka Mabadiliko, Aliwatukana Wale Ambao Wamenyimwa Haki Zao, Lakini Bado Wanaishabikia CCM.
 
CCM mshauri wao ni kipofu.Hivi utalipaje sasa wakati inaonekana kwamba hii ni hongo ya wazi.Kwa kuwa ni haki yenu,waalimu wekeni hela hiyo mfukoni,ila tarehe 25 kura UKAWA.

Kumbe wana hela ni kuto jali tu.
Baada ya "Serikali" ya CCM kuamua "kulipa madai" ya walimu huku wakiwabagua wai wa ka nyingine (madaktari, manesi, polisi, watumishi wa serikali za mitaa, wanajeshi, askari magereza, na baadhi ya walimu) watumishi hao wameonyesha kukerwa na kukatishwa tamaa na kitendo hicho cha kibaguzi. Aidha, watumishi hao wanashangaa kwanini malipo hayo yamefanyika KISIASA katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi ilhali siku zote wamekuwa wakiambiwa hakuna pesa.

Pamoja na hayo, sio walimu wote waliolipwa kwani madai ya baadhi yao yalitupwa kwa kisingizio kwamba hayasomeki vizuri baada ya kupigwa photocopy kwa muda mrefu. "Imagine kuna walimu hawajalipwa madai yao tangu mwaka 1980 hadi wino umefutika kutoka kwenye nyaraka zao halafu wanaachwa bila kulipwa eti nyaraka zao hazisomeki, hii ni haki kweli?!", alisikika akilalamika mwalimu mmoja.

MAONI YANGU
Hili suala la CCM kuwalipa walimu peke yao kwa kisingizio cha wingi wao (kura nyingi) ndicho kitanzi chao mwaka huu. Hii mbinu ni ya kizamani mno.

:yield:
 
Wanajamvi tusiwe watu wakuambiwa kila kitu tukadhani ni sawa,kweli walimu wanadai lakini Mwalimu mmoja kudai shs millioni 500 hapo kuna walakini.

kuna mwalimu mmoja alikuwa akidai malimbikizo ya tsh milioni 500 lakini serikali sikivu ya CCM ikamchakachua (kwa kumfichia baadhi ya nyaraka) na kuishia kumlipa tsh milioni 50 tu!
 
Kwanza malipo yenyewe hayajafanyika icpokuwa ni mkwara wa kisiasa tu ..
 
nimesoma kwenye bandiko sijaona chochote kuhusu huo mgomo zaidi ya matamanio yako.
nimeshindwa haswa kuelewa mantiki ya title yako. punguza panic mkuu.

Baada ya "Serikali" ya CCM kuamua "kulipa madai" ya walimu huku wakiwabagua watumishi wa kada nyingine (madaktari, manesi, polisi, watumishi wa serikali za mitaa, wanajeshi, askari magereza, na baadhi ya walimu) watumishi hao wameonyesha kukerwa na kukatishwa tamaa na kitendo hicho cha kibaguzi. Aidha, watumishi hao wanashangaa kwanini malipo hayo yamefanyika KISIASA katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi ilhali siku zote wamekuwa wakiambiwa hakuna pesa.

Pamoja na hayo, sio walimu wote waliolipwa kwani madai ya baadhi yao yalitupwa kwa kisingizio kwamba hayasomeki vizuri baada ya kupigwa photocopy kwa muda mrefu. "Imagine kuna walimu hawajalipwa madai yao tangu mwaka 1980 hadi wino umefutika kutoka kwenye nyaraka zao halafu wanaachwa bila kulipwa eti nyaraka zao hazisomeki, hii ni haki kweli?!", alisikika akilalamika mwalimu mmoja.

MAONI YANGU
Hili suala la CCM kuwalipa walimu peke yao kwa kisingizio cha wingi wao (kura nyingi) ndicho kitanzi chao mwaka huu. Hii mbinu ni ya kizamani mno.

:yield:
 
Wazee wa jumuia ya Aftika Mashariki nao pia walipwe haki zao.Kuna kufa wajameni viongozi na sijui mutasema nini mbele ya Mola wenu kuhusu hii dhulima munayowafanyia wazee wa EAC.
 
acha uchochezi wewe...Tanzania ni nchi ya amani.

kwanini unasema hivyo mkuu? amani yake inatokana na wananchi kukaa kimya kila wanapodhulumiwa na serikali ya CCM?
 
Ni aibu na fedheha kubwa kwa mfanyakazi wa Tz.kuipigia maficcm kura! kodi tunalipa 11% wala hawatuhurumii, wabunge hawalipi kodi kabisa! Tuachane na maficcm tufanye mabadilko tupate AHUENI, chagua LOWASA ewe mfanyakazi.

mkuu, kodi ya mishahara ni 18% sio 11%. yaani haya mafisiemu ni nyoka kabisa.
 
Back
Top Bottom