Mtendaji wa kaya
JF-Expert Member
- Mar 16, 2014
- 334
- 59
Ni mfanyakazi kwa jina la Fungwe Charles William amepotea chini ya ardhi tangu jana saa 2 usiku alipokwenda shift night! Tukio hili limekuwa la aina yake kwani mgodi umesitisha shughuli za ulipuaji miamba ya dhahabu!
Timu ya uokoaji ya mgodi hapa bulyanhulu inaendelea kumtafuta aidha akiwa hai au laaaaa.....kiukweli hofu imetanda huku wengine wakidhani pengine ameangukiwa na mwamba na wengine wakidhani kuwa labda alitumbukia kwenye Water Sump zilizopo chini ya ardhi!
Waliokuwa na mhanga kabla ya tukio wamesema mwenzao aliwaaga na kuondoka akiwa anaendesha mashine aina ya ceasar au UTV kwa jina ! mpaka naondoka mgodini saa nane na dakika arobaini na saba mchana huu bado mtu huyu hajapatikana.
Nitazidi kutoa habari zaidi kama zinavyopatikana...
==============================================
Latest 01/06/2014
Timu ya uokoaji ya mgodi hapa bulyanhulu inaendelea kumtafuta aidha akiwa hai au laaaaa.....kiukweli hofu imetanda huku wengine wakidhani pengine ameangukiwa na mwamba na wengine wakidhani kuwa labda alitumbukia kwenye Water Sump zilizopo chini ya ardhi!
Waliokuwa na mhanga kabla ya tukio wamesema mwenzao aliwaaga na kuondoka akiwa anaendesha mashine aina ya ceasar au UTV kwa jina ! mpaka naondoka mgodini saa nane na dakika arobaini na saba mchana huu bado mtu huyu hajapatikana.
Nitazidi kutoa habari zaidi kama zinavyopatikana...
==============================================
Latest 01/06/2014
Marehemu kapatikana saa tano asubuhi tukiwa tunafanya shaft inspection kati ya 4130 na 3980 level
kwenye maryan compatiment akiwa ananing'inia kavaa kila kitu boots, helmet na ear plugs kasoro miwani ila waya wa taa ukiwa
shingoni inaonekana ni suicide shaft imefungiwa tunasubiria mine inspector na polisi ndio mwili utolewe