Mfumo wa elimu Afrika haumwandai muhitimu kujiajiri

Mantombazane

JF-Expert Member
Sep 7, 2014
572
356
Mfumo wa Elimu ya Afrika tulioachiwa na Wazungu ni mfumo unaoharibu Akili na Saikolojia ya Wanafunzi.

Wazungu wao wanasoma Elimu ya Maarifa na Wanasoma Future, sisi Afrika tunasoma vitu visivyo na msaada katika Maisha ya kawaida na vingi ni Past. Elimu inakufanya utegemee kuajiriwa usipoajiriwa unapata Tabu kujikomboa kiuchumi.

Wazungu wanasoma vitu vilivyopo na vijavyo kwa hiyo Mwanafunzi anapata maarifa ya kuweza kuelewa Mambo yaliyopo na yajayo ili muda ukifika aweze kuishi na Mazingira anayoyakuta kwa wakati huo.

Mara nyingi Elimu ya Afrika tunafundishwa Vitu ambavyo ukihitimu Shule basi ulivyovisoma hautovikuta Mtaani, unafundishwa Maji Maji war sijui Vasco Da Gama alikuja mwaka gani, ukirudi Mtaani hautokutana na mambo hayo.

Njaa ikikuuma Mama Ntilie hatokuambia Taja mwaka ambao Maji maji war vilipiganwa ili tukupe Chakula.

Afrika tunajifunza vitu vilivyopita ambavyo haviendani na Mazingira ya sasa na havitokusaidia Chochote, Ulaya Wanafunzi hawafundishwi jinsi Wazungu alivyotutawala Waafrika, vitabu vya aina hiyo utavikuta Library ambapo mtu yeyote ataamua akasome au asisome.

Viongozi tulionao wametokana na Mfumo wa Elimu hii hii ndio maana wengi hawana Maarifa. Kauli yao ni Vijana mjiajiri wakati wao walishindwa kujiajiri.

Kijana amefundishwa Mambo ya Vasco Da Gama, amefundishwa kipeuo cha 2, amefundishwa Sehemu ya Kike ya ua inaitwa Sepali, amefundishwa jinsi kipepeo anavyozaliwa halafu unamwambia ajiajiri, atajiajirije wakati kichwani mwake kumejaa Matakataka hayo.

Mwanafunzi anakaririshwa mambo ya Zama za mawe, Kinjekitile, Vyura wanavyozalina halafu anaambiwa ajiajiri!

1630406014754.png

Source: FB, Romanticx Aloyce's post
 
Hapana napingana na hoja zako za kusema ulichofundishwa, mtaani haukikuti hata Bibi na babu kule vijijini wanatumia elimu ya kemia kuwasha Moto jikoni kwenye jiko la kuni (inflammable) kinachobadirika ni lugha lakini mambo ni Yale Yale.

kwhyo pia kuna mambo mengine ukiendelea kusoma utayafahamu na faida zake pia katika real life mfano mwanafunzi aliyemaliza kidato cha nne anahuelew kidogo kuhusu mnyama anayeitwa panzi (grasshopper) akimaliza atasema "huyu panzi mtaani ananisahidia nini?,alikuwa akinipotezea tu muda"jibu hamsaidii kwasababu elimu yake ni basically tu lakini hakisoma zaidi ya hapo atapata nafasi ya kumjua zaidi na jinsi gani anavyotumika.

Kuhusu swala la kujiajiri nitaongelea zaidi level ya technical instructions na vyuo vikuu kwa sababu primary & secondary school ni elimu basic vasco dagama lazima umsome milima ya uduzungwa pale moromoro ungeijuaje Kama historia usingeisoma primary school, pia hata tusingeweza kuwajua waasisi wa taifa letu na mkoroni pia.

Hili uweze kujiajiri unatakiwa uwe na maarifa ya kitu fulani (ulichokisomea), pia uwe na pesa za kukuwezesha kujimu hili kukuwezesha katika Safari yako ya kujiajiri.

katika maarifa kuna baadhi ya maarifa kujiajiri huwezi hii ni changamoto ambayo inawapata wale ambao wanaenda mavyuoni bila kujipanga wasome nini hii inatokana na ufaulu kwako na kujikuta wakiingia katika kozi ambazo hazina manufaa kwao hata kwa taifa kiujumla.
 
Hapana napingana na hoja zako za kusema ulichofundishwa, mtaani haukikuti hata Bibi na babu kule vijijini wanatumia elimu ya kemia kuwasha Moto jikoni kwenye jiko la kuni (inflammable) kinachobadirika ni lugha lakini mambo ni Yale Yale.

kwhyo pia kuna mambo mengine ukiendelea kusoma utayafahamu na faida zake pia katika real life mfano mwanafunzi aliyemaliza kidato cha nne anahuelew kidogo kuhusu mnyama anayeitwa panzi (grasshopper) akimaliza atasema "huyu panzi mtaani ananisahidia nini?,alikuwa akinipotezea tu muda"jibu hamsaidii kwasababu elimu yake ni basically tu lakini hakisoma zaidi ya hapo atapata nafasi ya kumjua zaidi na jinsi gani anavyotumika.

Kuhusu swala la kujiajiri nitaongelea zaidi level ya technical instructions na vyuo vikuu kwa sababu primary & secondary school ni elimu basic vasco dagama lazima umsome milima ya uduzungwa pale moromoro ungeijuaje Kama historia usingeisoma primary school, pia hata tusingeweza kuwajua waasisi wa taifa letu na mkoroni pia.

Hili uweze kujiajiri unatakiwa uwe na maarifa ya kitu fulani (ulichokisomea), pia uwe na pesa za kukuwezesha kujimu hili kukuwezesha katika Safari yako ya kujiajiri.

katika maarifa kuna baadhi ya maarifa kujiajiri huwezi hii ni changamoto ambayo inawapata wale ambao wanaenda mavyuoni bila kujipanga wasome nini hii inatokana na ufaulu kwako na kujikuta wakiingia katika kozi ambazo hazina manufaa kwao hata kwa taifa kiujumla.
umemaliza akijibu hoja zako nitakuja kujazia nyama hoja zako.
 
Back
Top Bottom