Mengi kusomewa albadiri Dar es Salaam

Mengi kusomewa albadiri Dar es Salaam

SHEIKH Maarufu jijini Dar es Salaam na nchini, Ali Bassaleh ametishia kusoma kisomo (albadiri) dhidi ya mfanyibiashara maarufu nchini Reginald Mengi iwapo hatalipwa fidia anayodai.

Sheikh Bassaleh amemfahamisha Mwandishi wiki hii kwamba, amefanya subira ya muda mrefu hivyo ameona wakati umefika kwa yeye kumlilia Mwenyezi Mungu (SW) dhidi ya dhuluma aliyodai kuwa imefanywa na mfanyabishara huyo.


Amesema anakusudia kusoma kisomo hicho muda wowote na atatangaza siku maalum kwa waumini wa dini ya kiislamu na watanzania kwa ujumla.


Amesema, madai ya fedha dhidi ya Reginald Mengi yanafuatia kumalizika kwa kesi ya kashfa dhidi ya chombo cha habari kinachomilikiwa na moja ya makampuni ambayo Mengi ana hisa.

Amesema, kufuatia kukashifiwa na chombo hicho cha habari, aliwasilisha malalamiko yake Baraza la habari ambako alishinda na kupewa ruhusa ya kwenda mahakamani.

“Nilimtumia Wakili Profesa Saffari, nikafungua madai, tukashinda kesi, chombo hicho na mmiliki wake wametakiwa kunilipa fidia ya shilingi Milioni 49”, ameeleza Sheikh

Amesema, tangu wakati huo amekuwa akisumbuliwa, hali inayoashiria mwenye fedha ndiye mwenye haki ambaye hata vyombo vya sheria vinaashiria kutokuwa tayari kukunjua makucha dhidi yake.

Akizungumzia kisomo cha Albadiri Sheikh Bassaleh amesema, ni dua maalum, yenye utekelezaji maalum wa maombi ya mdhulumiwa ambayo huelekezwa kwa Muumba wa Mbingu na Ardhi, Mmiliki wa vyote, ambaye ndiye Mmiliki wa uhai wa Mwanadaamu, huweza kuuchukua wakati wowote atakapo.

Amesema katika mafunzo ya dini ya kiislamu, Dua ya mdhulumiwa inapoombwa kinyenyekevu haina pazia, hupokelewa moja kwa moja na kwa haraka na Mwenyezi Mungu dhidi ya aliyedhulumu na kwamba zipo aina tofauti za kujibiwa.


Miongoni mwa majibu ya Mwenyezi Mungu kwa dua hiyo ni pamoja na kuondosha uhai wa aliyedhulumu ili asiendelee kukera waja wema wanyonge au kumpa maradhi yasiyotibika kwa dawa za Hospitali wala mitishamba ili iwe ujumbe wa wazi kwa wengine.

Majibu mengine ni pamoja na kumpa aliyedhulumiwa nafasi ya juu ili kumfedhehesha aliyedhulumu au mbadala mwingine ulio bora zaidi kuchukua nafasi ya alichodhulumiwa kama mali, wasifu au heshima katika jamii.

Katika madai yake dhidi ya taarifa iliyochapishwa na chombo kinachosemekana kumilikiwa na Mengi ni kwamba, ilichapishwa taarifa yenye kumkashifu na kumshushia hadhi na heshima yake kama kiongozi wa Dini na jamii kwa ujumla.

Hata hivyo, baadhi ya watu wameendelea kumsihi Sheikh Bassaleh asichukue hatua hiyo kwa haraka kutokana na madhara yake kuto komea kwa mtu mmoja bali huusisha mlolongo wa watu wote wanaohusika kwa namna moja au nyingine.

Uzi mreefu lakini hovyo kabisa.
 
Kama unataka kuelimika na unataka kuelewa na kufahamu usilolijuwa fungulia nyuzi na wenye jazba wawache na jazba zao. Hakugusi mtu humu.

Hahahaaa, nimecheka sana hiyo 'Hakugusi mtu humu'! Haya asante sana kwa ushauri wako, najikusanya nikuahidi nitakuja na uzi wa suala hili na nitakualika. Nitajitahidi kunyosha maelezo ili kupunguza kuwapa nafasi wenye jazba wasipate nafasi ya kuvuruga mapema.
Ova
 
Bado miezi 6 wafunge vidomodomo vyao hao ma shehe ubwabwa
 
Caliber ya Sheikh Basaleh hawezi kuongea upuuzi, source hakuna katika hiyo habari, sehemu inayoonekana kunukuliwa Sheikh Basaleh ni moja tu, nayo ni hii "Nilimtumia Wakili Profesa Saffari, nikafungua madai, tukashinda kesi, chombo hicho na mmiliki wake wametakiwa kunilipa fidia ya shilingi Milioni 49”, ameeleza Sheikh.

