Membe kuwania urais 2015...

Hakuna msafi ccm. Wote wako pale kwa interest zao. Muulize nyumba za serikali ziko wapi? yeye ndiye alikuwa master minder

Jaman wana JF. TUKUE BASI KIDEMOKRASIA HAKUNA AMBAYE ANAPENDA MAENDELEO YA KWELI asiyejua cv. Ya mtu kama sokoine mrema pamoja na hao wakina mwakyembe,selelii,ole sendeka,anne kilango, sitta, na pia Magufuli kutokana na wao kuwa na ukali kwenye maslahi ya Taifa hili lakini wanaonekana kama wasaliti wa ccm na ndiyo maana hata Dk. Silaa na chadema wamejipatia umaarufu kutokana kuwa kuwaandama wenye uchu wa nchi hii. Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni mimi sina chama navutiwa zaidi na sera na cv. Ya mgombea pia anajali masilahi kwa kiwango gani na kuhusu sauala la nyumba alikuwa anafuata amri za wakubwa zake wakina brother ben. Kama kweli tunataka mabadiliko ya kweli siyo suala la chama gani anakotoka ila ni cv.yake ndiyo inayomuuza na ukali wa magufuli utakuwa mwiba kwa mafisadi na wazembe waliojaa kila mahali serikalini.
 
Chama tawala kina mpango wa kuteuwa askari wake machachari John Pombe Maghufuli aukwae urais 2015 ili airejeshe heshima ya chama,kwani anajulikana kwa uchapa kazi,mpo hapo????

hawezi kupitishwa. Atakayepitiswa ni Lowasa. Kampeni yake inaendelea vizuri. Fanikio lake la tatu ni kuhakikisha Sita hawi spika.
 
Yaani JK angemweka Pombe kama PM wako ndo ange march ie raisi jokes kidogo alafu PM mnoko.
Ila Uraisi Pombe ni mkali mno kuna watu watahama nchi
 
Derimto, Nakwambia hakuna mtu msafi ccm maana wote wanalazimika kuwa kama wenzao wezi walivyo.
Nambie nani katika ccm ya Kikwete (Achilia mbali ya Kambarage) ni msafi? nambie na mimi nikutajie list ya wote na maovu yao mmoja baada ya mwingine!

Achana na hao wakina mama Kilango ni wasanii. Mtu aliyekelwa na wizi na kuamua kuondoka ni Mpendazoe tu ambaye hakuvumilia! Huyu ni msafi. Wengine ni kama kuku. akila hata kinyesi cha mtoto anapangusa mdomo na maisha yanakwenda mbele. Hao ndio wakina Kilango na Dr Mwakyembe. Hamna lolote!
 
Chama tawala kina mpango wa kuteuwa askari wake machachari John Pombe Maghufuli aukwae urais 2015 ili airejeshe heshima ya chama,kwani anajulikana kwa uchapa kazi,mpo hapo????

Huyo naye fisadi tu kama wengine ana issues nyingi tu zinamuandama mfano uuzaji wa nyumba za serikali. Kwa jinsi hali ilivyofikia rais bora hawezi kutoka sisiem. Hawana suluhu ya matatizo ya kweli ya watanzania. Kwa bahati mbaya kuanzia sasa kwenda mbele watatumia muda mwingi sana kulindana au kulinda mifumo yao badala kutafakari jinsi ya kuwaletea maendeleo wananchi.
 
umenena mjumbe
 
kwa mtazamo wangu mimi raisi wa 20015 awe Migiro,mwandosya,Magufuli tusiwachague wote lao moja sisi tusonge mbele na chama chetu cha ukombozi

mbona hamumtaji t.i.b.a.i.j.u.k.a haka ka mama tishio. Ila prezdaaa ajaye ni MARK MWAAAAAAAANTOOOOOOOSHA.
 
hahah hayo makabila makubwa Marehemu Baba wa Taifa alishaonya wasipewe nchi lol, ila lolote laweza tokea CCM hawamuenzi tena Baba wa Taifa kwa hiyo Tibaigana i mean Tibaijuka aweza kuendelea na mchakato lol:tape:
 
mmmh hayaaaa
 
Dah kaka umemaliza vizuri sana hapo mwishoni hahahaha
 
Mwandosya anafaa ila mi sitaki itokee ccm wamchague, ataleta upinzani kwa chama cha ukombozi!
Wampe fisadi Lowasa tu ili wananchi watende haki yao ya kuibwaga CCM 2015!
 
Sisi tunajipanga full force 2015 nyie endeleeni ni utabiri wenu wa kurudisha mafisadi muendelee kuliwa kaa samaki....president lazima atoke chadema 2015!
 

2015 change we can!
 
Ndiye kiongozi anayepiga debe kwa nguvu juu ya inji yetu kujiunga OIC. Havi karibuni wakati wa uchaguzi alifanya closed door meeting na viongozi wa madhehebu ya kikristo. Anataka kuelekea wapi........?
 
waache bana kwanza nakosea mi naona wajiunge na al kaida kabisa
 
Huyo nae ameshapotea, ametumiwa na JK bila kujua kumbe amejiaribia kotekote, na safari hii anaweza asirudi
 
Huyo nae ameshapotea, ametumiwa na JK bila kujua kumbe amejiaribia kotekote, na safari hii anaweza asirudi

Si rahisi JK amtose huyu ni mshikaji wake wa damu, ndio maana alisikitika mara ya kwanza kwa kumpa unaibu na chance ilipopatikana tu akampa wizara nyeti.
 
waache bana kwanza nakosea mi naona wajiunge na al kaida kabisa

Usichanganye mada ndugu, au kama vipi punguza munkari. Al Qaeda ni kikundi cha kigaidi wakati OIC ni taasisi ya maendeleo. Tunachotafuta hapa ni maslahi gani anatafuta BM kwa kujikomba kwa waumini wa kiislamu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…