Meya Boniphace Jacob amfungukia RC Makonda

Meya Boniphace Jacob amfungukia RC Makonda

Usipoteze mjadala kwa kuanza ku personalize ishu! Utumishi wa umma ukoje? Ukaguzi wa vyeti kwa watumishi wa umma unawahusu wakuu wa mikoa? Hayo ndio mambo mimi nimeona uyafahamu, kwangu makonda sio ishu, ishu na uelewa wako juu ya utumishi wa umma. Ungefahamu taratibu zilizvyo kwanza ndipo ungekuwa na uwanja mpana wa kujadili au kukiwasilisha hicho ulichotaka kukiwakilisha. Kuwakilisha jambo ambalo hulifahamu sawasawa si vyema, pengine ulikuwa na mawazo mazuri lakini kwa kuwa hufahamu vitu fulani fulani basi uwasilishaji wako ukavizwa. Makonda ni muda tu, nae atapita lakini taratibu zetu za kuongoza nchi zikoje basi? Zina ubora na uimara kiasi gani? Je kwanza tunazifahamu uzuri?
Nafikiri mleta uzi hajaleta mjadala wa taratibu za utumishi wa umma,ka base kuonesha udhalilishaji wa Makonda kwa watumishi na wasomi halali wa nchi hii!,kasababisha wasomi wafukuzwe kazi ivi unajua uchungu wa kusoma/kusomesha wewe?

Watu wanalia kukosa nafasi ya kusoma kwa umasikini na wengine kusoma kwa shida alafu kilaza anafanya usanii kwenye kibalua chao!

Mkuu inauma sana mtu kilaza akuchongee ukose kazi!

Kama unahisi Watanzania hatujui taratibu za utumishi wa umma unaweza anzisha uzi utupe elimu ila kwasasa tunajadili madudu ya huyu Mungu wa Dar!
 
Mtu anaepata division zero hivi ndio viwango vyake, dharau, kiburi, majivuno nk usitegemee mtu anaeshindwa kupata D hata 3 anaweza kutumia akili. Akili alizonazo ni za kuvukia barabara na si za kuishi na watu, wafanyakazi, nk.
mama kubwa kupata div 0 si mwisho wa maisha na wala haimaniishi huyo mtu hana faida kwa jamii yako wala si kiashiria cha ubora na wala uwezo kuongoza kwa level za ki mkoa au kibunge.
 
Plus, Kama nia ni kuondoa vihiyo, anza kuomba cheti cha Mbowe ambacho kimeshapigiwa kelele sana.
 
Ni kwamba alinunua vyeti original vya mtu, au ana vyeti vya kughushi naomba ufafanuzi kidogo [emoji412]
 
Ahahaha mako nipo karibu na bwana MKUBWA ngoja tuone maana wapo ....
 
Dear
Daudi Albert Bashite.

Naanza na salamu na badala ya salamu ni kujua kama umeamka vizuri hapo kwako Masaki,na shemeji yetu naye natumaini ni mzima wa Afya.

Kwa uchache wa Muda naomba niende moja kwa moja kwenye dhumuni langu la kukuandikia ujumbe huu,hakika ujue sikupi pole sababu mambo Mengi umejitakia katika safari yako ya kisiasa,iliyo jaa vishindo na mbwembwe za kila aina.

Vijana wenzio tulibahatika kufanya kazi na wewe Daudi, kwakweli hatukuwahi kujua siri ya "kiburi" chako na "majivuno" yako uliyatoa wapi? Kwa jinsi ulivyokuwa kijana wa "Mission impossible" katika kila matendo ya vijana wa kaida yanayotarajiwa wewe ulitenda yale ambayo watu wasinge tarajia kuona,

Na hayo ndiyo yakawa maisha yako,hukujali wakubwa wanastahili heshima,hukujali kila binadamu anastahili staha,huku jali viongozi kama Mawaziri wa kuu au majaji wataafu walipaswa kulindwa na kuhifadhiwa.

Leo kabla Dunia haijaona mwanzo mpya au mwisho wa safari yako,kwakuwa Kwa namna yoyote vile tuta ulilokutana nalo Masihani mwako halitakuacha kama awali,utabadilika tuh utake usitake Hata kama mabadiliko yako yawe ya Nafasi au Nafsi yanakukuta kwa aibu na fedheha.

