Mdude CHADEMA umejitakia mwenyewe

Mdude CHADEMA umejitakia mwenyewe

Tuko bize na covid20 (chadema) msitusumbue watalamu wetu wako kazini hili gonjwa halitibik wanachama chukueni tahadhari.
 
KAMANDA 'MDUDE' SIO SIRI UMEJITAKIA MWENYEWE.

Hivi hukumuona mwezako Roma Mkatoliki, alivyokimbilia nchini Marekani baada ya kunusurika kuuawa alipotekwa na watu wasiojulikana?

Hivi hukuwaona wenzako akina Maria Sarungi, Ansbert Ngurumo, Evarist Chahali, Mange Kimambi na Kigogo 2014 wanavyoikosoa Serikali huku wakiwa nje ya Tanzania?

Hivi Mdude hakujifunza kwa Ben Saanane au hakujifunza pale alipotekwa kwa mara ya kwanza?

Hivi ulipata ujasiri gani kuanza kuikosoa Serikali ya CCM kila kukicha mtandaoni huku ukiwa unaishi hapahapa nchini? Kwani akina Kigogo, Ngurumo, Chahali na Mange Kimambi uliona ni wajinga walipoamua kukimbilia ughaibuni?

Ndio maana nasema kuwa, Mdude Nyagali Chadema umeyataka mwenyewe... Ila shukuru tu kwamba utaendelea kuwa hai gerezani hata kwa muda wa miaka 10, kuliko kama ungetekwa tena na watu wasiojulikana...!!

Bai bai 'SUMU YA NYIGU'

Sent using Jamii Forums mobile app
kwa chadema walivyo,watamuacha apambane na hali yake
 
Usifanye harakati kama huna element za ujasus..!
Kwa mfano tuseme kweli kategwa kama alivyosema mababe wa twitter.

Hivi unawezaje kushitukia mchezo kama binti anatokea jimboni kwa mbunge wa CHADEMA, jimbo linalo dhaniwa hicho chama kina nguvu sana kuliko mahali popote duniani?

Mrembo anaigiza CHADEMA in blood, na anajitambulisha ni wa makabila yale ambayo CHADEMA iko damuni, huku akirusha mapicha au twitt kibao za kichadema?

Anakusifia kwa ujasriri wako wa ajabu kuongea lolote dhidi ya dola na mwenye kushika dola.

Anakupa pole na kukuonesha nia ya kukupunguzia machungu ya kutenguliwa nyonga ama 'center bolt' kama alivyo wahi kuiita mdudde mwenyewe. Kisha anakurushia muamla 1M na kitu tarehe hizi ngumu kiuchumi.

Ukimcheki mtoto mwenyewe pengine kwa mtazamo wako (sio wangu) mzuri balaa anakuahidi kuja kukutunuku tufaa(apple) lililomponza adamu.

Tuwe wakweli jamani hivi nani kati yetu angechomoka huo mtego hasa sisi wenye kipato cha kawaida kama mdude?
Tuache kumdhihaki mdude, tuache unafiki tuwe wakweli na tuseme kamanda imemkuta ajali kazini kama nzi kufia kwenye kidonda.

Zingatia elimu na umri wa Mdude kabla huja mhukumu au kumdharau kunasa kijinga hata kwa yale aliyokuwa anatuma mitandaoni bila tahadhari au kufanya yale yaliyo pelekea kuingia mikononi mwa vyombo vya sheria.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mfano tuseme kweli kategwa kama alivyosema mababe wa twitter.

Hivi unawezaje kushitukia mchezo kama binti anatokea jimboni kwa mbunge wa CHADEMA, jimbo linalo dhaniwa hicho chama kina nguvu sana kuliko mahali popote duniani?

Mrembo anaigiza CHADEMA in blood, na anajitambulisha ni wa makabila yale ambayo CHADEMA iko damuni, huku akirusha mapicha au twitt kibao za kichadema?

Anakusifia kwa ujasriri wako wa ajabu kuongea lolote dhidi ya dola na mwenye kushika dola.

Anakupa pole na kukuonesha nia ya kukupunguzia machungu ya kutenguliwa nyonga ama 'center bolt' kama alivyo wahi kuiita mdudde mwenyewe. Kisha anakurushia muamla 1M na kitu tarehe hizi ngumu kiuchumi.

Ukimcheki mtoto mwenyewe pengine kwa mtazamo wako (sio wangu) mzuri balaa anakuahidi kuja kukutunuku tufaa(apple) lililomponza adamu.

