Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 137,661
- 272,490
Mfungwa wa kisiasa Kamanda Mdude Nyagali leo ametimiza siku 244 Jela ambako amewekwa kwa kesi isiyo na dhamana
Kwa mara ya kwanza alishitakiwa kwa makosa ya Uhujumu uchumi lakini baada ya kuthibitika kwamba Mhujumu uchumi huyo mpya mapato yake kwa mwezi hayafiki hata Tsh laki moja, akabadilishiwa mashitaka na kushitakiwa kwa kosa la kukutwa na madawa ya kulevya , huku ushahidi ukionyesha kwamba hajawahi kuuza wala kumiliki hata Ugolo.
Nachukua nafasi hii kumuomba Mwenyezi Mungu ili aingilie kati na kuhakikisha haki inatendeka.