Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Hapana mkuu canaan alilaaniwa sababu inadaiwa ham alimlala mama yake yaani mke wa Noah ndio akazaliwa canaan ila nadharia nyingine inasema canaan ndio aliona uchi wa nuhu ndio akaenda kumwambia ham ambaye naye ndio akaenda kuwaambia kina shem na japhet nadharia ya tatu inasema Ham alimuhasi Nuhu ndio maana hakupata watoto wengine baada ya gharika hivyo kwa hasira akamlaani canaan sababu ni kizazi cha HAM maana HAM aliua kizazi cha nuhu pia so bado kuna debate god willing ntapandisha uzi tujadili kwa kina

Kuhusu watu weusi kutokana na canaan kunaweza kuwa na ukweli ila kizazi cha canaan kibiblia kilifutika 90% hivyo hata kma walibaki walimezwa na semites wengine wa mashariki ya kati hivyo wakaishia huko yemen au qatar ila hawakufika afrika however watu weusi hatukulaaniwa kokote kumbuka waafrika wametoka kwa watoto wa ham wale wakubwa yaani Cush mizraim na phut ambao laana ya nuhu haikuwapata hivyo sio kweli kwamba ile laana ndio ilitufanya tukawa weusi na hta kma ni kweli ingemhusu tu canaan ambaye kizazi chake kilishapotea so sioni wapi laana imetufikia waafrika

Ni uelewa wangu tu huu wajuzi wanaweza tusaidia
mitale na midimu Malcom Lumumba Eiyer
Duh! Yani hamu alimgegeda Mama yake? Mkuu, kitabu gani unasoma kupata hizo nadharia nami nikitafute?

Maana Mwanzao 9: 20 na kuendelea mbona inasema Nuhu alilewa kupindukia akawa hajitambui mwisho akakaa uchi ndo huyo Hamu akauona uchi wa Babake.

Pombe zilivomuisha ndo akatambua Hamu kamuona uchi na ndo laana ikaanzia hapo
 
Duh! Yani hamu alimgegeda Mama yake? Mkuu, kitabu gani unasoma kupata hizo nadharia nami nikitafute?

Maana Mwanzao 9: 20 na kuendelea mbona inasema Nuhu alilewa kupindukia akawa hajitambui mwisho akakaa uchi ndo huyo Hamu akauona uchi wa Babake.

Pombe zilivomuisha ndo akatambua Hamu kamuona uchi na ndo laana ikaanzia hapo
Kumbukumbu la torati 27:20
20 Na alaaniwe alalaye na mke wa baba yake, kwa kuwa amefunua mavazi ya babaye. Na watu wote waseme, Amina

Sasa hapa ndio watu wakaja na theory kwa kuwa musa alisema mtu akilala na mamake amemvua babake nguo basi wakaconclude ham alilala na mamake na akabeba mimba ya CANAAN ndio maana akalaaniwa CANAAN na sio ham.....ni nadharia tu mkuu bado sio FACT
 
View attachment 758692
Mfalme OG anatajwa kwenye vitabu vya dini kuu tatu za mashariki ya kati i.e uislam,ukristo na uyahudi....

Inaelezwa alikuwa ni mfalme aliyetawala eneo la Canaan (palestina/israel ama jordan ya sasa )katika ulimwengu wa kale takriban miaka zaidi ya 6000 iliopita.... Na inaelezwa ndio mwanadamu aliyeishi zaidi kutokana na kuwa na mwili mkubwa sana aliishi zaidi ya miaka 3500!!! Alikuwa ni mfalme aliyeogopeka sana mashariki ya kati maana alikuwa jitu lenye nguvu na mrefu zaidi ya minazi kama anavyoelezwa na Nabii Amos

Amos 2:9
9 Lakini nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni; lakini naliyaangamiza matunda yake toka juu, na mizizi yake toka chini.

Umaarufu wa Mfalme Ogu wa bashan umekuja baada ya historia kubainisha kwamba ndio binadam pekee aliyesalia kwenye gharika nje ya Nuhu na familia yake!!

