Membe: Msije Dar wakati wa ziara ya Obama

Membe: Msije Dar wakati wa ziara ya Obama

Waziri wa mambo ya nje bwana Benard Membe anapothubutu kusema eti kuimarisha ulinzi katika ujio wa Obama anawashauri waTz walioko mikoani wasiende Dar kwa kweli ametusikitisha sana, Membe mbona unavunja taratibu za misingi ya kiusalama, kwani ujio wa Obama ndio uzuie shughuli za kiuchumi za nchi, Membe unajuwa misingi namna ya kujipanga katika ulinzi leo unaivunja , nakumbuka wewe ulihudumu katika idara ya usalama wa taifa [TISS] enzi hizo ukiwa na akina marehemu Benald Walingozi,Peter Kuhanwa,Ally Nissi,Mwasokwa. n.k leo papara zako zinakupelekea siko.
Tukiandaa kombe la dunia nadhani mwezi mzima tutakuwa off
 
hivi kikwete akienda kwa obama kunakuwa na hali hii?
Hapana
tofauti ya nchi zilizoendelea na hizi za huku katika mambo ya usalama ni moja tu. Kwa wenzetu ukitenda uhalifu uwewzekano wa kukamatwa ndani ya saa 48 ni asilimia 93, huku kwetu uwezekano wa kukamatwa ni asilimia 4 ndani ya wiki moja!
 
Hivi mbona Vasco kila mara yupo nje ya nchi ina maana huko anakoenda huwa wanamfanyia wananch wao tunayofanyiwa sie? Eti watu wasije Dar, Khaaa!
 
Simpendi kabisa huyu Obuma pamoja na Serikali yake, wanyanganyi tu na anakuja kupora rasilimali zetu hamna jipya. Tatizo viongozi waliopo katika Serikali ya Tz ni bora viongozi lakini si viongozi bora yaani I hate this government!!!

Sent from my BlackBerry 9380 using JamiiForums
 
naon ainabidi watangaze public holidays, barabara zote zinafungwa duh
 
Huyu naye anadhani Dar es Salaam ni kwake huko Posta, Mbezi na Oysterbay tu! Yeye ampokee Obama sisi tutaendelea kuja Dar na kuvinjari maeneo mengine kama kawa. Ebo!
 
Marekani ninakwenda na kurudi bongo kwangu. Kwani presidaaa wetu akienda marekani wamarekani huwa wanahaha kama tunavyohaha sie sasa hivi?


kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, presidaa wa states ni ugeni mzito , sana... hata akienda china , wachina watahangaika tu mpaka pale atakapoondoka
 
Hahaaa mkuu unanichekesha. Air force ikitokea SA inapita juu ya anga la Msumbuji usawa wa bahari kuna monowari zipo bahari ya Hindi zinafuatilia nyendo zake

anataka kuona gesi ya kule kusini si unajua ile ndege ina kamera za hali ya juu sana anaona mpaka panya ardhini :glasses-nerdy:
 
watu8..
anasema kwetu tanzania ni Mgeni njoo Mwenyeji........

Nakumbuka waliwahi kudeki barabara toka KIA hadi ARUSHA, ilikuwa ujio wa BUSH akasepa na gold akatuachia net! Nchi y2 tusisafiri yani tusizalshe tufe njaa! Kwn OBM analeta hela kwa kila mtz? Au ni kwa wachache watakaosaini mikataba ya kutapeli GAS YETU NA URANIUM YETU? Membe iv nae anaotaga urais?
 
Last edited by a moderator:
kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, presidaa wa states ni ugeni mzito , sana... hata akienda china , wachina watahangaika tu mpaka pale atakapoondoka
Haya bana mie nakujua wewe jinsi ulivyo mtetezi wa presidaa wetu.
 
Sitaisahau 1994 na 2008!! 1994 alipokuja Mzee Mandela, manake ilinibidi nitembee na begi la madaftari mgongoni toka Makutano ya Kilwa Rd/Bandari hadi Posta Mpya!!! 2008 alipofika Bush, siku anaaondoka nilijikuta nafika kazini saa tano....ajabu mie ambe nilifika saa 5 nilikuwa nimewahi sana kwani kuna wengine walifika kuanzia saa 6 mchana!!!
 
kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, presidaa wa states ni ugeni mzito , sana... hata akienda china , wachina watahangaika tu mpaka pale atakapoondoka
Tena hata Huko Ulaya kwenyewe wanahangaika, seuze sisi huku!!
 
Viongozi watakaohudhuria mkutanohuo ni Waziri Mkuu wa Malayasia, Najib Razak, Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, Uhuru Kenyetta (Kenya), Boni Yayi (Benin), Ali Omar Bongo (Gabon), Ikililou Dhoinine (Comoro), Faure Gnassingbe (Togo), Ernest Koroma (Sierra Leone), Blaise Compaore (Burkina Fasso), Mahinda Rajapaska (Sri Lanka) na Mfalme waSwaziland, Mswati II, ambaye aliwasili jana.

Chanzo: MCL
Kagame vipi, ye hataki Smart Partnership au amesusa?!
 
Back
Top Bottom