Mfumuko wa bei: Vifaa vya ujenzi na vyakula vyapaa

Mfumuko wa bei: Vifaa vya ujenzi na vyakula vyapaa

Bei za vifaa vya ujenzi na vyakula zimepaa maradufu mara baada ya kuanza kwa awamu ya tano. Mfano,wilayani Kibaha mfuko wa saruji unauzwa kwa 13500 kutoka 13000 ya mwanzo. Bei pia imeongezeka kwa bati na hata mbao.

Bei za nyama zimepaa huko Zanzibar na hata mkoani Mtwara. Huko Mtwara,kilo ya nyama inauzwa 8000 badala ya 6000. Huko Zanzibar,kilo ya nyama imefika kati ya 10000 na 15000.

Na mfumuko wa bei utupiwe jicho. Kimsingi,bei za bidhaa ndizo zinazogusa maisha ya siku hadi siku ya wananchi wa kawaida.

Mimi naona bei ya nyama haijapanda,waongeze ifike kilo sh.20000 labda serikali itaona umhimu wa wafugaji

Wanathamini nyumbu, pundamilia na sokwe kuliko hata binadamu. Wafugaji wanapigwa risasi na wanafukuzwa kila sehemu, wanaambiwa wapunguze idadi ya ng'ombe. Sasa wameitikia wito ng'ombe wamepungua imekuwa malalamiko kila kona.

Nafikiri sasa serikali iruhusu tuanze kutumia nyumbu kama kitoweo maana ng'ombe hawana thamani kama nyumbu.Ndiyo maana sijawahi kusikia serikali ikisema ipunguze maeneo ya hifadhi ili wafugaji wapate malisho.

Anaye lalamikia bei ya nyama ajuwe sababu ni sisi wenyewe pamoja na serikali kupuuza na kudharau mahitaji ya wafugaji.

Nyama ndo kilikuwa kitoweo rahisi na kinachopatikana popote karibu na maeneo tunayoishi, serikali haioni umhimu huh,sasa ngoja tuisome namba.
 
Hello Ndugu Sometimes, nakujibu hivi kitaalamu.

Bei ya bidhaa inatokana na vitu hivi

A - Malighafi

B- Gharama za uzalishaji ambazo ni wafanyakazi, umeme, maji na simu

C- Kodi za serikali

Maelezo:

Wafanyakazi wa Tanzania wanalipwa mshahara mdogo sana ukiondoa management ambao ni wachache

Malighafi nyingi inapatikana Tanzania, ni udongo wetu.

Kitu ambacho kinaleta bei kuwa kubwa ni Kodi za serikali..... Raisi anaweza kuchukua hatua mfano kupunguza kodi, badala yake akawaagiza TRA kukusanya kodi kutoka wafanyabiashara wakubwa

Kuacha matumizi makubwa mfano sasa anavyofanya sasa.

----Wewe Ndugu Sometimes, Mh. Rais ameshasema ataleta mabadiliko, na ameanza.... Kama wewe umebaki kizamani zamani na awamu ya 4 -- Pole sanaaa.....
Kaka mbona unanionea! Ni wapi nimeandika kuhusu masuala ya bei na vinginevyo. Mimi nilichoandika ni kuuliza kama kweli mfumuko wa bei umetokea baada ya kuanza Awamu ya 5 inayoongozwa na Magufuli kama mtoa mada anavyotuaminisha! Au kuna Sometimes mwingine unayemjibu!
 
Mh. Rais Magufuli aliahidi Cement na vifaa vya Ujenzi vitashuka bei.Kwenye Stronghold za CCM kama Dodoma, Morogoro, Iringa, Singida, na Tanga pembezoni Nyumba ni za Udongo..Tembe na hazina Bati...Nyasi au tope..... Sasa huu ni mtihani kwa Mh. Magufuli..please take action.Kuna tetesi zimesambaa sana Tanzania nzima kuwa DANGOTA Alitaka kuuza Cement kwa 8500 Tshs kwa mfuko...ETI CCM Wakakataa. Mh... Rais, look at this.Mh. Rais, usipofanyia kazi haya mambo, ujue wapiga kura wako DODOMA, Singida, Morogoro umewaonea sana....Kwa nini Cementi Ktoka Kenya ni bei rahisi kutoka Tanzania?Kwa nini Cementi ya Pakistani ni rahisi kuliko ya Tanzania?
Nilisimama Ujenzi nikitegemea Rais ajaye angepunguza gharama za vifaa.vya ujenzi ila nilivyoona CCM wamepita nikajua tayari nimeshaumia
 
Hali hii ilianza wakati wa kampeni za uchaguzi, na wala sio baada ya uchaguzi...
 
kila kitu unaweka siasa, kwani kamtaja magufuli hapo?

Amesema tangu awamu ya tano ianze mfumuko wa bei umeongezeka mara dufu, siasa imewekwa na mleta mada, in fact bei ya kila kitu itashuka muda si mrefu iwapo kasi ya udhibiti wa matumizi ya hovyo itaendelea maana hela za kifisadi hataingia kwenye mzunguko.
 
Wengi humu kula kulala kwa mama hata hamjui mfumuko wa bei
 
Kila kitu kinaweza kuwa usanii, ila haya mawili kamwe huwezi kufanya usanii wa kudumu. Robert Mugabe anajua vema.

1. Kushusha bei ya bidhaa muhimu, mfano mbao, bati, cement, vyakula, nguo, nk. (Human basic needs = shelter + food + clothes).

