maliyamungu
JF-Expert Member
- Aug 14, 2011
- 564
- 412
Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya Motisun Group ambaye anatajwa kuwa miongoni mwa Mabilionea wachache nchini Tanzania na mfanyabiashara, Subhash Patel inadaiwa amefariki leo.
UPDATES:
MFANYABIASHARA maarufu wa Tanzania ambae ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya Motisun Group, Subhash Patel amefariki dunia leo Desemba 15, 2020.
Miongoni mwa makampuni na bidhaa alizokuwa akimiliki Subhash Patel, ni kiboko Plastics, Kiboko Protected Sheets, MM Estates, White Sands Hotel, MMRDL, Neeklanth Cables, Pearlsun Hotel & Resorts, Sayona Drinks Ltd, Sea Cliff Hotel, Best Bite, Mamba Cement na nyingine nyingi.
=====
WAZIRI MKUU ATUMA SALAAM ZA RAMBIRAMBI KIFO CHA SUBHASH PATEL
DAR ES SALAAM: DESEMBA 15, 2020
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa, ametuma salaam za rambirambi kutokana na kifo cha Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya Motisun Group, Subhash Patel, kilichotokea leo jijini Dar es Salaam.
“Hayati Shubash, ana mchango wake kwenye sekta ya viwanda, alikuwa rafiki wa wote, mcheshi, ametoa msaada kwa maskini na matajiri na hakuwa mbaguzi,”
“Ninatoa pole kwa wanafamilia, ndugu na wote walioguswa na msiba huu. Taifa limempoteza mmoja wa wazalendo wake. Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina.” Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Katika salamu alizozitoa Waziri Mkuu, amesema amehuzunishwa na kifo cha mfanyabiashara huyo maarufu nchini ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Viwanda Nchini (CTI) na mjumbe wa Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).
Mmoja wa wanafamilia amesema, Bw. Patel amefia nyumbani kwake, Kisutu jijini Dar es Salaam ambako alikuwa akiendelea na matibabu na anatarajiwa kuzikwa keshokutwa (Alhamisi, Desemba 17, 2020) kwenye makaburi ya Wahindu yaliyoko Kijitonyama, Dar es Salaam.
Tanzania: Subhash Patel dies of MOTISON Group of Companies dies
Mfanyabiashara Subhash Patel enzi za uhai wake
Soma pia:
1) Subhash Patel ni nani ?!
2) Forbes: Top 10 Richest Men in Tanzania for October, 2018.
3) Subash Patel: Wafanyabiashara na wenye viwanda tunamuunga mkono Rais Magufuli anayetupeleka kwenye uchumi wa kati
4) Interview with CTI Chairman Mr. Subhash Patel on channel TV-E(TANZANIA)
5) Ugomvi wa mali wamsukuma bilionea kumkana mtoto wake. Ni ugomvi wa Ukurugenzi wa MOTISUN Group
UPDATES:
MFANYABIASHARA maarufu wa Tanzania ambae ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya Motisun Group, Subhash Patel amefariki dunia leo Desemba 15, 2020.
Miongoni mwa makampuni na bidhaa alizokuwa akimiliki Subhash Patel, ni kiboko Plastics, Kiboko Protected Sheets, MM Estates, White Sands Hotel, MMRDL, Neeklanth Cables, Pearlsun Hotel & Resorts, Sayona Drinks Ltd, Sea Cliff Hotel, Best Bite, Mamba Cement na nyingine nyingi.
=====
WAZIRI MKUU ATUMA SALAAM ZA RAMBIRAMBI KIFO CHA SUBHASH PATEL
DAR ES SALAAM: DESEMBA 15, 2020
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa, ametuma salaam za rambirambi kutokana na kifo cha Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya Motisun Group, Subhash Patel, kilichotokea leo jijini Dar es Salaam.
“Hayati Shubash, ana mchango wake kwenye sekta ya viwanda, alikuwa rafiki wa wote, mcheshi, ametoa msaada kwa maskini na matajiri na hakuwa mbaguzi,”
“Ninatoa pole kwa wanafamilia, ndugu na wote walioguswa na msiba huu. Taifa limempoteza mmoja wa wazalendo wake. Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina.” Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Katika salamu alizozitoa Waziri Mkuu, amesema amehuzunishwa na kifo cha mfanyabiashara huyo maarufu nchini ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Viwanda Nchini (CTI) na mjumbe wa Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).
Mmoja wa wanafamilia amesema, Bw. Patel amefia nyumbani kwake, Kisutu jijini Dar es Salaam ambako alikuwa akiendelea na matibabu na anatarajiwa kuzikwa keshokutwa (Alhamisi, Desemba 17, 2020) kwenye makaburi ya Wahindu yaliyoko Kijitonyama, Dar es Salaam.
Tanzania: Subhash Patel dies of MOTISON Group of Companies dies
Mfanyabiashara Subhash Patel enzi za uhai wake
1) Subhash Patel ni nani ?!
2) Forbes: Top 10 Richest Men in Tanzania for October, 2018.
3) Subash Patel: Wafanyabiashara na wenye viwanda tunamuunga mkono Rais Magufuli anayetupeleka kwenye uchumi wa kati
4) Interview with CTI Chairman Mr. Subhash Patel on channel TV-E(TANZANIA)
5) Ugomvi wa mali wamsukuma bilionea kumkana mtoto wake. Ni ugomvi wa Ukurugenzi wa MOTISUN Group
Yussuf Makamba amwinda Reginald Mengi, yeye awataja mafisadi Papa rasmi!
Makamba amwinda Mengi Ahoji safari za mikoani Mwandishi Wetu Aprili 22, 2009 Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo HUKU kukiwa na shinikizo la kutaka kumuondoa katika nafasi yake Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yussuf Makamba, mwanasiasa huyo machachari, ametajwa sasa...
www.jamiiforums.com