Membe, honestly hatukuelewi!

Membe, honestly hatukuelewi!

Sio Membe peke yake tu.
Yeye akili zimeanza kumrudia mapema.

Wengi wako nyuma yake,ni suala la muda tu

Umenikumbusha Kipindi cha kampeni team Lowasa walivyokuwa na propaganda za vigogo wa ccm kuhamia Chadema.
 
Hukumuelewa wewe na siyo wote,wengi tumemuelewa vizuri sana.
 
Kuna watu ambao hata ukinambia unilipe mill 100 niwasikilize kwa nusu saa siwezi. membe ni mmoja ya watu wa namna hiyo. huyu jamaa...duh hata sijui. watu wngine wangenyamaza tu kwan mpaka nao waseme? au hawapend kuonekana wana hekima? kunyamaza huwa kuna saidia sana .membe?? one of the people ambao wanastaajabisha sana tanzania hii.
 
tatizo la ccm hamtaki kushauriwa wala kukosolewa. na sasa tangu aingie magufuli uki kusoa serekeli unaonekana wewe sio mtanzania mzalendo.. kila anachofanya magufuli lazima wote tukiunge mkono hata kama ni ujinga... kwani magufuli yeye ni mungu hakoseagi? membe ana uhuru wa kutoa maoni yake na hii inaonesha jinsi gani ccm ni chama dhaifu kwani hawako tayar kumsikia mtu ambae haungi mkono sera zao
Wanaomshangaa Membe si ccm tu. Hata wapinzani hawakubaliani na kauli yake. Magufuli anakosea kama binadamu yoyote. Kinachoangaliwa ni makosa kulinganisha na mafanikio. Halafu wepesi wake kusahihisha mokosa yake na jinsi gani ni msikivu kwa wananchi wake.
 
Hoja ya Membe inafanana na uamuzi wa Mkapa aliposema uchaguzi 2000? hautarudiwa kwa ujumla, utarudiwa tu kwenye vituo vilivyokuwa na matatizo. Sioni hili likijadiliwa humu ma GT wanalumbana tu.
 
tatizo la ccm hamtaki kushauriwa wala kukosolewa. na sasa tangu aingie magufuli uki kusoa serekeli unaonekana wewe sio mtanzania mzalendo.. kila anachofanya magufuli lazima wote tukiunge mkono hata kama ni ujinga... kwani magufuli yeye ni mungu hakoseagi? membe ana uhuru wa kutoa maoni yake na hii inaonesha jinsi gani ccm ni chama dhaifu kwani hawako tayar kumsikia mtu ambae haungi mkono sera zao

Unafikiri Membe ni mkosoaji? Ni namna ya kuendelea kuishi ndio tatizo. Madaraka na muda umempa kisogo
 
ameibuka gafla na kuanza kuuza sura kunako vyombo vya habari huyu membe anataka kutumia ujanja kujenga jina lake kisiasa kwa upya bila shaka ni mkakati wake kuanza tena mbio za kwenda ikulu amenukuliwa na gazeti la mwananchi akiunyooshea kidole utawala wa magufuli lakini pia akaendelea na mgogoro wa zanzibar kila mtu anajua uzito wa haya yote mawili kwa sasa hivyo mr membe anatumia hiyo fursa kuliunda upya jina lake pengne kwa jinsi anavyopima upepo anaona mr magu hawezi kusurvive mpaka mwisho wa mihula miwili hivyo anataka awe kariba kama chochote kitatokea
 
Kwanza hata tano bora asingestahili kama siyo kubebwa mfukoni,
 
Ulikuwa mgombea wa kiti cha urais, wengine walienda mbali kudai ulikuwa wa mfukoni!
Bahati haikuwa yako, dhoruba za yule kada maarufu, Eddo, zilikupulizia mbali.
Hukuwa peke yako, vumbi zili ziliwapuliza wengi.

Ulipoukosa urais ukawa kama umeingia kauzezeta fulani hivi.
Ni kama hukuamini kilichotokea, Mwenyekiti aliyekubeba alizidiwa kete.

Kaingia mzee wa pish up, hata ukatibu wa chama wa kijiji hakuwahi kuukwaa.
Sasa leo ndo Rais.
Tena Rais mtumbuaji majibu.

Mengine ya hayo majipu ni yale Membe and co. waliyalea na kukomaa.
Kwa kauli yake Membe alisema watu wanapaa angani kuelekea majuu, utafikiri nchi inaungua.
Aliyekuwa kinara wa kupaa angani tunamjua, our very own Mkulu wa Msoga.

Sasa leo sijui Membe kala maharagwe ya wapi vile, utafikiri kaamka nazo.
Mara Baraza la Mawaziri hakuna kilichofanyika, mara kuzuia kusafiri nje hamna lolote!
Sasa ati uchaguzi Zanzibar ungefutwa kwa nafungu!

Hivi vikao vya chama kuongelea haya masuala vilikufa?
Au siku hizi ni siasa huria?
Au Membe naye anataka mageuzi nje ya chama?

Maswali ni mengi, honestly Membe hatukuelewi!
Humuelewi kwasababu wewe na wenye akili kama zako mmekosa akili za kujiongeza...tatizo lenu mmetanguliza ushabiki maandazi.
 
