Membe kuwania urais 2015...

FJ kuna mtu ametuloga. Sasa hivi tunasahau hoja za leo na kuingia kwenye ramli zinazohusiana na miaka karibu sita ijayo. Kujadili kufaa au kutokufaa kwa Membe au mwanasiasa yeyote kwa sasa ni pre-mature na kwa maoni yangu hakuna tija yoyote maana hao tunaowaona leo siyo lazima wawepo ulingoni wakati huo na wala hawana hati miliki ya siasa za nchi hii. Kumbuka miaka sita ijayo population ya nchi hii itaongezeka by more than 5% na wapiga kura wa ngazi mbalimbali watabadilika kwa kiasi kikubwa na hata utashi wao na vipaumbele vyao vitabadilika. Hata hivyo, who said that Membe is interested in the presidency? He has not declared his intention or ambition. Mimi nadhani apimwe kwa nafasi yake badala ya kupaza sauti za watu ambao wamejazwa na hofu kuwa candidature yake (perceived) ita-scuttle bids za wanaoutaka kweli. Mimi nashauri tusiangukie kwenye mtego wa watu wanaoendesha opinion poll kupitia JF na kupima upepo wa kukubalika kwao kwa kuchochea mijadala isiyo na tija. Tujadili ya leo na vita ya karibu kwetu ambayo ni 2010 maana hatujui kama hata huyo Membe atatetea kiti chake cha ubunge, achilia mbali kuteuliwa tena kwenye uwaziri huo. Nionavyo mimi politics za 2015 zitatengenezwa 2012 kwenye chaguzi za chama chao CCM.
 
Nyie ngojeni ipigwe kura ya maoni kuondoa vikomo vya urais.. kwa kisingizio cha demokrasia.. mnaye Kikwete hadi Ridhiwanni atakapomrithi.
 

- Mkuu ninakubali hoja zako, kwa sababu ni vyema kujadili tulichonacho kuliko kujadili tusivyonavyo, ukweli ni kwamba in the next 25 years, ma-Rais wetu wa Tanzania wataendelea kurithishwa na incumbents, ni waste of our time kujadili uchaguzi wa Rais 2010 ambao tayari hata Wapinzani wetu wamekubali kwamba umeshaamuliwa,

- Kuacha some few mistep ya Waziri Membe, kama ile ishu ya IOC, UN na silaha na pale alipowafokea mabalozi wa nje kwamba wasijiingize kwenye uchaguzi, sioni tatizo kubwa sana kwake kuwa Rais, na the fact kwamba sasa yeye na Lowassa and the gang ni maadui wa ajabu sana inatia moyo kidogo kwamba somehow huenda yuko sober, lakini in the end sina uhakika sana ndio maana nikaiweka hapa ichambuliwe. Ingawa pia katika ulimwengu wa siasa between now and 2015 a lot can happen.

Respect.


FMEs!
 
Kwa maono yangu ni kuwa, kama JK akiruhusiwa kuendelea na uraisi, basi 2015 tunaweza tusiwe na uchaguzi maana nchi itakuwa iko kwenye civil war au vurugu nyingine zinazofanana na Civil War. Mola tuepushe na hili.

Hakuna Civil war wala vurugu Kikwete ni Rais miaka mingine mitano! The only advantage ya hilo ni kwamba wananchi watakuwa kama ni somo wamelipata kisawasawa hapo labda tunaweza kuanza kufikiria upinzani pia.

Membe ni Business as usual! Unatumia vigezo gani kumfikiria Membe kuwa Rais wa Tanzania! He is an ordinary Politician with an ordinary record! Hana record yeyote ya kufanya mambo extraordinary! Tunataka watu wanaothubutu kubaibadilisha hii situation ya business as usual, People who can turn things around! Magufuli can be a very very credible candidate, the only problem with people of such a record are public enemy number one!!!! they will not allow Him even near the Presidency form.
 
Huu ni upotoshaji,kwa nini kuzungumzia 2015 badala ya 2010? Tunataka Rais mpya 2010 kisha tutajadili hayo ya 2015.
Hapo pekundu hebu tutajie mmoja tu atakayeweza kusimama na Mh. J.K 2010?,Kwa sasa tuachane na 2010 kwani inaonekana watu wanamkwepa wanaanza mchakato wa 2015, sasa ni bora tuanze kujadili ya 2015.
 

Not that much powerful! If he was such influential He wouldn't have quitted. So far He doesn't have the majority in the party!! So usimpe kichwa bure!
 


kwa uchaguzi wa 2015 ambapo makundi ndani ya mtandao yanaanza kusigana nasema wazi ni mara mia rais awe bernard membe kuliko edward lowassa nitaendelea kutaja sababu mbalimbali katika hilo, however bado tukiamua asha rose migiro anaweza kutusaidia pia.
 

Tanzania ya leo hii haihitaji mtu wa aina ya Membe!.i see him as too linient, na amekaa kisherehesherehe zaidi...Membe kauli zake kila siku ni za kitatanishi tu, na ana hali ya kupendelea baadhi ya nchi!....Tanzania hii by 2015 inahitaji rais ambaye ni 50%coctail ya udikteta na Busara!...Punda haendi, ila kwa mjeredi!
 

kwani uchaguzi wa mwaka huu tayari matokeo?
 
Baada ya huyu mtu wenu, ni bora tukapata mtu asiye fungamana na chama cho chote cha siasa hasa ccm (better awe na dictatorship mind set) na siyo membe wala yeyote kutoka ccm
1-avunje na kuunda upya tume ya uchaguzi na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa kwa mwonekano wa kitaifa na si kisiasa, kabila wala dini
2-arekebishe au asimamie kuandikwa upya katiba
3-ikiwezekana hata mahakama iundwe upya na ipractice kuwa chombo huru
4-ikiwezekana hata vyama vya siasa vivunjwe na kuundwa upya
 


Hii demokrasia feki haijatusaidia lolote! Naunga mkono tunahitaji dictator kama yule aliyewahi twala South Korea baada ya vita vya Korea
 
Whaat? Tafadhali usifanye utani!!
 

Asha rose mingiro hana uwezo hata nusu wa kuiongoza tz, Tanzania inahitaji watu wenye mukrari na force ya nguvu kwenye utendaji. Hata kama Lowasa hata kubalika, tunatakiwa mtu mwenye aina ya utendaji wa kilowasalowasa madarakani. hapo ndo tutafika. hivi wewe kwa akili yako umeona acha rose mingiro anaweza chochote, au kwasababu alipigiwa pande aende UN, hivi kila mtu aliyepata habati ya kwenda UN unafikiri ana uwezo wa kuwa rais?....unafikiri kama wangesema tuchague sisi watz kwa kura mtu wa kwenda UN asha angeenda? si bahati yake tu ilimdondokea.....hebu leta wazo lenye akili tafadhali, ondoa fikra za ajabuajabu hizi.

Lowasa anatakiwa kurudi, amejeruhiwa na akirudi lazima atahakikisha anasafisha jina na kuweka historia kuwa yeye si mtu mbaya, hiyo iko wazi. kama akiwa rais atajitahidi uwezo wake wote kufanya kitu cha maana ili ionekane kuwa yeye ndo alikuwa bora na safi kuliko wote. NA HAKUNA UBISHI KUWA KATIKA SELIKALI YOTE YA TZ, HAKUNA MCHAPAKAZI KAMA LOWASA...namfananisha na Kagame, akiwa kazini hataki kunegotiate ujinga, hataki utani ni kupiga kazi kwenda mbele. huu ndo ukweli wenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…