Mfumuko wa bei: Vifaa vya ujenzi na vyakula vyapaa

Mfumuko wa bei: Vifaa vya ujenzi na vyakula vyapaa

Bei za vifaa vya ujenzi na vyakula zimepaa maradufu mara baada ya kuanza kwa awamu ya tano. Mfano,wilayani Kibaha mfuko wa saruji unauzwa kwa 13500 kutoka 13000 ya mwanzo. Bei pia imeongezeka kwa bati na hata mbao.

Bei za nyama zimepaa huko Zanzibar na hata mkoani Mtwara. Huko Mtwara,kilo ya nyama inauzwa 8000 badala ya 6000. Huko Zanzibar,kilo ya nyama imefika kati ya 10000 na 15000.

Na mfumuko wa bei utupiwe jicho. Kimsingi,bei za bidhaa ndizo zinazogusa maisha ya siku hadi siku ya wananchi wa kawaida.


Hizo nyama zinatakiwa zibaki zinaliwa na viongozi tu ndio tutaamka na kudai haki zetu za msingi,nyama iuzwe laki moja,cement mfuko 150000/=hako AKILI ZA KUINGIA barabarani zitakuja zenyewe bila kulazimishwa.
 
Magufuli afanye mbwembwe zote anazozijua ila sie tunasubiri viwanda na milioni 55 kila kijiji

Tunataka amuenzi Nyerere kwa kuhamia Dodoma ili jijini la Dsm liondokane na misafara na foleni zisizokwisha.
 
Unafikiri haya yanawezekana bila ya hayo anayoyafanya sasa? Hakuna mahusiano? Acha Magufuli apige mzigo, tusijifanye tunajua kuliko rais.

Akiweza huu mfupa uliwashinda mwinyi, mkapa na Kikwete wa kuhamia Dodoma hakika atakuwa Rais milele, Nigeria Malawi walikuja kujifunza CDA jinsi ya kuhamia miji mipya leo hii wamehamia huko na kuacha miji ya biashara ikifanya biashara pasipo usumbufu wa foleni, Tanzania sasa inadanganya Dunia kwenye ramani wanasema mji Mkuu ni Dodoma lakini kumbe ni mji mkuu kivuli tu Kama kila kitu kipo Dsm, wakaige South Africa Serikali ipo pritoria na bunge lipo Cape Town huku jiji kubwa la Johannesburg likiwa huru kufanya biashara.
 
mtoa mada nakuunga mkono.duniani hakuna watu wajinga kama watanzania .wameridhika na viongozi wasanii.jpm ni msanii zaidi ya jk
 
Kwa kweli huyu JPJM anatakiwa kutulia na kuweka misingi ya utendaji wa kidemocrasia zaidi; asionekane kuongoza kwa kutoa maagizo yeye badala ya mawaziri. Hakuna haraka; kinachotakiwa ni kufanya kazi systematically. kwa hii style yake anset standards ambazo inaweza kuwa ngumu kufikiwa na mawaziri wake na pia inaweza kusababisha ukiukwaji wa kanuni. Lipumba alishauri vizuri: bana matumizi weka misingi imara. hatimaye sarafu iimarike na mfumuko wa bei udhibitiwe.
 
Kila jambo linakuwa na mwanzo wake, alichokifanya Mh. Raisi ni mwanzo mwema kuona kila jambo halina maana ni kukosa busara. Hongera Raisi JPM kwa mwanzo mwema tunakutakia kila la heri.Watanzania tupo bega kwa bega nawewe.
 
mtoa mada nakuunga mkono.duniani hakuna watu wajinga kama watanzania .wameridhika na viongozi wasanii.jpm ni msanii zaidi ya jk

Akiweza kuhamia Dodoma mie nitamwamini lakini mengineyo naona kama ni upepo yatapita tu.
 
Kwa kweli huyu JPJM anatakiwa kutulia na kuweka misingi ya utendaji wa kidemocrasia zaidi; asionekane kuongoza kwa kutoa maagizo yeye badala ya mawaziri. Hakuna haraka; kinachotakiwa ni kufanya kazi systematically. kwa hii style yake anset standards ambazo inaweza kuwa ngumu kufikiwa na mawaziri wake na pia inaweza kusababisha ukiukwaji wa kanuni. Lipumba alishauri vizuri: bana matumizi weka misingi imara. hatimaye sarafu iimarike na mfumuko wa bei udhibitiwe.

Kwa sasa hakuna mawaziri ndiyo maana anapiga mzigo mwenyewe akiwaekekeza cha kufanya pindi wakiteuliwa.
 


2. Imarisha sarafu. Ukiwa na sh. 1,000,000 leo hii unajiona kama mwenye sh 100,000 tu. Wakati Kenya sh 1,000,000 ni hela nyingi sana. Hii inatufanya kufanya kazi kubwa na kupewa hela nyingi lakini hazionekani kuwa na nguvu kiuchumi.

...
Umenikumbusha nimeenda ng'ambo, siku moja nikatoa note ya EURO 500 kununua Bidhaa kwenye Mall moja; wee...! acha muuzaji ahangake....piga simu mpaka manager mauzo akaja mwenyewe na sefu...eti kuninurudishia change Euro 275...! Kule cent moja inafanya kazi.
 
Hiyo ndiyo Tanzania ya Maghufuri kama Kikwete

Msemo wa kizungu, '' LIKE DADDY LIKE SON'' !
Hakuna jipya hapo. JPM anajaribu kutwanga maji kwenye kinu, hii longolongo ya Muhimbili, kukata pesa ya sherehe za Bunge, kufuta sherehe za Uhuru, kuzuia ziara nje ya nchi ni NGUVU YA SODA TU!

We' ll be witnesses, as time ticks away, JPM is getting tired,exhausted,weared and weathered. Believe me, after a year or 2, things will be back to norms. Hiyo ndiyo Tanzania ya Magufuli na Tanzania ya CCM!

Poleni sana Watanzania mliomchagua dikteta Magufuli. Katika miaka 5 ijayo hakika mtaisoma namba ya Magufuli chini ya sera za CCM. Time gonna tell!!!!!!!!!!!!!!
 
Nimechoka kuishi kwenye nyumba za tembe na kwenye vibanda km mnyama.Tafadhali tupeni timeline ya hizi ahadi tujipange! Ahadi ni deni!
 
Back
Top Bottom