Daaah!, masikini Mheshimiwa Wakili Bwana Oguda, huyu ndugu alikuwa ana dharau na mnyanyasaji mkubwa wa wanafunzi pale St. John's University hasa akina dada wamenyanyasika sana kijinsia na huyu Mungu mtu!.
Hata hivo watanzania hatuna tabia wala tamaduni ya kufurahia matatizo ya binadamu wenzetu.
Nilipokuwa Rais wa Serikali ya wanafunzi hapo chuoni ndugu Oguda ulisimama kidete kutengeneza fitna ili nifukuzwe Chuo eti kwa kuwa nilipinga sana tabia yako ya kuwaonea wanafunzi hasa wa kike na mpaka Israel anainyemelea roho yako leo nina kesi na Chuo hicho ambapo wewe kwa kiherehere chako ndo wakili unaesaini viapo vya chuo!, natamani upone haraka ili ushuhudie nitakavo wahenyesha hapo Mahakama Kuu ya Dodoma.
Mungu akunusuru Wakili Msomi Joshua Oguda, nimeguswa na kusikitishwa sana kama binadamu kwa kweli nakuombea upone haraka lakini ujue dunia ni mapito mheshimiwa hivo si uungwana kuharibu ndoto za watoto wa watanzania wenzio!
Daaaa, kaka!,Samahani sana. Nasukumwa na roho ya ubinadamu walau kusema chochote kwako. Nimesoma posts zako humu ndani kuhusu vifo vya hawa marehemu, mwili umenisisimuka.
Inaonekana umeshawahi kujeruhiwa au na marehemu mwenyewe au kwa niaba yake. Nakupa pole kwa hilo.
Lakini, pamoja na yote hayo,kwa kawaida binadamu yeyote mwenye ufahamu hata juu kidogo ya ngazi ya ukichaa(above the level of insanity),linapotokea swala la kifo huwa anasamehe.
Na iwapo itatokea hajasamehe humshukuru Mungu na kuchekelea kimoyomoyo kwamba mbaya wake afadhali ameondoka.
Jambo unalolifanya la kutoa hisia zako waziwazi si tu unamkwaza marehemu huko aliko bali pia unawakwaza binadamu wengine na hasa ndugu zake marehemu na wengineo wote waliokuwa karibu naye.
Mbaya zaidi unajitambulisha kwamba umewahi kuwa nadhani Rais wa serikali ya chuo hicho, hii maana yake ni kwamba unafahamiika hata kwa wengi wa wana jf.
Kaka, binadamu hatuishi hivo. Najiuliza kama wewe umewahi kuwa Rais wa chuo kikuu, je walifanya makosa kukuchagua au wewe ndo ulikuwa mwenye uafadhali katika hicho chuo kwa mda huo? ?? ,Hapana. Sitaki kabisa niamini hivo kwa sababu chuo cha kanisa kama kile kupata wahitimu kama wewe nadhani ni bahati mbaya sana.
Nahitimisha kwa kukushauri ujifunze nini cha kuandika kwenye kadamnasi na hasa unapotaka elezea hisia zako. Ukitaka chukua usipotaka potezea.
Raha ya milele uwape hao marehemu wote ee bwana, na mwanga wa milele uwaangazie. Wapumzike kwa amani-AMINA.