Walio karibu yako Daudi wanadai unawakati Mgumu,tukuombee,sitaki kuwa mnafki kwako,Daudi nikwambie tuh sitokuombea bali kabla ujamaliza kujutia Nafsi yako nikukumbushe tuh machache ili uyaingize kwenye sala ya toba.

1.Akilini kwako unamkumbuka baba wa watu? Mkurugenzi injinia mussa Natty,ulivyo muandama mpaka kusimamishwa kazi ulipokuwa DC KINONDONI? huku jali elimu yake aliyosomeshwa na wazazi wake masikini huko shinyanga,kwa UBASHITE WAKO ukamuumiza yeye na familia yake.

2.Je unawakumbuka wahandisi wa Halmashauri ya manispaa ya Kinondoni?,uliowasemea Mbele ya mheshimiwa Rais,siku ile Pale Biafra,wenzio wakasimamishwa kazi,na kuhamishiwa vijijini,hukujali elimu yao ya kweli si kama yako,waliyo ipata kwa shida wala familia zao masikini zilizo wategemea,Kwa UBASHITE WAKO ukawatokomeza na kuwaharibia majina na kazi zao.

3.Je unawakumbuka Maafisa ardhi? ukitoa amri wakamatwe kule Wazo mivumoni tuh kwa sababu walichelewa kufika eneo la tukio baada yako,hukujali Elimu zao na utaalamu wao wa ardhi waliosotea mashuleni na vyuoni ,kitichako kilikuwa na mamlaka ya kuwalaza wote sita mahabusu kituo cha mabatini KWA UBASHITE WAKO ukajiona wewe ni alpha na omega.

4.Je unamkumbuka yule dada Afisa ardhi uliye Muita "Tahira" kule kwenye mkutano wako mabwepande? Tena mbele za Tv na Radio zikiwa Mubashara,Hukujali mwenzio ana vyeti halali na amepimwa kwenye mitihani na amefaulu, KWA UBASHITE WAKO ukaona hakuna atakacho kufanya wala pakukimbilia.

5.Je unakumbuka ile kauli yako kwamba wewe ufanyalo Dar es salaaam,na kuliamua juu yake ni kwamba ameamua Mungu,Hata watu walipo toa miguno ya kulewa kwako madaraka hukuwahi kujutia kijivika utukufu wa Mungu,wala kujifananisha naye au kujipa unabii juu ya Dar es salaam,KWA UBASHITE WAKO ulidhani na yeye Mungu alipata zero? Au Mungu alinunua vyeti?

6.Je unaikumbuka ile kauli yako ya mara kwa mara uliyopenda kuitoa kwamba "Mimi nimbabe wa vita" ulimaanisha vita vya kufeli na kufanya "manuva" vita ya kutorudia au kukariri Darasa? Na ukazani umevishinda vita kwa kununua jina jipya, KWA UBASHITE WAKO,Ukasahau kuwa wazungu wanasema "There is no short cut in alife" isipokuwa wewe ukazani umeyapitia Denge maisha,wenzio wasome wafaulu,wewe ufeli ujekuwa boss wao.

7.Je unakumbuka Ile kauli yako ya kuwa ofisi ya mkuu wa mkoa Dar es salaam nzima inawafanyakazi 4,wengine wote ni mizigo? ,sasa utawaonea wivu hao mizigo kwakuwa wenzio wanavyeti na walifaulu wapo kihalali serikalini basi huenda utawaacha hapo na wewe mzigo namba moja utaondoka badala yao.KWA UBASHITE WAKO uliona kila mtu aliyesoma vigezo siyo kusoma ila ujanja kama uliotumia wewe.

Na mengine Mengi sababu ya Muda Nikuache na hayo,Niwache na boss wako muamue Mpangiane kazi gani nyingine,na kwa bahati mbaya mfumo wa nchi yetu,mwenye division zero,hastahili kuwa hata Dereva serikalini.