JE ALIPONAJE GHARIKA

1. Nadharia ya kwanza inasema alikuwa mrefu sana kiasi kwamba maji ya gharika yalimfikia kiunoni!!!!

2. Nadharia ya pili inasema kuwa alikuwa na ukaribu sana na Nuhu hivyo alipewa kazi ya kuiangalia safina kwa nje kuhakikisha haigongi mwamba au mawe makubwa ambayo yangeweza kuipasua safina na hiyo ndio ikawa pona yake!!! Inadaiwa alijishikiza pembeni ya safina ya nuhu ivo hakubebwa na maji ya gharika. Nadharia hii ina mashiko sababu hata baada ya gharika tunaona safina hii ilitua palepale ilipokuwa kabla ya gharika yaani haikuenda mbali kabisa kitu ambacho hakiwezekana kama nguvu ya mafuriko ikizingatiwa lazima boti ingesukumwa maili kadhaa mbele. Kingine kwa akili ya kawaida tu dunia nzima izame alafu ww pekee uwe kwenye boti hivi wanaokufa watakuacha kweli?? Lazima wangetaka kuivamia boti waingia na ukizingatia yalikuwa majitu marefu yangeweza kuipasua pasua ila kwa uwepo wa OG walishindwa maana wangekutana na kipigo cha mbwa mwizi!!

3. Nadharia ya tatu inasema kipindi cha gharika Ogu alikuwa bado hajazaliwa ila mimba yake ilikuwa imeshatungwa na mama yake aliekuwa mke wa Ham hivyo ham asingeweza kumuacha nyuma ingawa inadaiwa mimba hiyo haikuwa ya Ham bali ya Malaika aliyeitwa shamael!! Hivyo damu ya wanefili ikaweza kuvuka gharika kwa staili hiyo kupitia mtoto aliyezaliwa yaani mflame ogu ama canaan ambae watoto wake kwenye biblia wanatajwa kma majitu makubwa ambayo yaliona wanadamu kma panzi!!! Mfano amori aruba anak hivi gilgal amoni yebusi n.k

4. Nadharia ya tatu inasema alienda milimani hivyo gharika haikumkuta. Biblia iko wazi kuwa maji yalifunika MILIMA mirefu kwa futi 15 kwenda juu ina maana kma hyu OG alikuwa na futi zaidi ya 13 pengine 28 kama inavyoelezwa kwenye biblia ina maana kama alipanda milima mrefu zaidi basi hakuweza kumalizwa na gharika!! Simple logic

Mwanzo 7
20 Maji yakapata nguvu, hata ikafunikwa milima kiasi cha mikono kumi na mitano.

Najua kufikia hapa wengi mtasema ni upotoshaji na kwamba ni stori za kijiweni ila hoja hii inapata mashiko kupitia biblia kuwa mfalme OGU alikuwa ndio mnefili pekee aliyepona gharika.

Kumbukumbu la torati 3:11
11 (Kwani aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani; tazama, kitanda chake kilikuwa kitanda cha chuma; kitanda hicho je! Hakiko Raba kwa wana wa Amoni? Urefu wake ulikuwa ni mikono kenda, na upana wake mikono minne, kwa mfano wa mkono wa mtu).

hapa biblia inasema OG NI MREFAI ALIYESALIA tafsiri ya kiingereza inasema LAST OF THE REPHAIMS ikimaanisha ni mnefili pekee aliyesalia baada ya gharika!!!!

BAADA YA GHARIKA
Kupitia vitabu vya dini na kihistoria tunaelezwa kuwa baada ya gharika aliendelea kutawala maeneo ya mashariki ya kati eneo la bashan huko Canaan walipoishi majitu mengine kma wayebusi waamori waamaleki wagilgashite n.k na inasemekana aliishi miaka 3500!! Yaani alikuwepo toka kizazi cha adam hadi kipindi wana wa israel wanarudi canaan !!

MWISHO WAKE
Vitabu vya kidini na historia vinasema mfalme OG au UJ BIN ANAQ kiarabu.... Alipambana na waisraeli waliokuwa wametoka misri kuelekea canaan na katika vita hiyo inaelezwa mfalme Og aliweza kunyanyua mlima mzima!!!! Na kutaka kuutupa kwenye kambi ya waisraeli lakini Inadaiwa kwa bahati mbaya au nzuri mlima ukavunjika katikati hivyo ukamnyima balance akaangukiwa na kipande cha mlima hivo kuumia vibaya na ndipo musa akapata fursa ya kumchoma na mkuki na vita ikawa kma imemalizwa na wanajeshi wake kwa hofu wakakimbia huku na kule na waliobaki wakamalizwa na waisraeli

