Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,891
Kwema Wakuu!
Membe Vs Musiba; Huwezi Kuomba Msamaha Baada ya Hukumu, Msamaha unaomba Wakati wa kesi au Kabla ya Kesi.
Kuna Watu bhana wanafurahisha Sana. Hivi uliona wapi mtu akapewa Msamaha pasipo ya yeye kuomba Msamaha? Wapi? Na lini? Uliona wapi mtu anasamehewa ikiwa alipewa muda wa kutosha, nafasi za kutosha za kuomba Msamaha lakini Kwa Ujeuri, ukaidi, dharau na Kiburi akakataa? Uliona au kusikia wapi?
Kusamehe ni Jambo zuri la hiyari, hakuna sheria yoyote duniani, Kuzimu na akhera inayomlazimisha MTU kusamehe. Kwa sababu kikawaida Msamaha ni Neema, na neema ni kinyume na HAKI. Kuomba Msamaha unapokosea ni Jambo Zuri, na unaomba Msamaha sio ili usipewe adhabu Bali kuonyesha kujuta, na unataka kufanya Amani na MTU.
Msamaha pia unahusisha kulipia Gharama Fulani kama sehemu ya fidia ili kuweka Mambo Sawa na uliyemkosea.
Msamaha ni kitu cha thamani Kwa Watu wanaotafuta Amani na Furaha. Msamaha hautolewi na kupewa Watu wapumbavu ambao huweza kuutumia vibaya. Msamaha unatolewa Kwa Watu waliojifunza kuwa ni kweli wamefanya Makosa na wanajutia Makosa Yao.
Huwezi omba Msamaha siku ya Hukumu, na kamwe haitowezekana kusamehewa siku ya Hukumu. Ni mtu mwenye Jeuri, kiburi, dharau, na muovu anayeweza kuomba Msamaha siku ya Hukumu yaani Baada ya kuhukumiwa ilhali alipewa nafasi za kutosha ili kuweka Mambo Sawa.
Ni Watu wanafiki pekee wanaoweza kuomba Msamaha Kwa namna hiyo. Halikadhalika ni Watu wanafiki pekee wanaoweza kuwa upande wa Watu wa namna hiyo. Msamaha hauwafai Watu wanafiki, kwani Wanafiki wanatabia ya Kisasi na usaliti. Kwao Msamaha huitumia kama mbinu ya kishetani kujisalimisha(Jambo ambalo wanaona aibu na hawataki litokee).
Vipo visa na reference nyingi zinazoeleza kile nikisemacho, mtu ukishafanya madhara Fulani kuna hatua za kuchukua, huwezi fanya kitu Makusudi alafu Kwa kiburi na Jeuri uliyemkosea anakusihi uachane na tabia yako Mbaya tena umuombe Msamaha lakini unakuwa mkaidi, yakikupata ndio unaona ndio Wakati Sahihi Kwa vile umeshindwa. Wewe ni Shetani na watakaokutetea pia ni vibaraka wa Shetani.
Ni vizuri kama Watu waungwana tukikosea tuombe Msamaha Kwa Wakati, na jukumu la kusamehewa litabaki Kwa tuliowakosea, na sio Haki yetu kusamehewa, itategemeana na uliyemkosea.
Narudia hakuna sheria popote duniani, Mbinguni, na akhera inayoamrisha Watu au kiumbe kitoa Msamaha. Isipokuwa Msamaha ni hiyari ya MTU. Kitu kikiwa hiyari sio amri wala sheria. Labda sheria za Kinafiki.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Membe Vs Musiba; Huwezi Kuomba Msamaha Baada ya Hukumu, Msamaha unaomba Wakati wa kesi au Kabla ya Kesi.
Kuna Watu bhana wanafurahisha Sana. Hivi uliona wapi mtu akapewa Msamaha pasipo ya yeye kuomba Msamaha? Wapi? Na lini? Uliona wapi mtu anasamehewa ikiwa alipewa muda wa kutosha, nafasi za kutosha za kuomba Msamaha lakini Kwa Ujeuri, ukaidi, dharau na Kiburi akakataa? Uliona au kusikia wapi?
Kusamehe ni Jambo zuri la hiyari, hakuna sheria yoyote duniani, Kuzimu na akhera inayomlazimisha MTU kusamehe. Kwa sababu kikawaida Msamaha ni Neema, na neema ni kinyume na HAKI. Kuomba Msamaha unapokosea ni Jambo Zuri, na unaomba Msamaha sio ili usipewe adhabu Bali kuonyesha kujuta, na unataka kufanya Amani na MTU.
Msamaha pia unahusisha kulipia Gharama Fulani kama sehemu ya fidia ili kuweka Mambo Sawa na uliyemkosea.
Msamaha ni kitu cha thamani Kwa Watu wanaotafuta Amani na Furaha. Msamaha hautolewi na kupewa Watu wapumbavu ambao huweza kuutumia vibaya. Msamaha unatolewa Kwa Watu waliojifunza kuwa ni kweli wamefanya Makosa na wanajutia Makosa Yao.
Huwezi omba Msamaha siku ya Hukumu, na kamwe haitowezekana kusamehewa siku ya Hukumu. Ni mtu mwenye Jeuri, kiburi, dharau, na muovu anayeweza kuomba Msamaha siku ya Hukumu yaani Baada ya kuhukumiwa ilhali alipewa nafasi za kutosha ili kuweka Mambo Sawa.
Ni Watu wanafiki pekee wanaoweza kuomba Msamaha Kwa namna hiyo. Halikadhalika ni Watu wanafiki pekee wanaoweza kuwa upande wa Watu wa namna hiyo. Msamaha hauwafai Watu wanafiki, kwani Wanafiki wanatabia ya Kisasi na usaliti. Kwao Msamaha huitumia kama mbinu ya kishetani kujisalimisha(Jambo ambalo wanaona aibu na hawataki litokee).
Vipo visa na reference nyingi zinazoeleza kile nikisemacho, mtu ukishafanya madhara Fulani kuna hatua za kuchukua, huwezi fanya kitu Makusudi alafu Kwa kiburi na Jeuri uliyemkosea anakusihi uachane na tabia yako Mbaya tena umuombe Msamaha lakini unakuwa mkaidi, yakikupata ndio unaona ndio Wakati Sahihi Kwa vile umeshindwa. Wewe ni Shetani na watakaokutetea pia ni vibaraka wa Shetani.
Ni vizuri kama Watu waungwana tukikosea tuombe Msamaha Kwa Wakati, na jukumu la kusamehewa litabaki Kwa tuliowakosea, na sio Haki yetu kusamehewa, itategemeana na uliyemkosea.
Narudia hakuna sheria popote duniani, Mbinguni, na akhera inayoamrisha Watu au kiumbe kitoa Msamaha. Isipokuwa Msamaha ni hiyari ya MTU. Kitu kikiwa hiyari sio amri wala sheria. Labda sheria za Kinafiki.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam