Mfumuko wa bei waongezeka kutokana na Bei ya Nyama, Gesi, Ngano na Maziwa ya unga

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,501
9,280
Bidhaa za nyama, gesi ya kupikia, mkaa na viazi mviringo zimetajwa kuongeza mfumuko wa bei kutoka asilimia 3.8 Agosti hadi asilimia 4.0 kwa Septemba mwaka huu.

Taarifa ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Oktoba 8 jijini Dodoma, imetaja bidhaa nyingine zilizoongeza mfumuko wa bei ni ngano na maziwa ya unga.

Akisoma taarifa hiyo kwa waandishi wa habari, Kaimu Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii, Ruth Minja alisema sababu za kuongeza mfumuko ni kutokana na kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma.

Minja alisema mabadiliko hayo ni kwa mwaka ulioishia Septemba ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia Agosti 2021.

Amesema badiliko hilo la asilimia 0.2 limechangiwa na kasi ya mabadiliko ya bidhaa za vyakula kama unga wa ngano kwa asilimia 6.8, nyama ya ng’ombe kwa asilimia 3.4, maziwa ya unga kwa asilimia 9.2, mayai kwa asilimia 5.0 na viazi mviringo kwa asilimia 4.7 na kufanya kuongezeka kwa asilimia 4.0 kutoka asilimia 3.6 mwezi Agosti.

Amesema pia bidhaa zisizo za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko ni gesi ya kupikia kwa asilimia 2.7, mkaa kwa asilimia 3.5, na huduma ya malazi katika nyumba za kulala wageni kwa asilimia 5.7na kufanya bidhaa hizo kuongezeka hadi asilimia 4.1 kutoka asilimia 4.0 mwezi Agosti.


Mwananchi
 
😁😁😁
20210809_145036_temp.jpg
 
Bidhaa za nyama, gesi ya kupikia, mkaa na viazi mviringo zimetajwa kuongeza mfumuko wa bei kutoka asilimia 3.8 Agosti hadi asilimia 4.0 kwa Septemba mwaka huu.

Taarifa ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Oktoba 8 jijini Dodoma, imetaja bidhaa nyingine zilizoongeza mfumuko wa bei ni ngano na maziwa ya

Mwananchi
Mfumuko uko chini Sana kulingana na Target ya 5% ya serikali ilivyokadiria, kwa hiyo hiyo inflation ni nzuri kwenye uchumi..
 
Huo ni mwanzo tu, picha ndio kwanza inaanza, tutafika 15% sio muda.
Will never happen and had never ever happened before..

Ukifika huko ujue uchumi hauzalishi na labda kuwe na ukame wa bidhaa za chakula..

Kila siku nasema inflation yoyote ya single digit ni afya kwa uchumi kwa hiyo hakuna shida hususani kama pesa inapatikana na vyakula viko bei chini.
 
Will never happen and had never ever happened before..

Ukifika huko ujue uchumi hauzalishi na labda kuwe na ukame wa bidhaa za chakula..

Kila siku nasema inflation yoyote ya single digit ni afya kwa uchumi kwa hiyo hakuna shida hususani kama pesa inapatikana na vyakula viko bei chini.
Kusema it will never happen hapo ndio ujinga wako ulipojidhihirisha bila kificho.

Kwenye uchumi anything can happen. Kusema it will never happen inaonyesha kabisa jinsi ulivyo mweupe kichwani.
 
Kusema it will never happen hapo ndio ujinga wako ulipojidhihirisha bila kificho.

Kwenye uchumi anything can happen. Kusema it will never happen inaonyesha kabisa jinsi ulivyo mweupe kichwani.
Wewe ndio mweupe ,kutokea hayo ni lazima Nchi iwe kwenye majanga,kama kuna nchi huo mfumuko ulitokea under normal circumstances itaje hapa..

Ndio maana nimekwambia under normal conditions hakuna kitu kama hicho..

Kenya growth rate ya uchumi ni 5.2% , inflation 7% vs Tzn growth rate average 4.5% inflation ni 4% unadhani nani anafaidika hapo?
 
Wewe ndio mweupe ,kutokea hayo ni lazima Nchi iwe kwenye majanga,kama kuna nchi huo mfumuko ulitokea under normal circumstances itaje hapa..

Ndio maana nimekwambia under normal conditions hakuna kitu kama hicho..

Kenya growth rate ya uchumi ni 5.2% , inflation 7% vs Tzn growth rate average 4.5% inflation ni 4% unadhani nani anafaidika hapo?
Hakuna mahala umesema under normal circumstances. Wewe umesema tu it will never happen as is you have seen the future.

Wewe unajua mwakani kitatokea nini kwenye uchumi wa nchi?

Msiwe mnakurupuka tu kujiandikia vitu ambavyo hamuelewi.
 
Will never happen and had never ever happened before..

Ukifika huko ujue uchumi hauzalishi na labda kuwe na ukame wa bidhaa za chakula..

Kila siku nasema inflation yoyote ya single digit ni afya kwa uchumi kwa hiyo hakuna shida hususani kama pesa inapatikana na vyakula viko bei chini.
Pesa inapatikana wapi?
 
Back
Top Bottom