Kumbukumbu la torati 3
1 Ndipo tukageuka, tukakwea njia ya Bashani; na Ogu, mfalme wa Bashani, akatutokea juu yetu, yeye na watu wake wote, kuja kupigana huko Edrei.
2 BWANA akaniambia, Usimwogope; kwa kuwa nimemtia mkononi mwako, yeye na watu wake wote na nchi yake; nawe utamtenda mfano wa ulivyomtenda Sihoni, mfalme wa Waamori, aliyekuwa akikaa Heshboni.
3 Basi BWANA, Mungu wetu, akamtia mikononi mwetu na Ogu mfalme wa Bashani, na watu wake wote; tukampiga, asisaziwe cho chote.
4 Tukatwaa miji yake yote wakati huo; hapakuwa na mji tusiotwaa kwao miji sitini, nchi yote ya Argobu, ndio ufalme wa Ogu ulio katika Bashani.


NB:kwenye vitabu vya kiyahudi vinadai Mungu wao Israel yaani YHWH alishusha nzige/nyuki wakaula ule mlima kutokea katikati ndio ukagawanyika nusu ila najiuliza nyuki waule mlima ndani ya dakika??? Aseee!!!

Anyway hicho ndio kifo cha mfalme huyu aliyetikisa dunia kwa miaka yake na mpaka leo waisraeli wanatambua ushindi ule kma mkubwa kabisa kwenye historia ya taifa lao!! Hata amos na mfalme daudi huwa wanakikumbuka kisa hiko miaka zaidi ya 600 baadae!!!

Amos 2:9
9 Lakini nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni; lakini naliyaangamiza matunda yake toka juu, na mizizi yake toka chini.

Zaburi 135:
10 Aliwapiga mataifa mengi,Akawaua wafalme wenye nguvu;
11 Sihoni, mfalme wa Waamori,Na Ogu, mfalme wa Bashani,Na falme zote za Kanaani


USHAHIDI WA KISAYANSI/KIHISTORIA

Rujm-El hiri or Circle of the rephaites
View attachment 758680
Hii inaelezwa ndio ilikuwa kasri au jumba la ibada la mfalme ogu na mpaka leo masalia yapo huko golan heights, syria (linakaliwa kimabavu na israel).... Mawe yaliyobaki kwa sasa ni zaidi ya 40,000 yamepangwa hadi futi 15 kwenda juu je kuna mtu wa miaka ile angeweza kupanga mawe mazito kwa urefu wa zaidi ya futi 50 kwa wakati huo kama hakua JITU la mfano wa OGU.

2. Karne ya 20 mwanzoni watafiti wa kijerumani waligundua makaburi makubwa ya mawe ambayo yanafanana na hesabu zilizopigwa kuhusu urefu wa mfalme ogu kwenye kitabu cha kumbukumbu la torati..... Kaburi hilo lilipatikana eneo la mto Jabbok, Bashan ambako ndipo mfalme ogu alifia. Na kwa hesabu zao kaburi hilo lina umri wa zaidi ya miaka 6000!!! Muda ambao ndio inasemekana og aliishi hapa duniani
View attachment 758687

3. Mfalme ogu pia alifanikiwa kuandika kitabu chenye sura 7 ambacho kilipatikana takriban miaka 1400 kabla ya kristo ila kilifichwa huko maktaba ya vatican kuaniza karne ya 5 ila baadae kilivujishwa je huu ni ushahidi mwingine kuwa JITU hili liliexist kweli na kuutesa ulimwengu!!!

Karibuni wanajukwaa kwa michango
Naomba kuwasilisha

View attachment 758716
Nimependa sana hii historia imenifanya kwa muda nijaribu kufuatilia historia ya biblia ila nmesoma andiko la mwanzo 15:18-20 inaonekana warefaimu walikua kikundi(jamii) waliojulikana pamoja na jamii zingine na ni tofauti na wanefiri wanaotajwa kwenye mwanzo sura ya 6 pia nimeona 2sam 21:16 inatoa wazo kama warefaimu walikua wakubwa na nguvu kuliko wengine na ilikua jamii kulingana na kitabu kimoja insight on the scriptures kinataja hawa walikua wazao wa mtu mmoja alieitwa Raphah(ha`Ra•phah)
 
