Commonwealth realms ni muunganiko wa nchi 14 zilizopo chini ya Ufalme wa Uingereza. Hizi ni nchi ambazo Mkuu wa Nchi yao (Japo ni ceremonial tu) ni Mfalme, kiongozi wa Serikali ni Waziri Mkuu.
Nchi hizi ni kama Uingereza yenyewe, Canada, Australia, Grenada, n.k. Hawa ndiyo wana haki ya kusema "he is not my king" kwa kuwa kodi zao zinatumiwa na Ufalme.
Commonwealth countries ni Muunganiko wa nchi 56 (ukitoa Uingereza) ambazo nyingi zake zilikuwa chini ya Ukoloni wa Uingereza (Nchi nyingine kama Rwanda, Togo, n.k. hayakuwa makoloni ya Uingereza).
Sasa hapa ndiyo kuna nchi kama Tanzania, Kenya, Uganda, n.k. Lengo la Muungano huu ni kutumia Ushawishi wa Uingereza (na Ufalme wake) kupata fursa mbalimbali kama attention juu ya changamoto wanazozikabiri, misaada, faida za kibiashara, n.k.
Hizi nchi hazipo chini ya Ufalme wa Uingereza, sema zinatumia Ushawishi wa Uingereza kufaidika lakini pia Uingereza inaendeleza ushawishi wake kwenye masuala kama ya Demokrasia, n.k.
Raia wa Commonwealth countries hamna haki ya kusema "he is not your king" kwa kuwa hakuna kodi yoyote anayoitumia kutoka kwenu. Nyie ndiyo mnafaidika naye zaidi.