MEMBE AMEICHOKA CCM,hilo liko wazi na ndio maana amewashangaa viongozi wa CCM kumshawishi Jecha kuzuia kampeni zanzibar na kufuta matokeo ya kila kituo. Pia amesupport msimamo wa Fatma Karume kuhusu hali ya Zanzibar.
 
ameibuka gafla na kuanza kuuza sura kunako vyombo vya habari huyu membe anataka kutumia ujanja kujenga jina lake kisiasa kwa upya bila shaka ni mkakati wake kuanza tena mbio za kwenda ikulu amenukuliwa na gazeti la mwananchi akiunyooshea kidole utawala wa magufuli lakini pia akaendelea na mgogoro wa zanzibar kila mtu anajua uzito wa haya yote mawili kwa sasa hivyo mr membe anatumia hiyo fursa kuliunda upya jina lake pengne kwa jinsi anavyopima upepo anaona mr magu hawezi kusurvive mpaka mwisho wa mihula miwili hivyo anataka awe kariba kama chochote kitatokea
Daah this is beyond stupidity...
 
MTAMUELEWA TU MEMBE,WAZALENDO WA NCHI HII WALISHAMUELEWA KIJANA.....alishaichoka CCM tokea October 2015, wewe ndio unashangaa hilo leo?
 
Ulikuwa mgombea wa kiti cha urais, wengine walienda mbali kudai ulikuwa wa mfukoni!
Bahati haikuwa yako, dhoruba za yule kada maarufu, Eddo, zilikupulizia mbali.
Hukuwa peke yako, vumbi zili ziliwapuliza wengi.

Ulipoukosa urais ukawa kama umeingia kauzezeta fulani hivi.
Ni kama hukuamini kilichotokea, Mwenyekiti aliyekubeba alizidiwa kete.

Kaingia mzee wa pish up, hata ukatibu wa chama wa kijiji hakuwahi kuukwaa.
Sasa leo ndo Rais.
Tena Rais mtumbuaji majibu.

Mengine ya hayo majipu ni yale Membe and co. waliyalea na kukomaa.
Kwa kauli yake Membe alisema watu wanapaa angani kuelekea majuu, utafikiri nchi inaungua.
Aliyekuwa kinara wa kupaa angani tunamjua, our very own Mkulu wa Msoga.

Sasa leo sijui Membe kala maharagwe ya wapi vile, utafikiri kaamka nazo.
Mara Baraza la Mawaziri hakuna kilichofanyika, mara kuzuia kusafiri nje hamna lolote!
Sasa ati uchaguzi Zanzibar ungefutwa kwa nafungu!

Hivi vikao vya chama kuongelea haya masuala vilikufa?
Au siku hizi ni siasa huria?
Au Membe naye anataka mageuzi nje ya chama?

Maswali ni mengi, honestly Membe hatukuelewi!
Ukiona hivyo ameshaTUMBULIWA
 
Mawazo yake hayana tija kwa sasa. Kuna kipindi yangekua na msaada mkubwa sana lakini kuyatoa kwa sasa ni 'uharibifu tu'. Ingekuwa anakosoa chama angehojiwa na kamati kuu ya Chama lakini kwa kuwa anaikosoa serikali huenda akaviponza vyombo vya habari vinaripoti kauli zake.
 
MEMBE AMEICHOKA CCM,hilo liko wazi na ndio maana amewashangaa viongozi wa CCM kumshawishi Jecha kuzuia kampeni zanzibar na kufuta matokeo ya kila kituo. Pia amesupport msimamo wa Fatma Karume kuhusu hali ya Zanzibar.


Jamani vipi huko Lumumba watu hawana uhuru wa kufikiri ? Tunakuwa na nchi ya namna gani watu hawawezi kutoa ya mioyoni na akili zao ? Hata wakati wa Mwl haikuwa hivi ?

Zanzibar mabaya yamefanyika na hatuwezi kuishi huku nafsi zikitusuta kisa chama. Hiki chama si dini kiasi watu wawe watumwa wa fikra . Membe au mtu mwingine yeyote aachwe a seme aweza kulisaidia taifa hili
 
Kuna watu ambao hata ukinambia unilipe mill 100 niwasikilize kwa nusu saa siwezi. membe ni mmoja ya watu wa namna hiyo. huyu jamaa...duh hata sijui. watu wngine wangenyamaza tu kwan mpaka nao waseme? au hawapend kuonekana wana hekima? kunyamaza huwa kuna saidia sana .membe?? one of the people ambao wanastaajabisha sana tanzania hii.
Miaka yote Membe anaimba "his Masters Voice".
Sasa leo sijui nani kamtuma?
 
Mawazo yake hayana tija kwa sasa. Kuna kipindi yangekua na msaada mkubwa sana lakini kuyatoa kwa sasa ni 'uharibifu tu'. Ingekuwa anakosoa chama angehojiwa na kamati kuu ya Chama lakini kwa kuwa anaikosoa serikali huenda akaviponza vyombo vya habari vinaripoti kauli zake.
Watu hawamuelewi kwa vile hata serikali si niya CCM, sasa anaongea kwa niaba ya nani?
Kama ana uchungu ki hivyo , vipo vikao rasmi vya chama anheongelea huko.
Sasa hivi anaonekana wazi kuwa pamoja na donge la rohoni mwake kuna kofia anitegemea , kofia ile ile iliyotaka kumchomoa mfukoni.
 
Kwamba siku hizi anaandika vitabu. Aombe hata balozi wa Tanzania huko Ughaibuni
 
Back
Top Bottom