Nimependa sana hii historia imenifanya kwa muda nijaribu kufuatilia historia ya biblia ila nmesoma andiko la mwanzo 15:18-20 inaonekana warefaimu walikua kikundi(jamii) waliojulikana pamoja na jamii zingine na ni tofauti na wanefiri wanaotajwa kwenye mwanzo sura ya 6 pia nimeona 2sam 21:16 inatoa wazo kama warefaimu walikua wakubwa na nguvu kuliko wengine na ilikua jamii kulingana na kitabu kimoja insight on the scriptures kinataja hawa walikua wazao wa mtu mmoja alieitwa Raphah(ha`Ra•phah)
Nashukuru mkuu kwa taarifa yako ya kwamba umefanya utafiti kwa kusoma biblia ubarikiwe sana na ndio nia ya mada hii sio kupinga maandiko ila kufanya watu tusome maandiko na vitabu mbalimbali tuongeze maarifa so heshima kwako

Tukirudi kwenye hoja nafkiri warefai kuitwa wanefili ni sawa sababu kiebrania warefai maana yake ROHO ZA MIZIMU yaani kwa kirefu ni UZAO WA ROHO/MIZIMU/MAPEPO/MAJINI.... Hivyo hiyo ni tafsiri sawa na WANEFILI kwa kiebrania....

Ukitaka kuprove hilo soma upya kuna mistari zaidi ya 20 inayotambua warefai kama wanefili tuangalie huu mmoja

Hesabu 13
33 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.

Hivyo tunaweza hitimisha warefai na wanefili ni kitu kimoja

Barikiwa
 
Nashukuru mkuu kwa taarifa yako ya kwamba umefanya utafiti kwa kusoma biblia ubarikiwe sana na ndio nia ya mada hii sio kupinga maandiko ila kufanya watu tusome maandiko na vitabu mbalimbali tuongeze maarifa so heshima kwako

Tukirudi kwenye hoja nafkiri warefai kuitwa wanefili ni sawa sababu kiebrania warefai maana yake ROHO ZA MIZIMU yaani kwa kirefu ni UZAO WA ROHO/MIZIMU/MAPEPO/MAJINI.... Hivyo hiyo ni tafsiri sawa na WANEFILI kwa kiebrania....

Ukitaka kuprove hilo soma upya kuna mistari zaidi ya 20 inayotambua warefai kama wanefili tuangalie huu mmoja

Hesabu 13
33 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.

Hivyo tunaweza hitimisha warefai na wanefili ni kitu kimoja

Barikiwa
Asant sana
 
Kingine huyo musa alimchoma na mkuki may ambaye ni mkubwaaa kana kwamba musa alionekana kama panzi je kwa skill yako panzi anawezakukuchoma na mkuki ukafa?
Namaanisha kama Mimi mwanadamu nina saizi ya panzi kimwonekano hata mkuki wangu ni sawa nakijiti cha unyasi hakuna ukweli hapo

Yasiyo wezekana kwa watu kwa Mungu yanawezekana
Goliath alikuwa jitu kubwa sana DAUD alionekana kama kifaranga na jiwe aliloweka kwenye kombeo ni kama punje ya harage kwa Goliath lakini alianguka jiulize aliangukaje pia mkuki wa Goliath ulikuwa wa shaba uzani zaidi kilo 20 na urefu sawa na mikono sita lakini (huenda DAUD wakati huo alikuwa na kilo 45 maana alikuwa kijana mdogo sana ) lakini aliunyanyua na kumuua goliath
 
Yasiyo wezekana kwa watu kwa Mungu yanawezekana
Goliath alikuwa jitu kubwa sana DAUD alionekana kama kifaranga na jiwe aliloweka kwenye kombeo ni kama punje ya harage kwa Goliath lakini alianguka jiulize aliangukaje pia mkuki wa Goliath ulikuwa wa shaba uzani zaidi kilo 20 na urefu sawa na mikono sita lakini (huenda DAUD wakati huo alikuwa na kilo 45 maana alikuwa kijana mdogo sana ) lakini aliunyanyua na kumuua goliath
Aseee upo deep mkuu umetoa mfano wenye mashiko sana.... ubarikiwe
 
Nadharia No2 mkuu naipinga japo sio msomaji wa bible vizuri ,ila kibinadamu.

Hata angekuwaje hivi kama inavyosema biblia kuwa maji yalijaa duniani kote mikono kumi na tano (mikono kumi na tano ya wakati huosio sasa) ina maana yalikua maji marefu yenye nguvu unadhani kuna kiumbe kingeweza kabisa kushika safina ili kisiangamie kingali nje ya safina?


