mtwa mkulu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2013
- 8,098
- 9,994
Wakuu heshima kwenu,
Huu mfumo wa wajumbe kwa maoni yangu nimeona unamatatizo mengi sana kuliko faida.
Ni mfumo ambao chama kitakuja kuutafakari kwa upya na kuutupilia kando.
Dhumuni la huu mfumo ilikuwa ati kupunguza rushwa lakini sivyo ilivyo,
Nina Hakika sana hakuna mwaka ambao fedha imenunua kura za watu Kama mwaka huu, Nadhani hata ripoti ya Takukuru ikitolewa itakuwa ushahidi mzuri na sababu kubwa Ni hii
Watia Nia hawakuruhusiwa kuendesha kampeni baada ya kuchukua fomu kueleza kusudio kwa wagombea, badala yake unapewa dakika mbili jukwaani kujieleza wewe Ni nani na utafanya nini.
Hii imewawia ugumu watu wenye nia ya dhati kupambanua kwa upeo namna ambavyo watawahudumia wajumbe, badala yake kumekuwa na kampeni za chini kwa chini, watia Nia wameendesha kampeni za chini kwa chini kwenye mito, miti na makaburi usiku wa manane kwa hofu ya Takukuru. Sambamba na Hilo kuwakutanisha wajumbe inahitaji mafungu, watu wametoa pesa na kupewa kwao kura kumepimwa kwa ukarimu wao.
Mfumo huu pia, unaweza kutoa kiongozi asiye chaguo la wengi, mfano panapotukia viongozi wawili wenye Nguvu sana basi kiongozi watatu anaweza kuibuka mbabe kwakuwa wale wawili watagawana kura na hii imetokea maeneo Mengi kiasi kwamba wale wajumbe wametoka ukumbini wakiwa hawaelewi walicho kifanya.
Mimi nilidhani, mfumo ule wa mwanzo uliwapa mzigo mkubwa wa kuhonga jamii nzima na hivyo wahongaji wengi walipata umaskini mkubwa, mfumo huu wasasa unawapa nafuu wahongaji.
Mimi nilidhani, mfumo ule wa zamani uliwapa nafasi wana CCM kujinadi mara mbili yaani kampeni za Chama na Zile za NEC, watanzania wakaelewa nini chama chao kina kusudia kuwafanyia, mfumo huu wa sasa unatoa dakika 2 za kuonesha sura yako!
Mimi nilidhani, mfumo wa mwanzo ulisababisha watu kuchagua kiongozi wao kwa sauti ya wengi "voix populii"
Mfumo wa sasa hauwapi wanachama uhuru wa kuchagua, badala yake kikundi Cha wajumbe wachache wanachagu, wakitumia matumbo yao kutoa kilio Cha wengi.
Huu mfumo wa wajumbe kwa maoni yangu nimeona unamatatizo mengi sana kuliko faida.
Ni mfumo ambao chama kitakuja kuutafakari kwa upya na kuutupilia kando.
Dhumuni la huu mfumo ilikuwa ati kupunguza rushwa lakini sivyo ilivyo,
Nina Hakika sana hakuna mwaka ambao fedha imenunua kura za watu Kama mwaka huu, Nadhani hata ripoti ya Takukuru ikitolewa itakuwa ushahidi mzuri na sababu kubwa Ni hii
Watia Nia hawakuruhusiwa kuendesha kampeni baada ya kuchukua fomu kueleza kusudio kwa wagombea, badala yake unapewa dakika mbili jukwaani kujieleza wewe Ni nani na utafanya nini.
Hii imewawia ugumu watu wenye nia ya dhati kupambanua kwa upeo namna ambavyo watawahudumia wajumbe, badala yake kumekuwa na kampeni za chini kwa chini, watia Nia wameendesha kampeni za chini kwa chini kwenye mito, miti na makaburi usiku wa manane kwa hofu ya Takukuru. Sambamba na Hilo kuwakutanisha wajumbe inahitaji mafungu, watu wametoa pesa na kupewa kwao kura kumepimwa kwa ukarimu wao.
Mfumo huu pia, unaweza kutoa kiongozi asiye chaguo la wengi, mfano panapotukia viongozi wawili wenye Nguvu sana basi kiongozi watatu anaweza kuibuka mbabe kwakuwa wale wawili watagawana kura na hii imetokea maeneo Mengi kiasi kwamba wale wajumbe wametoka ukumbini wakiwa hawaelewi walicho kifanya.
Mimi nilidhani, mfumo ule wa mwanzo uliwapa mzigo mkubwa wa kuhonga jamii nzima na hivyo wahongaji wengi walipata umaskini mkubwa, mfumo huu wasasa unawapa nafuu wahongaji.
Mimi nilidhani, mfumo ule wa zamani uliwapa nafasi wana CCM kujinadi mara mbili yaani kampeni za Chama na Zile za NEC, watanzania wakaelewa nini chama chao kina kusudia kuwafanyia, mfumo huu wa sasa unatoa dakika 2 za kuonesha sura yako!
Mimi nilidhani, mfumo wa mwanzo ulisababisha watu kuchagua kiongozi wao kwa sauti ya wengi "voix populii"
Mfumo wa sasa hauwapi wanachama uhuru wa kuchagua, badala yake kikundi Cha wajumbe wachache wanachagu, wakitumia matumbo yao kutoa kilio Cha wengi.
Nakipenda Chama Cha Mapinduzi lakini siupendi mfumo wa watu hawa