Membe kuwania urais 2015...

Membe kuwania urais 2015...

- Dalili zote huko nyuma ya mlango according to the dataz, zinaonyesha kwamba Waziri Membe ana nafasi kubwa sana ya kushika nchi ifikapo mwaka 2015, sio vibaya kwa sisi wananchi tukaanza kujiuliza mapema je tunaweza kuwa better off na Membe kuliko wengine na hawa wa sasa? Au yatakuwa ni yale yale?

Respect.


FMEs!

hana akili ,hana upeo ,mwingi wa blah blah hafai hata kukaa hapo alipo sasahivi sembuse urais
 
hana akili ,hana upeo ,mwingi wa blah blah hafai hata kukaa hapo alipo sasahivi sembuse urais
JK kaweza atakuwa huyu. Ana sifa moja nzuri inayowafaa marais wa nchi hii: Anatoka kwenye kakabila kadogo ka nchi hii, ka watu ambao hawajasoma sana, sio wafanyabiashara sana, sio wadinidini sana.
 
nchi hii kila kitu kinawezekana...mimi itashangaa kuokana nauhusiano wa membe na JK, JK anahitaji mtu atakayemmudu..... kisifa sioni uzito wa membe, nimkurupukaji na mbabaishaji tu
 
- Dalili zote huko nyuma ya mlango according to the dataz, zinaonyesha kwamba Waziri Membe ana nafasi kubwa sana ya kushika nchi ifikapo mwaka 2015, sio vibaya kwa sisi wananchi tukaanza kujiuliza mapema je tunaweza kuwa better off na Membe kuliko wengine na hawa wa sasa? Au yatakuwa ni yale yale?

Respect.

FMEs!

Wabongo mnakera sana, yaani huyo biskuti ndo awe Rais!!!
Hivi Unatutafuta nini wewe!!! Haki ya mjomba Membe atakulaumu kwa hili.

Ngoja nikavae magwanda yangu nikukute hapa na hii 3di yako, Membe atakulaumu.
 
Ni kitu gani hasa kitakachomfanya yeye awe bora zaidi ya hao walio katika Boti moja na yeye??....Membe ...Profile. 2015 -Prezident ..not so sure
 
We will cross that bridge when we finish the elections in 2010, it at all elections will be there!!!!! I am afraid they may be postponed!!!
 
wote ni wale wale!
ANAFAA TU kama ndugu yake
 
its possible kwa yeyote kuwa Raisi, we lack leadership ethics, we lack national priorities, we don know where we are goin as the nation! with no direction any one can take us as we are sure we wont get lost! For wherever he/ she will take us, we cant say we are lost! If no serious changes in between, I wont wonder If MAghembe will be our president, or Even Marmo for experience sake!
 
Mkuu FMES,

Mbona ni mapema sana? Miaka mitano ni mingi sana kwenye siasa.

Mambo yote yasipobadilia, mimi nitamfagilia mama Magiro kwa mwaka 2015. Umefika wakati wa kuongozwa na mwanamke maana kama ni wanaume tumevuruga vya kutosha.


Mkuu,

It sounds like utafagilia jinsia.

Nwei, Mama Migiro anafaa lakini sidhani kama ataweza mikiki mikiki maanake lazima tuangalie taifa litakuwa linapita katika wakati mgumu kiasi gani huo muda.Inabidi huo muda tuwe na rais mchapa kazi zaidi na asiye na woga kwani nafasi ya Tanzania ndani ya EAC pia ni changamoto kwa kiongozi wa muda huo

Membe,huyu jamaa ni afadhali kuliko Jk coz anajua kujenga hoja za maana kulingana na profession yake ingawa si mbunifu.huyu ni mtu wa kulinda status quo

Huko CCM nadhani John Pombe Magufuli ndiye ambaye angetufaa kwa muda huo au Samweli Sitta.

Magufuli ni mchapakazi na ni mbunifu,ana moyo wa Ujasiri nk

Sasa mleta hoja sijui atakua amezingatia ndani ya chama Tawala tu ama,maanke tuna wachapakazi kama akina Dr.Slaa huko opposition.

Si vibaya kuwajadili potential leaders wetu kama wengine wanavyotaka kuonyesha.Nasizitiza,ni bora kuwajadili sasa hivi tuwajue kuliko kusubiri yatufike ya Benjamini Mkapa.

Ingawa najua hata JK alijulikana tangu mwanzo lakini still tukaambulia maumivu

 
Mkuu FMES,

Mbona ni mapema sana? Miaka mitano ni mingi sana kwenye siasa.

Mambo yote yasipobadilia, mimi nitamfagilia mama Magiro kwa mwaka 2015. Umefika wakati wa kuongozwa na mwanamke maana kama ni wanaume tumevuruga vya kutosha.

Haya mambo ndiyo yalitufanya tukampata Vasco da Gama wetu huyu na sasa tunalia, tuliamua kumfagilia mtu basi tu eti kijana.....
Sasa hivi na wewe unakuja eti mwanamke full stop! Mwanamke tu ndiyo sifa kuu uliyotanguliza!! aibu gani hii!
 
