Mengi kusomewa albadiri Dar es Salaam

User Name: kahtaan User Title: Banned Last Activity: Yesterday 01:23
 
Unataka Ufafanuzi wa Nini?
Umeskia Mi Mganga wa Loliondo?

Muulizenu Yule mchaga Kwanini kala cha Mtu?

Na kama kala Jasho la Mtu basi Akisomewa hio Utashangaa mwenyewe.
Kwa hiyo unapingana na THE BIG SHOW!? anasema hiyo ni shirki... Kuna mtu kauliza hapo juu ingekuwa ni virahisi namna hiyo, Basi Obama na Netanyau wangekuwa tayari wamekwisha somewa...
 
Last edited by a moderator:
albadil huwa haitangazwi kama unasoma na kama umedharirishwa usingeshitaki ungesoma moja kwa moja.
na ipo siku na muda wa kusoma.
 
Caliber ya Sheikh Basaleh hawezi kuongea upuuzi, source hakuna katika hiyo habari, sehemu inayoonekana kunukuliwa Sheikh Basaleh ni moja tu, nayo ni hii "Nilimtumia Wakili Profesa Saffari, nikafungua madai, tukashinda kesi, chombo hicho na mmiliki wake wametakiwa kunilipa fidia ya shilingi Milioni 49”, ameeleza Sheikh.

Katika andiko zima sijaona sehemu nyingine yenye nukuu ya Basaleh, kwa hiyo ni wazi kabisa ni porojo za mleta mada.

Hata mimi sijaamini, Sheikh Basaleh si mtu wa vitisho kama ninavyoviona katika taarifa hii isiyo na chanzo chochote.
Na vipi kuhusu hili suala la Al Badir, ni kweli liko kwenye dini, au ni shirki tu kama nyingine? Shukrani sana.
Ova
 
albadil huwa haitangazwi kama unasoma na kama umedharirishwa usingeshitaki ungesoma moja kwa moja.
na ipo siku na muda wa kusoma.

pia hili nishawahi sikia albadili haisemwi unaenda kusoma moja kwa moja

ila swali ni je hicho kitu kipo?????UKIACHANA NA STORY YA MLETA MADA AMBAE YAWEZEKANA KAAMBIWA

JE ALBADILI IPO NA INAFANYA VIPI KAZI?
 
Hata mimi sijaamini, Sheikh Basaleh si mtu wa vitisho kama ninavyoviona katika taarifa hii isiyo na chanzo chochote.
Na vipi kuhusu hili suala la Al Badir, ni kweli liko kwenye dini, au ni shirki tu kama nyingine? Shukrani sana.
Ova

Fungulia nyuzi yake tutakuja kukupa darsa.
 
Naona wengi humu mnajibu kwa jazba na hasira, ni vema SHEIKH akashauriwa kutumia njia za kistaarabu na ikiwezekana pia kumuelemisha jinsi yakushughulikia shauri zinazoelekezwa kwenye limited companies, hiyo tu ili weze kufuatilia madai yake ipasavyo.
 
Fungulia nyuzi yake tutakuja kukupa darsa.

Shukrani kwa nia yako, ila tatizo la humu masuala ya dini hujadiliwa kwa jazba sana hadi unaweza juta kuanzisha nyuzi.
Yaani tunahamishia vurugu za siasa kwenye mijadala ya dini ambayo naamini tunapaswa kuheshimiana kwanza kisha tupeane darsa.
Ova
 
Shukrani kwa nia yako, ila tatizo la humu masuala ya dini hujadiliwa kwa jazba sana hadi unaweza juta kuanzisha nyuzi.
Yaani tunahamishia vurugu za siasa kwenye mijadala ya dini ambayo naamini tunapaswa kuheshimiana kwanza kisha tupeane darsa.
Ova

Kama unataka kuelimika na unataka kuelewa na kufahamu usilolijuwa fungulia nyuzi na wenye jazba wawache na jazba zao. Hakugusi mtu humu.
 
SHEIKH Maarufu jijini Dar es Salaam na nchini, Ali Bassaleh ametishia kusoma kisomo (albadiri) dhidi ya mfanyibiashara maarufu nchini Reginald Mengi iwapo hatalipwa fidia anayodai.

Sheikh Bassaleh amemfahamisha Mwandishi wiki hii kwamba, amefanya subira ya muda mrefu hivyo ameona wakati umefika kwa yeye kumlilia Mwenyezi Mungu (SW) dhidi ya dhuluma aliyodai kuwa imefanywa na mfanyabishara huyo.


Amesema anakusudia kusoma kisomo hicho muda wowote na atatangaza siku maalum kwa waumini wa dini ya kiislamu na watanzania kwa ujumla.


