Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

zitto junior kwanza hongera kwa utafiti uliofanya,umefukua sehemu nyingi sana. Ila nakataa hoja yako.

1. Wanefili walikua nusu malaika nusu binadamu na hakuna alieponyoka gharika. Wengine walijivua miili ya kibinadamu na kurudi mbinguni na wengine waliangamizwa.

2. Baada ya gharika dunia ilikuwa na wanadamu 8 tu. Unaweza kupitia tena Mwanzo sura 6 na ya 7 inatosha kabisa kukupa jibu.

3. Mfalme Ogu alikuwa Mrefaimu (kabila)kuna tofauti na wanefili na warefaimu. Warefaimu walikuwa warefu kiasili hata Goliathi alikuwa na asili hiyo.

Natamani sana kujadiliana mengi na wewe, inaonekana unaijua biblia kwa kiasi niPM kama vip
Nashukuru kwa insight zako makini, lakini utusaidie kuhusu huu mstari kama basis ya Hoja.

Hesabu 13:33
33 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.

Assuming wote walikufa kwa gharika iliwezekana vipi hawa wana wa Yakobo wawaone tena kule Canaan?

Kuhusu watu 8 kupona unajua its tricky bible ikisema WATU specific inaweza kuwa ni walengwa tu..... Mfano

YUDA
14 Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu

Lakini ukisoma mwanzo utagundua Cain alishazaa vizazi vingi mpaka seth anazaliwa ambaye ndio lineage ya Henoko. So haiwezekani akwa literally mtu wa 7 kama Yuda anavyosema? So naweza adress hivo hiyo nadharia ya watu 8 kupona kwamba ili focus kwa context ya eneo hilo.
 
Swali muhimu ni , je, mama yake alikuwa mtu wa namna gani.
Mkuu hata watu warefu duniani walizaliwa tu kma mimi na wewe sema wanaendelea kukua kwa kasi ya ajabu kuliko average human being kwa sababu za kijenetiki. So Mama yake hta akiwa Giant au mtu wa kawaida bado angezaa mtoto wa kawaida tu ila baada ya mwaka ukuaji wake unakua tofauti na watoto wenzie waliozaliwa siku moja.

But kwa muktadha huu kulikua na kizazi kabusa cha ma giants kwenye biblia tunaona koo kma Anakim, Rapha, zinatajwa kama majitu makubwa kuliko kawaida. Mfano soma 2 Samuel 21 kuna njemba zenye mikuki ya kilo 7 so unaweza ona Walioa na kuzaliana wakiwa giants kabisa.

Hata kwenye Quran ukisoma Surat Hud utaona alitumwa kwenda kwenye jamii ya giants ambao walikua wakubwa kuliko average humans waliitwa AaD. So unaweza ona ni hereditary Mama akiwa giant na mtoto naye giant.
 
Grahnman. Mkuu kwani kuandika malaika kulishindikana nini mbona bible haiandiki vitu kwa kuficha kama bible inaandika wafiraji sembuse kuandika malaika ukweli unabaki wanefili ni wanefili na malaika ni malaika huu ndio ukweli wa maandiko.
Na wanefili walikuwako kabla ya wanadamu

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Mwanzo 6 :4
mi sijaona sehemu inasema wanefili walikuwepo duniani kabla ya binadamu
 
Nadhani huyu Ogu alipona na gharika japo hatujui ni kwa jinsi gani,vinginevyo inabidi tuambiwe ilkuwaje Wana wa Israel wakamkuta tena huko Kaanani ilihali viumbe wote walikufa kipindi cha Gharika isipokuwa familia ya Nuhu tu.

Swali langu lipo hapa:

Hesabu 13:32 SRUV

Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala wakazi wake; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu wakubwa mno.

Je huyu Ogu na wakazi wa nchi yake walikuwa wakila watu?naombeni ufafanuzi hapa,kama ni kweli.
 
zitto junior. Kuna vitu tumefichwa lakini ukweli ni kuwa Mungu alimuumba mwanadamu kukiwa kuna maisha ya viumbe kama binadamu tayali.
Na sijui kwanini Mungu aliamua kutupunguzia maisha wakati viumbe wake waliotutangulia ndio wametufanya tuingie katika majaribu ya kutuhadaa

Ushahidi wa viumbe waliokuwepo kwa mjibu wa Biblia

5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.
Mwanzo 3 :5

Hapa Mungu anatufananisha na viumbe waliotangulia hapa kuna kitu ukitafakari unapata jibu la kuwepo maisha yaliyoendelea

3 Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.
Mwanzo 6 :3
Kwanini Mungu atupunguzie umri ili hali yeye ndiye katuumbia vitu vya kutupotosha?

Kwanini Mungu asingetupeleka sayari nyingine tuanze maisha yetu yasiyo na mchanganyiko wowote?

Kwanini Mungu asinge tupeleka hata kwenye nyota (jua) proxima century mbali na hapa tukawa mbali na wanefili?

Maana wanefili bado wanaishi ila Mungu kawapunguzia uwezo wa nguvu lakini ndiyo jamii zenye ushawishi na nguvu kiuchumi kuindesha Dunia ndio wazungu wenye macho njano.

Kwa picha hii ni uthibitisho tosha kuwa wapo ila hawana nguvu za mwili ila wamebaki kiakili
Ya wezekana
 
Back
Top Bottom