Mdahalo ni lazima sio hiari

Mdahalo ni lazima sio hiari

Ccm ndio waanzilishi wa kukimbia midahalo.. Kimewakumba nn mwaka huu? Wanatapa tapa..
 
siku lowasa akienda mdahalo kura yangu naiondoa...
na sisi tuonyeshe dhalau zile za mwaka 2010 tulizo onyeshwa....
kama na ww utaondoa kura jamaa akikubali kuburuzwa ungana na mm
 
Ha ha ha ha ha ha ha ha mmepatikana nyie mafisadi na hilo fisadi lenu lazima asimame jukwaani atuambie atatufanyia nini vinginevyo tupa kure.

Ameahidi elimu elimuu elimuuu
 
Hakuna mdahalo na hakuna Sheria inayomlazimisha kufanya hivyo. Halafu wabasilishe kampemi zao kudai asichaguliwe kwa sababu alikataa kwenda kwenye mdahalo...
 
Tunataka mdahalo wa kina kuhusu masuala kitaifa tujue jinsi gani tutakaowapa dhamana wataendesha nchi
yetu , jinsi gani ilani zao zitatekelezwa, utamaduni huu ujengeke kwenye chaguzi zetu , tena sio tu kati ya wagombea urais wa vyama vya siasa , bali pia ndani ya vyama wakati wa mchujo (a.k.a kukatwa) , kama wenzetu wenye demokrasia imara wanavyofanya , wataokaoshiriki ndio tutawapima na ndio tukaowachagua , wasioshiriki midahalo inaashiria hawajiamini na sera zao hazitekelezeki, nachelea kusema ni "wasanii wa kisiasa"! Hatutawamini bila kuwapima , jaribu kutafakari kama Donald Trump angekacha kwenye mdahalo wa Republican, au Obama wakati ule, Obama angekimbia , ingekuwaje ? Tujifunze kwa wenzetu , tuache kujitoa ufahamu kuwa hatujui umuhimu na mchango wa debates,ili tujenge demokrasia yetu iwe pana ,imara, ya uwazi , na ushirikishwaji wa wananchi. Tume ya taifa ya uchaguzi pia iangalie ni jinsi gani hili linaweza kusimamiwa iwe ni lazima na sio hiari. Itoshe tu kusema , asiyeshiriki midahalo hana nia ya kujenga demokrasia yetu, na kwa maana hio hafai kupewa dhamana ya kuongoza nchi yetu, na hivyo ndugu zangu wasioshiriki tusione haya "kuwakata" tar 25 October !



Defiant Donald Trump dominates US Republican TV debate - BBC News

kweli kabisa mkuu waache kusingizia historia.
 
inafurahisha sana lowasa kukimbia mdahalo.
nadhani anaogopa atashindwa simama zaidi ya 30 minutes

mimi nadhani waruhusiwe kukaa kama mtu hawezi kusimama na hilo lisitunyime Rais bora kama kweli ni bora, mradi tu kila mtu ashiriki tumpime uwezo wake wa kufikiri na kuchambua mambo.
 
Asante kwa kuchagua mdahalo tu kati ya kijifunza kutoka Marekani na nchi zilizoendelea kidemokrasia na kuacha mambo kama tume huru ya uchaguzi, polisi wasoegemea upande wowote, vyombo huru vya habari nk
 
siku lowasa akienda mdahalo kura yangu naiondoa...
na sisi tuonyeshe dhalau zile za mwaka 2010 tulizo onyeshwa....
kama na ww utaondoa kura jamaa akikubali kuburuzwa ungana na mm

mkuu nadhani hatutakiwi kuendesha nchi hivyo kama kweli tuna nia ya kweli, mbona Lowasa kapokelewa CHADEMA pamoja na kuwa walimpinga muda mrefu kwa hoja ya kutaka mabadiliko, ndo maana wanamabadiliko wamesahau yote ya nyuma, vivyo hivyo na hili suala la midahalo ni dai la muda mrefu la watanzania, si vyema kulikaaa kisa tu waliwahi kulikataa, twendeni tukashindanishe hoja.
 
Donald Trump is the worst debater so far still he is leading all other candidates in the Republican side,you can see how less effective the debate can be in rallying the support behind you.People don't wanna hear sweet promises anymore, all they want to see happening is a change, that's it.

We are not judging who is the best or worst debater, we simply want to know if he is fit enough to be president, can he handle the pressure now? Because he failed being under simple premiership pressures 8 years ago.
 
Tunataka mdahalo wa kina kuhusu masuala kitaifa tujue jinsi gani tutakaowapa dhamana wataendesha nchi
yetu , jinsi gani ilani zao zitatekelezwa, utamaduni huu ujengeke kwenye chaguzi zetu , tena sio tu kati ya wagombea urais wa vyama vya siasa , bali pia ndani ya vyama wakati wa mchujo (a.k.a kukatwa) , kama wenzetu wenye demokrasia imara wanavyofanya , wataokaoshiriki ndio tutawapima na ndio tukaowachagua , wasioshiriki midahalo inaashiria hawajiamini na sera zao hazitekelezeki, nachelea kusema ni "wasanii wa kisiasa"! Hatutawamini bila kuwapima , jaribu kutafakari kama Donald Trump angekacha kwenye mdahalo wa Republican, au Obama wakati ule, Obama angekimbia , ingekuwaje ? Tujifunze kwa wenzetu , tuache kujitoa ufahamu kuwa hatujui umuhimu na mchango wa debates,ili tujenge demokrasia yetu iwe pana ,imara, ya uwazi , na ushirikishwaji wa wananchi. Tume ya taifa ya uchaguzi pia iangalie ni jinsi gani hili linaweza kusimamiwa iwe ni lazima na sio hiari. Itoshe tu kusema , asiyeshiriki midahalo hana nia ya kujenga demokrasia yetu, na kwa maana hio hafai kupewa dhamana ya kuongoza nchi yetu, na hivyo ndugu zangu wasioshiriki tusione haya "kuwakata" tar 25 October !



