Kiukweli kauli ya Membe ni upuuzi mbele yawananchi na walipa kodi wanaomlisha na kumlipa mshahara wake anaoringia.
Kitendo cha serikali kujali wapita njia wa siku 2 kwakupulizia madawa yakuua mbu namazalia yake nakuacha wananchi wakifa kwa Malaria kila kukicha, hapa hatuoni usikivu wa Serikali ya CCM badala yake ni unafiki na upuuzi mkubwa wakuficha udhaifu mbele yamabepari nawaporaji wa rasilimali zetu.
Napenda kutoa masikitiko makubwa sana kwamba siku zote atakazokuwepo mshkaj hapa nchini wananchi watakuwa jela bila kujijua sababu biashara namabanda yawamachnga yamevunjwa eti kisa Obama, nanukuu "baadhi ya barabara zitachukuliwa zitumike na wageni hao" mwisho wanukuu. (source Tanzania Daima June 29/2013)
Tusiulizane zitaenda wapi mulizeni Membe, taxi zote stop eti kisa Obama, barabara kupigwa deki eti kisa Obama, wananchi wasiende mjini aidha ktafuta riziki zao au mahitaji yakawaida eti kisa Obama, Namengne mengi yafananayo naunyanyasaji. Kiukweli hapa sichelei kusema HUU NI UPUUZI MTUPU.
Membe haya yote mnaishia kutusomea bajeti ya Ziara wakati kila kitu jamaa kaja nacho, aibu tupu mnajikosha, badilikeni viongoz. Lakini nawashukuru kuendlea kurefusha futi la kaburi manake kaburi mlishachimba la chama kilichomo serikalini.
Poleni wananchi