Hao walimu waliolipwa ni wa wapi...? Mbona mimi sijalipwa??
utaratibu gani? utaratibu wa kuwakusanya walimu na "kuwalipa" kipindi cha uchaguzi? kwanini madaktari na manesi hawajalipwa madai yao wala kuongezwa mishahara kama mlivyokubaliana kabla ya kujaribu kumuua dr ulimboka? hebu tuambie utaratibu huo ukoje.
Mwalimu gani kalipwa wewe boya?
Hv ni walimu gani wamelipwa?Tangazo limetoka kwamba wataanza kulipa malimbikizo ya wafanyakazi kuanzia October na kukamilishwa November.Fahamu kuwa haki za watumishi zıko palepale,ashnde Lowasa au Magufuri ama hata aendelee Kikwete.Na hawa hawalipwi na mtu binafsi kwa hela zake bali kodi za Watanzania.
Walimu wanajitambua sana kwa taarifa yako. Hao vijana kuamka kisiasa namna hii walianzia madarasani kwa walimu!na haohao walimu wanaopuuzwa kila siku ndio wanamuita JK "shemeji". kipindi walimu wakianza kujitambua ndipo ukombozi wa nchi hii utakapopatikana.
Walimu ndio wenye malimbikizoBaada ya "Serikali" ya CCM kuamua "kulipa madai" ya walimu huku wakiwabagua watumishi wa kada nyingine (madaktari, manesi, polisi, watumishi wa serikali za mitaa, wanajeshi, askari magereza, na baadhi ya walimu) watumishi hao wameonyesha kukerwa na kukatishwa tamaa na kitendo hicho cha kibaguzi. Aidha, watumishi hao wanashangaa kwanini malipo hayo yamefanyika KISIASA katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi ilhali siku zote wamekuwa wakiambiwa hakuna pesa.
Pamoja na hayo, sio walimu wote waliolipwa kwani madai ya baadhi yao yalitupwa kwa kisingizio kwamba hayasomeki vizuri baada ya kupigwa photocopy kwa muda mrefu. "Imagine kuna walimu hawajalipwa madai yao tangu mwaka 1980 hadi wino umefutika kutoka kwenye nyaraka zao halafu wanaachwa bila kulipwa eti nyaraka zao hazisomeki, hii ni haki kweli?!", alisikika akilalamika mwalimu mmoja.
MAONI YANGU
Hili suala la CCM kuwalipa walimu peke yao kwa kisingizio cha wingi wao (kura nyingi) ndicho kitanzi chao mwaka huu. Hii mbinu ni ya kizamani mno.
:yield:
Nani kakwambia majeshi yanamigomo?
acha uchochezi wewe...Tanzania ni nchi ya amani.
Nani kakwambia majeshi yanamigomo?