KAMANDA 'MDUDE' SIO SIRI UMEJITAKIA MWENYEWE
Hivi hukumuona mwezako Roma Mkatoliki, alivyokimbilia nchini Marekani baada ya kunusurika kuuawa alipotekwa na watu wasiojulikana?
Hivi hukuwaona wenzako akina Maria Sarungi, Ansbert Ngurumo, Evarist Chahali, Mange Kimambi na Kigogo 2014 wanavyoikosoa Serikali huku wakiwa nje ya Tanzania?
Hivi Mdude hakujifunza kwa Ben Saanane au hakujifunza pale alipotekwa kwa mara ya kwanza?
Hivi ulipata ujasiri gani kuanza kuikosoa Serikali ya CCM kila kukicha mtandaoni huku ukiwa unaishi hapahapa nchini? Kwani akina Kigogo, Ngurumo, Chahali na Mange Kimambi uliona ni wajinga walipoamua kukimbilia ughaibuni?
Ndio maana nasema kuwa, Mdude Nyagali Chadema umeyataka mwenyewe, ila shukuru tu kwamba utaendelea kuwa hai gerezani hata kwa muda wa miaka 10, kuliko kama ungetekwa tena na watu wasiojulikana.
Bai bai 'SUMU YA NYIGU'
Sent using
Jamii Forums mobile app