Ni mawazo chakavu yenye chembechembe za KIKADA na vumbi vumbi la UFISADI yaliyoathiriwa na kansa ya TAMAA kuanzisha kampen kwa mgongo wa nyuma, kama Magufuli hafai basi 2015 CCM wasiweke mgombea (Hawana mwenye sifa hata ya kuwa diwani).jadili Role ya membe sasa sio baadae.kama hafanyi kitu sasa KWA NINI TUTEGEMEE miujiza mbele!!!!!!!!!!!!!
 
Membe? A joke? Labda kwa vile inasemekana yeyote aweza kuwa Rais Tz almuradi abebwe na CCM. Vinginevyo, huyo mh. Membe hana visheni wala mtazamo wowote binafsi unaoshawishi kimantiki. Sanasana ni kipaza sauti cha mfumo choka uliopo sasa ambao hauleweki unakotupeleka. Simuoni Membe kama mtu mwenye sifa za uongozi makini na fresh wa kisiasa anayeweza kushughulisha bongo zetu kumjadili hapa. No value added.

Halafu, tuwe wakweli; hawa watu wengine hawana sifa za uongozi wa kisiasa. Nafirikiri baada ya kipindi cha mzee Mwinyi ni kama vile kila mtu alianza kuamini anaweza uongozi wa kisiasa na hata u-Rais. Watu kama Mkapa, sifa ya uongozi wa kisiasa hakuwa nayo labda ya uendeshaji (management) ambayo nayo baadaye aliiharibu kwa kuamua kuzama kwenye ufisadi. Muungwana naye ana kipaji cha siasa lakini kwenye uongozi ni dhahiri kuwa ni hasi. Pinda ndio taabani kwa kila upande. Shein is just a nice guy. We are lost.
 
- dalili zote huko nyuma ya mlango according to the dataz, zinaonyesha kwamba waziri membe ana nafasi kubwa sana ya kushika nchi ifikapo mwaka 2015, sio vibaya kwa sisi wananchi tukaanza kujiuliza mapema je tunaweza kuwa better off na membe kuliko wengine na hawa wa sasa? Au yatakuwa ni yale yale?

respect.

fmes!


mku sidhani kama huo mlango wa nyuma ndio unaopiga kura!!!!kila mtanzania anayohaki ya kuwa kiongozi wa juu ya nchi yetu kwa kuchaguliwa na wananchi kutoka na taratibu ziliwekwa na chama chake(kura za maoni).
 
Hapa bado ngoma ni nzito nikianza kupanga 2015 ni kama ifuatavyo,
1. Prof. Mwandosa
2. Edward Lowassa
3. B. Membe
4. Pombe Magufuli
5. Six (6)


Hivi kada wa chama ni nani kati ya hawa?

Moja mpaka tano wakiwasha moto, Kuna kila dalili Rais kutoka upinzani

 
Kwa historia ni kweli membe ndio boss wa baraza la mawaziri ajae, kukumbusha tu inaonekana mawaziri wote wanaokuwa mabosi pale wizara ya mambo ya nje ndio huja kuwa marahisi ( ndio maRAHISI sio RAIS)! lakini hakutakuwa na uhafadhali wowote, ni sawa na kusema afadhari shubiri kuliko kwinini, yote ni yaleyale vyote ni vichungu
 
Huu ni upotoshaji,kwa nini kuzungumzia 2015 badala ya 2010? Tunataka Rais mpya 2010 kisha tutajadili hayo ya 2015.
Ni kweli kuzungumzia 2015 ni kufunga mjadala wa 2010. Kikwete hatakiwi kupewa Green Light na mtu yeyote hata kama ni humu JF.
 
Ni kweli kuzungumzia 2015 ni kufunga mjadala wa 2010. Kikwete hatakiwi kupewa Green Light na mtu yeyote hata kama ni humu JF.

Mkuu,

Kujadili mambo ya 2015 haimanishi mambo ya 2010 yakatazwe.Tusipokuwa makini tutajikuta immediatelly after october election watu wana-rush kuanza kampeni,kenyan political style.watu hawatafanya kazi tena watakuwa busy kuongelea mambo ya 2015

Wanaweza kulipa hilo suala kipaumbele kisichostahili na kwenye nchi hii itakuwa ni siasa na udaku tu.Kama hapa JF kutakuawa kituo kikuu cha tetesi
 
Wakuu inaelekea tumesahau au tunajaribu kufumbia macho ukweli....

hivi hatujui CCM ni ya nani....si ni wazi kwamba CCM ni ya EL na RA na wapambe wao...kumbukeni Bi SS alisema nini kwenye kamati ya Mzee Mwinyi....EL ni mwanaume wa shoka........

mimi nadhani nani awe Raisi itategemea EL anamtaka nani kama hayuko tayari kujipa ufalme yeye mwenyewe...
 
Back
Top Bottom