Fedheha na aibu imepanda gari lako la kifahari,imeingia ndani ya jumba lako hapo masaki,walinzi wote polisi na wanajeshi wameshindwa kuizuia,ipo mpaka sebuleni na sasa ujue Dar es salaam haitokubali itawaliwe na kuongozwa na KILAZA.......KUSOMA RAHA SANA

Na
BONIFACE JACOB
Senior councilor ubungo
Mstahiki meya
Manispaa ya ubungo
Shikamoo meya, muosha huoshwa!!!!!!!![emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Nafikiri mleta uzi hajaleta mjadala wa taratibu za utumishi wa umma,ka base kuonesha udhalilishaji wa Makonda kwa watumishi na wasomi halali wa nchi hii!,kasababisha wasomi wafukuzwe kazi ivi unajua uchungu wa kusoma/kusomesha wewe?

Watu wanalia kukosa nafasi ya kusoma kwa umasikini na wengine kusoma kwa shida alafu kilaza anafanya usanii kwenye kibalua chao!

Mkuu inauma sana mtu kilaza akuchongee ukose kazi!

Kama unahisi Watanzania hatujui taratibu za utumishi wa umma unaweza anzisha uzi utupe elimu ila kwasasa tunajadili madudu ya huyu Mungu wa Dar!

Sasa mjadala hauwezi kuwa haphazadly na wa upotoshaji. Unapodai kuwa ukaguzi wa vyeti ulifanyika kwa watumishi wa serikali halafu unashangaa mbona Makonda hakufanyiwa uhakiki ina maana unafikiri wakuu wa mikoa ni waajiriwa serikalini. Wengine wakisoma wanaweza wakaamini. Hilo mimi ndio nakataa. Mtu unapojadili elimu na kazi ya Makonda yakupasa ujue yeye ni mteuliwa wa rais na sifa za uteuzi zikoje. Inawezekana ukadhani mambo ya vyeti madudu ya Makonda kumbe ni madudu ya mtu mwingine kabisa. Kama madudu ya Makonda yapo katika utendaji wake sawa akosolewe kama alivyowakosoa wenzake. lakini pia kusema Makonda alifanya makosa alipowakosoa watendaji wazembe hili nalo si sawa. Aidha kama tumeamua kuwa wanafiki au tumeamua kuwa taifa lilioza na kulea uozo. Kila mmoja kwa nafasi yake afanye kazi kwa kutenda haki, asimuonee wala kumpendela mtu hii ndio maana ya check and balance. Usipowashughulisha walio chini yako utashughulikiwa wewe, ukiwashughulikia wenzako iko siku moja na wewe ukikosea utashughulikiwa. Hakuna ubaya katika hilo. Ubaya ni pale kuonesha kushughulikiana eti ni jambo baya. Ili tutoke hapa tulipo ni lazima tuwe wakweli, tukosoe na tukubali kukosolewa, tuwataje wale unga na sisi watutaje katika mambo yetu yaleeee. Nyumba itakuwa safi, tuache kulea uozo na tujishughulishe kufahamu taratibu.
 
Dear
Daudi Albert Bashite.

Naanza na salamu na badala ya salamu ni kujua kama umeamka vizuri hapo kwako Masaki,na shemeji yetu naye natumaini ni mzima wa Afya.

Kwa uchache wa Muda naomba niende moja kwa moja kwenye dhumuni langu la kukuandikia ujumbe huu,hakika ujue sikupi pole sababu mambo Mengi umejitakia katika safari yako ya kisiasa,iliyo jaa vishindo na mbwembwe za kila aina.

Vijana wenzio tulibahatika kufanya kazi na wewe Daudi, kwakweli hatukuwahi kujua siri ya "kiburi" chako na "majivuno" yako uliyatoa wapi? Kwa jinsi ulivyokuwa kijana wa "Mission impossible" katika kila matendo ya vijana wa kaida yanayotarajiwa wewe ulitenda yale ambayo watu wasinge tarajia kuona,

Na hayo ndiyo yakawa maisha yako,hukujali wakubwa wanastahili heshima,hukujali kila binadamu anastahili staha,huku jali viongozi kama Mawaziri wa kuu au majaji wataafu walipaswa kulindwa na kuhifadhiwa.

Leo kabla Dunia haijaona mwanzo mpya au mwisho wa safari yako,kwakuwa Kwa namna yoyote vile tuta ulilokutana nalo Masihani mwako halitakuacha kama awali,utabadilika tuh utake usitake Hata kama mabadiliko yako yawe ya Nafasi au Nafsi yanakukuta kwa aibu na fedheha.

Walio karibu yako Daudi wanadai unawakati Mgumu,tukuombee,sitaki kuwa mnafki kwako,Daudi nikwambie tuh sitokuombea bali kabla ujamaliza kujutia Nafsi yako nikukumbushe tuh machache ili uyaingize kwenye sala ya toba.

1.Akilini kwako unamkumbuka baba wa watu? Mkurugenzi injinia mussa Natty,ulivyo muandama mpaka kusimamishwa kazi ulipokuwa DC KINONDONI? huku jali elimu yake aliyosomeshwa na wazazi wake masikini huko shinyanga,kwa UBASHITE WAKO ukamuumiza yeye na familia yake.

2.Je unawakumbuka wahandisi wa Halmashauri ya manispaa ya Kinondoni?,uliowasemea Mbele ya mheshimiwa Rais,siku ile Pale Biafra,wenzio wakasimamishwa kazi,na kuhamishiwa vijijini,hukujali elimu yao ya kweli si kama yako,waliyo ipata kwa shida wala familia zao masikini zilizo wategemea,Kwa UBASHITE WAKO ukawatokomeza na kuwaharibia majina na kazi zao.

3.Je unawakumbuka Maafisa ardhi? ukitoa amri wakamatwe kule Wazo mivumoni tuh kwa sababu walichelewa kufika eneo la tukio baada yako,hukujali Elimu zao na utaalamu wao wa ardhi waliosotea mashuleni na vyuoni ,kitichako kilikuwa na mamlaka ya kuwalaza wote sita mahabusu kituo cha mabatini KWA UBASHITE WAKO ukajiona wewe ni alpha na omega.

4.Je unamkumbuka yule dada Afisa ardhi uliye Muita "Tahira" kule kwenye mkutano wako mabwepande? Tena mbele za Tv na Radio zikiwa Mubashara,Hukujali mwenzio ana vyeti halali na amepimwa kwenye mitihani na amefaulu, KWA UBASHITE WAKO ukaona hakuna atakacho kufanya wala pakukimbilia.

5.Je unakumbuka ile kauli yako kwamba wewe ufanyalo Dar es salaaam,na kuliamua juu yake ni kwamba ameamua Mungu,Hata watu walipo toa miguno ya kulewa kwako madaraka hukuwahi kujutia kijivika utukufu wa Mungu,wala kujifananisha naye au kujipa unabii juu ya Dar es salaam,KWA UBASHITE WAKO ulidhani na yeye Mungu alipata zero? Au Mungu alinunua vyeti?

6.Je unaikumbuka ile kauli yako ya mara kwa mara uliyopenda kuitoa kwamba "Mimi nimbabe wa vita" ulimaanisha vita vya kufeli na kufanya "manuva" vita ya kutorudia au kukariri Darasa? Na ukazani umevishinda vita kwa kununua jina jipya, KWA UBASHITE WAKO,Ukasahau kuwa wazungu wanasema "There is no short cut in alife" isipokuwa wewe ukazani umeyapitia Denge maisha,wenzio wasome wafaulu,wewe ufeli ujekuwa boss wao.

7.Je unakumbuka Ile kauli yako ya kuwa ofisi ya mkuu wa mkoa Dar es salaam nzima inawafanyakazi 4,wengine wote ni mizigo? ,sasa utawaonea wivu hao mizigo kwakuwa wenzio wanavyeti na walifaulu wapo kihalali serikalini basi huenda utawaacha hapo na wewe mzigo namba moja utaondoka badala yao.KWA UBASHITE WAKO uliona kila mtu aliyesoma vigezo siyo kusoma ila ujanja kama uliotumia wewe.

Na mengine Mengi sababu ya Muda Nikuache na hayo,Niwache na boss wako muamue Mpangiane kazi gani nyingine,na kwa bahati mbaya mfumo wa nchi yetu,mwenye division zero,hastahili kuwa hata Dereva serikalini.

Fedheha na aibu imepanda gari lako la kifahari,imeingia ndani ya jumba lako hapo masaki,walinzi wote polisi na wanajeshi wameshindwa kuizuia,ipo mpaka sebuleni na sasa ujue Dar es salaam haitokubali itawaliwe na kuongozwa na KILAZA.......KUSOMA RAHA SANA

Na
BONIFACE JACOB
Senior councilor ubungo
Mstahiki meya
Manispaa ya ubungo
Stupidly nonsense
 
Back
Top Bottom