Na hio hoja ya kusema kuwa watu wangemvamia.. mkuu maji unayajua nadhani hivi yanavyojua kuwa na nguvu mtu unaweza kumvamia mwenzio? au hata kufikiria kumvamia bila kujiokoa.. Haiwezekani kwakweli.
Tuelimishane vizuri
Hio nadharia ya 3 naweza kuikubali ina make sense mkuu.


Nami pia naomba nikuunge mkono kuipinga hoja number tatu, kwa facts kinzani kutoka kwenye maandiko ya biblia kama ifuatavyo;kwa kulinganisha sehemu zilizo in red(hapo chini) ni wazi kuwa maji yalimzidi kimo huyo mfalme Ogu au sio???? naomba kuwasilisha hili........

-Mwanzo 7
20 Maji yakapata nguvu, hata ikafunikwa milima kiasi cha mikono kumi na mitano.

-Kumbukumbu la torati 3:11
11 (Kwani aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani; tazama, kitanda chake kilikuwa kitanda cha chuma; kitanda hicho je! Hakiko Raba kwa wana wa Amoni? Urefu wake ulikuwa ni mikono kenda, na upana wake mikono minne, kwa mfano wa mkono wa mtu).
 
Nami pia naomba nikuunge mkono kuipinga hoja number tatu, kwa facts kinzani kutoka kwenye maandiko ya biblia kama ifuatavyo;kwa kulinganisha sehemu zilizo in red(hapo chini) ni wazi kuwa maji yalimzidi kimo huyo mfalme Ogu au sio???? naomba kuwasilisha hili........

-Mwanzo 7
20 Maji yakapata nguvu, hata ikafunikwa milima kiasi cha mikono kumi na mitano.

-Kumbukumbu la torati 3:11
11 (Kwani aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani; tazama, kitanda chake kilikuwa kitanda cha chuma; kitanda hicho je! Hakiko Raba kwa wana wa Amoni? Urefu wake ulikuwa ni mikono kenda, na upana wake mikono minne, kwa mfano wa mkono wa mtu).
Mkuu vipimo vya kitabu cha mwanzo na kumbukumbu la torati ni tofauti kabisa mind you ilishapita miaka maelfu sasa inakuaje vipimo mlinganishe kama hii ni hoja mbona hatuchukui vipimo vya Nabii Amos aliyemfananisha urefu wake na miti ya mwerezi ilio sawa na MINAZI ya huku pwani

Amos 2:9
9 Lakini nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni; lakini naliyaangamiza matunda yake toka juu, na mizizi yake toka chini

Hivyo tusilinganishe vipimo kwenye karne tofauti na ndio maana kwenye vitabu vya kumbukumbu waisraeli wanasema walikuwa wadogo kama PANZI mbele yao ikimaanisha jamaa walikuwa warefu sana maana huwezi ukawa panzi kwa mtu wa futi 14!! Za karne ya sasa
 
Mkuu vipimo vya kitabu cha mwanzo na kumbukumbu la torati ni tofauti kabisa mind you ilishapita miaka maelfu sasa inakuaje vipimo mlinganishe kama hii ni hoja mbona hatuchukui vipimo vya Nabii Amos aliyemfananisha urefu wake na miti ya mwerezi ilio sawa na MINAZI ya huku pwani

Amos 2:9
9 Lakini nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni; lakini naliyaangamiza matunda yake toka juu, na mizizi yake toka chini

Hivyo tusilinganishe vipimo kwenye karne tofauti na ndio maana kwenye vitabu vya kumbukumbu waisraeli wanasema walikuwa wadogo kama PANZI mbele yao ikimaanisha jamaa walikuwa warefu sana maana huwezi ukawa panzi kwa mtu wa futi 14!! Za karne ya sasa


Ila mkuu Zitto unaposema tusilinganishe vipimo vya karne tofauti natatizika kidogo....maana hoja inabaki kuwa garika ilitokea karne moja wakati huyo mfalme Ogu akiwa bado yupo au sio???....na si ndo maana kichwa cha Uzi kinasema mfalme aliyepona kwenya gharika......au gharika zilikuwa mbili kwa utofauti wa karne na uwepo wa mfalme Ogu????......pia niogezee kuwa kitabu cha mwanzo na kumbukumbu LA torati vinabiki kuwa ni vitabu tu vilivyo rekodi tukio husika pasipo kujali viliandikwa wakati gani!!....

Naomba kuwasilisha hoja mkuu!!!
 
