Membe - Chadema walikuja kwangu wakiwa na njaa

[h=1]There are three sides to every story; their side, his side, and the truth[/h]
 
jamani tuwe wakweli. ukiandaliwa chakula chako cha mchana nyumbani na mkeo huwa ni shea ya familia inayowekwa mezani kufuatana na kipimo. sasa kundi la g lema na wenzie wanagonga mlango wakati membe ana kihot pot cha nusu kilo kipo mezani angewezaje kuwakaribisha kina lema waliokuwa na njaa na kiu kali na wakashiba? tuanzie hapo kudiscuss.
 
Membe kanisikitisha sana, hata kama propaganda membe umetia aibu, hadi najiskia kinyaa na kutapika kuongozwa na kiongozi mpumbavu na anae ongea maneno ya ovyo kama membe. Anatuambia ye akila itv wanakaa pembeni yake, ye akila huwaga sebleni kwake panapambwa maua kama ya harusi. Membe jipange upya acha uzalilishaji
 
Wakati wa mchakato wa uteuzi wa wagombea Ubunge mwaka juzi (2010) Membe alikuwa 'amepita bila kupingwa' katika Jimbo lake lakini NEC baada ya rufaa iliwarudisha wapinzani wake, na hivyo kulazimika kufanya kampeni.

Inasemekana alimaliza waganga wote wa kulke kusini pamoja na wa Mlingotini kule kwa binamu wake.
 
anataka kupoteza maboya wenzake wa ccm...cc tuna mwangalia tu..kuna siku atakanusha huyu cc tunamjua..mtu mfupi hakosi lakusema daima...wangekuwa na njaa wangekuwa wanatembea na mashangingi kama yeye?..analinda nafasi yake maana kuna wana ccm hawajui maana ya vyama vya ushindani na hawataki kusikia ukweli aliousema membe akiwa jimboni kwake huko Mtama
 
Wema aliouonyesha Membe kwa wana CDM ni wa kufaa kuigwa na mtu yoyote.

Honngera sana Mh. Membe, mungu atakulipa.

Sasa naanza kuamini kuna vijana walioenda kufuata M4C kusini ilibidi kulawitiwa kwanza ndio wakapewa posho zao.
 
sasa kama walikua na njaa si angewakaribisha wale na waongee kuhusu mambo ya familia na watoto kama wameenda shule au wanaumwa..sasa mbona akaanza kuwaambia wajitayarishe kuchukua nchi? huyu anajikanyaga ndio wale wale
 
Alisema hivi

Wakati wanajiandaa kula mlinzi wake alikuja kumwambia kuna vijana wa CHADEMA walikuwa wanagonga mlangoni, yeye akamwambia awakaribishe

akasema pia na "walikuwa na njaa"

mwisho wa kunukuu

Swala la kusema walikuwa na njaa sana,kwani njaa ni
 
Naomba niulize maswali machache tu.
1.Anasema alikuwa anakula akamwambia mlinzi awakaribishe alipoambiwa vijana wa Chadema,
je,alijua hao vijana ni kina nani?

2.Hicho chakula alikuwa amekiandaa akijua kuwa wanakuja?

3.Mbona kwenye taarifa ya siku ile ITV alionekana akiwapokea nje
akawakaribisha ndani,au analiaga nje?

4.Hao waandishi wa habari walitoka wapi?

5.Hata mimi nikijitambulisha kama kijana wa chadema atanikaribisha chakula cha mchana?
 
Ukweli na mi nilibahatika kusikiliza hadi nilichelewa kufika ofisini maana nilidhani ana jipya. Nitaomba mniiwie radhi kwa hii kauli nitakayosema hv hapa Pwani chakula kina thamani kubwa hivo hadi mtu uthubutu kusema publically kusimanga uliwakaribisha chakula? Kauli yake imeonyesha kuwa ameumia sana na kauli ya kuwa ameifagilia cdm. Kwetu sisi wabara chakula ni mavi tu na mwanaume huwa hazungumzii masuala ya chakula eti fulani amekula kwetu hayo ya kitoto kabisa ya kusemeleana eti mwenzako alikula ubwabwa kwetu. Du chakula tu nongwa aisee hafu unataka uraisi siutauwa watoto a senior minister amabaye chakula ni bure tu hapana mheshimiwa ujitahidi kujiepusha na hoja legelege mwe!?
 
Maneno ya kwenye vijiwe vya Ghahawa yeye ndiyo anawalisha?inaingia hakilini?Inabidi kupima maneno mengine wakati wanaongea.
 
Niliambiwa na mlinzi kuna vijana wa chadema wapo nje ya geti wanagonga
Nikawaambia waache waingie
wakaingia ndani wakala chakula kweli kweli manake walikuwa njaa sana na wakanywa kweli kweli

Nyumbani kwa Mbunge na Waziri unaandaa chakula cha watu zaidi ya ishirini
maneno ya mpuuuzi waziri wetu hajaongelea kitu chochote kuhusu wananchi wanaokufa mahospitalini kwa mgomo wa madaktari na vipi nchi yetu inaonekana mbele ya uso wa dunia kwa serikali yake kushindwa kuwathamini madaktari

Akaongeza kama nilisema na nilirecodiwa si wangeweka kwenye u-tube si unawajuwa hao mbona ya Lusinde iliwekwa katika kila mtandao
Akaongeza mimi nilirudi kwenye maeneo waliyopita ni kunipaka matope nikawaambia wananchi na wamenielewa kwamba hawa watu wa Kasikazini watakujaje kuwakombowa nyie wakati walipopangiwa kufanya kazi Lindi walikataa ndio waliodumaza maendeleo ya Lindi
Nimedharau Membe kuliko kawaida kati ya watu nilikuwa nadhani zinawatosha kidogo ni huyu Muheshimiwa lakini leo amethibitisha kuwa ni mjinga haijatokea
Anasema kuna wanajimu wanatabiri nani anaweza kuwa raisi lakini mimi sijaoteshwa sasa huo si unajimu pia mtu unafanya kampeni unamanupulate minds za watu eti mpaka uje uoteshwe ndio uutake wakati unautaka kwa njia mbalimbali eeh bwana usituchezee sisi watanzania CCM nzima hakuna jipya
 
Yote kwa yote mimi aliniacha hoi pale aliposema anasubiri KUOTESHWA kama agombee au asigombee Urais. Hana tofauti na Babu wa Loliondo

Hando akamtia Moyo kwamba kuanzia sasa atakuwa anamuombea sana ili AOTESHWE ha hah a ahaaa fan politician.
 
Back
Top Bottom