Membe kuwania urais 2015...

Membe kuwania urais 2015...

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, amesema hajaoteshwa kugombea Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2015.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Waziri Membe alisema harakati za kugombea urais siyo kitu kidogo cha kukurupuka, kwani unatakiwa kuwa na muono unaokujia kuwa mgombea.

“Usikurupuke tu, lazima uwe na kitu kinakutuma kuomba kugombea Urais, lakini sasa ninachosikia ni kutoka kwa watu kuwa nataka kugombea kitu ambacho hakina ukweli,” alisema Membe.
Membe alisema wakati alipotaka kugombea ubunge, alisikia sauti ikimtaka kugombea na akafanya hivyo, lakini kwa sasa bado sauti hiyo haijamjia.

“Sauti kama hii ilinijia wakati nilipotaka kugombea ubunge nami nilifanya hivyo, lakini sasa bado sauti hiyo haijanijia,” alisema Membe.
Namkubali
 
Yani atakayemrithi JK itakua ni chaguo la JK kwanini?? ndio kulindana huko sio....anamueka mtu wake ili amfichie madhambi na madili yake sio.....haya we!!
 
Jambo moja nina uhakika kuhusu Membe na Urais.
Awali ya yote, wa kwanza kabisa kuzungumzia suala la Member na Urais ni gazeti Rai miaka kadhaa iliyopita pale alipomuumbua Hassy Kitine. Wakati huo Membe alikuwa ni Mbunge tu...enzi za Mkapa. Likewise, wengi wakati huo walikuwa hawamfahamu Membe.

Baada ya Kombora la Membe ambalo lilimwondoa Kitine kwenye nafasi ya Uwaziri, Rai ikafanya mahojiano na Membe na moja ya maswali ambayo ilimuuliza ni kama ana mpango wa kugombea Urais 2005. Membe akasema wazi kwamba hana mpango huo.

Baada ya kuingia JK, Membe alianza unaibu Waziri (if am not mistaken, mambo ya ndani au nishati). Later akateuliwa Waziri Mambo ya Nje! Kama ilivyo mazoea yetu, tunazani kila anayekuwa Mambo ya Nje, ni move towards Urais...hili lilitokana na Mkapa na JK kuwa Mambo ya Nje b4! Hapa sasa, ndipo Wabongo tukaendelea kuitilia nia suala la Membe na Urais. nakumbuka hata yeye mwenyewe aliwahi kujibu kwamba, hadi yeye, kuna Mawaziri 13 ambao walipitia nafasi hiyo, na only 2 ndio wamepata kuwa marais.

So, kama kweli Membe ana nia na Urais, basi nia hiyo ilijengwa na vyombo vya habari pamoja na wananchi. Katika hali ya kawaida, ikiwa watu wanakuzungumzia zungumzia kuhusu post fulani, basi huenda nawe ukajikuta unajihisi labda unastahili kwa nafasi hiyo!! Na as far as nae ni Mtanzania basi anastahili nafasi hiyo....Wapiga kura ndio watakaomua kama anafaa au hafai.

Binafsi, sijaona move yoyote ya Membe kutaka Urais sana sana ninachokiona ni hofu ya wanaotaka urais pamoja na wapambe wao. Hawa watu inaonesha dhahiri kwamba wanamuhofia Membe...!!!

Bla bla
 
Wadau kama inavyofahamika Waziri Wa mambo ya Nje ndie anaekuwa Rais, Mhe. Maembe anajiandaa kumridhi JeiKei hapo 2015. imeshapangwa Kaarume ndo atakuwa Makamu wakati huo huo Mtoto wa Mkulima ataendelea kuwa PM. HABARI NDO HIYO
 
HAPO CHADEMA MLIE TU hamana chenu labda 2020.SLAA Kajipange upya kama 2020 utakuwa bado na nguvu ya kusimama jukwaani
 
Hivi na Membe anauota Uraisi? duuh! basi hata mimi nitakuja kuwa Rais 1 day.SERIOUS!
 
