Membe kuwania urais 2015...

Membe kuwania urais 2015...

Chama tawala kina mpango wa kuteuwa askari wake machachari John Pombe Maghufuli aukwae urais 2015 ili airejeshe heshima ya chama,kwani anajulikana kwa uchapa kazi,mpo hapo????
Huyo ndo mtu pekee anayeweza kuiokoa CCM vinginevyo kwa kasi iliyoonyeshwa na wanamapinduzi kwenye uchaguzii huu CCM itakufa 2015 hata kama watachakachua na kuchekecha kama wanabomboka enzi hizo kwa wale wazee wenzangu.
 
Ukumbuke ndani ya CCM mara mbili sasa maraisi wametoka Bara, wazanzibar nao watakuja juu watataka this time atoke Zanzibar

Hilo si swala zuri hata kidogo labda waache kuchakachua katiba ................................. wapimwe kwa uwezo wao si uzanzibari. wangombanie nafasi kama kawaida. Ikitokea hivyo basi wazanzibari watakuwa wana marais wawili kwani Znz sasa ni nchi kamili.

Unonaje
 
lakini nilisikia kuwa Benard Membe ndiye atasimamishwa na CCM kugombea nafasi ya Urais.
 
Ukumbuke ndani ya CCM mara mbili sasa maraisi wametoka Bara, wazanzibar nao watakuja juu watataka this time atoke Zanzibar

hawa wazenj kwanza idadi yao hata m na nusu hawafiki, wanatupeleka peleka kutaka usawa..ccm watajiju, wamweke mzenj, m'bara chadema itashinda tuu..amani kwa wote.
 
Asitoe ahadi ya hii kitu kama mwenziye

apecallesinofront.jpg

Yafaa kuwa Ambulance hii!
 
Magufuli hawezi, yeye ni mtu wa amri-amri tu.urais unataka busara na hekima kama za DR wa ukweli!!!

kaka huyo ndo tunayehitaji sasa hivi mafisadi wananguvu sana lazima apatikane mrema au paul kagame type akitoa amri saa mbili saa nne imeishatekelezeka tanzania nzima,sio hawa wa kupenda busara,kuunda tume za uchunguzi ili kupoteza muda na pesa
 
ccm isubilie kuangukia pua maana wameishiwa wa kumsimamisha.........adi wana taka waiweke pombe igombee urais Dkt slaa jiandae kuchukua nchi
 
Ni ngumu sana rafiki yangu si magufuri si lolote kama nindani ya CCM hakuna wa maana wote wamo katika Boat moja. Cha maana mtu atoke nje ya CCM. However, CCM huu ni muhula wao wa mwisho. Muhula ujao wajaribu na wengi tuone. tumechoka nao kishenzi.
 
Chama tawala kina mpango wa kuteuwa askari wake machachari John Pombe Maghufuli aukwae urais 2015 ili airejeshe heshima ya chama,kwani anajulikana kwa uchapa kazi,mpo hapo????
Raisi ajaye ni Dr. Slaa kwani hawezi kuchakachuliwa mara mbili.......................aliyeumwa na nyoka akiguswa na jani hufanya nini?.................hushtuka..........................Mwenye macho aone na mwenye masikio asikilize hili baragumu.................
 
Si kama napenda sanaaana rais atoke chi chi emu hta kma angekua msafi kama theruji inayokwisha mlima kil.hapa ni chamgema kwa kwenda mbele
 
Chama tawala kina mpango wa kuteuwa askari wake machachari John Pombe Maghufuli aukwae urais 2015 ili airejeshe heshima ya chama,kwani anajulikana kwa uchapa kazi,mpo hapo????

Tatizo chama kinamilikiwa na MAFISADI, kwa hiyo sidhani kama hilo linaweza kutokea, na hata ikitokea ninamashaka huyo Magufuli kama anaweza kuwa yule wa enzi ya Mkapa. Mkumbuke kuwa hata JK watu walimwona anafaa kutokana na msimamo wake, hasa anakumbukwa pale mwaka 94/95 alipopewa wizara ya fedha mara moja alifunga akaunti ya Kighoma Malima kule UK, na wabongo wakamwona anafaa na anaweza kuwa mtetezi wa wanyonge, kumbe wa mafisadi.

By the way, yetu macho.
 
Chama tawala kina mpango wa kuteuwa askari wake machachari John Pombe Maghufuli aukwae urais 2015 ili airejeshe heshima ya chama,kwani anajulikana kwa uchapa kazi,mpo hapo????

hatupo! si tunajua lowasa ndiye mgombea 2015!
 
Back
Top Bottom