Zack Abdul
JF-Expert Member
- Mar 9, 2026
- 319
- 314
1. Mohamed Chande Othman ni jaji mwenye uadilifu mkubwa na ujuzi wa hali ya juu katika sheria.
2. Amewahi kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania (2010-2017), akiongoza mahakama kwa haki na uwazi.
3. Aliaminiwa na Umoja wa Mataifa kufanya kazi za haki za binadamu, jambo linaloonyesha uaminifu wake.
4. Alikuwa miongoni mwa waanzilishi (pioneer) wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), akionesha uwezo mkubwa katika sheria za kimataifa.
5. Amefanya kazi kama mwendesha mashtaka wa kimataifa katika kesi muhimu (Timor-Leste na Rwanda).
6. Aliongoza Tume ya kuboresha mfumo wa haki jinai nchini Tanzania, iliyoleta mapendekezo muhimu ya kuboresha mfumo wa haki jinai Tanzania.