Mfanano wa mafundisho ya Yesu na mafundisho ya Krishna unakupa picha gani?

DR Mambo Jambo

JF-Expert Member
May 10, 2012
8,598
17,735
Amani iwe nanyi

Angalizo: Kabla ya yote Enyi ndugu zangu napenda kutoa angalizo kwamba Yatakayoongelewa hapa ni kwa lengo la kujifunza na si katika muktadha wa maana yoyote nyingine..

Kama mada inavyojieleza Kuhusu Mafundisho ya hao watakatifu wawili..

watakatifu hao wamekuwa sio tu na mfanano wa Mafundisho hata mfanano wa maisha yao pia...

MFANANO WA BAADHI YA HAIBA..

  • kuzaliwa kwao wote walitabiriwa
  • Wote walizaliwa kwenye mazingira mabaya Yesu alizaliwa Kwenye hori la ng'ombe na Krishna alizaliwa Gerezani..
  • wote walizaliwa na baba fundi seremala..
  • wote walizaliwa na mama Bikra..
  • wote waliishi maisha matakatifu wakifundisha..
  • wote walijinasibu ama kunasibiwa kuwa wana wa Mungu..
  • wote walisema kuwa wao si wa ulimwengu huu na walikuwepo tangu kuumbwa kwa ulimwengu...
  • wote walihubiri upendo
  • Sote walitabiriwa kwa kuonekana kwa nyota ya mashariki
  • krishana alijitambulisha kama cowherd (Mchungaji wa ngombe), na yesu alijitambulisha kama Shephard (Mchungaji wa mifugo)
  • wote kipindi wanazaliwa watoto katika mji wote waliuawa na kiongozi au watu waliohofia kuzaliwa kwao
KUZALIWA KWAO NA UJUMBE (MAFUNDISHO)

Yesu
anakadiriwa kuzaliwa mwaka 6 B.C.E ,japo kuna baadhi ya Nyaraka zinasema ni 7 BCE

na Krishna anakadiriwa kuzaliwa mwaka 400 B.C.E Japo kuna baadhi ya nyaraka zinasema ni mapema sana kabla ya hapo kama 1000 BCE kutokana na maandiko mengi kuandikwa kipindi cha vita ya kurukshetra ambayo wanahistoria wanakadiria ilikuwa kati ya mwaka 1000 BCE Na 400 BCE

kwa hiyo krishna alikuwepo duniani miaka 400 kabla ya kuwepo kwa Yesu...Au 1000 Kabla ya Yesu

MAFUNDISHO YAO..


YESU


Yesu
alifundisha katika Yerusalem, Mji wa yuda Galilaya na Israel kwa ujumla, Mafundisho ya Yesu yanapatikana katika Biblia ,Quran na kitabu cha mormons..

Japo kitabu bora cha kupata Mafundisho yenye wingi wa Maelezo ni Biblia hasa agano Jipya..


Mafundisho mengi yamejikita kwenye Dialogue na maelezo aliyokuwa akiwaambia wanafunzi wake na baadhi ni yale aliyomfundisha Paulo kuyasema (Kwa mujibu wa paulo mwenyewe kupitia nyaraka)



KRISHNA

mafundisho ya krishna yanapatikana katika vitabu vitakatifu vya Hinduism kama Bhagavata Purana ,Garga Samhita ,Harivamsa,Vishnu Purana,Mahabharata (ambapo ndani kuna Bhagavad Gita), Brahma Vaivarta Purana..


katika vitabu vyote hivyo kitabu changu pendwa na nitakachokitumia ni Bhagavad Gita kwa sababu kimeeleza zaidi maneno mengi na kina mafundisho mengi sana.

Huenda kuliko hata vitabu vingine na kinatumika almost na wahindi wa madhehebu yote...

Mafundisho mengi ni aliyokuwa akiongea au kumwambia mwanafunzi wake mpendwa Arjun katika vita ya kurukshetra



INAENDELEA SOMA HAPA...
MFANANO WA MAFUNDISHO YA YESU NA MAFUNDISHO YA KRISHNA UNAKUPA PICHA GANi 2
 
inaendelea...
MFANANO WA MAFUNDISHO YAO...
1.
Bhagavad Gita: ..(chapter 10 verse 20)

I am the beginning, the middle and the end of things
(Mimi ni mwanzo, Kati na mwisho wa mambo yote)

Biblia: ..(Ufunuo wa Yohana 1:8)
I am Alpha and Omega, the beginning and the ending...
(Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho....... )




2.
Bhagavad gita: ..( Chapter 17 verses 28
)
Whats Sacrifice,almsgiving or austerity, anything is done without faith is evil.
(Kafara,zaka au sadaka/ misaada kitu chochote kikifanyika bila imani ni dhambi)


Biblia:.. (Warumi 14:23)
And he that doubteth is damned if he eat, because he eateth not of faith: for whatsoever is not of faith is sin.
(Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi. )


3.
Bhagavad gita:..(chapter 6 verses 29)

Those who believe in me,With true Devotion are in me and I in them
(Wote wanaoniamini kwa imani ya kweli, Watakuwa ndani yangu na mimi ndani yao.)


Biblia:..(Yohana 17:23)
I in them, and thou in me, that they may be made perfect in one; and that the world may know that thou hast sent me, and hast loved them, as thou hast loved me.
(Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi. )


4.
Bhagavad Gita:..(Chapter 9 verses 31)

Be assured that, He who believe in me perishes not.
(Aminini ya kuwa, Atakayeniamini Mimi hatapotea/Hatoangamia!)


Biblia..(yohana 3:16)
that whosoever believeth in him should not perish, but have everlasting life.
(ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.)



