kbmk
JF-Expert Member
- Feb 22, 2013
- 776
- 158
Kweli kabisa mmmh
Siasa kazi!
Siasa kazi!
Kazi Ya Dr.Slaa Imetukuka,hata CCM Wanajua Hilo.Msindai Anakijua Chama?Acha Uzushi,apewe Hon.J Mnyika
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
Kwa siku kadhaa ndani ya mitandao ya kijamii wamachama wa chama cha mapinduzi (CCM) wamekuwa wakilitumia jina langu kwamba eti wamenishawishi kujiunga na chama chao na kuwa siku ya jumapili tarehe 23/08/2015 nitajiunga na chama chao, katika uzinduzi wa kampeni zao
WALIYOYAFANYA.
1. Ni kweli na dhahiri kwamba CCM wamenishawishi kwa fedha na vyeo ili nijiunge na chama chao.
2. Wamewatuma wazee wengi sana kuja kunishawishi akiwemo katibu mkuu wao, mkuu wa usalama wa taifa, wazee wa chama chao nk.
MASWALI YA KUJIULIZA.
1. Kwa nini CCM wananifuata wakati huu na sio wakati mwingine?
2. Je, mbona mwaka 1995 walinitusi sana nilipoamua kuhama CCM, hali kadhalika mwaka 2010?
3. Je, sio kwamba CCM maji ya shingo yamewafikia?
4. Je, kwa nini wananiahidi vyeo vikubwa na mapesa mengi wakati huu na sio wakati mwingine kama wao walitambua kwamba nilistahili kuyapata hayo miaka iliyopita?
TAHADHARI.
1. Kwa hatua hiyo ni kwamba CCM wanatambua kwamba wamepoteza mvuto kwa wananchi hivyo hatuna budi kuyatafuta mabadiliko nje ya CCM.
2. Sina mpango wala sifikirii kukihama chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) chini ya mwavuli wa UKAWA.
3. Baada ya CCM kuyaona mafuriko ya ukawa sasa wamegundua kwamba kuelekea uzinduzi wa kampeni zao walitumie jina langu ili angalau wapate watu wengi kwa sababu wanaelewa fika kwamba wamepoteza mvuto (MSIDANGANYIKE).
4. Siwezi kuyasaliti matumaini ya watanzania kwa maslahi yangu binafsi.
5. Hilo ndio goli la mkono wanalolisubiri kwa miujiza (Yesu atakapokuja kwa mara ya pili).
MWISHO.
Nawatakia kila la kheri katika kuyatafuta mabadiliko nje ya CCM, daima tusife moyo tupo pamoja na tutashinda kwa nguvu ya umma.
Wenu katika ukombozi,
Dr. Wilbrod Slaa,
KATIBU MKUU, CHADEMA.
CCM km waliinvest kwa mama wa kihaya Basi wajue Dr. kwa sasa anahitaji malizia honey moon na pengine tutakuwa na mdogo wetu very soon..Naamini baada ya CCM kufa Dr. atarudi gombea nafasi aliyoiachia muda huu.
Zipo taarifa kwamba lowassa amependekeza nafasi ya Dr.Slaa kama katibu mkuu wa chadema ijazwe na aliyekua mwenyekiti wa ccm mkoa wa singida comrade Mgana Msindai (pichani).Kama taarifa hizi ni za kweli,unadhani mzee msindai anao uwezo wa kuvivaa viatu vya slaa na vikamtosha???kama hapana unadhani ni nani anaefaa kumrithi Dr.slaa ambae hakuna dalili zinazoashiria kama atarejea ofisini mapema.
![]()
MGANA MSINDAI
HIvi nyie ndio wale ambao bado mnaamini Busha ni barka na busara kubwa eh?Sasa akitokezea baada ya uchaguzi atakuwa na madhara gani tena au faida gani kwa CCM?atakuja ifufua CCM?Damn ..akili za mgagaa na pwani hazitoshi...Haha mkuu naona unaota ndoto. Dr Slaa hawezi kurudi huko kwenu tena. Ila tunachojua anasubiri uchaguzi uishe na awe salama na familia yake baada ya kumtishia. Akiibuka atakuwa na mengi ya kusema. We either ni delusional au a total fanatic, lakini Dr Slaa is out. Na wale wote wenye akili kidogo wameshapotea .. yu wapi Halima Mdee? John Mnyika? Tundu Lissu? Wanewekwa pembeni au wamekaa pembeni? Mbona jana hawakuwepo kumpokea Sumaye?
Pengine utusaidie CCM B imekuwaje na Nguvu kuliko A?Ukawa imegeuka ccm b mbowe kaamua kuuza upinzani
NIamini kipi kwamba Lowasa anaumwa sana au Lowasa ndie anaongoza indirectly..pengine kipimo ch akupima km mpo sawa nikuulize tuu km ..Unaamini nini Kuhusu Busha?kama Lowasa ameweza kuvivaa indirectly atashindwaje Msindai , hoja sio unanini kichwani bali unanini mfukoni
slaa sio muungwana,kwanini hakubaliani na wenzake,siasa za slaa za kutaja wezi ,bila kueleza yeye atafanya nini zimepitwa na wakati.aondokee tuHizi taarifa kama ni za kweli....hii itakuwa sio habari njema kwa upande wangu....kumpa nafasi ya Slaa bwana Mgana Msindai ni sawa na kumtusi kamanda Slaa...
😳😳😳😳😳 ndio huyu 👆🏼👆🏼👆🏼👆🏼
CCM wanahhaha kama kuku wanaotaka kutaga... Jielezeni kwa Watanzania kuwa mmewafanyia nini so far Zaidi ya kuwatesa kwa maisha magumu katika ardhi yao iliyojaa neema lukuki za allah S.W.T