Ulikuwa mgombea wa kiti cha urais, wengine walienda mbali kudai ulikuwa wa mfukoni!
Bahati haikuwa yako, dhoruba za yule kada maarufu, Eddo, zilikupulizia mbali.
Hukuwa peke yako, vumbi zili ziliwapuliza wengi.
Ulipoukosa urais ukawa kama umeingia kauzezeta fulani hivi.
Ni kama hukuamini kilichotokea, Mwenyekiti aliyekubeba alizidiwa kete.
Kaingia mzee wa pish up, hata ukatibu wa chama wa kijiji hakuwahi kuukwaa.
Sasa leo ndo Rais.
Tena Rais mtumbuaji majibu.
Mengine ya hayo majipu ni yale Membe and co. waliyalea na kukomaa.
Kwa kauli yake Membe alisema watu wanapaa angani kuelekea majuu, utafikiri nchi inaungua.
Aliyekuwa kinara wa kupaa angani tunamjua, our very own Mkulu wa Msoga.
Sasa leo sijui Membe kala maharagwe ya wapi vile, utafikiri kaamka nazo.
Mara Baraza la Mawaziri hakuna kilichofanyika, mara kuzuia kusafiri nje hamna lolote!
Sasa ati uchaguzi Zanzibar ungefutwa kwa nafungu!
Hivi vikao vya chama kuongelea haya masuala vilikufa?
Au siku hizi ni siasa huria?
Au Membe naye anataka mageuzi nje ya chama?
Maswali ni mengi, honestly Membe hatukuelewi!