Ameshasikia sauti? maana amekaririwa mara kadhaa akisema kuwa bado hajasikia sauti ikimwambia agombee Urais
 
Tuache misimamo hasi na yenye harufu ya wivu.Dual Citizenship ni nafasi kwa watanzania wote waliopo hapa, waliopo nje badokama watanzania na walio na passport za nje, ni kwa wote hawa, ni kwawatanzania wote. Cho chote kizuri kwa mtanzania mwenzangu na ambacho ni halaikisheria yeye kupata hata kama sinufaiki nacho moja moja kwa moja ni wajibukukiunga mkono 100% (maana huenda rafiki au ndugu yangu akanufaika na kwa maanahiyo pia mtanzania yeyote ni ndugu). Ni wachache wanahitaji passport, mbonahatupingi uwepo wake ili iwe kwa safari za kiserikali tu. Tayari raia wa nje(ambao ndio wakuhofia au kuonea wivu) Tanzania inawapa uria (passport nimakaratasi ukweli tunamwamini tu kwa matumaini) - Sasa ni yupi wakuhofia kuwana passport ya Tanzania ni huyu mzawa wa nchi ya nje au huyu mzawa waMtanzania. Narudia tuache mtazamo hasi na wivu.
 
Hii habari wala haikukaa sawa zaidi ya kuzungumzia maudhi ya Mudhihir..Kinachonishinda kuelewa ni kwamba Membe pia ni Mbunge wa Mtema huko Lindi iweje awe mtu asiyependa maendeleo ya Lindi?..Hicho kiwanda cha saruji ambacho wanadai Membe anakiwekea ngumu, tuambiwe sababu basi! na kinajengwa na nani na kwa kibali gani hata Membe aweze kuzuia uwekezaji huo..

....

Mkandara,

Nadhani ugomvi mkubwa ni kwamba kiwanda kinajengwa jimbo la Membe wakati malighafi inapatikana Mchinga jimbo la Mudhihir kitu kama hicho..si unajua kila muamba ngoma
 
Mkandara,

Nadhani ugomvi mkubwa ni kwamba kiwanda kinajengwa jimbo la Membe wakati malighafi inapatikana Mchinga jimbo la Mudhihir kitu kama hicho..si unajua kila muamba ngoma

Maundumula hauko sahihi, Lindi mjini anakotaka Membe kijengwe kiwanda sio jimbo la Membe. Fanya utafiti kabla hujarukia keyboards!!
 
Maundumula hauko sahihi, Lindi mjini anakotaka Membe kijengwe kiwanda sio jimbo la Membe. Fanya utafiti kabla hujarukia keyboards!!

Ndio maana nilitumia neno "nadhani" kuonesha kwamba sipo certain.

Nashukuru kwa kunifahamisha.
 
Je anazo qualities zote za kiongozi? Ni zipi? Je ni kweli ana hasira? na itakuwaje watu ambao aliwakosea au walimkosea siku za nyuma? Maana mmoja kati ya sifa kuu za kiongozi ni kuwa mvumilivu ama sivyo itakuwa kila kukicha unanyonga watu.

Je wanaompinga wana mawazo gani kuhusu huyu mheshimiwa? Nazungumzia kuanzia akina Mudhihir mpaka waliopo madarakani juu.

Je tangu aingie Foreign kuna mabadiliko gani makubwa kashafanya?

Nauliza kwa sababu inaonekana kuwa kuna kila dalili anaweza kuwa rais wetu 2015 lakini je watanzania wategemee rais wa namna gani na presidency yake itakuwa ya namna gani?
 
Ameweza kufanya rais wetu atalii dunia nzima kwa kumuandalia safari hata ambazo hakustahili, kajenga hotel yake kule kwao, pia ni kiongozi ambaye yupo kuonewa huruma.
 
Back
Top Bottom