Katika andiko zima sijaona sehemu nyingine yenye nukuu ya Basaleh, kwa hiyo ni wazi kabisa ni porojo za mleta mada.
Zinatakiwa nukuu ngapi ndo habari iwe real?
 
ha ha ha ha ha ha

ha ha ha ha ha ha

Mengi kaaga kwao moshi

halafu kusema Mengi amemchafua ni kutafuta kick kupitia kwa Mengi kwani Mengi si mwandishi wa habari na sijui huo ulozi anamfanyia nani

all in all kwanini utumie ushirikina kudai chako ??

Mil 49 ni nyingi labda hana

Kaka huomsio ushirikina. Nimkumlilia na kumuachia MUNGU? Yeye ndie atakaye amua.
 
SHEIKH Maarufu jijini Dar es Salaam na nchini, Ali Bassaleh ametishia kusoma kisomo (albadiri) dhidi ya mfanyibiashara maarufu nchini Reginald Mengi iwapo hatalipwa fidia anayodai.

Sheikh Bassaleh amemfahamisha Mwandishi wiki hii kwamba, amefanya subira ya muda mrefu hivyo ameona wakati umefika kwa yeye kumlilia Mwenyezi Mungu (SW) dhidi ya dhuluma aliyodai kuwa imefanywa na mfanyabishara huyo.


Amesema anakusudia kusoma kisomo hicho muda wowote na atatangaza siku maalum kwa waumini wa dini ya kiislamu na watanzania kwa ujumla.


Amesema, madai ya fedha dhidi ya Reginald Mengi yanafuatia kumalizika kwa kesi ya kashfa dhidi ya chombo cha habari kinachomilikiwa na moja ya makampuni ambayo Mengi ana hisa.

Amesema, kufuatia kukashifiwa na chombo hicho cha habari, aliwasilisha malalamiko yake Baraza la habari ambako alishinda na kupewa ruhusa ya kwenda mahakamani.

“Nilimtumia Wakili Profesa Saffari, nikafungua madai, tukashinda kesi, chombo hicho na mmiliki wake wametakiwa kunilipa fidia ya shilingi Milioni 49”, ameeleza Sheikh

Amesema, tangu wakati huo amekuwa akisumbuliwa, hali inayoashiria mwenye fedha ndiye mwenye haki ambaye hata vyombo vya sheria vinaashiria kutokuwa tayari kukunjua makucha dhidi yake.

Akizungumzia kisomo cha Albadiri Sheikh Bassaleh amesema, ni dua maalum, yenye utekelezaji maalum wa maombi ya mdhulumiwa ambayo huelekezwa kwa Muumba wa Mbingu na Ardhi, Mmiliki wa vyote, ambaye ndiye Mmiliki wa uhai wa Mwanadaamu, huweza kuuchukua wakati wowote atakapo.

Amesema katika mafunzo ya dini ya kiislamu, Dua ya mdhulumiwa inapoombwa kinyenyekevu haina pazia, hupokelewa moja kwa moja na kwa haraka na Mwenyezi Mungu dhidi ya aliyedhulumu na kwamba zipo aina tofauti za kujibiwa.


Miongoni mwa majibu ya Mwenyezi Mungu kwa dua hiyo ni pamoja na kuondosha uhai wa aliyedhulumu ili asiendelee kukera waja wema wanyonge au kumpa maradhi yasiyotibika kwa dawa za Hospitali wala mitishamba ili iwe ujumbe wa wazi kwa wengine.

Majibu mengine ni pamoja na kumpa aliyedhulumiwa nafasi ya juu ili kumfedhehesha aliyedhulumu au mbadala mwingine ulio bora zaidi kuchukua nafasi ya alichodhulumiwa kama mali, wasifu au heshima katika jamii.

Katika madai yake dhidi ya taarifa iliyochapishwa na chombo kinachosemekana kumilikiwa na Mengi ni kwamba, ilichapishwa taarifa yenye kumkashifu na kumshushia hadhi na heshima yake kama kiongozi wa Dini na jamii kwa ujumla.

Hata hivyo, baadhi ya watu wameendelea kumsihi Sheikh Bassaleh asichukue hatua hiyo kwa haraka kutokana na madhara yake kuto komea kwa mtu mmoja bali huusisha mlolongo wa watu wote wanaohusika kwa namna moja au nyingine.

ndomaana ponda yuko ndani.akili za mashekhh njaa ni tatizo
.upewe milion 49 kirahisi
 
Huyo shehe angesem anaidai kampuni ya ipp kiasi cha sh 49mill,kwani kampuni nayo ni entity ambayo inaweza ikashitaki na kustakiwa,ipp inaweza hata ikamshitaki mengi na mengi kuishtaki ipp,business and the business owner are separtely
 
Ninachojua mimi, ni kweli Mengi anamiliki vyombo vingi vya habari. Ukweli huu unakwenda sambamba na ukweli kuwa Mengi sio mwandishi wa habari wala sio mhariri wa chombo chochote cha habari kati ya anavyomiliki. Vyombo vyote vina watendaji kulingana na taaluma zao. Huyu Mengi anaingiaje hapa kusomewa ilibadiri ana ni njia ya vitisho kutafuta mshiko. Wewe Shekh unatakiwa ukikomalie chombo husika wala sio Mengi. Unaweza ukakaza hukumu kama kweli ulishinda kesi ya msingi na mali za chombo husika zikakamatwa kwa amri ya mahakama, zikapigwa mnada ili kulipia kiasi unachodai. Bili hivyo wewe ni mbabaishaji.
 