2. Imarisha sarafu. Ukiwa na sh. 1,000,000 leo hii unajiona kama mwenye sh 100,000 tu. Wakati Kenya sh 1,000,000 ni hela nyingi sana. Hii inatufanya kufanya kazi kubwa na kupewa hela nyingi lakini hazionekani kuwa na nguvu kiuchumi.


Haya mawili tu ukiyashughulikia miaka yako mitano madarakani, nakwambia umemaliza kila kitu!

=====================================================================================

Hadi sasa naona unafanya usanii tu, sijaona lolote la maana. Siwezi kuthibitisha kuwa kweli umeacha kufanya sherehe za uhuru kisa unaokoa hela, mbona mwakani zinarudi?

Siwezi kuthibitisha kuwa ni kweli maafisa 50 wa serikali wamenyimwa kusafiri kwa nia ya kubana matumizi, najua ni usanii tu.

Siwezi kuthibitisha kwamba vitanda vya muhimbili ni real, najua ni usanii tu!

Siwezi kuthibitisha kuwa ni kweli umevunja bodi ya muhimbili wakati tayari ilishamaliza muda wake, najua ni usanii tu!

Kimsingi, hela za matumizi ya sherehe ya uzinduzi wa bunge ni usanii tu. Lazima walikuambia zilizochangwa, that means zilikwishatumika maana hawakuombi namna ya kuzitumia. So ni usanii tu!

=========================================================================

Wewe nifungie yale magoli mawili ya ushindi, kila mtanzania atakuelewa!

Nakumbusha tena:

1. Kushusha bei ya bidhaa muhimu!
2. Kuimarisha sarafu!

Kila la kheri Magu!
 
Unafikiri haya yanawezekana bila ya hayo anayoyafanya sasa? Hakuna mahusiano? Acha Magufuli apige mzigo, tusijifanye tunajua kuliko rais.
 
Magufuli asipite huku JF hadi mwezi wa 5 mwakani.
Anaweza changanyikiwa.
Moderator mpigeni ban Mh.JPM.
 
Bei za vifaa vya ujenzi na vyakula zimepaa maradufu mara baada ya kuanza kwa awamu ya tano. Mfano,wilayani Kibaha mfuko wa saruji unauzwa kwa 13500 kutoka 13000 ya mwanzo. Bei pia imeongezeka kwa bati na hata mbao.

Bei za nyama zimepaa huko Zanzibar na hata mkoani Mtwara. Huko Mtwara,kilo ya nyama inauzwa 8000 badala ya 6000. Huko Zanzibar,kilo ya nyama imefika kati ya 10000 na 15000.

Na mfumuko wa bei utupiwe jicho. Kimsingi,bei za bidhaa ndizo zinazogusa maisha ya siku hadi siku ya wananchi wa kawaida.


Tuache unafiki hakuna mfumuko wa bei,ungekuwepo na ukawa mkali kiasi cha kutosha watanzania wangeandamana,kilo ya nyama bei bado iko chini inatakiwa iwe elfu 30,000/=
 
Nafikiri haujasoma vizuri mtoa mada alichoandika. Amesema "Bei za vifaa vya ujenzi na vyakula zimepaa maradufu mara baada ya kuanza kwa awamu ya tano." Sasa unatajaje Awamu ya tano bila kumhusisha Mhe. Magufuli? Kuhusu maharage nimekula ya kwenu!
Sawa, na ndio maana amesema Magufuli atupie jicho huko. Hajasema Magufuli ndiye amesababisha. Unamaanisha hayo yote tunayoona anafanya leo kama njia ya kuondoa matumizi mabaya ya fedha yeye ndiye alisababisha?
 
Kila kitu kinaweza kuwa usanii, ila haya mawili kamwe huwezi kufanya usanii wa kudumu. Robert Mugabe anajua vema.

1. Kushusha bei ya bidhaa muhimu, mfano mbao, bati, cement, vyakula, nguo, nk. (Human basic needs = shelter + food + clothes).

2. Imarisha sarafu. Ukiwa na sh. 1,000,000 leo hii unajiona kama mwenye sh 100,000 tu. Wakati Kenya sh 1,000,000 ni hela nyingi sana. Hii inatufanya kufanya kazi kubwa na kupewa hela nyingi lakini hazionekani kuwa na nguvu kiuchumi.


Haya mawili tu ukiyashughulikia miaka yako mitano madarakani, nakwambia umemaliza kila kitu!

=====================================================================================

Hadi sasa naona unafanya usanii tu, sijaona lolote la maana. Siwezi kuthibitisha kuwa kweli umeacha kufanya sherehe za uhuru kisa unaokoa hela, mbona mwakani zinarudi?

Siwezi kuthibitisha kuwa ni kweli maafisa 50 wa serikali wamenyimwa kusafiri kwa nia ya kubana matumizi, najua ni usanii tu.

Siwezi kuthibitisha kwamba vitanda vya muhimbili ni real, najua ni usanii tu!

Siwezi kuthibitisha kuwa ni kweli umevunja bodi ya muhimbili wakati tayari ilishamaliza muda wake, najua ni usanii tu!

Kimsingi, hela za matumizi ya sherehe ya uzinduzi wa bunge ni usanii tu. Lazima walikuambia zilizochangwa, that means zilikwishatumika maana hawakuombi namna ya kuzitumia. So ni usanii tu!

=========================================================================

Wewe nifungie yale magoli mawili ya ushindi, kila mtanzania atakuelewa!

Nakumbusha tena:

1. Kushusha bei ya bidhaa muhimu!
2. Kuimarisha sarafu!

Kila la kheri Magu!

Pia kuhamia Dodoma kupunguza foleni jijini Dsm
 
Back
Top Bottom