Defiant Donald Trump dominates US Republican TV debate - BBC News

Mbona 2010 hamkuzunguza haya. Watu walikimbia mdahalo na bado wakashinda. Hatutaki mdahalo kashtaki Polisi
 
Mawazo yako ni mazuri, tuanze na katiba ya wananchi, ambayo itatulazimisha kuwa na mdahalo, Tume huru ya uchaguzi, mgombea binafsi n.K. Haya CCM wameshindwa, tuchague UKAWA watuletee mdahalo 2020.
 
Kufanya mdahalo na Mtu ambaye hamjui Rais wa Libya alikuwa nani, Rais Saddam alikuwa anaongoza nchi gani na tofauti ya Iraq na Kuwait ni nini huko ni kupoteza muda kijinga.
Ni kama Mhe Msigwa alivyo kataa pale Bungeni mara nyingi kujibu taarifa zilizokuwa zinatolewa na Lusinde na Asumpta Mshama na wote hata wabunge wa ccm wakaona Msigwa ameutendea haki muda.
Magufuli huyu ambaye anaiga mpaka slogan za chama pinzani ndio wakufanya nae mdahalo? Huo utakuwa mdahalo au mipasho isiyo kuwa na tija? Na kwa vile Watanzania wengi wamenyimwa Elimu basi kwao mdahalo huo ambao utaambatana na vijembe basi mwenye vijembe ataonekana mshindi na taifa kwa upande wa wachache wenye uelewa hawatakuwa wamenufaika.
 
mimi kwa mawazo yangu mdahalo ni sawa ila kwa sasa mgombea wetu yupo busy kutafuta support kwa wazee na akina mama kwa sababu vijana wote numemkubali, sasa ushauri wangu kwa makamba ni kwamba mdahalo huu uwe kwa wenyeviti wa vyama vikuu MH. BOWE VS MH. KIKWETE ,,, NAPE VS MNJIKA ,,,,,,, HAPO PATACHIMBIKA.
Mkuu kwanza hakuna mgombea alielala wote wapo busy kutafuta kura na ktk mdahalo pia ni fursa nzur ya kujenga hoja na kunadi sera kwa wapiga kura ili wakuchague kwa hiyo ni vizur wagombea wa urais ndio washiriki mdahalo sabab wao ndio waliopewa dhamana ya kuongoza nchi na vyama vyao na sio wenyeviti wa vyama na mwisho ukumbuke NAPE NA MNYIKA sio wenyeviti wa vyama!!.
 
Ccm wakipenda midahalo itafanyika wasipopenda hakuna ulazima wowote.tuliona wagombea wao wakiondolewa kwenye midahalo 2010.na Dr slaa alikimbiwa 2010 ile leo kulikoni
 
hivi mwaka 2005 na 2010 wakina nani walikimbia mdahalo na kwasasa kwann wanataka kisa mzee ni wa vitendo sio wa kuongea sana
ukiondoa 1995, miaka mingine yote ccm walikimbia midahalo. 2000 na 2005 walimtuma ngasongwa, 2010 hata wabunge na madiwani waliwakataza, jk alihojiwa peke yake na tbc, leo kimewasibu nini?
 
kuna midahalo ya ubunge kwa majimbo inaendelea kule azam tv chini ya tido mhando..... wagombea wa ccm wanakimbia kama vichaa.... alianza wa segerea akamkimbia mtatiro, jana wa ccm kwa jimbo la kawe kamkimbia halima mdee sasa unajiuliza hawa watu wanataka mdahalo kweli au wanatishia kujamba wakat wanaharisha? wanabip wanapigiwa halafu hawapokei!!!!!

Wanavyoipotezea hii post!!! ....kweli kuna watu wanafiki....
 
Donald Trump is the worst debater so far still he is leading all other candidates in the Republican side,you can see how less effective the debate can be in rallying the support behind you.People don't wanna hear sweet promises anymore, all they want to see happening is a change, that's it.
Una kiingereza kizuri ila inakupasa ujifunze matumizi ya nukta na comma
 
ukiondoa 1995, miaka mingine yote ccm walikimbia midahalo. 2000 na 2005 walimtuma ngasongwa, 2010 hata wabunge na madiwani waliwakataza, jk alihojiwa peke yake na tbc, leo kimewasibu nini?

Nyani haoni la kwake. Wanadhani mgombea wetu ni dhaifu, wanajidanganya.
 
Sina umeme,mdahalo nitaonaje,

MM nataka umeme kwanza,sioni umuhimu wa midahalo maana yatakuwa yaleyale SAADAM Raisi wa KUWAIT..

MIMI sitaki kabisa..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom