Membe - Chadema walikuja kwangu wakiwa na njaa

kuna ukweli mwingi unajificha hapa, kamwe Membe hawezi uweka wazi, hata lema hawezi jibu lolote hapa as mambo mengine inabidi yaendelee kuwa siri ya chama katika level fulani, tusitegemee kuambiwa kila kitu kama kilivyo.
 
membe yuko clouds FM anahojiwa na Gerald hando, anasema hakuwaalika Godless lema na wengine kwake ila alipokuwa mezani mlinzi alimwambia vijana wa chadema wako nje akawakaribisha, wakaingia na walikuwa na njaa kwelikweli wakala

Pili anasema watanzania wanajua kamwe hawezi kuifagilia chadema na hata Clouds wanajua kwanini hawezi mmmh?

kauli hizo zenye rangi nyekungu ndo zinanipa dukuduku, ile story ilikuwa ni propoganda ama kweli?

kasema kama kuna mkanda waliurekodi na wautoe ...atajiudhuru hata sasa!

Nimestaki kidogo
ngoja niendelee kumsikiliza nakuja kuleta uptodate




This is from a rude guy on the Strit, busara ni maneno na vitendo. Membe hana busara hata kidogo analeta michezo ya uswazi au kota "Karibu ule japo kidogo, ukionja tu kazunguka mtaa wa pili kukutangazia kwenu kuna njaa"
 
kwani mwana cdm kula kwa ccm ni kosa jamani?it seams sasa wanasiasa wanataka kutugawa kiasi cha kunyimana hata maji!
Mbona ni suala la kawaida tu mtu kula kwa mtu mwingine.
Mimi nikionacho hapo sio kula tu,bali ni kauli zilizotolewa na membe.
 
watu wana njaa....wakaenda kudowea msosi...wakala wakashiba na kusaza...na uzushi wakatunga....Kweli shibe mwana malevya...
 
W
aziri wa mambo yanje Bernard
Membe amekitabiria ushindi chama cha Demokrasia namaendeleo-CDM katika uchaguzi mkuu unaokuja.

Waziri
Membe amesema chama cha CDM kimetokea kupendwa nawananchi katika kila kona ya nchi na hata operesheni yao ya kusini imekitikisachama tawala.

Waziri
Membe aliyasema hayo katika chakula cha mchanaalichowaandalia viongozi wa CDM nyumbani kwake waliokuwa katika jimbo lake laMtama.

Viongozi hao ni mjumbe wa kamati kuu Godbless Lema,kamanda James Millya naviongozi wakuu waandamizi.

Waziri
Membe aliwaambia viongozi hao ameishi nchimbalimbali duniani zenye demokrasia ya hali ya juu hivyo hatashangazwa hatakidogo CDM kuingia Ikulu.

Kuhusu kesi iliyotengua ubunge Lema waziri
Membe amedaikushtushwa na kusema kwa vile amekata rufaa anaamini mahakama ya rufaaitamrejeshea ubunge wake.


Bernard Membe
Nimefafanua kuhusu uvumi uliotolewa na vyombo vya habarikuhusu kukutana kwangu na vijana wa CHADEMA waliofika nyumbani kwangu jimboni

Bernard Membe

Nimewaeleza kuwa upinzani si uadui na wapinzani si maaduizetu.

Bernard Membe
Sijawahi kuitabiria CHADEMA ushindi kwa kuwa sina kipaji hicho ambacho kinapatikana kwa Synovate,Mtoto wa Sheikh Yahya na TD Joshua

Bernard Membe

Upinzani upo kwa mujibu wa kanuni, sheria na Katiba hivyohauwezi kuwa uadui. Wapinzani wako ndani ya vyama vyetu wenyewe


Bernard Membe

Nina imani uvumi huu haujaenezwa na CHADEMA bali watu nje ya CHADEMA wenye malengo yakisiasa haswa kunifitinisha na wana CCM na CHADEMA

Bernard Membe

Kamwe watanzania tusikubali kulishwa kasumba ya kuwaUpinzani wa kisiasa ni uadui. Tusigawanywe kwa itikadi wala dini


Bernard Membe
Nawapenda watanzania wote bila kujali itikadi zao, dinizao, makabila yao na marika yao. Umoja wetu ndio nguvu yetu.

mlagha
Bahati nzuri miminimeshiriki press Conference hii. Mhe. Membealitumia fursa hiyo kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu Wizara ambayoyamekuwa yakiandikwa na kutangazwa na vyombo vya habari isivyo.

Masuala hayo ni pamoja na taarifa kuhusu uwasilishwaji wa Ripoti ya Tanzaniakuhusu Mpango wa Nchi za Afrika Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM).

Katika suala hili Mhe.
Membe alitoa ufafanuzi kuwa, ni kweli Mhe. Rais hatowezakuwasilisha ripoti ya tathmini ya Tanzania katika Mkutano ujao wa Wakuu wa Nchina Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) unaotarajiwa kufanyika mjini Addis Ababamwezi Julai, 2012 kwa kuwa Timu ya Umoja wa Afrika chini ya APRM inayopitiaripoti hiyo ya Tanzania haijakamilisha kazi hiyo. Hivyo Tanzania itawasilisharipoti yake Januari 2013baada ya timu hiyo kuipitia na si kwa sababu Tanzaniainadaiwa Dola za Marekani laki nane (800,000) kama mchango wake kwa mpango huo.

“APRM ni chombo kilichoanzishwa na Serikali za Afrika na kwa hapa Tanzaniakinaratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje, ni chombo cha hiari kwa nchi za Afrikakujitathmini zenyewe kiutawala bora, si kweli kuwa Rais atashindwa kuwasilishaRipoti ya Tanzania AU kwa sababu hatujalipa deni, bali ni kwa sababu timuinayopitia ripoti hiyo ya Tanzania haijakamilisha kazi yake hivyo tunatarajiakuwasilisha ripoti yetu mwezi Januari 2013 wakati wa kikao kingine cha Wakuu wanchi wa AU,” alisema Mhe.
Membe.

Kuhusu suala la fedha zilizotoweka Wizarani, Mhe.
Membe alieleza kuwa hakuna fedha zilizopotea isipokuwaWizara imewasimamisha kazi Watumishi watano waliofanya mchakato wa kuhamishakiasi cha shilingi bilioni 3.5 kutoka Hazina kuja Wizarani kwa ajili ya ziaraza Mhe. Rais za Addis Ababa, Geneva,…na Arusha bila kibali cha Afisa Masuuliyaani Katibu Mkuu ambaye hakuwepo wakati mchakato huo unafanyika.

Aliongeza kuwa, Watumishi hao wamesimamishwa kazi ili kupishauchunguziunaofanywa na kamati iliyoundwa ili kujiridhisha kama taratibu zakifedha zilifuatwa au kukiukwa katika mchakato huo mzima.

“Tarehe 1 Machi, 2012 wakati mimi sipo Wizarani wala Naibu Waziri, Katibu Mkuu,Naibu Katibu Mkuu na Mhasibu Mkuu kuna mchakato wa kuhamisha fedha kiasi chashilingi bilioni 3.5 ulifanywa kutoka Hazina kuja Wizarani kwa ajili ya safariza Mhe. Rais za Geneva, Addis Ababa,…..na Arusha bila kibali cha Afisa Masuuli.Timu inayojumuisha watu kutoka TAKUKURU, Usalama wa Taifa, Wizara na Ofisi yaMkaguzi Mkuu wa Serikali imeundwa ili kuchunguza suala hilo ili kujua kamataratibu za kifedha zilifuatwa au kukiukwa na uchunguzi ukikamilika tutawekahadharani hakuna cha kuficha,” alisema Mhe.
Membe.

Vile vile, Mhe.
Membe alipinga uvumi unaoenezwa kuwa amekitabiria ushindiChama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 kwa kusema kuwa yeye si mtabiri nakwamba yeye ni mwanachama halisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa maneno na kwamatendo.

Mhe. Membe aliongeza kuwa alichokifanya ni ukarimu kwakuwakaribisha Vijana wa CHADEMAjimboni kwake Mtama mkoani Lindi na kushiriki nao chakula nyumbani kwake.

“Ukarimu hauna udini, rangi wala itikadi, vijana wa CHADEMA
walikuja nikawakaribisha kwa chakula nyumbani, na leonataka niwape somo kidogo, upinzani sio uadui, nchi inayoona upinzani ni uaduihaiko salama wala haitaendelea,”alisisitiza Mhe. Membe
.


Membe anafikiri tumeshasahau aliyoyasema majuzi tu.......... Hivi ile tap ya ITV akiongea hakuna mtu aliye nayo aiweke You Tube ili tuone atasemaje!!
 
biblia inatuambia kuwa hata watu wa Mungu walipotembelea mji flani mwanamke mmoja malaya aliwakaribisha kwake kwa siri sana na kuwapa chakula hatimae wakafanya uchunguzi waoo na walipomaliza akawatorosha ...hatimae yule mwanamke akaokoka
 
CCM inatoa pilau kwa wote, hata wa upinzani njaa ikizidi wanapewa wali.

Kwa mantiki hiyo ukiwapa watu chakula kisha unalewa wewe na kuamua kuropoka tu!napata mashaka na kauli yake kama kweli ina uhalisia wa alichokizungumza kuwaponda CDM
 
Wakuu hebu nipeni title ya kile kitabu alichotaja membe chenye full story ya uchakachuaji wa rada yetu. Nipe title na mwandishi, ukiweza nipe website niwacheki hao wezi wetu. Nimetuma thread naona huyu mwenhe jf ananibania kuiweka. Nataka nikifika home leo niwasome hao wezi wetu. Msaada tafadhali.
 
Membe hoja zako ni dhaifu sana,eti waje na mkanda wa video,kwani wao walikutembelea kwa shari kiasi kwamba waje wakijihami na recorder? After all, ulichokiongea siku zile kilinukuliwa na magazeti mengi tu na sidhani kama waandishi wote wana lao moja. Mjinga gani atakuelewa kwamba Dr Slaa, Mbowe au Lema anaweza kosa walau cash ya kula! This is UTOPIAN
 
Kwahiyo issue nzima ya kukutana na vijana wa CHADEMA, inageuka kuwa 'vijana niliwapa chakula, walikuwa wana njaa sana'.

Viongozi wa ccm wana matatizo makubwa sana.
Hawa si walipanga kukutana??? kwasababu kulikuwa na waandishi wa habari na walirekodi videos kwa mijibu wa Membe??
Sasa kama hao vijana waliibuka tu kwa Membe, waandishi na recording devices vilitoka wapi??

Huyu nae ni aina flani ya kenge anayeogopa kukatwa mkia kwenye lichama lake.
 
W





Membe anafikiri tumeshasahau aliyoyasema majuzi tu.......... Hivi ile tap ya ITV akiongea hakuna mtu aliye nayo aiweke You Tube ili tuone atasemaje!!

Hahahahahahahaaaaa!!!!!

Ma-ccm pumbafu sana!!
Unawaalika watu nyumbani kwako halafu kesho yake unasema walikuwa na njaa nikawapa msosi!!

Ujuha umeansikwa usoni kwake!!
 
Mara ya kwanza alisema kuwa alikuwa jimboni kwake na akasikia CHADEMA wako huko hivyo akawaalika kwa chakula. Na akaendelea kusema kuwa upinzani sio uadui, yeye amekaa nje ya nchi kwa muda mrefu hivyo anajua demokrasia.

Sasa week mbili baadae naona memory box yake imeingiliwa na kuja na ngonjera nyingine. Lakini tunatakiwa pia tuunganishe dots, leo bungeni kuna mbunge wa viti maalum kutoka Lindi amesema wachaga ni wezi. Hivi ni bahati mbaya Membe amegeuza maelezo yake za zamani kuhusu chakula alichotowa kwa CHADEMA siku ambayo mbunge wa Lindi anasema kuwa ndio wamesababisha umaskini wa Lindi?
 
membe yuko clouds FM anahojiwa na Gerald hando, anasema hakuwaalika Godless lema na wengine kwake ila alipokuwa mezani mlinzi alimwambia vijana wa chadema wako nje akawakaribisha, wakaingia na walikuwa na njaa kwelikweli wakala

Pili anasema watanzania wanajua kamwe hawezi kuifagilia chadema na hata Clouds wanajua kwanini hawezi mmmh?

kauli hizo zenye rangi nyekungu ndo zinanipa dukuduku, ile story ilikuwa ni propoganda ama kweli?

kasema kama kuna mkanda waliurekodi na wautoe ...atajiudhuru hata sasa!





Nimestaki kidogo
ngoja niendelee kumsikiliza nakuja kuleta uptodate

hiyo ya kuwa hakuwaalika sina atatizo nayo...
ya pili nayo hiana mashiko sana
lakini ya tatu inanisumbua,,, clouds ni akina nani mpaka wajue hilo analolisema?
 
kwa wanafasihi jambo hili halitupi shida kwani hii haimaanishi kuwa walihitaji kula. njaa hapo tunajua maana yake. vijana wakapewa chakula hapo ina maana yake pia.
 
Membe anapaswa kuzungumzana Masha na Mongela habari ya M4C ndo imetua Mtama! Ritz Mungu hawabariki wezi hatasiku moja.
 
Back
Top Bottom