Mfahamu dereva aliyetumia saa 12 Dar - Songea miaka 90

Mfahamu dereva aliyetumia saa 12 Dar - Songea miaka 90

Mbona huyo cha mtoto, kulikuwa na ligi ya masia express Tzj 3360 matema beach Tzj 7104 , Tawaqal Tzk110 etc , hizi zilikuwa zikikutana dae mnaingia saa nane mchana ,yani kipindi cha dj show ya radio one ya kina mike mhagama ndo kinaanza
Hood ye alikuwa ana game lake la kuingia saa kumi Tunduma ,
Mkwema bus Msm 34 , nayo ilikuwa inaingia Tunduma saa kumi jioni , ikitokea Dar.
Umenikumbusha Mwanahapa a.k.a M Sleeping Coach
 
Yes mkuu hii Matema Beach Yes ilikua ni moto, pia kiswele route ya dar to songea hii bus nayo ilitamba sana, eti leo unatoka Dar saa 6am na unaingia tunduma 20:00hrs, si bora nipande baiskeli
Na watu wanasifia sauli na dazu ya golden ati zinakimbia , huwa nachefuka sana
Adidas ya Tawfiq ilishwahi kukamatwa overspeed mpemba saa tisa alasiri , yani mwamba (almarhum mzee jamali )alikuwa nanaenda kuweka rekodi ya kuingia Tunduma saa tisa na robo
 
Safina na zile Scania zake nyekundu aisee. Nissan Diesel (Saitama na Yokohama) zilikuwa ni special kwa njia ya Mbeya Sumbawanga

Miaka ya karibuni walioweza kidogo kuurudisha ule moto walikuwa Nganga, Happy Nation na Majinjah...

Wateja wakubwa walikuwa wafanyabiasha na madavoo wa IT, hapo raia wanawaishwa kuja kufunga mzigo K'koo kesho yake wageuze chap...

Nishawahi kupanda Happy Nation, toka Mbeya na ikafika Dar saa kumi kasoro jioni...(hii ni 2000 mwanzo hapo)...
 
hayajapita masaa 24 toka Tanzanite Bus ichinje watu 10 Singida, ambao bado hawajazikwa wala kutolewa kwenye mabati ya basi, tushasahau, tuko hapa tunawajaza upepo madereva wanaokwenda kasi wazidi kushindana.....

vichwa panzi vya abiria wa dunia ya tatu.... Foolishness distilled...
 
Ni miaka ile ya 90. Ni Likungu Trans, ISUZU MV 118, TZK6150, Dar Njombe Songea. Dereva Selepion huyo wa Katikati na aliyeshika kiuno ni Juma Ndang'o.

Alisumbua sana njia ya Songea - Dar. Alishawahi kuingia Songea saa 12 kasoro jioni akitokea Dar, dereva, alikuwa ni Selepion.

Ilikuwa ni vigumu sana kuamini kama ISUZU inaweza kukimbia hivyo. Lakini Likungu ndiyo ilikuwa hivyo. Hatari sana, watu wa Songea hawawezi sahau hii gari.

Hakuna kitu cha namna hiyo usidanganywe! Labda kama alikuwa anaendesha helkopta! Basi likiondoka Dar saa 12 asubuhi linaingia Njombe saa 12 jioni, na toka Njombe hadi Songea ni masaa matatu na nusu hadi manne. Unamdanganya nani wewe!
 
Unaikumbuka Upete Television Coach, je Safina au ile Zainab za zamani (achana na zile Volvo), au Kwacha (Nissan Diesel) na mtemi wa kusini enzi hiyo Kiswele
Mkuu umeua kabisa mada hii, yeee Safina hii bus(mahenge wa kibao mufindi)ilikua majembe sana n dereva wao yoso!,zainab za mwanzo iringa to Dar, kwacha kwangu ni Ile bus ya Navolonge swela CD Leyland, Ile bus ikishamaliza kitonga pass, tuonane mnazi mmoja stendi,Scania zote zitafuata nyuma
 
Ni miaka ile ya 90. Ni Likungu Trans, ISUZU MV 118, TZK6150, Dar Njombe Songea. Dereva Selepion huyo wa Katikati na aliyeshika kiuno ni Juma Ndang'o.

Alisumbua sana njia ya Songea - Dar. Alishawahi kuingia Songea saa 12 kasoro jioni akitokea Dar, dereva, alikuwa ni Selepion.

Ilikuwa ni vigumu sana kuamini kama ISUZU inaweza kukimbia hivyo. Lakini Likungu ndiyo ilikuwa hivyo. Hatari sana, watu wa Songea hawawezi sahau hii gari.
Okalla na Yoge wa Kiswele walikuwa wanatoka Dar saa 12 asubuhi na kufika Songea saa 11 jioni

Kadhalika John Africa na Mapunda wa Special couch

Sasa mchizi Rwambo wa Kiswele alikuwa anaingia saa 9:45
 
Hakuna kitu cha namna hiyo usidanganywe! Labda kama alikuwa anaendesha helkopta! Basi likiondoka Dar saa 12 asubuhi linaingia Njombe saa 12 jioni, na toka Njombe hadi Songea ni masaa matatu na nusu hadi manne. Unamdanganya nani wewe!
No mkuu why bus itembee 700km kwa masaa 12,it's craze mkuu,huu ni mwendo wa masaa 8 tu,soma hii kutoka kapiri mposhi hadi nakonde ni 800km,power tools anafukia hiki kipande kwa 8hrs na hakuna ajali yeyote
 
Hakuna kitu cha namna hiyo usidanganywe! Labda kama alikuwa anaendesha helkopta! Basi likiondoka Dar saa 12 asubuhi linaingia Njombe saa 12 jioni, na toka Njombe hadi Songea ni masaa matatu na nusu hadi manne. Unamdanganya nani wewe!
Usikariri

Lupelo yenyewe na Widambe zilikuwa zinaingia Njombe saa 9 ndio viwe Vyuma vya Songea!!

Okalla, Rwambo na Yoge walikuwa wanapita Njombe saa.7 na zile.Kiswele
 
No mkuu why bus itembee 700km kwa masaa 12,it's craze mkuu,huu ni mwendo wa masaa 8 tu,soma hii kutoka kapiri mposhi hadi nakonde ni 800km,power tools anafukia hiki kipande kwa 8hrs na hakuna ajali yeyote

Kwa hiyo hapa mnachojadili ni nini?
 
Miaka ya karibuni walioweza kidogo kuurudisha ule moto walikuwa Nganga, Happy Nation na Majinjah...

Wateja wakubwa walikuwa wafanyabiasha na madavoo wa IT, hapo raia wanawaishwa kuja kufunga mzigo K'koo kesho yake wageuze chap...

Nishawahi kupanda Happy Nation, toka Mbeya na ikafika Dar saa kumi kasoro jioni...(hii ni 2000 mwanzo hapo)...
Yooooo Nganga nhe, nini kiliua makampuni haya jamani?
 
Kwa hiyo hapa mnachojadili ni nini?
Jadili hoja sio matusi, hakuna aliyekuita wewe any names, show respect kama huvutuwi na mada no one kakushikia bunduki ujibie, soma mada zingine mkuu, wewe kwa upeo wako unaona speed but wengi wetu we bring back our good memories, next time shirikisha ubongo kabla ya kujibu mada humu
 
Back
Top Bottom