Isis, alshabab, hamas, bokoharam kwa nini washike silaha na mabomu kama albadir inafanya kazi
 
Aende akasome tu kama anaamn aende wala asizuiliwe. Ila ajue kuna walidhulumiwa zaid yake, kuna walio asi dini, kuna wachawi walisome na bado wanadunda tena wamefanikiwa sana. Asiuchafue Uislam kwa matakwa yake binafs. Akumbuke kuna wez waliwah kuiba makanisan na misikitn wakaombewa xaana madua lakn badala ya kufa au kuwa makn au machz, ndyo kwaanza wananeemeka. InaJamaa kama anadaiwa alipe, siyo kuchenga chenga tu.
 
Hawa ndugu waliwahi kumsomea Prof JK kadua flan kanaitwa "itikhafu" ndio akapata tezidume ha ha ha! Ngoja tuone kwa Mengi.
 
Mie walishanisomea sana huo upuuzi wao, na bado nadunda tu mtaani.

Ni upuuzi uliopitiliza, ni wa kuwapuuza tu
 
Aende akasome tu kama anaamn aende wala asizuiliwe. Ila ajue kuna walidhulumiwa zaid yake, kuna walio asi dini, kuna wachawi walisome na bado wanadunda tena wamefanikiwa sana. Asiuchafue Uislam kwa matakwa yake binafs. Akumbuke kuna wez waliwah kuiba makanisan na misikitn wakaombewa xaana madua lakn badala ya kufa au kuwa makn au machz, ndyo kwaanza wananeemeka. InaJamaa kama anadaiwa alipe, siyo kuchenga chenga tu.

Mkuu kanisan hawaombi madua ya mtu kufa au kuwa chizi hata mtu akiiba ,na kwenye ukristo hamna kitu kinachoitwa madua,shetani peke yake ndio usoma madua ya watu kufa na kupata matatizo,Mungu ni pendo hata kama umeiba kanisan,still atakupenda.
 
Huo si ushirikina ni dua ya kuomba kwa kile unacho amini mtu amekudhulumu .
Ikiwa ni mwizi au uonevu au kufanyiwa fitina basi kama unashindwa kupata haki yako kutokana na fisadi basi unaweza kusoma dua hii maaruf na ikisomwa ipasavyo mwenye kudhulumu kama amefanya hivyo basi madhari yake yapo wazi.
Hii dua inatokana na mashahid wa mwanzo katika uislam walio kufa katika vita vya badr.
Miongoni mwa watu waliosomewa dua hii ni Augustine Mrema kutokana na kuwapiga masheikh na kuwaua kutokana na kadhia ya nguruwe.pia mrema aliamrisha kukamatwa kwa Sheikh Kassim Bi Jumaa na kuamuru kuteswa minduli na dar es salam huku akiwa mgonjwa. SHEIKH Kassim alifariki muda mfupi baada ys kuachiwa na kupewa sumu.
Waislam kwa umoja wao walifunga na kusoma dua kuomba adhabu kwa mrema kutokana na jeuri na dhulma dhidi ya uislam.
Yalofata mrema kaachishwa unaibu waziri mkuu na baaddae kufukuzwa kazi na mpaka leo hakulipwa hata penseni yake
Pia alijiunga na nccr na hatimae akadhiriwa kwa kukimbia kutoka dirishani kule mkonge tanga.
Mpaka leo yupo yupo tu uso umeharibika utafikiri chura.
Hivyo mengi bora amwite sheikh wayamalize kiutu zima. Kama anedhulumu basi dua hii itampata.
 
Ninachojua mimi, ni kweli Mengi anamiliki vyombo vingi vya habari. Ukweli huu unakwenda sambamba na ukweli kuwa Mengi sio mwandishi wa habari wala sio mhariri wa chombo chochote cha habari kati ya anavyomiliki. Vyombo vyote vina watendaji kulingana na taaluma zao. Huyu Mengi anaingiaje hapa kusomewa ilibadiri ana ni njia ya vitisho kutafuta mshiko. Wewe Shekh unatakiwa ukikomalie chombo husika wala sio Mengi. Unaweza ukakaza hukumu kama kweli ulishinda kesi ya msingi na mali za chombo husika zikakamatwa kwa amri ya mahakama, zikapigwa mnada ili kulipia kiasi unachodai. Bili hivyo wewe ni mbabaishaji.

Mengi Yeye ndie alieshtakiwa kama mmiliki hivyo yeye ndie mlipaji
 
Back
Top Bottom