Mgogoro ndani ya CHADEMA!?

Na bado! Zitto vipi mbona hajasusa?

mkuu jamani tusameheni, mmetushika pabaya mpaka juzi tukawatuma usalama wa taifa wachomoe cable ya satellite ya TBC ili watanzania wasishuhudie upuuzi tunaoufanya bungeni kwa kujaribu kupindisha kanuni ya 77 ya bunge.
Mmetushika babaya mpaka tukatuma vijana waende kurusha mawe kwenye mkutano wenu huko singida hadi kijana wetu mmoja akafa.
Mmetushika pabaya mpaka tumeamua kumchinja kiongozi wenu wa chama huko arumeru
Mmetutushika pabaya mpaka tumewakata kwa mapanga wabunge wenu pale ilemela.
Mmetushika pabaya mpaka tumetuma vijana wetu wavamie na mapanga kwenye mkutano wenu pale nduli.
Jamani mkuu mmesababisha tumechanganyikiwa kwa hili vuguvugu lenu la mabadiliko.
Tusameheni jamani.
:A S cry:
 
Kuna watu wanatamani CHADEMA kuwe na mgogoro kwa hali na mali.
Hivi sehemu kama kuna mgogoro si inajulikana tu! kuna haja ya kufosi watu?
 
Kuna watu wanatamani CHADEMA kuwe na mgogoro kwa hali na mali.
Hivi sehemu kama kuna mgogoro si inajulikana tu! kuna haja ya kufosi watu?

Kupandikiza mgogoro CDM ndiyo njia pekee itakayowahakikishia CCM kubakia madarakani mpaka 2020! Hata Mungu hawezi ruhusu hiyo, Watanzania wameteseka sana.
 



Umekaa tu na Ndg zako,na ama jopo lako mkaanzisha thread hii ama?
Umetoa wapi maneno haya yasiyo na mbele wala nyuma?
Kweli watu wengine wakishakuwa WATUMWA basi wanapoteza hata dira ya uwepo wao ktk jamii!

Ila inaweza ikawa si kosa lako,"MSAFARA WA MAMBA HAKIKA KENGE WAMO" Pole!

Acha kutumika Kijana kalale!!
 



NINGEKUWA NAIONA KITUFE CHA "like" NINGE ELIKE HII POST MARA KADHA!

Pamoja sana DM!
 
​kwa uzushi hatuwawezi mna madiploma hayo ndio maana mnaishia kukodi bodaboda kwenye mikutano yenu ha hahaha
Ukiwashika patamu magwanda tazama wanavyoporomosha matusi! kwi kwi kwi teh teh teh!
 
Ovyo! Sikuwa nikifahamu kwamba kuwa mwanachama wa CCM ni kuwa na tabia za fisi ambaye hachoki kufuatia nyuma ya binadamu anayetembea kwa matumaini ya eti mikono inayoning'inia huenda ikadondoka ajipatie kitoweo! Ama kweli mmeshikwa pabaya na mnahangaika kujinasua na bado maana sasa mmeashikwa kwa kabari ya mikono; itakuwaje watapabowashika kwa prize?
 


Hapa ndugu yangu naona umetumia neno mgogoro vibaya, hapo hakuna mgogoro hayo ni mambo ambayo yametokea na watu wanatafuta namna ya kuayamaliza siyo mgogoro hata kidogo, na hii ndiyo siasa inavyokwenda. Mnyika kateleza basi anaambiwa hivi sivyo, kwa upande wa Zitto alichokifanya siyo kigeni, kama mbowe alimtumia ujumbe ni katika kumwambia tu tumeona unakosimamia na inajulikana wazi. Zitto anayo hiyo historia ya misimamo ya hivyo hajaanza leo na anjua mwenyewe anachokifanya.
 
Hizi thread za kimbea huwezi kuwa kosa ritz rejao na zomba kwa mfano ile thread ya ndoa ya slaa walikesha hapo lakini nyingine hawatii team hasahasa rejao
 
Hizi thread za kimbea huwezi kuwa kosa ritz rejao na zomba kwa mfano ile thread ya ndoa ya slaa walikesha hapo lakini nyingine hawatii team hasahasa rejao
Hivi, mbona huyu Ritz sijamwona kwenye ile thread inayozungumzia jinsi Riziwani anavyojilimbikizia mali Tanzania kote?
 
Hii ni Propaganda maalum..mara mbowe ni kibaraka.,mara ndoa ya Dr slaa- ila kila singo mnayotaka kuipigia promo dhidi ya cdm inaskrach..
 
Yaani mleta hoja hapo kwenye CHADEMA ungeweka CCM watu wote wangekuunga mkono lakini ukishaiongelea CDM tu tegemea matusi hata kama ukiweka vyanzo vya kuaminika.Hili si jukwaa huru tena bali ni jukwaa la kukisifia chama.Hili linanikera sana,binafsi sina chama maana kwangu siasa za bongo ni za waganga njaa tu lakini kama tunaongelea siasa jamani tukubali na kukosolewa au vinginevyo yaanzishwe majukwaa ya vyama kimoja kimoja ndani ya Jamiiforum kwamba nikiingia jukwaa la CCM nikaisema vibaya nitukanwe na vivi hivyo kwa CDM.
 

Hapo kwenye red, anzisha hilo jukwaa la mabwepande uone kama kutakuwa tofauti na hili. labda muweke mtambo wa kuchakachua post za watu kama mlivyofanya kwenye sms za mchemba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…