Mfumo (software) Kusomana na NMB account

Sasa unauhakika gani na kampuni yake mkuu? Hakuna sehemu amesema kama kampuni yake ni ndogo au kubwa ila kuna sehemu amesema amewahi kushindwana terms za kiasilimia na kampuni fulani which hizo terms za asilimia huko ulikomtajia ataenda kukutana nazo pia, so probably kama Alishindwa huko kwa 2% hata huko ataenda kushindwa.
 
Kampuni kubwa ije kuomba msaada jamii forum una akili wewe NMB hawatoi api kwa company ndogo elewa dogo
 
Kampuni kubwa ije kuomba msaada jamii forum una akili wewe NMB hawatoi api kwa company ndogo elewa dogo
Kwamba jamiiforum sio jukwaa lifaalo kuomba msaada sio? Ni majukwaa gani ambayo kampuni kubwa huenda kuomba misaada?

By the way hiko kitu nimeongea hapo niko na uhakika nacho 95% so bwana Fanton Mahal kama utahitaji zaidi nicheck pm, achana na Hawa wanaojifanya wanajua kila kitu while hakuna wajuacho.
 
Ahsante chief kwa maelezo. Nitafanya hivyo.
Most if not all Intergrations huwa namaliza mwenyewe sijawah kukutana na API documentation complicated. Shukran sana mkuu. Nitakupa mrejesho
 
Achana na hao maselikumu watakuua😅, nenda direct uingie nao ubia ufanye integration moja kwa moja, kuna mtu aliwahi kuniambia kwenye upande huo hiyo bank wako smart sana so kama ukikutana na mtu sahihi na mkafikia muafaka mtafanya biz.
Na hiki ndio ninakitafuta sana mkuu. Nitafuatilia selcom pia nijue nao wakoje especially kwenye charges ndio concern yangu kubwaa
 
Poa poa mkuu, ila bank pinzani (washindani wao wakuu) nina contract nao kabisaaa licha ya kwamba kampuni yetu si kubwa
 
Na hiki ndio ninakitafuta sana mkuu. Nitafuatilia selcom pia nijue nao wakoje especially kwenye charges ndio concern yangu kubwaa
Hawa provider wengi huwa asilimia zao zinacheza hapo 3, 2 lakini labda kama mtakaa mezani vizuri mkaongea kwa kina mnaweza kufikia eneo zuri... Kitu kizuri kuhusu providers ni kwamba simple kufikia makubaliano ya kibiashara ila wewe unakua hauko na full control coz hapo unakua unadeal na watu wawili, kwakuanzia sio mbaya hasa kama startup yako ni ndogo ila kama ni Fintech idea ambayo inahitaji kugrow na kushindana na hizo zilizopo nenda front na ufanye integration zako kwenye zero margin (najua unaelewa coz wewe ni mtu wa tech).

Hiyo bank uliyoiendea hawana changamoto sana kwenye huo upande, kama vitu vimenyooka na business ipo mtafanya biashara mkuu.
 
Ahahahaahah..tuachane na hayo ya ukubwa au udogo nahitaji ushauri tu kama mtu anavyoomba ushauri kwa washkaji kijiweni. Ndio la msingi
 
Umenena vyema. Changamoto za aggregators bwana, incase of downtime unashindwa kujua troubeshooting ni upande wa bank au aggregator. Hata kama ni wao ,simply wanaweza kukuambia "kuna issues with bank" na wewe huwez fanya kitu inabid uwe mpoleee 😂
 
Now you know mkuu... Na pia wakiona unapiga kazi sana wanabadili terms ili wakuumize kwakua wanajua ni ngumu kuhama ghafla kwakua tayari umekua stable... Ndio maana kama uwezekano wa kuwaepuka hao watu upo ni Bora kuwaepuka tu, ogopa sana terms ambazo zinaweza kubadilikia online na si kuitana kukaa kwenye kikao ili mpitie makubaliano yenu upya.

Yeye Kila akikaa kwenye kikao akiona terms zimembana yeye kidogo nae anakuja kuwabana ninyi ili aendelee kubaki salama.

Ushauri, hiyo ifanye iwe option yako ya mwisho baada ya kuona imeshindikana kabisa.
 
Ahahahaahah..tuachane na hayo ya ukubwa au udogo nahitaji ushauri tu kama mtu anavyoomba ushauri kwa washkaji kijiweni. Ndio la msingi
Ndio maana nilijaribu kutoa ushauri kulingana na msingi wa andiko lako, kwamba namna ya kuepuka 2% na uwezekano wa kupata integration ya moja kwa moja, nami nakwambia uwezekano upo coz hakuna kampuni ambayo ilianza ikiwa kubwa, watu wanaangalia vision yako na namna ambavyo wao wataenda kunufaika kupitia hiyo aina ya biashara mnayotaka kufanya.
 
Yeah. Na hii ni changamoto sana, maana inakufanya uonekane hauko reliable kwa clients wako. Na kiukwel unakua huna controll kabisaa.

Japo i hope kuna namna watakua na mkataba w makubaliano kwaajili ya mambo kama haya, i guesse
 
Sahihi kabisa
 
Yeah. Na hii ni changamoto sana, maana inakufanya uonekane hauko reliable kwa clients wako. Na kiukwel unakua huna controll kabisaa.

Japo i hope kuna namna watakua na mkataba w makubaliano kwaajili ya mambo kama haya, i guesse
Inawezekana, anzia huko coz kwenye biashara hakishindikani kitu.
 
Mkuu, omba NMB moja kwa moja. Nitakupa muongozo unapo hitajika
 
Reverse engineer API/Key kutoka kwenye POS, machine yao itaona POS imefanya request kumbe ni app Yako!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…