Tuwe wakweli jamani hivi nani kati yetu angechomoka huo mtego hasa sisi wenye kipato cha kawaida kama mdude?
Tuache kumdhihaki mdude, tuache unafiki tuwe wakweli na tuseme kamanda imemkuta ajali kazini kama nzi kufia kwenye kidonda.

Zingatia elimu na umri wa Mdude kabla huja mhukumu au kumdharau kunasa kijinga hata kwa yale aliyokuwa anatuma mitandaoni bila tahadhari au kufanya yale yaliyo pelekea kuingia mikononi mwa vyombo vya sheria.

/one good thing about music/
/when you dance you feel no pain/
 
KAMANDA 'MDUDE' SIO SIRI UMEJITAKIA MWENYEWE.

Hivi hukumuona mwezako Roma Mkatoliki, alivyokimbilia nchini Marekani baada ya kunusurika kuuawa alipotekwa na watu wasiojulikana?

Hivi hukuwaona wenzako akina Maria Sarungi, Ansbert Ngurumo, Evarist Chahali, Mange Kimambi na Kigogo 2014 wanavyoikosoa Serikali huku wakiwa nje ya Tanzania?

Hivi Mdude hakujifunza kwa Ben Saanane au hakujifunza pale alipotekwa kwa mara ya kwanza?

Hivi ulipata ujasiri gani kuanza kuikosoa Serikali ya CCM kila kukicha mtandaoni huku ukiwa unaishi hapahapa nchini? Kwani akina Kigogo, Ngurumo, Chahali na Mange Kimambi uliona ni wajinga walipoamua kukimbilia ughaibuni?

Ndio maana nasema kuwa, Mdude Nyagali Chadema umeyataka mwenyewe... Ila shukuru tu kwamba utaendelea kuwa hai gerezani hata kwa muda wa miaka 10, kuliko kama ungetekwa tena na watu wasiojulikana...!!

Bai bai 'SUMU YA NYIGU'

Sent using Jamii Forums mobile app

For whatever reason,mkosoaji ni mkosoaji!

Ana haki zake sawia

Siwezi kua hapa nashabikia pure uonevu kutoka kwa oppressing govt kwa innocent victims

Instead the same govt inatakiwa ilinde haki za wakosoaji hao hao

Sad ni kinyume!

Hii stupid move ya uonevu by this oppressing govt imeichafua na chuki level imeongezeka against it,next level!

Sijui akili mnaweka wapi?

Kazi zenu za kuendesha hii nchi ni kubwa maajabu mnapata muda wa kuonea powerless critics who are doing their job
 
Mtego wa wanawake ni wanaharakati wachache saana waliweza kuuepuka, nashindwa kumlaumu katika hili.

Haya mambo aliyaweza fidel castro.

Jamaa mapema saana angeikimbia hii nchi, wenzie kinas chahali na ngurumo wakula kuku ughaibuni.
 
Kuna kitabu nimesoma,
Kinaitwa Blowing up Russia, kiliandikwa na jasusi wa zamani wa KGB/FSB,(alexander Livinenko)huyu aliuliwa na sumu.
Mbinu anazotumia Putin raisi wa Russia,kuwamaliza wapinzani wake,zinafanana kabisa na hizi harakati za Wasiojurikana wa hapa bongo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kigo
Kigogo atawaponza vijana wajingawajinga wengi Kwa uwongouwongo wake wa kujipatia umaarufu!

Alishindwa vipi kumtahadharisha mdude mapemaa kabla ya kupatwa na lolote?

Vijana endeleeni na Ujinga, Wakati nikiwa Kwa wazazi wangu mara Kwa mara walikuwa wakiniusia kuwa, mwanangu, kuwa makini ktk maisha Maana ikiwa hutafuata malezi Yetu kama wazazi wako,Dunia itakufunza Kwa lazima!

Ndio hivyo, usipofunzwa na mama yako, Dunia itakufunza, Wakati mwingine, usipelekwepelekwe Kwa mkumbo na watu Kwa kutaka umaarufu, unakufa na hakuna wa kukutetea, Vinginevyo twendeleeni kutukanana hapa Mitandaoni, mdude ndo hivyo tena
 
Kwangu mdude ni jemedali wa kweli aliyebaki katika vita baada ya waoga wengi kukimbia, ni ujasiri wa hali ya juu aliokuwa nao huyu jamaa na anastahili tuzo ya Nobel, popote niendeka utabaki kuwa moyoni mwangu daima like Mawazo, Ben, Lissu.Revolution n long process inayohitaji watu waliojitoa kweli kweli kupigania kile wanachokiamini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom