Menu ya chakula kwenye meli ya White Star Line

Menu ya chakula kwenye meli ya White Star Line

Ohooooo! Bahari ichafuke au kuzuke gonjwa la kuambukizana humo. UTAJUTA Mkuu!!!
Hilo la magongwa, ndo hatari zaidi lakini hilo la bahari kuchafuka, ndo travelling adventure zenyewe hizo kiongozi!!

Makashikashi safarini yana zake bhana....

Kuna siku tulikuwa angani... dadeki tulikutana na turbulence kwa zaidi ya dakika moja!! Ndege ilikuwa inayumba utadhani mashua baharini...

Sa' si ndo adventure zenyewe hizo!! Sio safari imepooza kama maiti kwenye jeneza bhana...
 
Tuachani masihara, hakuna usafiri amazing kama wa majini...

Najua nimechelewa sana, lakini naendelea kuzichanga taratibu hadi nichukue 14 days cruise ship manake nitakuwa sijaitendea haki nafsi yangu endapo nitadanja kabla sijaikamilisha hii ndoto!!
Ha ha ha ha nakumbuka mwaka 2003 Kama sikosei nlipanda Santorini kwenda Mtwara daaaah Ile burdan acha tu kabisa nikaja 2021 kupanda ya bukoba mwanza unashindia kule kwe mziki tu.
 
😂😂😂😂😂 I’ll take air turbulence any day as compared to rough sea. Nakumbuka tulikuwa wanne tunaenda Zenj kikazi basi badala ya kuchukua usafiri wa ndege tukaamua kupanda speed boat. Basi kuna sehemu wote kama 20 to 30 hivi tulisikia kichefu chefu cha hali ya juu. Yaani unajisikia vibaya mno lakini bahati nzuri hakuna kati yetu aliyetapika. Sijawahi kujisikia vibaya kiasi kile kwa usafiri wa ndege.

Hilo la magongwa, ndo hatari zaidi lakini hilo la bahari kuchafuka, ndo travelling adventure zenyewe hizo kiongozi!!

Makashikashi safarini yana zake bhana....

Kuna siku tulikuwa angani... dadeki tulikutana na turbulence kwa zaidi ya dakika moja!! Ndege ilikuwa inayumba utadhani mashua baharini...

Sa' si ndo adventure zenyewe hizo!! Sio safari imepooza kama maiti kwenye jeneza bhana...
 
Tukifika huko unaweza kuchukua meli mpaka Seashells ukarudi kwa ndege na ni package. Wanafanya Ulaya unaondoka Portugal to France, France London na unarudi Portugal ndani ya masaa 24.
Unajua umeongea jambo la maana sana...

Yaani nina mizuka kweli kweli ya kufika Ushelisheli

ZNZ ni kwavile ndo "home" but I'm more in love with Seychelles as compared to ZNZ!

Lakini kama package yenyewe itakuwa ya kufika na kuunganisha kwa flight, kwangu haitanifaa! Natamani nikifika pale nikae kama wiki mbili hivi ya kujenga mahaba na mchanga wa bahari!
 
Ha ha ha ha nakumbuka mwaka 2003 Kama sikosei nlipanda Santorini kwenda Mtwara daaaah Ile burdan acha tu kabisa nikaja 2021 kupanda ya bukoba mwanza unashindia kule kwe mziki tu.
Usafiri wa baharini una raha bhana...

Huku meli, kule mashua...

Miaka ya nyuma nilikuwa naenda naenda sana Mafia! Siku nimeacha kupanda boti (yenye mashine) ni siku ambayo mashua ilitupita na kutuacha kama tumesimama!!

Yaani tulikuwa tunaiona kama kisufuria vile kwa mbaaaaaaaali, kina kuja!! Nikajua jamaa hawatukuti wala nini!! Dadeki, ule "moto" ambao walituwashia, tangu siku hiyo nikahamishia mahaba kwenye mashua!!

Na utamu wa mashua, upepo ukiwapendelea ni kawaida sana kujikuta mmetokeza Comoro au Madagascar bila passport 🤣🤣🤣
 
😂😂😂😂😂 I’ll take air turbulence any day as compared to rough sea. Nakumbuka tulikuwa wanne tunaenda Zenj kikazi basi badala ya kuchukua usafiri wa ndege tukaamua kupanda speed boat. Basi kuna sehemu wote kama 20 to 30 hivi tulisikia kichefu chefu cha hali ya juu. Yaani unajisikia vibaya mno lakini bahati nzuri hakuna kati yetu aliyetapika. Sijawahi kujisikia vibaya kiasi kile kwa usafiri wa ndege.
Kama hujazoea, kichefu chefu baharini ni kama bia na nyama choma...

Lakini ukishazoea... basi kuwe na turbulance la kufa mtu hasa ndipo utakutana na wenge!! Binafsi nimekata maji hadi na mashua, lakini poa tu!!

Ila BAK usifanye masihara na air turbulence bhana!! Halafu turbelence yenyewe itokee ghafla na hujafunga mkanda, huku pembeni yako umekaa siti moja na mdada, halafu awe Evangelist 🤣😂😂😅!!

Wallah utaanza kukumbwa na mcheche zaidi kutoka kwa jirani yako kuliko turbulence yenyewe! Manake utaona kwa maombi haya... itakuwa keshapata ufunuo huyu kwamba biashara ndo inaishia hapa hapa!!
 
Tuachani masihara, hakuna usafiri amazing kama wa majini...

Najua nimechelewa sana, lakini naendelea kuzichanga taratibu hadi nichukue 14 days cruise ship manake nitakuwa sijaitendea haki nafsi yangu endapo nitadanja kabla sijaikamilisha hii ndoto!!
Mimi mbona usafir wa majini naona mateso makubwa maana natapika mpaka naona utumbo Una taka kutokea mdomo nau tatizo vyombo vyetu ya majini havina ubora.
 
Sijaona Ugali MAHARAGE hapo
IMG_20210917_181658.jpg
 
Pana waqt tumesafiri na mtumbwi wetu wa kasia tumejikimu kwa wali na samaki tuliotoka nao nchi kavu ila mtayarishaji wa kachumbari alitukomoa ile pilipili mpaka leo sijui ilikuwaje sasa his menu imenikumbusha mbali sana
 
Sky wewe ulipaswa kuwa Uingereza unapenda sana huko hasa story za royal family (jipige kifua useme one day yes)😂
Menu hiyo mimi sielewi chochote ningechaguliwa na muhudumu
.... ha ha ha! Unamwambia mhudumu niletee kama hicho anakula mteja aliyekaa kushoto apo! Kikiletwa hiyo taste usiombe na hiyo bei sasa kama hujajipanga imekula kwako.
 
Back
Top Bottom