Ila mkuu Zitto unaposema tusilinganishe vipimo vya karne tofauti natatizika kidogo....maana hoja inabaki kuwa garika ilitokea karne moja wakati huyo mfalme Ogu akiwa bado yupo au sio???....na si ndo maana kichwa cha Uzi kinasema mfalme aliyepona kwenya gharika......au gharika zilikuwa mbili kwa utofauti wa karne na uwepo wa mfalme Ogu????......pia niogezee kuwa kitabu cha mwanzo na kumbukumbu LA torati vinabiki kuwa ni vitabu tu vilivyo rekodi tukio husika pasipo kujali viliandikwa wakati gani!!....

Naomba kuwasilisha hoja mkuu!!!
Mkuu ukisoma biblia ya kiebrania hayo maelezo ya mikono 9 ni zaidi ya futi 28 !!! Maana wanadai MIKONO ilipimwa kwa kutumia mikono ya wacaanani yaani wanefili wenzake na ogu sio mikono ya zitto junior ama Mshana Jr .....

Mfalme OGU kwa simulizi hizi aliishi miaka kati ya 2000 hadi 3500 sababu ya ukubwa wake..... Kwahiyo ukisoma TALMUD yaani biblia ya wayahudi ambao ndio walimuona uso kwa uso... Talmud sura ya 61 utagundua hilo suala na hoja ya kwamba aliishi kuliko mwanadamu yeyote yule na alipona gharika hadi kuja kuuawa na MUSA

Kwahiyo kwa kujibu hoja yako ni kwamba tokea ogu anapona gharika hadi anakufa HAIKUWA WAKATI MMOJA ni GAP la miaka zaidi ya 1000

Ahsante
 
Mkuu ukisoma biblia ya kiebrania hayo maelezo ya mikono 9 ni zaidi ya futi 28 !!! Maana wanadai MIKONO ilipimwa kwa kutumia mikono ya wacaanani yaani wanefili wenzake na ogu sio mikono ya zitto junior ama Mshana Jr .....

Mfalme OGU kwa simulizi hizi aliishi miaka kati ya 2000 hadi 3500 sababu ya ukubwa wake..... Kwahiyo ukisoma TALMUD yaani biblia ya wayahudi ambao ndio walimuona uso kwa uso... Talmud sura ya 61 utagundua hilo suala na hoja ya kwamba aliishi kuliko mwanadamu yeyote yule na alipona gharika hadi kuja kuuawa na MUSA

Kwahiyo kwa kujibu hoja yako ni kwamba tokea ogu anapona gharika hadi anakufa HAIKUWA WAKATI MMOJA ni GAP la miaka zaidi ya 1000

Ahsante
Hivi mtu wa futi 28 akionekana leo pale mitaa ya posta mida kama ya mchana hivi, si itakuwa patashika nguo kuchanika watu kutoka ndukiii....!!!

Itakuwa ni kuanguka na kuzimia. Me futi tano manake kwa Ogu naingia mara tano na bado futi tatu atanidai duuuh!!! Mungu katuficha mambo mengi jamani....!!!!

Na kwanini iwe hivyo wakati katuumba yeye???
 
Hivi mtu wa futi 28 akionekana leo pale mitaa ya posta mida kama ya mchana hivi, si itakuwa patashika nguo kuchanika watu kutoka ndukiii....!!!

Itakuwa ni kuanguka na kuzimia. Me futi tano manake kwa Ogu naingia mara tano na bado futi tatu atanidai duuuh!!! Mungu katuficha mambo mengi jamani....!!!!

Na kwanini iwe hivyo wakati katuumba yeye???
Kwa namna moja inaweza kuwa Mungu ndio alitaka wanadamu wa kale wawe hivo sababu ya umri waliokuwa wakiishi..... Yaani mtu aliishi miaka 900+ kama Adam au Methuselah ni lazima mwili uwe wa kibabe ili iweze kuhimili miaka yote hiyo sidhani kama unaweza kuwa na kamwili kama wa joti alafu uishi miaka 900 never!! Sijasoma biology au genetics ila kwa mtazamo wangu naona kuna connection kati ya UIMARA wa mwili na kuishi miaka mingi

Na ndio maana baada ya kupunguza umri wa wanadamu yaani baada ya gharika tunaona watu waliishi miaka sio zaidi ya 300 na ndio maana hata majitu makubwa yalipungua yakabaki yenye damu ya wanefili pekee!! Hii pia inaweza kuongezea sababu kwenye hoja yangu ya hapo juu kuhusu UMRI=UIMARA WA MWILI

Hoja kinzani itasema kuwa huenda kuna ukweli kuwa walikuwa kizazi cha kitofauti yaani mchanganyiko wa kizazi cha nyoka + na kizazi cha Mungu na ndio maana wakazaliwa watu warefu na wenye nguvu za ajabu ni katika kipindi hiki ndipo simulizi za majitu mashujaa kma nimrod Saigon gilgamesh na Hercules Zilikuwa kipindi hicho hadi wakaitwa MIUNGU kwa wakati wao hivo hoja ya uzao wao kutokuwa wa kibinadamu inapata mashiko hapa sababu tuliona uzao wa wanadamu wengine nje ya wanefili hawakuwa warefu sana kufikia hawa warefai/wanefili

Anyway labda watalaamu wa genetics wanaweza kusaidia hapa cc Kiranga
 
Kwa namna moja inaweza kuwa Mungu ndio alitaka wanadamu wa kale wawe hivo sababu ya umri waliokuwa wakiishi..... Yaani mtu aliishi miaka 900+ kama Adam au Methuselah ni lazima mwili uwe wa kibabe ili iweze kuhimili miaka yote hiyo sidhani kama unaweza kuwa na kamwili kama wa joti alafu uishi miaka 900 never!! Sijasoma biology au genetics ila kwa mtazamo wangu naona kuna connection kati ya UIMARA wa mwili na kuishi miaka mingi

Na ndio maana baada ya kupunguza umri wa wanadamu yaani baada ya gharika tunaona watu waliishi miaka sio zaidi ya 300 na ndio maana hata majitu makubwa yalipungua yakabaki yenye damu ya wanefili pekee!! Hii pia inaweza kuongezea sababu kwenye hoja yangu ya hapo juu kuhusu UMRI=UIMARA WA MWILI

Hoja kinzani itasema kuwa huenda kuna ukweli kuwa walikuwa kizazi cha kitofauti yaani mchanganyiko wa kizazi cha nyoka + na kizazi cha Mungu na ndio maana wakazaliwa watu warefu na wenye nguvu za ajabu ni katika kipindi hiki ndipo simulizi za majitu mashujaa kma nimrod Saigon gilgamesh na Hercules Zilikuwa kipindi hicho hadi wakaitwa MIUNGU kwa wakati wao hivo hoja ya uzao wao kutokuwa wa kibinadamu inapata mashiko hapa sababu tuliona uzao wa wanadamu wengine nje ya wanefili hawakuwa warefu sana kufikia hawa warefai/wanefili

Anyway labda watalaamu wa genetics wanaweza kusaidia hapa cc Kiranga
Umenene Vyema
 
kweli mkuu, hata jamaa zitto junior anatusaidia kurudia kuisoma bibilia kwa akili na kwa maarifa.
anachokifanya waumini wengi hatujui, ikiwa sio mfuatiliaji utaona ni mambo mapya.

huyu jamaa, alinifanya nisome document moja ambalo nililichukua kutoka kwa mwanatheolojia mmoja msabato aliyofundishwa huko chuoni bugema uganda. Lilinishinda kuelewa, ila baada ya kukutana na bandiko lake la epics of gilgamesh na hadithi za zamani za mafuriko ya nuhu, akkida, summerian flood etc nilirudi fasta na nikajikuta nasoma kama maji na kuongeza uelewa...

tusome bibilia mpendwa...
Kweli mkuu
 
Wadau nimeona ITV habari za saa mbili usiku, wazee wa Ntwara aka Mtwara wameitaka serikali kulitumia pango flani hivi lipo huko ambalo wajerumani walilitumia kujificha wakati wa vita vya dunia. Pango Hilo linaitwa nyumba ya mungu sababu halijachongwa na mtu. Lina vyumba kibao. Lkn kingine walichongundua juu yake ni makaburi ya watu yaliyokuwepo juu ya huo mlima. Makaburi hayo ni ya watu waliokuwa na urefu wa futi nane hadi kumi. Hii inaendelea kuthibitisha hizi habari za giants existence pande hizi za bongo
 
Og aliweza kukata mlima, kuubeba na kuutupa? Na bado akaishi akapona gharika nje ya safina, wakati ambapo maji yalichukua mwaka mzima kukauka, nadharia nyingine, zinataka uvumilivu, kuzielezea!
 
Back
Top Bottom