INAENDELEA HAPA...MFANANO WA MAFUNDISHO YA YESU NA MAFUNDISHO YA KRISHNA UNAKUPA PICHA GANi 3
 
Inaendelea......
5.
Bhagavad gita:..(Chapter 7 verses 17)
The wise one who is in full knowledge (God) is in union with Me through pure devotional service,He is the best. For I am very dear to him, and he is dear to Me...

(Mwema na Ajuaje vyote (Mungu), Yu pamoja na Mimi (Yu ndani yangu nami ni ndani yake katika muungano) kupitia Huduma Takatifu na ni mbora wa vyote, Kwa kuwa mimi Ni mpendwa wake,Na yeye yu kipenzi changu..)

Biblia: .. (Yohana 14:20-21)
At that day ye shall know that I am in union with my Father, and ye in me, and I in you.
(He that hath my commandments, and keepeth them, he it is that loveth me: and he that loveth me shall be loved of my Father, and I will love him, and will manifest myself to him.)
(Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu.
Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.)



6...
Bhagavad gita:.. (Chapter 9 verses 18)
I am the way, the life ,the sustainer,the Lord ,the witness,the abode, the refuge and the most intimate friend. I am the creation and the dissolution, the basis of everything, the resting place and the eternal seed..
(Mimi ni ni Njia,uzima, Muongozaji,Bwana,Shahidi, Mnyenyekevu, Mwokozi,na Rafiki wa karibu,Mimi ni Uumbaji,na Uharibifu,mimi ni Mwanzo wa kila kitu , Sehemu ya Pumziko na Mbegu (Chachu) ya milele.)


Biblia:..(Yohana 14:6)

Jesus saith unto him, I am the way, the truth, and the life: no man cometh unto the Father, but by me.
(Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. )


7....
Bhagavad Gita:..(Chapter 6 verses 30)
For one who sees Me everywhere and see him through everything in Me, I am never depart from Him, and he never depart from me!
(Kwa wanaoniona Mimi kila sehemu,Humuona yeye kupitia kila kitu changu , Naishi kwake na Yeye huishi kwangu (Hajaondoka kwangu na mimi sijaondoka kwake)..

Biblia: Yohana 6:57

As the living Father hath sent me, and I live by the Father: so he that eateth me, even he shall live by me.
(Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi.)


8...

Bhagavad gita:..(chapter 18 verses 66)
I will deliver thee from all sins,Do not grieve
(nitawakomboa kutoka katika dhambi zenu zote,Msifadhaike..)


Biblia: Mathayo 9:2
Son, be of good cheer; thy sins be forgiven thee.
(Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako. )



9.
Bhagavad gita: (Chapter 2 verses 20-21)
They can kill your Body but bot your soul,The soul can never be killed,Except the wise on can..
(Wanaweza kuua MwIli, ila sio roho yako,hawawezi kuua roho isipokuwa Mungu)

Biblia:
Mathayo 10:28
And fear not them which kill the body, but are not able to kill the soul:..
(Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; .)



10.The most interested story ambayo ipo kote kote


Bhagavad gita: chapter 4 verses 2-4

This supreme Knowledge was thus received through the chain of disciplic succession, and the saintly kings understood it in that way. But in course of time the succession was broken, and therefore the knowledge as it is appears to be lost.
That very ancient knowledge of the relationship with the Supreme God is today told by Me to you because you are My devotee as well as My friend; i told this knowledge to vivasvan (sun) and then was given to Manu by Sun..

Arjun said,Many have seen your Birth and your Mother still alive and live among us,how can you said that you instructed this knowledge to vivasvan and you were born many years After him?
lord krisna answer, both you and i have many birth and i remembered them all but you dont remember ,verily before vivasvan born i was...
( Hii ni elimu Takatifu ambayo imekuwa ikirithishwa kutoka kizazi mpaka kizazi yenye masimulizi/mapokeo ya wale waliopewa,Na wafalme watakatifu ambayo inaeleweka hivyo lakini kuna muda ilipata Hitilafu katika uwasilishaji wake kwahyo elimu hii ilipotea hii ndiyo nayokufundisha wewe kwa sababu ni mtiifu kwangu na mwaminifu kama nilivyomfundisha vivasvan na yeye akamdundisha Manu..
Arjuni akasema, watu wengi wameona Ukizaliwa na mama yako bado anaishi miongoni mwetu ,Unasemaje basi kuw umefundisha elimu hii kwa Vivasvan wakati kazaliwa miaka mingi ilopita..
Krishna akajibu,Wote mimi na wewe tumeishi miaka mingi mimi nakumbuka maisha yote ila wewe hukumbuki niamini kuwa
kabla ya vivasvan hajakuwepo mimi nilikuwepo..)

Biblia:Yohana 8:56-58
Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.
Your father Abraham rejoiced to see my day: and he saw it, and was glad.
Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?
Then said the Jews unto him, Thou art not yet fifty years old, and hast thou seen Abraham?
Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Jesus said unto them, Verily, verily, I say unto you, Before Abraham was, I am.




Huu ni mfano tu wa aya hizo Asanteni
 
Miungu mingi hupenda kujitukuza kwa namna mbalimbli

Hivyo sishangai kuwa na maneno yenye ufanano na aliyoyasema yesu

Hata mizimu ya mababu ikipanda huwa inadai yenyewe ndio kila kitu.
 
Miungu mingi hupenda kujitukuza kwa namna mbalimbli

Hivyo sishangai kuwa na maneno yenye ufanano na aliyoyasema yesu

Hata mizimu ya mababu ikipanda huwa inadai yenyewe ndio kila kitu.
Ahhahaha lakini mkuu Krishna ni wa zamani kuliko yesu
 
Back
Top Bottom