Amesema, madai ya fedha dhidi ya Reginald Mengi yanafuatia kumalizika kwa kesi ya kashfa dhidi ya chombo cha habari kinachomilikiwa na moja ya makampuni ambayo Mengi ana hisa.

Amesema, kufuatia kukashifiwa na chombo hicho cha habari, aliwasilisha malalamiko yake Baraza la habari ambako alishinda na kupewa ruhusa ya kwenda mahakamani.

“Nilimtumia Wakili Profesa Saffari, nikafungua madai, tukashinda kesi, chombo hicho na mmiliki wake wametakiwa kunilipa fidia ya shilingi Milioni 49”, ameeleza Sheikh

Amesema, tangu wakati huo amekuwa akisumbuliwa, hali inayoashiria mwenye fedha ndiye mwenye haki ambaye hata vyombo vya sheria vinaashiria kutokuwa tayari kukunjua makucha dhidi yake.

Akizungumzia kisomo cha Albadiri Sheikh Bassaleh amesema, ni dua maalum, yenye utekelezaji maalum wa maombi ya mdhulumiwa ambayo huelekezwa kwa Muumba wa Mbingu na Ardhi, Mmiliki wa vyote, ambaye ndiye Mmiliki wa uhai wa Mwanadaamu, huweza kuuchukua wakati wowote atakapo.

Amesema katika mafunzo ya dini ya kiislamu, Dua ya mdhulumiwa inapoombwa kinyenyekevu haina pazia, hupokelewa moja kwa moja na kwa haraka na Mwenyezi Mungu dhidi ya aliyedhulumu na kwamba zipo aina tofauti za kujibiwa.


Miongoni mwa majibu ya Mwenyezi Mungu kwa dua hiyo ni pamoja na kuondosha uhai wa aliyedhulumu ili asiendelee kukera waja wema wanyonge au kumpa maradhi yasiyotibika kwa dawa za Hospitali wala mitishamba ili iwe ujumbe wa wazi kwa wengine.

Majibu mengine ni pamoja na kumpa aliyedhulumiwa nafasi ya juu ili kumfedhehesha aliyedhulumu au mbadala mwingine ulio bora zaidi kuchukua nafasi ya alichodhulumiwa kama mali, wasifu au heshima katika jamii.

Katika madai yake dhidi ya taarifa iliyochapishwa na chombo kinachosemekana kumilikiwa na Mengi ni kwamba, ilichapishwa taarifa yenye kumkashifu na kumshushia hadhi na heshima yake kama kiongozi wa Dini na jamii kwa ujumla.

Hata hivyo, baadhi ya watu wameendelea kumsihi Sheikh Bassaleh asichukue hatua hiyo kwa haraka kutokana na madhara yake kuto komea kwa mtu mmoja bali huusisha mlolongo wa watu wote wanaohusika kwa namna moja au nyingine.

Loh naona ulimwengu una mambo mengi ila jambo lenyewe liko kama mleta mada hataki liwe wazi kwa sababu;
Haelezi chombo husika kilichomkosea ila anamtaja mengi kama moja ya wana hisa
Pili kosa lenyewe halitajwi kuonesha uzito wake kama umeamua kuiambia jamii yote
Tatu hivi kila mtu akiazimia kuchukua hatua hiyo kwa kila anaemkosea ni wangapi wangekua hai leo

Kama kuna watu wanaostahili kupewa hii adhabu basi ni wale wanaowadhulum watz maskini yaani mafisadi; tusaidiane kama ni applicable tuchukue hatua
 
Amekashfiwa ....
Kwenye chombo cha habari....
Kwa maana nyingine kuna mwandishi aliyeandika...
Pia kuna mhariri................................................................
Kuna kampuni inayochapisha na wanahisa wengine..........
Ameonekana MENGI TU.?!,,
 
aende kusoma tuu hizi ni hujuma za Muhongo kumchafua Mengi haziwezi kufanikiwa kamwe.
 
mimi nimuislamu nijuavyo mm suala la albadiri hamna ktk uislamu wala halijafundishwa ktk vitabu vyote ama kuhusu dua ya alie dhulumiwa ni dua tu ya kawaida ambayo mtu yyt akiomba kwa aina yyte kwa lugha yyt huwa haina pazia lkn hayo mambo ya albadiri ni ushirikina tu.
 
hiyo albadiri ni kuchafua uislamu hlf neno albadiri ni wale waliopigana vita vya badr ninachoshangaa hao wanauhusiano gani na kudhulumiwa kwako?km sio uchawi?waache kuchafua dini!!
 
ukimsomea ....amewaajiri waislamu wenzio nao watakusomea wewe unayewakosesha riziki (hasi -ve jumlisha chanya +ve ) = zero.......na WALEMAVU NDIO KABSAAAAAAAAAAAAA WATAKULAANI HATA USIONE MBINGUUUU
 
Back
Top Bottom